Biashara ya Kuonesha Mpira wa Miguu (Kibanda-umiza): Fahamu Kiasi cha Mtaji, Vifaa na Mbinu za Uendeshaji

Biashara ya Kuonesha Mpira wa Miguu (Kibanda-umiza): Fahamu Kiasi cha Mtaji, Vifaa na Mbinu za Uendeshaji

wakuu nataka nianze biashara ya kuonyesha ball kupitia dstv,so kwa wenye uzoefu wa biashara hii naomba kujua costs za production na sehemu ya kuonyeshea nnayo n n kubwa pia ni sehemu y mkusanyiko wa watu.
 
Mkuu biashara hii inalipa sana cha msingi sehemu iwe na mkusanyiko wa watu, nunua dstv dish na decoder yake na unakuwa unalipia kila mwezi kama tsh.80000/-

Pia tafuta wanachama wa kudumu wanakuwa wanalipa tsh.10000/- kwa mwezi, wakiwa 50 sawa na tsh.500000/- achilia mbali wale wa rejareja watatoa 500/- au 1000/- kila mechi.
 
Mkuu biashara hii inalipa sana cha msingi sehemu iwe na mkusanyiko wa watu, nunua dstv dish na decoder yake na unakuwa unalipia kila mwezi kama tsh.80000/-

Pia tafuta wanachama wa kudumu wanakuwa wanalipa tsh.10000/- kwa mwezi, wakiwa 50 sawa na tsh.500000/- achilia mbali wale wa rejareja watatoa 500/- au 1000/- kila mechi.

asnte mkuu
 
Hii 80000 haitoshi kama kweli unataka kufanya biashara. Unahitaji tsh 130000 hivi kwa mwezi ili kupata premium bouquet. Aidha decoder 1 huenda ickutoshe, unaweza kutafuta ya pili ambayo ikiunganishwa na ya kwanza itakufanya upate chnl 2 kwa wakati m1. Itakugharimu tsh 150000.
 
Mkuu aselona kwani hii biashara haiwezekani kutumia fta satelaits? Tuelimishe how not or posibo.
 
hii 80000 haitoshi kama kweli unataka kufanya biashara. Unahitaji tsh 130000 hivi kwa mwezi ili kupata premium bouquet. Aidha decoder 1 huenda ickutoshe, unaweza kutafuta ya pili ambayo ikiunganishwa na ya kwanza itakufanya upate chnl 2 kwa wakati m1. Itakugharimu tsh 150000.

Kaka umenivuruga kidogo, kama premium banddle ni 130,000 iweje vikiwa viwili unalipa 150,000.
 
yani nakupa bigup kwa kuweza kulitambua hilio kama una sehemu ya mkusanyiko wa watu wengi hasa uswazi ambako kuna watu wengi waweza fanya hiyo biashara

unachotakiwa ni kuwa na tv 2 au hata 1, uwe na decoda ya dstv, na kuwa na wanachama wasiozidi 5 wa kudumu na uwe na kianzio cha 150,000 hivi utafanya biashara vyema
 
Thanks Guys na nasubiri msimu uanze then nianze kwangu nione kama itantoa au lah
 
Imetulia kaka ila inategemea na location mana uswahilni ni uhakika maana watu ni wengi ila ushuani hamna kitu kaka na ubaya sasa hivi ni abu dhabi wamekosa power ya kuonyesha ambao walikua cheap so yabd utegemee DSTV ambao ni gharama c kitoto
 
Wadau nashukuru kwa maon yenu nakaribisha mwenye maoni pamoja na ushauri kuhusu aina ya projector na ubora wake ninayoweza kutumia kwa shughul hii


Jaribu kununua projector za Epson.

Vp unaendeleaje na ujasiriamali wako?
 
Kwa kweli hapa sina utaalamu. Lakini mambo ya free to air. yaani neno free, neno promotion neno lipia upate bure ni maneno sitakagi wala kuyasikia kwa sababu ni uzushi wa kijinga. Na wala usiwasikilize wajinga wa startimes au ting au wajinga wowote eti wataonyesha mpira wa majuu. Ni upuuzi mtupu. Jipige weka dstv simamia biashara yako hii waweza toka.

Kuna kitu nasikia sijui Arab sat sijui nini nasikia hii kitu ni nzuri na cheap pia. Ila gharama za mwanzo za kufungiwa ni za juu sana.
Unalipa kama laki tisa, wanakufungia upuuzi woooote halafu baada ya hapo kila mwaka, narudia tena kila mwaka unakua unalipa kama dolla 40 na unalipiA KWENYE MTANDAO hiyo pesa.
Ila hii kitu nimesikia tu, kuna ndugu yangu anajishughulisha na dili hizi A-town, ila kokote anafunga. Mimi hii huduma siiitumii

Mimi ntumia tu dstv kwa matumizi yangu binafsi
yhanx

Mkuu unaweza kunipatia hiyo namba yajamaa yako wa AR-town nikacheki nae na akanielewesa kimapana zaidi?
naomba uni pm kama utafanikisha kuwa nayo.
 
Kwenye hyo milion 2 nahitaji Screen 1 kubwa, projector na king'amuzi cha DSTV chenye uwezo wa kuonesha mechi mbili kwa pamoja. Je kwa mtahi huo nitaweza?
 
Iyo biashara ikopoa sana kwa uswazi,kikubwa miundombinu iweke fresh,viti vya plastik,jenga ukumbi mkubwa,feni za kutosha,stage iwe pana,vyoo, madirisha ya kutosha ukiweza weka kioo timtedi ili projector ioneshe vyema, vuta kafriji kako ka vinywaji na night wauza kahawa usiwatose
 
Kwa wenye mabanda bei za vifurushi ni kubwa sana hasa Dstv ili upate ligi ya uingereza epl hapa inakulazimu ununue kifurushi kuanzia hiki cha dstv compact plus 122500(laki moja na ishirini na mbili mia tano) hapo una kimoja kama una Tv mbili inakubidi uwe na decoder mbili na zote uzilipie ile huduma ya kuunganisha tv mbili kwa decoder moja na ionyeshe mechi tofauti wanadai ilitolewa anaejua mautundu tusaidiane.

Binafsi baada ya kuona hizo gharama hiyo ya kifurushi bado hujalipa kodi na umeme na kibaya eneo nilipoweka hii biashara haijachangamka kivile NILIFANYA HILI KUJIPUNGUZIA GHARAMA.

Nikanunua sattellite dish lile kubwa na receiver ili nipate chanell za bure kweli sport 24 Hd inarusha karibu mechi zote inanisaidia japo hapa karibuni imesumbua sana hii sport 24 Hd signal zilikuwa chini sana now ipo vizuri ila changamoto yake kuu NIONAVYO HII INAFAA KWA MATUMIZI YA NYUMBANI SIO KIBIASHARA.

SOLUTION NYINGINE KUNA HAWA WANAWEKA channell za mpira katika azam au star times hawa sijawajaribu kama yupo anaezitumia tusaidiane.

ILA NI BIASHARA NZURI UKIWA NA LOCATION NZURI INGAWA MAUMIVU VIFURUSHI wageni karibuni katika hii bussiness leteni na maswali.

Mliopo humu na mna mabanda ya mpira tushaurine tufanye nini tuendeshe kifaida zaidi.

Je, Bien Sport au super Sport hizo zinazowekwa kwenye decoder zinadumu kwa muda gani?
 
Mimi ninatumia Star Times. Hao wanaoweka channel za mpira wako wapi waniwekee?
 
mimi ninatumia star times. Hao wanaoweka channel za mpira wako wapi waniwekee?
Wapo nadhani hata ukiingia kupatana au hata humu kuna baadhi ya matangazo yao shida inadumu kwa muda gani?
 
Back
Top Bottom