Biashara ya kutengeneza na kuuza, ndio itakayo timiza ndoto zako

Biashara ya kutengeneza na kuuza, ndio itakayo timiza ndoto zako

Kilimo ni kizuri kama kuna uhakika wa maji au mvua; au unaweza ukagawa sehemu, nyingine ikawa ranch ya mifugo kama mbuzi au kondoo.
Au ukaanzisha kampuni ya kununua mazao na kuyaongezea thamani; hii haiathiriwi na ukosefu wa mvua vs mkulima.​
Hili ni wazo zuri sana, changamoto huwa inakuja kwenye ukusanyaji wa hayo mazao kutoka sehemu tofauti maana inahitaji uwe na stock ya kutosha kuhudumia kwa muda wa kipindi kirefu ndani ya mwaka.

Changamoto nyingine ni namna ya kupenya sokoni maana linapokuja swala la bidhaa za mazao ya chakula (mf mchele), waTz wengi wamezoea vitu local kuliko vile ambavyo vipo kwenye vifungashio tayari.
 
Huwa namtamania sana Super Loaf, mate wake umekuwa moja kati ya mikate bora sana jijini Dar, watu wa kati wengi wanainunua. Brand yake imekaa mahali pake tayari.
Changamoto ya hii biashara ni kuwatunza watu wa jikoni, ushindani huwa unakuwa mkubwa sana na wakiondoka tu dosari huanza kuonekana baada ya muda fulani.
 
Kuna haya magari ya kichina watoto wanakaa na kuendesha; unaweza kumtumia fundi wako wa uchomeleaji mkadizaini kitu kizuri cha muundo huo, na badaye kuuza.
Bahati nzuri kila kitu kinapatikana kwenye maduka ya wazawa hapa nchini.​
Hayo magari naweza pata picha au video yake??
 
kila mtu na bahati yake ndugu zanguni kila biashara inalipa mambo ya hii serikari ni toka enzi na mifumo ni hiyohiyo tu ukiiogopa huwez fanya kitu hata HUYO MULOKOZI ashafanya biashara kibao zakagoma we umefanya ngapi kama ela unayo wekeza huwezi jua
 
Biashara yoyote inahitaji uvumilivu; wengi wanaamua kufunga biashara zao na kulalamika kwa sababu wanakuwa wamekosa uvumilivu.

Na hasa ukiingia kwenye hii biashara ya kutengeneza na kuuza, muda mwingi wewe unakuwa unatoa pesa tu; mpaka uje uanze kuona faida inachukua muda mrefu.

Unapotaka kufanya biashara yenye mafanikio, ni lazima uwe na mtazamo wa mjasiriamali ''entrepreneur''; ambaye kwake kupata pesa, ni chaguo la pili na si la kwanza.

Biashara inaweza kuchukua miezi na miezi au miaka na miaka, mpaka kuja kukupa faida unayoitaka; muhimu uwe umeiwekea misingi mizuri ya kufika kule unakotaka kufika.

Mwanzoni ni lazima ukubali kupoteza pesa, ili baadaye ndio uje upate pesa.

Kwa mtu anayejiingiza kwenye biashara ya kutengeneza na kuuza; huyu anaingia gharama kubwa sana kuliko yule aliyeingia kwenye biashara ya kununua na kuuza (uchuuzi).

Ila huyu, anayetengeneza na kuuza (entrepreneur), huko mbeleni atakuwa na mafanikio makubwa sana, kwa sababu inampelekea kwenye kumiliki kiwanda kama sio viwanda.

Kama mjasiriamali, utajisikiaje pale unapotembelea duka la kwanza mpaka la 50 n.k, unakuta linauza bidhaa zako?

Kwa kifupi, hii biashara inalipa ingawa inachukua muda mrefu.

Karibu kwa maswali.​
Mtaalamu shukran
 
Back
Top Bottom