Biashara ya Madawa ya Kulevya: Wafungwa wa Kitanzania Hong Kong waendelea kufunguka

Biashara ya Madawa ya Kulevya: Wafungwa wa Kitanzania Hong Kong waendelea kufunguka

ha ha ha huu uzi hautalast a day ... Mods watauondoa

sijui ni kwa sababu ya hayo "majina makubwa" au vipi....ilipokuja ile ya mbunge iliachwa ila hizi za majina haya kila yakiwekwa uzi unakua deleted!
 
Mwandiko huu unanitia wasiwasi na naomba wachangiaji wanaojua kusoma miandiko watueleze kwani inaelekea mwandishi amejitambulisha kama Mohamed lkn mwandiko ni wa kike

Unataka ajitambulishe kwa jina lake halisi ili wamnyamazishe kwa kumuulia gerezani?
 
Du?? Kweli umelipwa shi ngapi, unaleta uongo huku, sasa jf imeshakuwa kituo cha kueneza uongo, mimi nilikuwa naitegemea sana jf km mahali pakuleta au kupata habari za uakika, lkn km mtu anajitungia tu, na kuja, na majina bila ushahidi basi hii noma, bas na mimi niwataje wa kwangu hapa,
mh sita, mh zito kwabwe, mh harison mwakwembe, mh, john mnyika, dr. Silaa, mboye, mh mwigulu,

note: No data/fact, because every ONE may mention as he/she like, reffer this post
 
Mungu na atunusuru!

Mtazamo:
Thread za habari nzito kama hizi ndizo vishoka wa mitandaoni hupiga deal za kutetea waharifu. Siku hizi habari kama hizi zikiwekwa mitandaoni, kuna cafe zinakodiwa na vijana wanalipwa kushinda kutwa hapa kuwatetea wanaowalipa. Klauz, Home Shopping Centre, Idd Azzan ni miongoni mwa waliowahi kufanya mchezo huu.
 
jamaa amepata taabu kweli ya kuchonga mwandiko ili asijulikane, hii vita ni kubwa tuwe waangalifu sana, watu wasipokuona lakini Mungu anakuona. "TUMCHE MUNGU KWA DHATI YA MKUMCHA"
Tena na hawa polisi wetu wanaongoja ushahidi wa kuletewa, ni balaa
 
Mimi kuziamini hizo barua mbona inakua ngumu kidogo, Mwenye proof kua kweli imetoka Hong Kong ajaribu kutu-convince kidogo tuone kama ataeleweka, maana nahisi ni jamaa tu yuko bongo anawahisi hao jamaa aliowaandika then kaamua kuwaandika majina, sioni sababu ya raia inayouza madawa kugeuka na kuanza kutaja waliomtuma kupeleka madawa huku anajua fika nguvu jamaa waliyonayo, unless ana ulinzi pembeni au kahukumiwa kifo au maisha sasa hana njia nyingine zaidi ya kutumia hii njia kama kutubu aliyofanya...

Still, hiyo sio evidence tosha maana yeyote anauwezo wa kuandika na kuweka kwenye net... mbona story ya kufikirika tu hiyo haina hata mishiko ya kutisha. Sababu zangu ni nyingi ila moja ya muhimu, em fikiria wewe ndio muuza madawa main, unataka kuwatuma vijana wayasambaze huku unajua kabisa ni risky, unadhani utaenda kujitambulisha kwao?

Obviously utatumia njia nyingine ya wao kuchukua madawa na kufikisha destination bila hata ya wao unaowatuma kukujua, pili mtu moja kadakwa atajuaje watu wote wanaohusika na madawa bongo? au kauliza wengine gerezani? na still hata kama ni hivo, hao jamaa wote na vyeo vyao serikalini si wajinga kujihusisha direclty na madawa tena kwa watu wanaowatuma, haileti sense kabisa, hii kitu imetungwa tu ni wazi kabisa.. hakuna proof yoyote, na since ni JF wabongo wao kazi kumeza tu kila kitu
 
Acheni kuchafuana kwa sababu za kisiasa.No data no right to mention a name.Acheni kuwachafua wengine kwa ajili ya utashi wa mtu flani.Leteni proof za kueleweka.

Hapa hatumchafui mtu, Mi nadhani kwa habari kama hizi ndio muda muafaka kwa intelijensia yetu kuzifanyia kazi habari kama hizi na kutoa majibu kwa tatizo hili. Hawa wanasema ni wafungwa kule Hong Kong waliokamatwa na madawa ya kulevya na wanatumikia vifungo vya miaka 20-35. Serikali yenye nia ya kukomesha haya inaweza kuomba kupitia ubalozi kufanya mahojiano nao na kupata ukweli zaidi.

Ni kwa kufanya hayo hapo Juu pekee ndio tutapata ukweli na kila mtu atakuwa huru maana kweli humweka mtu huru.

Inawezekana kujikatia tamaa. Kifungo cha miaka 20-35 huku wengi wakiandika wana umri wa miaka 30-40 maana yake nini kama sio ndo FOR LIFE? Dreson4
 
Last edited by a moderator:
Hayo majina ya yanayotisha yako wapi hizi ni swaga tu,mimi nasubiri ya mwakyembe.
 
Na huu sasa ndiyo ukweli wenye mengine ya 250 ilukuwa wabebaji .Hapa ndipo sasa penyewe .wacha tusikie sasa kauli za wenye Nchi .
 
Mwandiko huu unanitia wasiwasi na naomba wachangiaji wanaojua kusoma miandiko watueleze kwani inaelekea mwandishi amejitambulisha kama Mohamed lkn mwandiko ni wa kike

Nani amekwambia huu mwandiko ni wa kike? Acha hizo Bwana!!!!!

Tiba
 
Ni habari zinazosumbua sana akili na mustakabali wa taifa,ila sasa tutawatia vip hao wahusika hatiani bila ushahid??

Na hawa wenye mamlaka hawaoni kuna haja ya kwenda kufatilia hizo agencies zilizotajwa za hongkong na china ili kujitosheleza na kufanya maamuz kwa manufaa ya taifa??

Au lisemwalo lipo hili,basi taifa linaangamia moja kwa moja,

Wacha tuendelee kulalamika nyuma ya keyboard zetu....
 
atafutwe alitoa kalamu iliyotumika kuandika hii barua alinunua karatasi na alieenda kluituma posta haraka sana
 
jamaa amepata taabu kweli ya kuchonga mwandiko ili asijulikane, hii vita ni kubwa tuwe waangalifu sana, watu wasipokuona lakini Mungu anakuona. "TUMCHE MUNGU KWA DHATI YA MKUMCHA"

Hisia zangu ni kwamba huyu mtu kaandikiwa na mfungwa mwenzie au msaidizi wa magereza aliyepata kujifunza kuandika Kichina kama lugha ya kwanza kimuandiko. Yawezekana baadaye huyo mtu alikuja kujifunza roman scripts ndo maana mwandiko wake umeathirika na scripts alizojifunza awali.

La muhimu kwama tungekuwa na dola iliyo serious kupambana na hii vita ingeenda Ubalozini (HK, Macau, China) na kuitisha file la wafungwa wa Kitanzania wa madawa ya kulevya na kujiridhisha kama kati yao yupo aitwaye Othman. Mengine yote yangetiririka kuanzia hapo kujua uongo na ukweli.

Kwa bahati mbaya tunayo dola inayolinda maslahi ya waharifu kwa hiyo haiwezi kujichunguza wala kushughulikia suala hili kwa maslahi ya Taifa
 
Back
Top Bottom