Biashara ya Madawa ya Kulevya: Wafungwa wa Kitanzania Hong Kong waendelea kufunguka

Biashara ya Madawa ya Kulevya: Wafungwa wa Kitanzania Hong Kong waendelea kufunguka

Mungu anasikia maombi ya WATANZANIA.....naona nuru mpya ndani ya TZ
 
Ndiyo maana Othmani kadai kama wako serious wawasiliane na vyombo husika huko Hong Kong. Actually, kama serikali iko serious ingeshaunda timu na kufanya uchunguzi kuanzi kwa hao waliopo gerezani huku wakishirikiana na serikali ya Hong Kong. Ni aibu kuwa na wafungwa zaidi ya 200 HK halafu serikali iko kimya kama vile hakuna kinachoendelea. So far nimeona usanii tu unaendelea hapa eti Mwakyembe anaamkia Airport sasa10 alifajiri. Huyu ni usanii wa hili ya juu. Bora angeuchuna tu kama wenzake.
 
Hayo maandishi sio ya Mtanzania huyo ni Mchina aliyeandika hayo sisi watanzania hatuna hiyo miandiko na hizo herufi A za kwenye magazeti
 
Hao Watz Waliokamatwa Mbona Hawawataji Hao Mapapa Waliowatuma?

This is Bull shit.......................Wawataje hao Mabosi wao waliowatuma

La sivyo waendeleee kutumikia Vifungo
 
Je Dr. Mwakyembe ataweza kumtaja "dogo" hadharani??ngoja tuone.
Kama yumo atatajwa tu,pia ni muda muafaka kwake kutathimini kazi zake kama zinauhalali pasipo na shaka!
Kutuhumiwa ni nusu ya ukweli hadi mahakama ikusafishe kuwa huna hatia,namshauri ajitathimini na achukue hatue haraka sana.
 
Nani muuza sembe?? Serikali haijui, JK ana majina lkn hayatoi, sijasikia kiongozi hata mmoja zaidi ya Mwakyembe akiongolea suala hili kwa undani.

Hivi aliyetakiwa ashughulike haswa na hili suala ni Mwakyembe au Nchimbi??

Hebu nifahamisheni hapa kidogo.
 
Nyumba ambayo inasemekana imeingia nyoka, utaona wakazi wake wakihaha kwa bidii zote kumtafuta huyo nyoka ili wamuue, hata kama si wote waliomuona. Je, hapa kwetu tunaona bidii hizo na bidii za kumtafuta huyo nyoka?
 
ngumu kumeza barua zime andikwa kwa ustadi kma zile za mabingwa wa kuandika essay
kuna mtu tena makini na msomi yuko behind hizi wala sio wabeba sembe
 
Kama Ridhiwan anafanya hii biashara na baba yake kama anajua halafu hamwambia chochote kuhusu hiyo biashara basi itakuwa hata Kikwete nae ni Drug dealer na Ikulu yetu imefanywa kuwa pango la kuuzuia madawa.
 
Ukisoma kwa makini utaona kuwa alieandika barua hizi ni mtu makini sana na mwenye utaalamu mzuri wa kuandika habari na wala si punde kama watu wanavyofikiria. Kama ni punda basi atakuwa ameandikiwa.
 
ngumu kumeza barua zime andikwa kwa ustadi kma zile za mabingwa wa kuandika essay
kuna mtu tena makini na msomi yuko behind hizi wala sio wabeba sembe

Kwa taarifa yako wapo mapunda wana degree,unadhani hii biashara ni ya darasa la saba na form four leavers tu?
 
Ili kukomesha biashara ya madawa ya kulevya watanzania tunatakiwa kufanya yafuatayo:
1. Kufanyike kura ya maoni kwa wananchi wote na wafungwa kuwataja wanaouza na kusafirisha madawa haya kura hiyo iratibiwe na taasisi inayoaminika Duniani kama ile iliyoshughulikia kesi ya change ya rada.
2. Bunge liunde tume itakayokwenda kuonana na wafungwa wanaotumikia vifungo kutokana na kesi za madawa ya kulevya katika magereza ya huko nje na taarifa yake kujadiliwa Bungeni.
3.Watakaobainika kujihusisha na biashara hiyo wafirisiwe na pia adhabu wanayostahili ni kifo. tena wapigwe risasi hadharani.
4. katiba mpya iweke pingamizi kwa wenye kutajwa na kushinda kura ya utambuzi wa kuhusika na biashara ya madawa kulevya kutopata uongozi katika jamii na katika utumishi wa umma.
MWENYEZIMUNGU IBARIKI TANZANIA
 
inakera sana watu wanavyobeza hizi barua

tanzania hatutafikia level ya maendeleo inayostahili mpaka wananchi watakapoamka na kuhoji utendaji wa serikali na bunge

swali kwenye hizi barua;

1. it is a fact kuna watanzania wamefungwa nje ya nchi kutokana na madawa ya kulevya, je jeshi letu makini la polisi limeomba ushirikiano wa uchunguzi ikiwezekana kwenda kuwahoji hawa wafungwa na kujua wamefikaje kwenye hayo matatizo?

2. kuna drugs lords wametajwa kwenye hizi barua, je jeshi la polisi limefanya uchunguzi wa awali kujua vipato vyao ni halali au hapana kwa kuanzia tu?

kuna mambo mengi ya kiuchunguzi jeshi la polisi makini linaweza faidika na hizi barua si kuzibeza tu
mambo hayo unayoyasema ufanyika kwenye nchi ya haki na sheria ya kweli sio ya mdomoni
 
Hao wafungwa mbona hawataji majina?! Wanaogopa nini wakati wako kifungoni na hakuan kuhatarisha maisha? Hizi barua siziamini....
 
Tunasubiri ngonjera ya JK mwisho wa mwezi! Hawezi kutaja majina aliyonayo kwa sababu anaogopa akimwaga ugali wengine watamwaga mboga, Tutaingia kwenye Uchaguzi na CCM itapigwa chini!!
 
Hao wafungwa mbona hawataji majina?! Wanaogopa nini wakati wako kifungoni na hakuan kuhatarisha maisha? Hizi barua siziamini....

Hawataji majina kwa kuogopa kuhatarisha maisha ya familia zao,wewe vip?
 
I see nchi imefika pabaya sana biashara haramu zimehalalishwa na wafanya maamuzi ndio wapiga dili sasa inatosha.

Tanzania kwa sasa imekuwa kama Somalia, hakuna serikali kila mtu anafanya anachojijisikia hakuna regulator..wala mamlaka yoyoyte..zote zimekufa
 
Ngoja nitulie. Barua ya pili inastahili kutafsiriwa. Sasa Ridhiwani katajwa wazi wazi!
 
Back
Top Bottom