Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Kuna sera/sheria imeanzishwa hivi karibuni kutaka wenye mashamba ya miti wawe wanaomba vibali kabla ya kuvuna miti yao. Jaribu kuitafuta uisome.
***
Miti yangu mwenyewe unipangie kuvuna,kwa hasira sipandi./
Kwa binafsi sinaufahamu wa kuwa kila ninapokata natakiwa kuotesha mpya maana ndio zao langu LA Kilimo.
 
pia kuna mpango wa kimataifa unakuja. Utakuwa unalipwa hela kutokana na idadi ya miti unayotunza...

This has been started by international organisations, concerning with environment and global warming.

Nia kubwa ni Ku_promote upandaji na utunzaji wa mazingira. So ukiwa na shamba la miti, utakuwa unalipwa kila mwezi hela kadhaa.

Mradi umeanza nchi za ulaya na asia. Kwa africa bado. Sina uhakika kwa nn kwa africa, bado haujaja.
Upo hapa hapa Mafinga watu washavuta hela za carbon credit
 
Kuna upcoming tree investors meeting/training in the southerh highland regions of Tanzania (Iringa). You will be exposed to a lit of things guys
 
pia kuna mpango wa kimataifa unakuja. Utakuwa unalipwa hela kutokana na idadi ya miti unayotunza...

This has been started by international organisations, concerning with environment and global warming.

Nia kubwa ni Ku_promote upandaji na utunzaji wa mazingira. So ukiwa na shamba la miti, utakuwa unalipwa kila mwezi hela kadhaa.

Mradi umeanza nchi za ulaya na asia. Kwa africa bado. Sina uhakika kwa nn kwa africa, bado haujaja.
Niliisikia kutoka kwa jamaa mmoja ila baadaye nikagundua ni tapeli. Kama ni kweli tujuze zaidi.
 
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.

Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.

Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.

Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
Wazo zuri. Nilipita maeneo ya Sumbawanga hasa Wilaya ya Kalambo,nako kuna mashamba haya japo kwa uchache! Issue kubwa hapa uwe na eneo. Huwezi kukodi kwa vile ni zao la kudumu na la muda mrefu.
 
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.

Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.

Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.

Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
Nilijaribu zoezi hili nimeishia kupanda hekari 18 tu za pines. Lakin natarajia kupanda zaid nikipata maeneo zaidi maana hilo ndilo tatizo kubwa zaidi.
 
Sijasikia mtu anayepanda mitiki hasa hasa maeneo ya morogoro. Au hamjasikia fursa upande huu?
 
Nimeshakupa mwaliko kupitia mail yako pamoja na wengine walioko kwenye ukurasa huu. Karibuni tufanye mambo.
Mkuu nebu basi tuwekee hapa ukokotozi wa heka 10 kwa mfano, ukianzia na
-Gharama za kununua shamba,
-Gharama za serikali ya kijiji,
-Gharama za miche
-Gharama za kupanda
-Gharama za kuweka mipaka/ikuza/kinga moto
-Gharama zingine

Msaada basi tujazie hapo utusaidie tujipime kaka
 
Mkuu nebu basi tuwekee hapa ukokotozi wa heka 10 kwa mfano, ukianzia na
-Gharama za kununua shamba,
-Gharama za serikali ya kijiji,
-Gharama za miche
-Gharama za kupanda
-Gharama za kuweka mipaka/ikuza/kinga moto
-Gharama zingine

Msaada basi tujazie hapo utusaidie tujipime kaka
Kwa kule niliko mimi ni kama ifauatavyo.

A) shamba bei ni, 80k, 90k na 100k, kwa hiyo hapa uchague wewe bei unayo mudu, mfano tuchukue 90k kwa eka.
90k x 10 sawa na 0.9M
B) Gharama za kijiji zitakuwa 9000/ x 10 sawa na 90k
C) 10 x 600 x 100/ sawa na 0.6M
D) Upandaji ni 50k x 10 sawa na 0.5M
E) Usafirishaji wa miche 0.15M
F) Chakula 0.1M
G) kuweka fire break kila mwaka 0.2M
I) Vifaa vya kazi 0.15M

Hata kama gharama zitapishana kidogo na maeneo mengine, lakini ziko katika range hizo.
 
Back
Top Bottom