Biashara ya Michezo ya Video (Video Games): Jifunze Uendeshaji, Changamoto na Faida Zake

Mbona unasema mtaji ulirudi baada ya 13 mnths maana 15k x26 x13 =5,070,000
 
Shukran kwa mchanganuo ..vp ps3 na ps4 mpya bei gani ?
Ps3 mpya bei 400k ( ukiuziwa zaidi ya hapo umepigwa budda DAI VICHELE VYAKO AKURUDISHIE) na sidhani kama mpya kwenye box lake ziko maana ni za muda sana

Ps4 inategemea ni fat au slim ila bei ni 750k mpaka 1m (hawana huruma)

ILA KAMA UNAANZA HII BIASHARA TAFUTA VITU USED UTAJIFUNZA MENGI NA CHANGAMOTO UTATATUA BILA PRESSURE..
 
Ushauri umepokelewa
 
Kuna utofaut gani kati ya PS3 na PS4 ..?
 
Nina mpango wa kuweka huu mradi.
Ila nataka kuanza na pes3.
Kwa pes3 inatakiwa uchezeshe bei gani kwa muda upi?
TV inch ngapi inapendeza?
Na mzunguko wake kwa siku ni shingapi(mapato)?

Legends kwenye hii biashara tupeni madini
 
[emoji122][emoji122][emoji122], watu wanashindwa kuelewa hicho kitu

Sent from my TECNO CD6j using JamiiForums mobile app
 
Mkuu unamaana kwamba ipo kinadharia zaidi, lakini kivitendo haitekelezeki kama ilivyokusudiwa?
Nina Ps2 mbili tu huku kijijini nafungua goli saa 2 asubuhi hadi mida ya jioni nikiona nimeipata 15K namuacha dogo hadi saa 4 usiku ananilete 5k had 7k.

Siku za weekend siganduki hadi saa 6 usiku, kwa siku hizo mbili nakuwa na uhakika wa 65K hadi 80K madogo wanagombaniana Pads[emoji23]
 
Nashukuru kwa majibu,
Mkuu kwa kijijini wanalipa Tshs ngapi kucheza games?

Unachezesha games aina ngapi mfano zile za mission kama GTa unacharge vipi??

Ps2 na TV unatumia za ukubwa gani?
 
Bosi halafu nasikia sikia mashine zilochipiwa ndiyo nzuri, inakuaje hii kama unajua kuchipiwa ndio nini, na inafaida zipi
Mkuu ngoja nimsaidie jamaa kwa ninavyoelewa, kuchip ps3 ni kama kuflash simu na kuipa uwezo PS3 kuweza kuwa na magame ndani kwenye HDD yake....hivyo unakuwa hautumii CD tena ila unaingiza magame kwa kutumia HDD iliyopo ndani ya PS3......

Faida za kuchip PS 3 au 4 ni inafanya usiingie gharama za kununua CD na kufix mambo ya lens....pia hata ubadilishaji wa game 1 kwemda nyingine ni rahisi sana...CD zinachoka na lens inachoka haswa vumbivumbi zikiingia kwenye PS3 yako.
 
Ps2 ikiwa complete ni 150k tu yaani pads 2 memorycard na flash yenye game zaidi 5+ waya wa power

Ps3 ikiwa complete ni 300k pads zake 2 waya wa power na game 5+ zenyewe zinakaa ndani kwa ndani haitaji memory card wala flash


Ps4 ikiwa complete ni 650k pads 2 waya wa power na game 5+ zenyewe zinakaa ndani kwa ndani haitaji memory card wala flash =ukiwa na accounts utaweka GAMES ndani kwa ndani ukiwa hauna utatumia CD kila mchezo yaani CD ya game ina bei yake kulingana na ukubwa na ubora mda wake au kupendwa na watu kama fifa21 zinafika mpaka 120k CD tu.ila kuna game mpaka za 15k 30k 50k 60k

HII NI MTUMBA TU

BEI ZA DUKANI YAANI MPYA
PS2 =250K-280K
PS3=350K-380K
PS4=750K-900K
HIZI MPYA KWENYE BOKSI

0783231177
 
Hujaongelea meza, viti, makochi, fan, kodi ya pango, ulinzi, umeme na mshahara wa msimamizi. Bila kusahau bei ya kila game la playstation ambapo unatakiwa uwe na ma game kama mawili au matatu tofauti kwa kila tv.
Ingekua ni kuweka tv na ps tuu ata mm nngekua nayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…