Biashara ya samaki

Dah hiyo uko poa sana mkuu
Swali la kizushi:umemaliza ile ban mkuu?
 

Mkuu hivi kwa bei hiyo ya samaki mmoja mwenye uzito wa nusu kilo sh 3,750/= inaweza kuleta faida kweli?Maana huku Dar nusu kilo ya samaki aina ya sato kwenye bucha nyingi ni sh 4,000/=
Je,kwa bei hiyo ya 3,750+usafiri unaweza kutoka?Naomba ufafanuzi maana hapa tupo darasani.
 
Zanzibar Spices kwa sasa sato bei gani kwa kg?kwa Zanzibar

Mkuu huku mie hata sijui wanapouzwa aisee.
Maana hakuna sehem wanapouza,ila kuna mama mmoja miaka ya nyuma alijaribu,sasa sijui kama bado anaendelea.
Kwa ufupi hakuna sehem ya wanapouzwa Sato penye kufahamika kwa huku.Ila kama mtu mjanja anaweza kupiga hela ila inabidi akomae sana hadi watu wajue
 
amu huyu Zanzibar Spices anafanya biashara ya bodaboda, biashara ya kirikou, biashara ya kuuza mashuka ya kigoma, biashara ya.... biashara ya.... sema ninachompendea huwa sio mchoyo wa maarifa.

Mi ni msemaji wake kwa siku ya leo tu. ha ha ha

Hahaha,Mkuu njaaa mbaya,ndio nahangaika aisee.
Nikweli Bodaboda nafanya,na Carry nafanya,ila mashuka niliacha muda mrefu,maana soko kwa Zanzibar lilikufa.Kuna mashuka yanatoka UK yanauzwa matatu kwa pamoja bei rahisi,na watu kujua ubora wa mashuka ya Kigoma ilikuwa mbinde sana.Na Mitumba grande ya mwanzo huku Zanzibar telee,so ni sheeda sana.

Nimeamua kuingia kwenye usafiri maana sijaona changamoto ya kunishinda kwa muda wote wa biashara zangu.Nipo Zanzibar ila mfumo wa biashara ya usafiri unanipa nafasi ya kufanya yangu bila usimamizi mkubwa zaidi ya ndugu yangu mmoja tu ndio namlipa mshahara kwa mwezi ili awe msimamizi na nilimpeleka Gerage Pale Magomeni then nikampandisha VETA,basi kesi za Gari zangu hizo mbili tatu,sina kabisaa na Drivers wangu wote watu wazuri saaana,maana nawafanya kama familiy members.

Na pia ununuzi wa Vigari hivi kwa Zanzibar kwa sie Wajanja mpaka 4m naitoa yard,maana huku Zanzibar ukitaka gari we chukua pesa weka ndani wala usiwe na haraka kabisaa,kuna siku utanunua gari ubweteee,maana kuna watu wanaleta gari ili kuziba gepu la pesa kidogo ya kutolea mizigo au gari nyingine bandarini,sasa hawa Magari kwao sio biashara.Na wapo ambao wao ni biashara na ndio ghali kiasi.Maaana Mwezi uliopita kabla sijasafiri kuna jamaa alikuwa na Noah kamnunulia mama yake anauza kwa 7m tu liteace mbichii,maana mama yake aliletewa gari nyingine na Kaka yake.
Mjini kaka ni kutuliza akili tu ndugu yangu,maana maisha haya ya wendawazim na wewe ukijifanya mstaarabu hamuendi,maisha yakiwa kichaa basi wewe kuwa kichaa zaidi,yakiwa yametulia na wewe tulia.Ila ukienda tofauti tu basi umepotea na ukipanic basi safari ya Dodoma hiyooo.

October mwishoni nataka kuingia kwenye NOAH,maana naanza na moja nikikolea naongeza.

Mkuu maisha safari ndefu kaka,niliuza Nyumba mie kwa ajili ya Biashara,nikatengwa na Brothers wa upande wa Baba na nilipata Support kubwa sana kwa Only Sister ambae tumezaliwa Mama mmoja kwa kunipa moyo sana katika mapito ya maisha baada ya kuachishwa Kazi kwa mambo ya Siasa.

Mafanikio ya Maisha kwa Vijana yapo kwenye Nyayo za Marafiki bora tu.Muhim ni kujitambua kwamba maisha yako ni wewe na sio mwingine.Na ukikosea wa kujilaumu ni wewe na sio Mzazi wako au mwenzio.Na waliofanikiwa weengi duniani ni wale waliokosea sana kwenye maisha ya kutafuta.Ukikosea na kujitambua kwamba umekosea basi jua Mungu anakupa njia ya kwamba ukipata ujue ulipotoka na ujue kwamba Maisha sio ya kuchezea.
Wapo waliopata mamilioni ya pesa na tunawajua mitaani kwetu au makazini kwetu ila leo wapo taabani sana.Wapo watakaoibuka tena upya na wapo wataopotea kabisa kama watamuweka mungu Mbali na kukubali makosa yao.

Hakuna kitu kinachotuangamiza vijana na kumkera Mungu saana pale anapotupa rizki na kuitumia kumuasi yeye mwenyewe alietupa tena mbaya zaidi kwa kile kipato cha mwanzo cha ufungua wa maisha ndio kinatumiwa vibaya,na ndio maana kwenye makanisa na miskiti kwa sasa weeengi sana ni Vijana.
Na kila mmoja kwenye maombi anaomba maisha mazuri,ila mungu anachelewa baadhi yetu kutupa kwakuwa anajua nafsi ya kila mmoja wetu,na wapo ambao wanaomba mungu huwezi amini haipiti mwezi wanafanikiwa,ila subiri muda mfupi tu,wanasahau kila kitu na kuona kwamba wao ndio wajanja na akili zao ndio zimefanya wafanikiwe,jeuri telee,dharau teleeee.Na kuona wanaoenda kwenye Nyumba za Ibada woote ni wenye Shida ya Utajiri wa Dunia kama yeye,na kuona kwamba wao hawawezi kufanikiwa kama yeye.Kumbe hajui kwamba Kule watu wanafuta Baraza za mungu tu,Unaweza kuwa Milionea na huna baraza za mungu ni sawa na Bure,na kuna mtu analalia ugali maharage akawa juu sana kwenye daraja la mungu kuliko wewe.Na akawa na amani na furaha na maisha na familia yake kuliko wewe mwenye kujiona Unakipato.

Na ndio maana pia unakuta kuna vijana mara miezi hii wapo nyumba za Ibada kama kawaida,mara baadhi ya miezi wakifanikia haoooo,wanasepa.

Mungu atubariki sote na atupe wepesi kwenye maisha yetu na atufungulie pale tumepokwama,na atupe maamuzi sahihi kwenye maisha kwa faidi ya vizazi vyetu na Imani zetu,na pia atuongoze pale anapotupa kipato ili tusiweze kukitumia kumuasi yeye mwenyewe "AMEEN"
 
Wadau nauliza upatiknaji wa soko la samaki waliokaangwa, kuokwa, kubanikwa na wabichi kutoka Mwanza kama sato, sangara, kamongo n.k namna ya kupata wateja na maeneo ya kuuzia pamoja na hatua za kufungua pamoja na uendeshaj wake (risks and benefits) wa biashara hii. Naomba msaada kwa 0764639286.
 
UNAO HAO SAMAKI??
 
Habarini wadau,

Nafikiri kila mtu anajua changamoto iliyopo katika kuchagua biashara ya kufanya kwa watu wenye mitaji midogo. Mara nyingi changamoto hizi huambatana na kuingiza pesa kwenye biashara ambazo zinapelekea kumaliza mtaji wote pasipo kukusudia. Kuna mawazo mengi ya kibiashara ambayo ni mazuri kama kilimo na utoaji huduma lakini kwa mtu mwenye mtaji mdogo huishia kupata hasara kama hamna usimamizi mzuri. Usimamizi huu ni pamoja na mfanyabiashara kujihusisha na shughuli za kila siku za biashara hio na sio ile ya kutoa tu maelekezo wakati upo mjini.

Baada ya kutoa utangulizi huo mfupi, nimepata wazo na biashara ya kuvua samaki (sio kufuga samaki). Ningependa;

1. Mawazo kama kuna mtu yeyote kashawahi kufanya biashara hii ili anijuze changamoto zipi kubwa zinazoambatana na biashara hii. Naongelea kumiliki Boti ndogo za uvuvi na kuwakabidhi wavuvi wakuletee hesabu kama unaponunua taxi na kumpa dereva alete hesabu.

2. Mchanganuo wa hesabu ukoje?? Yani kuanzia mapato yakoje, gharama zikoje, kodi za serikali na upatikanaji wa pesa una muingiliano ya hali ya hewa au msimu.

3. Gharama ya kutengeneza boti hizi ikoje? Maana najua kununua kwa mtu Boti unaweza pigwa bei kubwa sana.

Nitashukuru sana wadau mkinipa michango yenu na pia mchukue hii kama fursa ya kuangalia hii sekta maana sasa hivi samaki kutoka uchina na nchi zingine zinaletwa sana kwahio kwa hali ya kawaida hii inamaanisha soko letu bado halina mzigo wa kutosha kwa walaji.

Asante
 
mkuu nina wazo kama hilo natnimeshawishika kutokana na mafanikio waliyoyapta ndugu zang
 
Duh, nafikiri hakuwa na nia mbaya kusema ni'pm
Huyo Jamaa huenda yeye ndiye Tapeli humu au alishatapeliwa Sana na sasa utakuja kutapeliwa mpaka Mke Wako coz Unajifanya unajua kumbe Zuzu Tu .
Asha ngedele lengo halikua baya kukwambia npm anyway it's over.
 
tafuta eneo tengeneza bwawa la samaki watafute wataalam kwa maelezo zaidi tilapia wanafugika ukiwaweka 500 au 1000 miezi nane ni hela..hii ni rahisi unapata kitoweo na kipato na mtaji sio mkubwa wa kujenga na chakula kwa kipindi hicho..
 
tafuta eneo tengeneza bwawa la samaki watafute wataalam kwa maelezo zaidi tilapia wanafugika ukiwaweka 500 au 1000 miezi nane ni hela..hii ni rahisi unapata kitoweo na kipato na mtaji sio mkubwa wa kujenga na chakula kwa kipindi hicho..
Nafuga samaki mwenyewe ila sio raic kihivyo kma unavyosema wewe.
 
Nafuga samaki mwenyewe ila sio raic kihivyo kma unavyosema wewe.
mimi nimefuga samaki nikiwa mbeya ni rahisi kuriko iyo ya mashine kununua sijui ukodishe na dogo yupo dar anafuga vizur tuu nimehamia Ar pia ntafuga..
 
mimi nimefuga samaki nikiwa mbeya ni rahisi kuriko iyo ya mashine kununua sijui ukodishe na dogo yupo dar anafuga vizur tuu nimehamia Ar pia ntafuga..
Ngoja nikupe mchanganuo kidogo.

Samaki 1000 sato wanahitaji bwawa la atlst 200m2 ambalo uchimbaji ni kama 300000tsh Vifaranga vya sato 1000 ni 300,000tsh. Sato miezi minane kwenye earthen pond ukijitahidi sana ni 500g ambaye atakuwa amekula mara 3 ya body weight yake. Na pellet feed ya sato ni 3000 kwa kilo. Sato mmoja kufikisha 500g atakuwa kala chakula cha 4500. Wote 1000 watakuwa wamekula 4,500,000. Mwanza sato wa 500g bei yake haizidi 5000. Sasa sijui uko wewe ulipo. So kama ni sato 1000 utapata 5,000,000 sanasana. Ukitoa 5,100,000. Unapata hasara ya laki 1. Kumbuka apo sijaweka operation costs kama za ulinzi, management, usafiri, and pond Care.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…