Biashara ya samaki

Biashara ya samaki

Bei ya sangara na sato inatofautiana. Sato siku zote iko juu. Kwenye kipindi cha mvua samaki wanapatikana wengi na kwa Bei nafuu. Kipindi hiki samaki sangara kilo kwa jumla ni 4500. Wakati sato anaenda mpaka 5500.

Samaki wanapimwa kwa kilo. Unaweza kununua moja kwa moja kutoka kwa wenye mitumbwi yao au kutoka kwa walanguzi ambao wao huzinunua kwa wingi na kuzihifadhi Kwenye mafriza baada ya kuwatoa mautumbo na mabondo.

Hawa walanguzi ndiyo wenye Bei niliyokupa hapo juu. (Ukumbuke Bei hubadilika ) walanguzi hawahawa ukitaka samaki wanakufungia vizuri na kuwapakiza Kwenye mafuso. Fuso zote zinapakulia pale urafiki freti. Ila unalipia usafiri mwenyewe.

Kuhusu kibali mlanguzi huwa anakibali na mwenye fuso anakibali cha usafirishaji. Na ushuru utalipwa na mlanguzi. (Ukitaka namba ya mlanguzi utaniambia).

Bei ya kuuza huku samaki mbichi kilo ni kuanzia elf 8-10.
Of course ukitaka kuwa na frem lazima uwe na leseni nenda halmashauri na tra lazima ikuhusu.
Ukitaka nafuu sambazia mzigo ukiwa home kwako.
Mkuu nipm namba yako tuongee
 
Nina bwawa la samaki 5000-5500 waliokomaa aina ya trapia/ngege/sato, samaki hawa wana uzito kati ya kilo 1.2 hadi kilo 5, naombeni mniunge na masoko niweze ziuza, niingize mpya. Bwawa lipo Kigoma mjini.

Asanteni sana
Vifaranga vinapatikanaje na kwa bei gani?
 
Kisha niajiri mtu wa kukaanga na kuuza nitakuepo na mimi eneo la biashara mda wa jioni sababu mchana nitakua na vipindi.
Natafuta mtu wa kuniuzia samaki wabichi hapa mwanza kutoka huko ziwani kwa bei ya jumla au wajuvi nielekezeni soko zuri.
Naanza na mtaji wa 55k. mchanganuo ni kama hivi;

Mafuta lita tatu 10000/=,
Karai 5000/=,
Vitu vingine 10000/=,
Samaki wa kuanzia 30000/=

Location ni barabarani mtaa uliochangamka kiasi chake.
 
Soma hiooooooo
image_854d1476-4335-4bb7-9959-03a6f03bd35c20191208_181516.jpeg
 
Habar wakuu!
Mwenye kujua taratibu za kupata vibali vya kufungua butcher la samaki na nyama. Naomba msaada, hasahasa kuhusu TFDA na TRA.
 
Mkuu umefikia wap, nataka kuanzisha huu mradi dodoma nipe changamoto zake
Nilikuwa na mawazo sawa na wewe, kwa sasa nipo Dodoma ila nyumbani ni Mwanza, nimefanya uchunguzi binafsi kwa mda niliokaa hapa Dodoma nimegundua kuna uhitaji mkubwa wa samaki, nimejipanga kurudi nyumbani nikachangamkie hii fursa. Kama uko tayari tunaweza kupanga namna ya kufanya hii biashara!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nataka kuanzisha biashara ya samaki kwa kuchukua mzigo kutoka mwanza nakusambaza mikoani ila naitaji kujua ziadi kuhusi vibari na ushuru pia na nimikoa gani ina uhitaji sana wa samaki. Pia samaki nitakao kuwa nasambaza ni SATO na SANGARA
images%20(9).jpeg
images%20(10).jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nataka kuanzisha biashara ya samaki kwa kuchukua mzigo kutoka mwanza nakusambaza mikoani ila naitaji kujua ziadi kuhusi vibari na ushuru pia na nimikoa gani ina uhitaji sana wa samaki. Pia samaki nitakao kuwa nasambaza ni SATO na SANGARA
images%20(9).jpeg
images%20(10).jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom