Biashara ya Uchawi Tanzania

Biashara ya Uchawi Tanzania

Mkuu, Soft copy zake ninazo za kumwaga. Lakini zinaitwa Dangerous Prayers (zingatia hapo Red hapo)
kuna kosa tumeshafanyamahali fulani, tukawagaia watu Pamphlet Page mbili-mbili tu. wakazisimamia usiku wa manane kwa muda wa siku Nane. kweli waliwaburuza wale vigagula hadi vingine vikafa kabisa!
Sasa. illtakiwa ndio iwe maisha yao ya kila siku (Life styles) maisha ya maombi, ukijisahau tu ndugu; umemchokoza Joka shimoni mwake, na wewe una kiwembe tu mkononi! unategemea nini baba? ibilisi (wachawi) ana hasira kushinda unavyofikiria.
Lakini kama uko fiti wewe mwenyewe, ntakutumia volume 1 kwanza. ujipime ubavu

Please send me too these soft copies
 
Mbona unanitisha mkuu? mi si nafikiri ni vitabu vya usoma tu na kuongeza uelewa? Kwani kuna vitabu wachawi hawataki watu wasome? Mi sitaki ugomvi na mtu bwana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

du!Umechuja Mkuu!
 
By critical thinks i believe that:uchaw na mchaw ni fan ya kitu au ya mtu.dont matter kuwa mtakatifu au mwovu.ila IMANI ndiyo msing wa kuufikia uzima wa milele,mbali na din ambazo twajua fika zimeanzishwa na binadamu wa nyama na mifupa.kwa minajili hiyo bas,tujue uchaw na mchaw siyo vitu vya kutisha kwa mwenye iman.AMEN
 
Ukiona unga na mikaa imewekwa juu yake mitaani kwako, jua kuwa eneo hilo ni maskani ya wachawi wa nchi, na kama unaishi maisha ya hovyo hovyo, hakika wewe ni msukule mtarajiwa.[/QUOTE]
hii ni kali... vp na vpande vya mifupa ya nguruwe??
 
Maji moto njoo utupe njia ya kuondokana na hila zote za wakuu wa giza pamoja na wasaidizi wake. Kwa maana wengine tunapofanya maombi hatujui tuombe nini!
 
wapenda kwenda kwa waganga.......
1. high governmental officials, a)mawaziri b)wabunge c) mdiwani nk
2. viongozi wa dini (zote)
3. wfanya biashara ziwe kubwa au ndogo
4. wanawake kwa love affairs issues
5.wanafunzi mashuleni
 
LANGO LA KUZIMU LA TABORA

Mji wa Tabora ni moja ya miji ya zamani sana, mji huu ulianzishwa na wafanya biashara wa Kiarabu, na ulikuwa ni kiungo muhimu cha biashara ya watumwa, waliokuwa wanakamatwa kutoka mikoa ya ziwa, Kongo, Burundi na Rwanda, kabila ya kusafirishwa hadi Bagamoyo kisha kuingizwa kwenye majahazi na kusafirishwa hadi soko kuu la watumwa la Zanzibar.

Lango la kuzimu la Tabora liko ndani kabisa ya soko kuu, Mkuu wa lango hili anajulikana kwa jina la Swaheral, akisaidiwa na majini yafuatayo:-

1) Alibadiri ni jini katili sana, likitumwa linaua kifo cha aina yoyote lililotumwa kufanya kwa muda mfupi na kwa usahihi.

2) Anzula ni jini linalowaingia sana vijana wa kike na wa kiume, linawazuia vijana kuoa au kuolewa. Usiku wanaota wanafanya tendo la ndoa na msichana mzuri sana, na huwa wanamaliza hamu wenyewe. Raha anayopata ni zaidi ya anayopata akifanya mapenzi na msichana/mvulana.

3) Maimuna ni jini ambalo huwakamata kina baba wenye ndoa zao, usiku anaota anafanya mapenzi na msichana mzuri sana, kumbe anafanya tendo la ndoa na hili jini, baba anakuwa hana hamu kabisa na mke wake wa ndoa, hali inayosababisha ndoa kuvunjika na kuachana.

4) Makata (Simba au leo) hili jini linawaingia sana wanawake, usiku anaota ndoto anafanya mapenzi na huwa anapata raha kuliko anayoipata akifanya mapenzi na mume wake.

5) Kafurani ni jini linalofanya watu wawe bubu, utakuta mtu alizaliwa mzima kabisa lakini kwenye ujana wake anaanza kupoteza uwezo wa kuongea.

Jini hili pia ndilo linalosababisha watu kupooza, pia linasababisha au linaharibu kabisa nguvu za kiume za akina baba, na kuondoa uwezo wao wa kufanya tendo la ndoa.

6) Kabru jini hili likiingia kwenye ukoo wenu, linaua watu wasiopungua wawili kila mwaka, na vifo vinatokea miezi inayofanana kila mwaka. Kama limeanza kuuwa mwezi wa April basi kila mwaka mwezi huo ukifika ni lazima atakufa mtu.

7) Eziruni hili jini linatumwa kwa njia ya ujumbe. Linaweza kutumwa ndani ya barua na unapoifungua barua jini hili hukuingia na kukumaliza, au hujilaza barabarani eneo unalopita, ukilikanyanga, matatizo yanaanza kwenye mguu na kuenea mwili mzima.

8) Subha hili ni jini la kujiinua na kujiona sana, kuwa hakuna mwingine zaidi yako, pia linafanya mtu anakuwa kichaa au linamfanya mtu ananuka sana, kiasi kuwa unatumia kila aina marashi lakini hayasaidii.

9) Al-Maul hili jini linamfanya mtu anakuwa omba omba sana, kila siku yeye kazi hafanyi ni kuzunguka zunguka kila sehemu akiomba, na kila siku anakuwa ni mtu mwenye matatizo yasiyoisha.

10) Zuhura au Zohar ni jini la fujo, mtu wa namna hiyo ukimkosea yeye anachojua ni kupigana tu kitu kinachoitwa samahani kwake ni mwiko.

11) Araba jini hili linapenda sana harufu ya udi (ubani), unapochomwa ni lazima jini hili lifike eneo la tukio, na linapenda sana kutafuna tafuna vitu, hivyo hutafuna kitu chochote kitakachokuwa nyumbani kwako.

Mkuu hebu ongelea na visoke kidogo.
 
Yeyote yule anayetaka kufahamu uchawi na aina za wachawi atafute kitabu kinachoitwa "Mkuu wa wachawi sasa ampokea Yesu." Ukiachilia mbali kwamba alimpokea Yesu, kitabu hiki kimechambua habari zote muhimu za kichawi. Mwandishi Iyke Uzorma ni msomi PHD alikuwa na cheo cha juu mno katika uchawi na ametaja hata wachawi tishia Afrika (Yumo m-tz, aisee!). Ni kitabu kizuri sana.
 
Maji moto njoo utupe njia ya kuondokana na hila zote za wakuu wa giza pamoja na wasaidizi wake. Kwa maana wengine tunapofanya maombi hatujui tuombe nini!

Kwani iman yako haikufundishi?au huyu majimoto ndio iman yako?kazi unayo dogo
 
Huu utafiti unatakiwa uwe wazi zaidi. Inashangaza mikoa ya Kilimanjaro na Kagera kuongoza kwa kuwa wateja wa uchawi wakati huo huo ndiyo mikoa inayoongoza kwa elimu. Mtafiti anataka kuaminisha umma kuwa ukitaka kuendelea
kielimu nunua uchawi? Angetakiwa pia aonyeshe mahusiano ya uchawi na maendeleo kwa ujumla wake vinginevyo ni kupotea muda kwa kuwa hakuonyesha faida ya uchawi au hasara zake.
 
Mikoa saba nchini Tanzania ndiyo tishio kwa kuwa na nguvu kubwa za uchawi
1. Tanga ndio kinara
2. Lindi unafuatilia
3. Dar es Salaam
4. Mtwara
5. Tabora
6. Kigoma
7. Mwanza

Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Mikoa ambayo wananchi wake ndio wateja wakuu wa wachawi
1. Kilimanjaro inaongoza
2. Morogoro inafuatilia
3. Kagera

Wateja wengine wa wachawi
1. Wafanyabiashara
2. Wasanii
3. Kina mama wa nyumbani
4. Wanafunzi wa shule za sekondari hasa wa kidato cha pili.

Mkuu hizo takwimu za wateja wa uchawi umezipataje? Huo mkoa kinara naunga mkono mia mia..........wateja wazuri sana ..........cause they are very greed
 
Yeyote yule anayetaka kufahamu uchawi na aina za wachawi atafute kitabu kinachoitwa "Mkuu wa wachawi sasa ampokea Yesu." Ukiachilia mbali kwamba alimpokea Yesu, kitabu hiki kimechambua habari zote muhimu za kichawi. Mwandishi Iyke Uzorma ni msomi PHD alikuwa na cheo cha juu mno katika uchawi na ametaja hata wachawi tishia Afrika (Yumo m-tz, aisee!). Ni kitabu kizuri sana.

Kinapatikana wapi mkuu? kama unayo kopi laini itundike humu mkuu
 
Kinapatikana wapi mkuu? kama unayo kopi laini itundike humu mkuu

2.jpg


Kwenye stendi za vitabu Ubungo, Kariakoo, Mwenge n.k. Kitabu hiki kimebadili maisha yangu, huo ndio ushuhuda wangu mkuu.
 
Haujachelewa, tafuta Dangerous Prayers Books Part 1 na 2
visome usiku, utajionea mwenyewe mpendwa
 
Jamani naomba mnijuze, hivi mkoa wa mara hakuna uchawi?
Kule ni mapanga tu au vp?!
 
Hii thread nilikuwa kila siku naiona lakini sijawahi kuifungua. Leo sijui kitu gani kimenifanya nifungue, nimecheka sana kwenye hizo categories za wadau wa uchawi...
 
Back
Top Bottom