Biashara ya Uchawi Tanzania

Biashara ya Uchawi Tanzania

Nchi ya Japan ni mojawapo ya mataifa yanayoongoza duniani kwa maendeleo.

Wajapan wanazo dini kuu mbili ambazo ni Shinto na Buddha, asili ya dini ya Shinto haijulikani sana lakini imekuwepo nchini Japan kuanzia miaka 400 kabla ya Kristo. Buddha iliingia nchini Japan mwaka 538 ikitokea China, Wajapan wengi hawakuipokea hii dini hadi mwaka 587 wakati ufalme wa Mononobe uliposambaratishwa kwa kipigo, walikuwa ni wapinzani wakubwa wa dini ya Buddha, kuanzia kipindi hicho dini hiyo ilienea kwa kasi ya ajabu.

Baada ya karine mbili Mfalme Shomu's aliamuru ujenzi wa nyumba ya ibada ya Todaj-ji ijengwe kuanzia mwaka 752. Ni jengo kubwa la mbao duniani likiwa na urefu wa mita kumi na tatu, ndani yake waliweka sanamu ya shaba ya Buddha, baadaye ilibadilishwa na kuitwa The Great Sun Buddha au Dainichi Nyorai, Dainichi Nyorai wana uhusiano na Amaterasu na Shinto Sun Goddess.

Asili ya Japan ni nchi inayokumbwa na matetemeko makubwa ya ardhi ambayo yamekuwa yakisababisha maafa makubwa kwa raia wa Japan, kupitia dini zao kuu mbili Shinto na Buddha, ambazo asili yake ni kuzimu, waliazimia kuwa kila familia ya Kijapan ni lazima watoe Yen 3,000 kila mwezi kama sadaka kwa mizimu, kuwalinda na matetemeko ya ardhi yanayowakumba mara kwa mara.

Sadaka hiyo inapokusanywa hupelekwa kwenye hekalu lao la Todaj-ji, na watu wenye miili kabisa kutoka kuzimu hufika ndani ya hekalu hilo na kuchukua magunia kwa magunia yalijaa pesa za Yen, na kupeleka kuzimu. Inapotokea maafa kama haya ya jana, Mabuddha huanza ibada zao za kishetani na mizimu iliyovaa miili ya binadamu hufika na kuwaeleza ni kwa nini wameadhibiwa.

Kimsingi malalamiko ya mizimu wanapinga kuanza kuenea kwa dini nyingine zisizoamini mizimu katika taifa lao, ambao wanaona ni tishio kwa uchumi wa taifa la kuzimu kimapato, endapo Wajapan wataacha dini zao za Buddha na Shinto.
 
Sasa hivi zipo shule kabisa za kufundisha uchawi nchini Tanzania, Shule moja ipo Temeke masomo yake huchukua miaka saba hadi unahitimu.

Ukimaliza Temeke, unaweza kujiunga na elimu ya juu katika fani ya uchawi, chuo kipo Tanga hapo wanatoa digrii ya kwanza ya uchawi kwa miaka mitano.

Wanatoa pia digrii ya pili ya elimu ya ulozi ambapo utakaa darasani kwa miaka mingine mitano.

Master digrii ya ulozi, bado hapa nchini hakuna chuo, inapidi uende Mombasa nchini Kenya ndipo kilipo chuo kikuu cha elimu ya ulozi.

kaazi ipo! Muda wote huu?!

Lakini mtoa ada amejuaje hayo yote kama na yeye sio mchawi? (joke tuu)

Zindiko la taifa lililofanywa na wachawi wa mkoa wa Lindi, lilisababisha kusambaa kwa mapepo yaliyowafanya wananchi zaidi ya 75% kutokuwa na maamuzi yao wenyewe, au wawe wanaongozwa kwa remote control kutoka kuzimu, kwa maana kwamba watawala wakitaka uongozi au jambo lolote, hushuka kuzimu, na kutoa kafara ya damu, kisha hunuiza maneno ya jambo wanalotaka litendeke nchini, shetani wa kuzimu hutumia remote yake na watanzania waliopangawa na hayo mapepo uwezo wao wa maamuzi huondoka na kubaki watu wa kusema ndiyo,hata kama wanatukanwa.


Ulijuaje?

Utawala wa shetani ni wa kificho sana. Shetani hutawala dunia kwa kufuata mipaka ya nchi kama zilivyo, kama tulivyo na mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, katibu tarafa, mwenyekiti wa kijiji, shetani naye amepanga utawala wake kwa mfumo huo huo.

Anachofanya shetani ni kuhakikisha kuwa viongozi tunaowachagua au wanaopewa madaraka ya kuongoza, wizara, mikoa, wilaya, tarafa, kijiji, kaya nk. ni wale tu waliopitia kwa mawakala wake, tunaoishi nao ambao ni waganga wa kishenzi (kienyeji).

Ndiyo maana basi shetani anapofanikiwa kuwa mtawala wa ulimwengu usioonekana na ulimwengu unaoonekana, kamwe maendeleo ya eneo hilo huwa yanadumaa kabisa, kwani shughuli kubwa kabisa ya shetani ni kuharibu, kutesa na kuua.

Kuhusu maswali yako .Wateja wakuu ni watu ambao asili yao siyo wachawi, lakini wanatumia uwezo wao wa mapato kununua huduma ya uchawi.

Mikoa yenye nguvu kubwa ya uchawi, wao wanaishi kwa kutegemea uchawi kwa asilimia 100, na utakuta uchumi wa maeneo hayo upo nyuma sana, kwa mfano mkoani Tanga mchawi mwenye misukule 200 anaonekana ni mtoto katika mambo ya ulozi, biashara ya misukule ni biashara ya kawaida, bei ya msukule kwa sasa hivi ni kati ya shs. 300,000 hadi 600,000 kutegemea na umri na nguvu ya msukule, Ndiyo maana maeneo hayo utakuta siku nzima watu wamefunga misuri na kucheza bao, lakini wanaishi vizuri tu.

Mikoa yenye wachawi wengi, tuseme ni kama mila au utamaduni au wanachukulia kama ulinzi wa familia, ndiyo maana utakuta kila kaya kuna mchawi au familia nzima wanaujua uchawi. Wananchi wa maeneo haya wengi wanafanya kazi halali na zenye kuingiza kipato halali kwao na kwa taifa.


sasa wenye msukule 200 si mabilionnaire? hahahahah...bei ulijuaje?

Asili ya uchawi na majini ya nchi za Kiafrika ni kutoka Arabuni, ndiyo maana utakuta majini mengi yana majina ya Kiarabu. Miji au vijiji walivyokaa Warabu ndivyo vinaongoza kwa uchawi na havina maendeleo. Lakini utashangaa pia kuwa mtu kama Osama Bin Laden ambaye ni Mwarabu amefundishwa uchawi na Mtanzania wa Kigoma.

Tanzania tuko juu! lol ya kweli haya?
 
wos unanichekesha hapo juu

misukule 200 kumbe ndo nakuwa billionea...lol
 
wos unanichekesha hapo juu

misukule 200 kumbe ndo nakuwa billionea...lol

Misukule 200 huyo bado mchanga sana, wapo wanaomiliki zaidi ya 1,000 wanajulikana muda wote wamefunga misuri wako vibarazani, wanakula kashata na kahawa mitaani, watoto wako skuli za bei mbaya, ana nyumba nzuri, za gari ya kutembelea anazo.
 
I will preffer the tittle to be changed to UCHAWI NA MAJINI
 
Mbona matetemeko yametokea , Irani na Pakistani nchi ambazo hawaamini dini za masanamu?.
Je nchi ya Haiti nayo vipi?
 
Nchi ya Japan ni mojawapo ya mataifa yanayoongoza duniani kwa maendeleo.

Wajapan wanazo dini kuu mbili ambazo ni Shinto na Buddha, asili ya dini ya Shinto haijulikani sana lakini imekuwepo nchini Japan kuanzia miaka 400 kabla ya Kristo. Buddha iliingia nchini Japan mwaka 538 ikitokea China, Wajapan wengi hawakuipokea hii dini hadi mwaka 587 wakati ufalme wa Mononobe uliposambaratishwa kwa kipigo, walikuwa ni wapinzani wakubwa wa dini ya Buddha, kuanzia kipindi hicho dini hiyo ilienea kwa kasi ya ajabu.

Baada ya karine mbili Mfalme Shomu's aliamuru ujenzi wa nyumba ya ibada ya Todaj-ji ijengwe kuanzia mwaka 752. Ni jengo kubwa la mbao duniani likiwa na urefu wa mita kumi na tatu, ndani yake waliweka sanamu ya shaba ya Buddha, baadaye ilibadilishwa na kuitwa The Great Sun Buddha au Dainichi Nyorai, Dainichi Nyorai wana uhusiano na Amaterasu na Shinto Sun Goddess.

Asili ya Japan ni nchi inayokumbwa na matetemeko makubwa ya ardhi ambayo yamekuwa yakisababisha maafa makubwa kwa raia wa Japan, kupitia dini zao kuu mbili Shinto na Buddha, ambazo asili yake ni kuzimu, waliazimia kuwa kila familia ya Kijapan ni lazima watoe Yen 3,000 kila mwezi kama sadaka kwa mizimu, kuwalinda na matetemeko ya ardhi yanayowakumba mara kwa mara.

Sadaka hiyo inapokusanywa hupelekwa kwenye hekalu lao la Todaj-ji, na watu wenye miili kabisa kutoka kuzimu hufika ndani ya hekalu hilo na kuchukua magunia kwa magunia yalijaa pesa za Yen, na kupeleka kuzimu. Inapotokea maafa kama haya ya jana, Mabuddha huanza ibada zao za kishetani na mizimu iliyovaa miili ya binadamu hufika na kuwaeleza ni kwa nini wameadhibiwa.

Kimsingi malalamiko ya mizimu wanapinga kuanza kuenea kwa dini nyingine zisizoamini mizimu katika taifa lao, ambao wanaona ni tishio kwa uchumi wa taifa la kuzimu kimapato, endapo Wajapan wataacha dini zao za Buddha na Shinto.
Hii kama ni kweli basi wana hatari kubwa!
 
maji moto,sasa hzi ni Fixi,umesikia matetemeko ya Japan,umeanza kubadili Storyline kuelekea japan,please please ,chonde chonde kaka ,endelea na mambo yetu ya kilocal local,hapa hapa TZ,hayo ya Japani tuwaachie wao.
 
Wapo watu wengi sana wanafanya uchawi, lakini ni vingumu sana kuwagundua, wachawi wengi wanaishi katika nyumba za kupanga, na utakuta wengi wao wamepanga chumba kimoja au viwili vikitumiwa na familia yenye mke/mume na watoto.

Katika mazingara kama haya, mchawi wa aina hii anapata shida sana ya kuhifadhi baadhi ya zana zake za uchawi. Ili kupunguza kadhia hii wachawi wanavyo vijiji vyao vya kuhifadhia zana zao za uchawi, mojawapo ya vijiji hivi ambavyo ni maarufu sana kinaitwa Gamboshi kilichopo mkoani Shinyanga.

Ndani vijiji hivyo ndipo wanapoweka misukule, mifupa ya binadamu na zana nyingine kubwa kubwa, vijiji hivi huwa havionekani kwa macho ya kawaida, kwani vipo ndani ya ulimwengu usioonekana. Nilikutana na kijana mmoja ambaye alikuwa msukule na aliwekwa Gamboshi Shinyanga, anasema kuwa ndani ya kijiji hicho kuna kila kitu, kuna viwanda, maduka, kuna hoteli, kuna magari kuna uwanja wa ndege na wanazo ndege zao.

Mchawi yeyote akiwa safarini akiona kijiji cha aina hiyo, anaingia ndani na anahudumiwa kwa chakula, vinywaji na malazi. Kijana huyo wa Shinyanga alieleza kuwa alihamishwa kutoka Gamboshi na kupelekwa Bagamoyo baada ya kuuzwa kwa mchawi mwingine, anasema siku ya kupelekwa Bagamoyo waliingia kwenye ndege kabisa yenye plot hadi Bagamoyo.

Wachawi wa Dar es Salaam nao wana vijiji vyao vya kuhifadhi zana zao za kichawi, vijiji hivi vipo sehemu mbalimbali ndani ya Jiji letu, lakini kijiji chenye watu wengi na maendeleo ya kasi kipo Pugu Kajiugeni, kijiji hiki cha wachawi kinakisiwa kuwa na watu waliopugua alfu thelathini.
 
Wapo watu wengi sana wanafanya uchawi, lakini ni vingumu sana kuwagundua, wachawi wengi wanaishi katika nyumba za kupanga, na utakuta wengi wao wamepanga chumba kimoja au viwili vikitumiwa na familia yenye mke/mume na watoto.

Katika mazingara kama haya, mchawi wa aina hii anapata shida sana ya kuhifadhi baadhi ya zana zake za uchawi. Ili kupunguza kadhia hii wachawi wanavyo vijiji vyao vya kuhifadhia zana zao za uchawi, mojawapo ya vijiji hivi ambavyo ni maarufu sana kinaitwa Gamboshi kilichopo mkoani Shinyanga.

Ndani vijiji hivyo ndipo wanapoweka misukule, mifupa ya binadamu na zana nyingine kubwa kubwa, vijiji hivi huwa havionekani kwa macho ya kawaida, kwani vipo ndani ya ulimwengu usioonekana. Nilikutana na kijana mmoja ambaye alikuwa msukule na aliwekwa Gamboshi Shinyanga, anasema kuwa ndani ya kijiji hicho kuna kila kitu, kuna viwanda, maduka, kuna hoteli, kuna magari kuna uwanja wa ndege na wanazo ndege zao.

Mchawi yeyote akiwa safarini akiona kijiji cha aina hiyo, anaingia ndani na anahudumiwa kwa chakula, vinywaji na malazi. Kijana huyo wa Shinyanga alieleza kuwa alihamishwa kutoka Gamboshi na kupelekwa Bagamoyo baada ya kuuzwa kwa mchawi mwingine, anasema siku ya kupelekwa Bagamoyo waliingia kwenye ndege kabisa yenye plot hadi Bagamoyo.

Wachawi wa Dar es Salaam nao wana vijiji vyao vya kuhifadhi zana zao za kichawi, vijiji hivi vipo sehemu mbalimbali ndani ya Jiji letu, lakini kijiji chenye watu wengi na maendeleo ya kasi kipo Pugu Kajiugeni, kijiji hiki cha wachawi kinakisiwa kuwa na watu waliopugua alfu thelathini.
Interesting story, jee wewe haya umejifunza wapi mkuu? au babu yako member? na hapo kwenye "red" ya kwanza kama wana maendeleo kama haya basi kwanini wasituletee na sisi tuka-advance katika technologia?. "red" ya pili jee kuna malipo au ukiwa member unahudumiwa bure? Jee kuna temporary/short term membership huko kwa wenye kutaka kujiunga? Niliwahi kusoma/kusikia kua huko wanaruka kwa ungo au fisi, sasa wewe unasema kuna ndege....hebu fafanua zaidi tuelimike.
 
Interesting story, jee wewe haya umejifunza wapi mkuu? au babu yako member? na hapo kwenye "red" ya kwanza kama wana maendeleo kama haya basi kwanini wasituletee na sisi tuka-advance katika technologia?. "red" ya pili jee kuna malipo au ukiwa member unahudumiwa bure? Jee kuna temporary/short term membership huko kwa wenye kutaka kujiunga? Niliwahi kusoma/kusikia kua huko wanaruka kwa ungo au fisi, sasa wewe unasema kuna ndege....hebu fafanua zaidi tuelimike.

De Javu. Shetani au Lucifier alipoadhibiwa na Mwenyenzi Mungu na kutupwa duniani, Mungu hakumwondolea uwezo wake wa kutenda na kufikiri. Aliondoka na akili zake na uwezo wake kikamilifu. Kumbuka kuwa alikuwa ni mmoja wa wasaidizi wa karibu sana na Mwenyenzi Mungu. Tunaweza kusema kuwa kwenye baraza la mawaziri la Mbinguni Lucifier alikuwa mmoja wao, hivyo alijuwa mambo mengi sana ya uumbaji na utendaji kazi wa Mbinguni.

Kwa taarifa yako asilimia kubwa ya technologia inayotumika duniani sasa hivi inatokea kuzimu. Utajiuliza inakuwakuwaje?

Zamani huko kijijini kwetu ilikuwa ni nadra sana kusikia kijana amefariki dunia, na linapotokea tukio kama hilo wazee walikuwa wanakaa na kulitafakari sana. Mambo yamebadilika sana sana sasa hivi, wewe mwenyewe ni shahidi, vijana wanapuputika kama majani. Je tatizo ni nini hasa? Je ni kwa sababu ya maendeleo, au ni kwa sababu ya magonjwa yasiyo na tiba, kila siku tunapoteza vijana wazuri wasomi.

Mwanzo nilieleza uwepo wa malango ya kuzimu, na hapa Tanzania yapo malango makuu saba ya kuzimu. Wapo wachawi wa nchi wanaongia huko na kutoka, unaweza kufikiri malango haya yapo chini sana ya ardhi kiasi kwamba ni lazima utafute kamba ya kushukia chini, lakini siyo. Utakuta malango haya karibu yote isipokuwa lango la Tabora na Njombe ndiyo yako nchi kavu. Mengine yako ziwani au baharini. Wachawi wa nchi wanapotaka kuingia ndani, kuna dua zao wanasoma na lango linajitokeza juu ya bahari au ziwa na lango hufunguka. Malango yote unashuka ngazi tatu peke yake, na mara unakuwa kwenye nchi nyingine tofauti kabisa, kuzimu ni kuzuri hakuna maelezo.

Utendaji kazi wa kuzimu ni kama wa huku duniani, ni sawasawa na unapoingia nchi nyingine ni lazima ujaze taarifa zako mpakani au uwanja wa ndege, utakuta wasichana wazuri ajabu wakikukaribisha na kujaza taarifa zako kwenye vitabu vya wageni, na baadaye unapelekwa kwa wahusika. Kuzimu ni miji mikubwa ajabu yapo magari, zipo nyumba, vipo viwanda na kila kitu kipo.

Kuzimu hawana shule nzuri, hivyo tegemeo lao ni vijana wanaohitimu katika vyuo mbalimbali huku duniani, ndio huchukuliwa kuzimu kuendeleza viwanda na shughuli mbalimbali za maendeleo, ndiyo maana zamani vijana walikuwa ni nadra sana kufariki hovyo kwa sababu hawakuwa na soko kuzimu kwa kuwa hawakuwa na elimu bora. Sasa hivi utasikia kijana msomi bingwa wa kutegemewa alilala hakuamka, aliumwa kichwa kesho yake kafa, gari yake ilipata ajali akafa. Ndiyo maana utakuta vijana wezi, wavuta bangi, mateja hawafi, hakuna kazi wanayoweza kuifanya kuzimu, hivyo huishi maisha yao ya hovyo hadi siku zao zifike hapa hapa duniani ndipo wanakufa.

Kuna aina mpya kabisa ya chombo cha usafiri usiotumia mafuta kinakuja, technologia hiyo italetwa duniani na nadhani kuna uwezekano mkubwa chombo hicho kikaanza kutengenezwa nchini Japan.

Ndege zipo, zinaitwa ndege za kichawi zipo, na mabasi ya abiria ya kuzimu yapo mbona mengi tu yapo barabarani, mengi yanaenda Tanga, Mombasa na Zambia. Magari ya kuzimu yapo mengi sana barabarani, hivi karibuni wapo wakulima walikuwa wanaleta viazi sokoni kutokea kigamboni, mara likafika gari aina ya toyota pickup double cabin, walilisimamisha na likasimama dreva akawaambia anaishia kigamboni, kwa sababu walikuwa wamechelewa sana wakakubali, wakapakia magunia yao nyuma na wao wakaingia wakakaa viti vya nyuma, lakini walishangaa walipofika feri walikuta feri ndiyo linaondoka, hivyo gari lao lilienda moja kwa moja ndani ya bahari, lakini walishangaa sana kwani hawakuyaona maji na wakajikuta katika nchi ya ajabu, kwa kudra za Mwenyenzi Mungu wajikuta wametupwa ufukweni Kunduchi.

Ndugu usikubali kabisa kuingia kwenye mambo ya uchawi, shetani ni mwongo kupindukia, atakupa utajiri wa kishindo lakini wa muda mfupi utakaoteketeza familia yako na wewe mwenyewe, ridhika na hali yako ya kusaga lami ukitafuta riziki lakini upate kuishi maisha marefu na familia yako ibaki salama.
 
Mwishowe utatuambia kuwa wewe ulikuwa mchawi lakini sasa umehamua kumfuata Bwana Yesu.

Hizi hadithi zako ukimpatia shigongo, mzee utazikusanya sarafu.
 
Mikoa saba nchini Tanzania ndiyo tishio kwa kuwa na nguvu kubwa za uchawi
1. Tanga ndio kinara
2. Lindi unafuatilia
3. Dar es Salaam
4. Mtwara
5. Tabora
6. Kigoma
7. Mwanza

Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Mikoa ambayo wananchi wake ndio wateja wakuu wa wachawi
1. Kilimanjaro inaongoza
2. Morogoro inafuatilia
3. Kagera

Wateja wengine wa wachawi
1. Wafanyabiashara
2. Wasanii
3. Kina mama wa nyumbani
4. Wanafunzi wa shule za sekondari hasa wa kidato cha pili.
NB:Mtaa unaoongoza kwa wachawi dar es salaam- wakulima road,kinondoni hananasif,yaani huku kuna kingdom ya wachawi,kila baada ya nyumba wamo!!
 
Duh!maji moto,unamaanisha, hizi remote za tv ,toyota lexus na mobile phones from japan zote zilianzia kuzimu?!!
kazi kweli kweli kuamini
 
Majimoto shusha vitu mkuu kwani ninapita kila siku hapa. Ikiwezekana andaa pdf utuwekee tudownload. Ila upo juu kwenye habari za haya mambo. duu
 
we majimoto umeenda wapi Mkuu,embu copy na kupaste fasta fasta hizo Story,jamaa wameshaanza kukumiss leo 🙂
 
Back
Top Bottom