Watawala wa Taifa la Tanzania, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, walifanya kila aina ya mbinu chafu za kuimarisha utawala wao, ili waweze tena kuongoza taifa la Tanzania.
Nimesema walifanya mbinu chafu zenye makufuru makubwa, na katika ulimwengu usiooneka walionekana waziwazi waliyokuwa wakiyafanya.
Moja ya kufuru walilofanya ni kuwekwa ndani ya majeneza na kushushwa makaburini, ambako walilala huko usiku mzima, huku wachawi wa nchi wakicheza uchi wa nyama juu ya makaburi hayo. Kisha waliapishwa na majini.
Lakini kibao kiligeuzwa ghafula katika ulimwengu usiooneka baada ya kuingiliwa na kundi kubwa la wanadamu waliokuwa wanamlilia Mwenyenzi Mungu juu ya hatima ya baadaye ya taifa la Tanzania.
Katika ulimwengu usioonekana, utawala uliokuwa ukioonekana kama mlima Kilimanjaro, uligeuzwa kichwa chini miguu juu, ulisagwasagwa, ukasambaratishwa kutoka jiwe la mlima hadi kuwa mavumbi matupu.
Kimsingi utawala wa taifa la Tanzania ulioliongoza taifa hili kutoka mwaka 1961 ulikoma rasmi mwezi Septemba 2010 katika ulimwengu usioonekana.
Kazi inayoendelea sasa ni kufanya yale yaliyotendeka katika ulimwengu usioonekana, yadhihirike katika ulimwengu unaooneka. Kawaida nguvu ya mtu au ya taifa ipo katika ulimwengu usioonekana, na matokeo yake hujitokeza taratibu kwenye ulimwengu unaoonekana.
Kwa sababu taifa la Tanzania kwa sasa hivi halipo kabisa katika ulimwengu usioonekana, yapo mambo kadhaa ambayo ni lazima yajitokeze katika ulimwengu unaoonekana.
a) Watawala walioondolewa katika ulimwengu usioonekana, kila jambo watakalojaribu kulifanya au kutenda katika ulimwengu unaoonekana wataishia kwenye aibu ya kukata na shoka.
b) Mambo hayo ya aibu yatakuwa yanafuta hati yao batili ya utawala polepole kwenye utawala unaoonekana.
c) Mwenyenzi Mungu hawezi kusimamisha utawala mpya kwenye utawala uliofanya makufuru makubwa kiasi hicho hadi, utawala huo ufutike kabisa katika ulimwengu unaooneka kama ulivyogeuzwa mavumbi katika ulimwengu usioonekana.
d) Njaa italiandama taifa, kwa sababu Mungu amegeuka, uso wake haupo tena juu ya taifa hili hadi makufuru yaliyofanyika yafutike.
e) Waliofanya makufuru hayo wajitayarishe kwa hasira kali ya Mwenyenzi Mungu.
Hili jambo ni hakika na kweli, na litatimia kwa asilimia 100%