Biashara ya Usafirishaji kwa Bajaji: Ueandeshaji, Changamoto, Faida na Ushauri

aise nimepata kitu humu, je mnaweza kutapa ufafanuzi juu ya kirikuu? Ni ipi bora kati ya kirikuu na bajaji? na bei ya bajaji kwa sasa ni sh ngapi? min and maximum price
Kwa uzoefu wangu kirikuu nzuri mi carry ya kichwa kikubwa.
Hii iko kama mkate hivi,ina gia 5,na nzuri ni 4 wheel drive.
Hizi maderev wanasema zinanguvu sana hiyvo huweza kubebe mzigo mkubwa kidogo kulingana na nyingine,
Na pia 4wd inasaidi kupita kwenye barabara ngumu kama tope na kichanga.
 

Katika biashara ni hatari sana kuwekeza kwenye mradi mmoja (Concentration Risk) kwani ukipata hasara basi umepoteza kila kitu. Ni muhimu sana kupanga kuyaweka mayai yako kwenye makapu tofauti ili kapu moja likioza kwa sababu yai moja limeoza ndani ya kapu hilo basi makapu mengine yasalimike na hivyo kukuwezesha kuendelea na biashara yako (Diversification).

Ili kufanya diversification yenye tija basi hakikisha miradi unayotaka kuifanya in risk profiles ambazo hazishabihiani kabisa kwa maana kwamba kama vyanzo vya hasara vikitokea kwenye biashara moja basi vyanzo hivyo ni vyanzo vya faida kwenye biashara nyingine.

Kwa mfano kama unataka kufanya biashara ya kuuza mablanketi basi fikiria kufanya na biashara ya kuuza barafu pia kwa sababu kama hakuna baridi basi mablanketi hayatauzika lakini barafu zitauzika kutokana na watu kutumia sana vitu vya baridi wakati wa joto hivyo hasara utakayoipata kwenye uuzaji duni wa mablanketi itafidiwa na faida utakayoipata kwenye uuzaji mwingi wa barafu.
 
Shafi_Abeid,

Ingekuwa hivyo watu wasingenunua. Ni bora hasara niipate pesa ikiwa imepotea mikononi mwangu,kuliko kumpa mwingine kisha nipate hasara zaidi ya ufuatiaji kwenye ufilisi.

Hizi Promo nyingine hembu acheni bidhaa ijipe promo yenyewe. Kama unafanya vizuri watu watakuja tuu, maada nyingine umeleta vituvingine kabisaaa
 
Nauza bajaji yangu, TVS, ina hali nzuri bei 3.5M.
Sababu ya kuuza nataka nibadili biashara kutokana na kukosa muda wa kuisimamia ipasavyo.
Kama unahitaji ni PM tuongee biashara.
 
Mkuu hiyo bima kubwa ni shilingi ngapi?
 
C bora uwe na bodaboda 3 za mkataba wa miezi 12 wa elfu 10 kwa siku ambayo itakuletea kiasi kama hicho cha bajaj ambayo inachukua miez 18!!?
 
Only risk takers can survive and succeed in any business.
Acha kukatisha watu tamaa hapa.
 
Umesahau kuwa siku nyingine naye hapati kitu na ww unamkomalia hesabu yako bila huruma. Usiangalie upande mmoja wa shilingi mkuu.
 
Fanya hivi ingia na mtu mkataba wa mwaka mmoja. baada ya mwaka unamwachia. Terms ni kwamba kila siku lazima alete pesa endapo ikifika week hajaleta mnamnyang'anya. Matengenezo yoyote juu yake. Kila siku anakuletea 30k. 30,000*30*12=10,800,000
Huu ndio ushauri mzuri, ukitegemea kumuweka mtu akuletee tu ni kazi bure, mi hii kitu ilishaniliza, niliweka mtu ikawa ni usumbufu tu mwishowe nikauza, kama vipi unaweza endesha mwenyewe for supernormal profit.
 
Mkuu hamna biashara inayokosa changamoto so ni kumpa moyo na kumpa ushauri mzuri mkuu...karibu Sana Event 9 limited tukusaidie kuhusu biashara hii
Hiyo business kichefuchefu hata ukimpata kijana mstaarabu, labda tu uendeshe mwenyewe ndipo utaona faida, ni upuuzi kusubiri faida ya 2mln kwa mwaka mzima.
 
Habarini za muda huu,

Nikiwa kama kijana mtafutaji najiandaa na maisha yangu baada ya kumaliza chuo mwezi wa saba mwaka huu(2017) nimejibana hatimaye nimefanikiwa kua na mtaji wangu wa pesa taslimu 3.2Mil, natarajia kua hadi siku nitakapomaliza chuo nitakua na 4Mil cash.

Nimepanga nitakapomaliza chuo mwezi wa saba ninunue bajaji tvs-king kwa mtu(used) kisha niendeshe mwenyewe ili nijitafutie ridhiki yangu ya kila siku(maisha baada ya chuo) hapa jijini DSM.

Lengo la kuleta hoja hii ni kufahamishwa mambo yafuatayo kuhusiana na biashara hii ya bajaji.

1. Kununua bajaji kwa mtu hakutokatisha ndoto zangu? kama ni vibaya kwa biashara niachanenayo maana sina uwezo wa kununua mpya dukani

2. Changamoto za hii biashara ni zipi? (sitomkabidhi mtu bajaji, nitaendesha mwenyewe)
 
Umeona mbali sana maana ajira zinaonekana kwa Tochi. Hii biashara ni nzuri mkuu. Kikubwa wewe mwenyewe umejipangaje. Kama umeweza kujichanga 4m kupitia Boom lako Naamini hata hii utaweza kujichanga na kufanya makubwa.
 
Kiukweli mi nimmiliki wa bajaji changamoto kubwa huwa ni madereva kama utaendesha mwenyewe basi zingatia tu matunzo, pia unaponunua kwa mtu si ajabu ukahitaji matengenezo makubwa mwanzoni. Kila la kheri kijana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…