Biashara ya Vifaa vya Ujenzi (Hardware Store): Ushauri wa Mtaji, Uendeshaji, Changamoto na Faida

Biashara ya Vifaa vya Ujenzi (Hardware Store): Ushauri wa Mtaji, Uendeshaji, Changamoto na Faida

Unajua sio kwanba uzalishaji unazidi watumiaji ila garama za kununua ziko juu zaidi

Kwa mfano ukiwa mbeya cement yao inauzwa 14500 kwa 15500

Wakati huo ukifika Iringa inauzwa 13500 mpaka 14500 wakipunguza Bei Haita tosha na kwa cement inayo pelekwa nje inauzwa Bei ya chini kuliko bei tunayo uziwa huku kwetu
We unadhani kwa nini ikipelekwa nje iuzwe bei ndogo? Kwa taarifa nilizonazo hadi mwaka jana uzalishaji ni mkubwa kuliko mahitaji ya ndani na consumption growth rate ni moderate kuliko uwezo wa viwanda
 
Mkuu uzalishaji chini ya kiwango kunatokana na aina ya mitambo yao ya kuzalishia cement kwa mfano mtambo ulio zinduliwa na raisi ulikujengwa kwa mategemeo ya kuzalisha tani 100 kwa saa lakini unazalisha tani 55 mpaka 60 kwa SAA

Manake ni kuwa ukipiga hesabu ni kuwa uwezo wa kuzalisha tani 1000 kwa siku ni ngumu

Mkuu acha ubishi, navifahamu hivi viwanda vizuri sana.
Uwezo wa kiwanda unakuwa Determined na uwezo wa kiln kwa maana ya clinker inavyozalishwa, Cement mill mwisho wa siku ndio inaleta Cement, Hivyo viwanda nilivyokutajia hapo juu hasa hivi viwili vikubwa Dangote na Simba (Tanga) kila kitu kikiwa vizuri na cement mill zote zipo ok na kiln ziko ok na soko liko vizuri uzalishaji wa Dangote huwa ni 6000tone/day na Simba ni 4000tone/day.. Ila kukiwa na ups and downs huwa average per day ni 5000tone/day Dangote na 3000-3500tone/day Simba.

Hizo Tonnage ni Designed Capacity kwa maana ndio uwezo wa hizo plants, na kama kila kitu kipo ok tani hizo hupatikana bila shida. Breakdowns, maintenance, shutdowns, Hali ya soko ni vitu vya kawaida kwenye uzalishaji na huleta shida wakati fulani kiasi cha efficiency na production kupungua, Ila sio chanzo cha kusema eti haviwezi kuzalisha hizo tonnage. SI KWELI.
 
Mkuu dangote sina uhakika kama anazalisha hiyo tani unazo sema

Kwenye makaratasi huwa mandishi tofaut na vitendo

Mbeya cement wakijitahidi huwa wanafikisha tani 600 hapo wanatumia mill mbili

Nyati wao wakijitahidi sana wanaenda mpaka 800

Twigs kidogo wanasogea 900

Kwenye makratasi watambia tofauti ila kwa sisi tulio wahi kufanya kazi kwenye hivi viwanda tunajua
Hao Mbeya cement wanaongeza mtambo mwingine na rais alikuwa kuzindua majuzi Wana target kutoka tani 600,000 hadi tani 1,100,000 kwa mwaka by next year na wao wanalenga soko hilo la nje coz la ndani liko saturated
 
Hao Mbeya cement wanaongeza mtambo mwingine na rais alikuwa kuzindua majuzi Wana target kutoka tani 600,000 hadi tani 1,100,000 kwa mwaka by next year na wao wanalenga soko hilo la nje coz la ndani liko saturated
Hao mbeya cement ndio wauzaji wa hizo tani 2000 zilizo wekwa kwenye taarifa

Na huo mtambo mpya unashida kuliko wa zaman
 
Mkuu acha ubishi, navifahamu hivi viwanda vizuri sana.
Uwezo wa kiwanda unakuwa Determined na uwezo wa kiln kwa maana ya clinker inavyozalishwa, Cement mill mwisho wa siku ndio inaleta Cement, Hivyo viwanda nilivyokutajia hapo juu hasa hivi viwili vikubwa Dangote na Simba (Tanga) kila kitu kikiwa vizuri na cement mill zote zipo ok na kiln ziko ok na soko liko vizuri uzalishaji wa Dangote huwa ni 6000tone/day na Simba ni 4000tone/day.. Ila kukiwa na ups and downs huwa average per day ni 5000tone/day Dangote na 3000-3500tone/day Simba.

Hizo Tonnage ni Designed Capacity kwa maana ndio uwezo wa hizo plants, na kama kila kitu kipo ok tani hizo hupatikana bila shida. Breakdowns, maintenance, shutdowns, Hali ya soko ni vitu vya kawaida kwenye uzalishaji na huleta shida wakati fulani kiasi cha efficiency na production kupungua, Ila sio chanzo cha kusema eti haviwezi kuzalisha hizo tonnage. SI KWELI.
Kuvifahamu hakuondoi kusema ukweli kwanini watanzania tunapenda kuambiwa uongo zaidi

Mimi pia nimefanya kwenye hivi viwanda zaidi ya miaka nane nina uzoefu na ninacho kwambia

Baada ya kuacha kazi za viwandani nikahamia kazi ya udereva kusambaza hiyo mizigo mpaka naacha kazi ya udereva nimepita viwanda vyote vikongwe isipo kuwa dangote tu
 
Mkuu hakuna barabara yoyote inayojengwa kutoka Namanyere kwenda kasanga na wala sababu na huo mpango haipo ila kuna barabara iko hatua za mwisho kutoka sumbawanga/Matai kwenda kasanga
Pili kuna zaidi ya bandari ndogo 28 plus bandari kuu ya Kigoma kwenye mwambao wa ziwa Rukwa ambazo zinapatikana kwa kila mkoa mfano bandari ya Kabwe na New Kipili port zinajengwa huko Nkasi na serikali iko katika hatua za upembuzi yakinifu ili kuziunganisha na barabara za lami
Kwa Katavi kuna bandari ya karema nayo itapanuliwa mwaka huu wa fedha na mchakato wa kuiunganisha kwa lami kutoka mpanda mjini unaendelea
Mwisho ni kwamba ni bahati mbaya sana upande wa pili wa DRC hakuna miji mikubwa wala rasilimali za madini au nyinginezo za kuchochea biashara tofauti na kusini huko Lubumbashi na kaskazini jimbo la Bukavu thus why muingiliano wa biashara kati ya Tzn na drc mwambao mwa ziwa Tangangika ni kiduchu sana labda siku za baadae sana
Mkuu unajitahidi kunyumbulisha hoja mpaka hapo nimekuelewa
 
Mbugoti na Timu asanteni kwa elimu nzuri. Naomba kujua Wakala (middle man) wa Simenti aliyepo maeneo ya King'azi/mbezi ya kimara ili kupata simenti kwa bei nafuu kwa ajili ya ujenzi siyo kuuza.
Biashara ya cement hususan kama utakuwa unauza kwa bei ya rejareja inatoka zaidi ikiwa inauzwa na vifaa vingine vya ujenzi. Hii ni sababu wateja wengi wa ujenzi huka tayari una duka la hardware, hata kama halina vifaa vingi, unaweza kuanza na hata mifuko 100-200.

Ila kwa kiasi hiki kidogo cha cement, hutaweza kununua moja kwa moja kiwandani na kunufaika na bei ya kiwandani ambayo kwa sasa kwa mfano Dangote ni sh 9500/mfuko wa grade 32.5 na 10000/mfuko wa grade 42.5. Kiasi cha chini unachoweza kuagiza kiwandani ni tani 30 (mifuko 600) ambayo ni kati ya sh mil 5.7 - mil 6 kutegemea na grade. Kwa Dangote haultalipia usafiri na utaletewa hadi mlangoni. Kwa baadhi ya makampuni inabidi ujitegemee gharama za usafirishaji kutoka kiwandani hadi kwako.

Kwa mtaji wako wa mil 3, itabidi ununue kwa watu wa kati ambao wananunua kiwandani ambao wao huongeza faida ya kati ya sh 500-1000/mfuko. Kama utanunua zaidi ya mifuko 50, wauzaji wengi watakuuzia kwa bei ya jumla (10,000 au 10,500) kulingana na grade. Cha muhimu ni kuzungumza nao vizuri, maana mwingine anaweza hata kukuuzia chini ya hapo kama utachukua mzigo mkubwa kwa mara moja.

Ikija swala la faida, faida kwa mfuko wa cement ni ndogo sana (sh 500-1000) kulingana na soko na ushindani ni mkubwa. Ukinunua huo mfuko wa sh 10,000, ili kushindana na soko hutaweza kuuza zaidi ya sh 11,000 kutegemeana na eneo ulipo. Kama wauzaji ni wengi zaidi basi tegemea kuuza chini ya hapo. Biashara ya cement ni biashara ambayo inategemea "volume sale" ili uweze kuona faida ndio maana wafanyabiashara wengine wanaoagiza kutoka kiwandani wako tayari hata kupata faida ya sh 300/mfuko ili kuvuta wateja na kuhakikisha mzigo wa mifuko 600 au zaidi unaisha siku moja.

Kwa uzoefu wangu, biashara ya cement inahitaji mtaji mkubwa ili kuona faida nzuri. Fikiria mzigo wa tani 30 ambao ni sh mil 6 utazalisha faida ya laki 3 (sh 500/mfuko), ambayo si ndogo sana kama utaweza kuuza angalau tani 30/wiki lakini kama huo mzigo utakaa zaidi ya wiki 4 dukani (na hii inatokea kwa hali ya soko hivi sasa), utaona ni faida ndogo sana kwa uwekezaji huo. Maana kumbuka hapo kuna gharama za ushushaji wa cement ambayo kawaida ni sh 100/mfuko na kama umemweka mtu akusaidie naye inabidi umlipe. Kwa watu wenye mitaji mikubwa kidogo wanaongeza mzunguko wao cement kwa kuagiza mzigo mkubwa zaidi na kuisambaza kwa wafanyabiashara wadogo kwa faida si zaidi ya sh 500/mfuko. Lengo kuu ni kuhakikisha mzigo haukai dukani na unauzika kwa haraka.

Kwa uzoefu wangu changamoto kubwa kwenye cement ni kwamba wakati mwingine uzalishaji unakuwa si wa kuaminika, na hii ni kwa viwanda vyote (mara chokaa imeisha, makaa yameisha au malori ya kusafirishia hayatoshi n.k). Unaweza ukawa umelipia mzigo, halafu zikapita zaidi ya wiki mbili unazungushwa kupata mzigo. Sasa hii inaumiza especially kwa wenye mitaji midogo, maana hela umeshatoa kwenye mzunguko na wakati mwingine unakuwa umeshamwahidi mteja kwamba cement yake atapata kesho na hela yake ushachukua...

Pia kama unauza aina moja tu ya cement hio pia itakuwa changamoto, maana kuna wateja kwa mfano hawatumii brand yoyote zaidi ya twiga, kwa hio ni muhimu kuwa na angalau aina mbili au zaidi ya brand. Sasa kama mtaji mdogo itakuwa changamoto kuweza kuwa na brand tofauti za cement kwa wakati mmoja.

Changamoto nyingine hivi sasa ni soko. Kwa kweli soko limeshuka sana, lakini nafikiri hio si kwa cement tu, bali hata kwa bidhaa nyingine.

Ushauri wangu kwako:
1. Kama una duka la hardware na unataka kuongeza cement, basi anza na mifuko 100-200. Ingawa faida si kubwa, lakini uwepo wa cement kwenye duka la hardware inasaidia sana vitu vingine kuuzika kwa vile mteja wa cement mara nyingi atataka vitu vingine vya ziada zaidi ya cement.

2. Kama huna duka la hardware na unataka kufanya biashara ya cement peke yake nakushauri uongeze mtaji ili uweze kuagizia kiwandani. Hii itakusaidia kwenye ushindani wa bei ambayo itakuwezesha kuvuta wateja. Kumbuka wenye maduka ya hardware wana bidhaa nyingi ambazo humvuta mteja, lakini kwa upande wako itakubidi bei yako iwe ndo kigezo kikuu cha kumfanya mteja aje kwako kununua cement tu kwako, halafu atoke aende duka jingine kununua mahitaji mengine ya ujenzi badala ya kufanya manunuzi yote kwenye duka moja.

3. Kama ushindani si mkubwa eneo lako, unaweza ukaanza na mifuko 200-300 kwa biashara ya cement pekee, lengo lako la awali likiwa ni kutengeneza soko na kujifunza biashara huku ukikuza mtaji ili kuweza kuagiza kutoka kiwandani.
 
Ndugu, habari zenu

Nina kiasi cha mil 10 hivi kwa sasa nategemea kuanzisha biashara ya kuagiza cement kutoka kiwandani na kuiuza rejareja ila kwa mtaji wangu huo nahisi utatosha kwa kuanzisha duka la uuzaji cement tu.

Sasa naomba mwenye mtazamo mpana kuhusu biashara hii aweze kunishauri kwa mapana.
 
Kwa huu mdororo wa uchumi bora ufanye biashara za vyakula au duka la dawa bro.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama yupo interested na hiyo biashara anaweza kuchukua nafaka mikoani akaweka stoo kuanzia mwezi wa 9 huko anaweza kupata faida nusu ya mtaji wake.

Kwa hali ya sasa biashara anayowaza huwenda isiwe na faida pia kwa sababu ya upya wa biashara pale anapoenda kuisimika. Yaani ataanza kazi ya kutengeneza jina la biashara yake kisha atengeneze wateja ni tofauti na vyakula huuzika kwa haraka ukiotea sehemu nzuri.
 
Back
Top Bottom