ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
We unadhani kwa nini ikipelekwa nje iuzwe bei ndogo? Kwa taarifa nilizonazo hadi mwaka jana uzalishaji ni mkubwa kuliko mahitaji ya ndani na consumption growth rate ni moderate kuliko uwezo wa viwandaUnajua sio kwanba uzalishaji unazidi watumiaji ila garama za kununua ziko juu zaidi
Kwa mfano ukiwa mbeya cement yao inauzwa 14500 kwa 15500
Wakati huo ukifika Iringa inauzwa 13500 mpaka 14500 wakipunguza Bei Haita tosha na kwa cement inayo pelekwa nje inauzwa Bei ya chini kuliko bei tunayo uziwa huku kwetu
Mkuu uzalishaji chini ya kiwango kunatokana na aina ya mitambo yao ya kuzalishia cement kwa mfano mtambo ulio zinduliwa na raisi ulikujengwa kwa mategemeo ya kuzalisha tani 100 kwa saa lakini unazalisha tani 55 mpaka 60 kwa SAA
Manake ni kuwa ukipiga hesabu ni kuwa uwezo wa kuzalisha tani 1000 kwa siku ni ngumu
Hao Mbeya cement wanaongeza mtambo mwingine na rais alikuwa kuzindua majuzi Wana target kutoka tani 600,000 hadi tani 1,100,000 kwa mwaka by next year na wao wanalenga soko hilo la nje coz la ndani liko saturatedMkuu dangote sina uhakika kama anazalisha hiyo tani unazo sema
Kwenye makaratasi huwa mandishi tofaut na vitendo
Mbeya cement wakijitahidi huwa wanafikisha tani 600 hapo wanatumia mill mbili
Nyati wao wakijitahidi sana wanaenda mpaka 800
Twigs kidogo wanasogea 900
Kwenye makratasi watambia tofauti ila kwa sisi tulio wahi kufanya kazi kwenye hivi viwanda tunajua
Mwaka huu wa fedha wataitengeneza plus barabara ya kutoka mpanda kuwa na subiraWangetutengenezea na bandari ya Kakola/Kalema pia hapo ziwa Tanganyika ingependeza sana
Hao mbeya cement ndio wauzaji wa hizo tani 2000 zilizo wekwa kwenye taarifaHao Mbeya cement wanaongeza mtambo mwingine na rais alikuwa kuzindua majuzi Wana target kutoka tani 600,000 hadi tani 1,100,000 kwa mwaka by next year na wao wanalenga soko hilo la nje coz la ndani liko saturated
Sasa mimi mambo ya mitambo watajua wenyewe lakini na dangote saizi ameanza kuuza jongo kupitia kasanga portHao mbeya cement ndio wauzaji wa hizo tani 2000 zilizo wekwa kwenye taarifa
Na huo mtambo mpya unashida kuliko wa zaman
Kuvifahamu hakuondoi kusema ukweli kwanini watanzania tunapenda kuambiwa uongo zaidiMkuu acha ubishi, navifahamu hivi viwanda vizuri sana.
Uwezo wa kiwanda unakuwa Determined na uwezo wa kiln kwa maana ya clinker inavyozalishwa, Cement mill mwisho wa siku ndio inaleta Cement, Hivyo viwanda nilivyokutajia hapo juu hasa hivi viwili vikubwa Dangote na Simba (Tanga) kila kitu kikiwa vizuri na cement mill zote zipo ok na kiln ziko ok na soko liko vizuri uzalishaji wa Dangote huwa ni 6000tone/day na Simba ni 4000tone/day.. Ila kukiwa na ups and downs huwa average per day ni 5000tone/day Dangote na 3000-3500tone/day Simba.
Hizo Tonnage ni Designed Capacity kwa maana ndio uwezo wa hizo plants, na kama kila kitu kipo ok tani hizo hupatikana bila shida. Breakdowns, maintenance, shutdowns, Hali ya soko ni vitu vya kawaida kwenye uzalishaji na huleta shida wakati fulani kiasi cha efficiency na production kupungua, Ila sio chanzo cha kusema eti haviwezi kuzalisha hizo tonnage. SI KWELI.
We unadhani kwa nini ikipelekwa nje iuzwe bei ndogo? Kwa taarifa nilizonazo hadi mwaka jana uzalishaji ni mkubwa kuliko mahitaji ya ndani na consumption growth rate ni moderate kuliko uwezo wa viwanda
Mkuu dangote ameanza baada ya mbeya cement kuyumba kutokana na matatizo ya mitambo na mashart kuwa mengiSasa mimi mambo ya mitambo watajua wenyewe lakini na dangote saizi ameanza kuuza jongo kupitia kasanga port
Mkuu unajitahidi kunyumbulisha hoja mpaka hapo nimekuelewaMkuu hakuna barabara yoyote inayojengwa kutoka Namanyere kwenda kasanga na wala sababu na huo mpango haipo ila kuna barabara iko hatua za mwisho kutoka sumbawanga/Matai kwenda kasanga
Pili kuna zaidi ya bandari ndogo 28 plus bandari kuu ya Kigoma kwenye mwambao wa ziwa Rukwa ambazo zinapatikana kwa kila mkoa mfano bandari ya Kabwe na New Kipili port zinajengwa huko Nkasi na serikali iko katika hatua za upembuzi yakinifu ili kuziunganisha na barabara za lami
Kwa Katavi kuna bandari ya karema nayo itapanuliwa mwaka huu wa fedha na mchakato wa kuiunganisha kwa lami kutoka mpanda mjini unaendelea
Mwisho ni kwamba ni bahati mbaya sana upande wa pili wa DRC hakuna miji mikubwa wala rasilimali za madini au nyinginezo za kuchochea biashara tofauti na kusini huko Lubumbashi na kaskazini jimbo la Bukavu thus why muingiliano wa biashara kati ya Tzn na drc mwambao mwa ziwa Tangangika ni kiduchu sana labda siku za baadae sana
Biashara ya cement hususan kama utakuwa unauza kwa bei ya rejareja inatoka zaidi ikiwa inauzwa na vifaa vingine vya ujenzi. Hii ni sababu wateja wengi wa ujenzi huka tayari una duka la hardware, hata kama halina vifaa vingi, unaweza kuanza na hata mifuko 100-200.
Ila kwa kiasi hiki kidogo cha cement, hutaweza kununua moja kwa moja kiwandani na kunufaika na bei ya kiwandani ambayo kwa sasa kwa mfano Dangote ni sh 9500/mfuko wa grade 32.5 na 10000/mfuko wa grade 42.5. Kiasi cha chini unachoweza kuagiza kiwandani ni tani 30 (mifuko 600) ambayo ni kati ya sh mil 5.7 - mil 6 kutegemea na grade. Kwa Dangote haultalipia usafiri na utaletewa hadi mlangoni. Kwa baadhi ya makampuni inabidi ujitegemee gharama za usafirishaji kutoka kiwandani hadi kwako.
Kwa mtaji wako wa mil 3, itabidi ununue kwa watu wa kati ambao wananunua kiwandani ambao wao huongeza faida ya kati ya sh 500-1000/mfuko. Kama utanunua zaidi ya mifuko 50, wauzaji wengi watakuuzia kwa bei ya jumla (10,000 au 10,500) kulingana na grade. Cha muhimu ni kuzungumza nao vizuri, maana mwingine anaweza hata kukuuzia chini ya hapo kama utachukua mzigo mkubwa kwa mara moja.
Ikija swala la faida, faida kwa mfuko wa cement ni ndogo sana (sh 500-1000) kulingana na soko na ushindani ni mkubwa. Ukinunua huo mfuko wa sh 10,000, ili kushindana na soko hutaweza kuuza zaidi ya sh 11,000 kutegemeana na eneo ulipo. Kama wauzaji ni wengi zaidi basi tegemea kuuza chini ya hapo. Biashara ya cement ni biashara ambayo inategemea "volume sale" ili uweze kuona faida ndio maana wafanyabiashara wengine wanaoagiza kutoka kiwandani wako tayari hata kupata faida ya sh 300/mfuko ili kuvuta wateja na kuhakikisha mzigo wa mifuko 600 au zaidi unaisha siku moja.
Kwa uzoefu wangu, biashara ya cement inahitaji mtaji mkubwa ili kuona faida nzuri. Fikiria mzigo wa tani 30 ambao ni sh mil 6 utazalisha faida ya laki 3 (sh 500/mfuko), ambayo si ndogo sana kama utaweza kuuza angalau tani 30/wiki lakini kama huo mzigo utakaa zaidi ya wiki 4 dukani (na hii inatokea kwa hali ya soko hivi sasa), utaona ni faida ndogo sana kwa uwekezaji huo. Maana kumbuka hapo kuna gharama za ushushaji wa cement ambayo kawaida ni sh 100/mfuko na kama umemweka mtu akusaidie naye inabidi umlipe. Kwa watu wenye mitaji mikubwa kidogo wanaongeza mzunguko wao cement kwa kuagiza mzigo mkubwa zaidi na kuisambaza kwa wafanyabiashara wadogo kwa faida si zaidi ya sh 500/mfuko. Lengo kuu ni kuhakikisha mzigo haukai dukani na unauzika kwa haraka.
Kwa uzoefu wangu changamoto kubwa kwenye cement ni kwamba wakati mwingine uzalishaji unakuwa si wa kuaminika, na hii ni kwa viwanda vyote (mara chokaa imeisha, makaa yameisha au malori ya kusafirishia hayatoshi n.k). Unaweza ukawa umelipia mzigo, halafu zikapita zaidi ya wiki mbili unazungushwa kupata mzigo. Sasa hii inaumiza especially kwa wenye mitaji midogo, maana hela umeshatoa kwenye mzunguko na wakati mwingine unakuwa umeshamwahidi mteja kwamba cement yake atapata kesho na hela yake ushachukua...
Pia kama unauza aina moja tu ya cement hio pia itakuwa changamoto, maana kuna wateja kwa mfano hawatumii brand yoyote zaidi ya twiga, kwa hio ni muhimu kuwa na angalau aina mbili au zaidi ya brand. Sasa kama mtaji mdogo itakuwa changamoto kuweza kuwa na brand tofauti za cement kwa wakati mmoja.
Changamoto nyingine hivi sasa ni soko. Kwa kweli soko limeshuka sana, lakini nafikiri hio si kwa cement tu, bali hata kwa bidhaa nyingine.
Ushauri wangu kwako:
1. Kama una duka la hardware na unataka kuongeza cement, basi anza na mifuko 100-200. Ingawa faida si kubwa, lakini uwepo wa cement kwenye duka la hardware inasaidia sana vitu vingine kuuzika kwa vile mteja wa cement mara nyingi atataka vitu vingine vya ziada zaidi ya cement.
2. Kama huna duka la hardware na unataka kufanya biashara ya cement peke yake nakushauri uongeze mtaji ili uweze kuagizia kiwandani. Hii itakusaidia kwenye ushindani wa bei ambayo itakuwezesha kuvuta wateja. Kumbuka wenye maduka ya hardware wana bidhaa nyingi ambazo humvuta mteja, lakini kwa upande wako itakubidi bei yako iwe ndo kigezo kikuu cha kumfanya mteja aje kwako kununua cement tu kwako, halafu atoke aende duka jingine kununua mahitaji mengine ya ujenzi badala ya kufanya manunuzi yote kwenye duka moja.
3. Kama ushindani si mkubwa eneo lako, unaweza ukaanza na mifuko 200-300 kwa biashara ya cement pekee, lengo lako la awali likiwa ni kutengeneza soko na kujifunza biashara huku ukikuza mtaji ili kuweza kuagiza kutoka kiwandani.
Hio n bei ya kiwandani na ukienda kiwandan lazma upakue si chin ya mifuko 500 kwa hio bei.Tafakali,chukua hatua!
Dawa za binadam au mifugo boss kama za binadamu lazima uwe mfamasia ndgKwa huu mdororo wa uchumi bora ufanye biashara za vyakula au duka la dawa bro.
Sent using Jamii Forums mobile app
Zingatia ushauri huu.Kwa huu mdororo wa uchumi bora ufanye biashara za vyakula au duka la dawa bro.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama yupo interested na hiyo biashara anaweza kuchukua nafaka mikoani akaweka stoo kuanzia mwezi wa 9 huko anaweza kupata faida nusu ya mtaji wake.Kwa huu mdororo wa uchumi bora ufanye biashara za vyakula au duka la dawa bro.
Sent using Jamii Forums mobile app