Biashara za mitandao (kuunganishana) zinavyowaliza first year vyuoni

Sasa kama ni hivyo inamaana hata hao wanaokuja kushawishi watu watoe pesa nap wanatapeliwa. Inaonekana kuna kikundi cha watu wachache sana ndani au nje ya nchi waliobuni hii biashara ndio wanafaidika na mtandao huu
 
Sasa kama ni hivyo inamaana hata hao wanaokuja kushawishi watu watoe pesa nap wanatapeliwa. Inaonekana kuna kikundi cha watu wachache sana ndani au nje ya nchi waliobuni hii biashara ndio wanafaidika na mtandao huu
Jibu ni NDIYO.
Ila wanatumia saikolojia kubwa sana kukuaminisha kuwa wewe ndie mnufaika zaidi kuliko pesa ambayo umewapelekea.
 
Wala usipate shida, hapa hapa nitatoa maelezo ya QNET wanavyofanya kazi zao, maana wapo jamaa kadhaa waliingia mkenge kujiunga huko wakalizwa hatari.

-Kifupi kabisa, msingi wao mkuu ni ule ule kama Forever Living, Alliance in motion nk, zote ni PYRAMID SCHEME (Yaani wachache wanaotangulia kujiunga wanavuna zaidi kupitia migongo ya wengine wengi wanaofuata nyuma yao katika mnyororo) Katika hilo hakuna tofauti.

-Kuna gharama(mtaji) wa chini wa kujiunga, ambazo kwa sasa ni zaidi ya shilingi 4.5milioni. Bila hicho kiasi kukilipa kwa mara moja huwezi kujiunga na QNET. Wao watakwambia sio gharama za kujiunga bali ni pesa yako unayotumia kununua bidhaa au huduma za Qnet! (Hapo utaambiwa bidhaa zenyewe ni Saa ya mkononi, Pafyumu, kulala kwenye hoteli kali ya kitalii huko Asia nk.)

-Kamwe hawatakwambia kinagaubaga biashara yao kirahisi mtaani, lazima watakuita uje kwenye ofisi zao(ndani ya chumba maalum!), hapo watajipanga watu kadhaa kukufanyia 'brain washout' na kukupa maelezo marefu mazuri na matamu ya kukufanya uwe milionea kupitia Qnet kwa muda mfupi na bila kuhangaika kabisa, na hicho kitu watakifanya kwa ustadi mkubwa sana, kwa hatua au siku kadhaa kabla ya kukwambia utoe pesa kujiunga. (Wakati wote huo watakwambia hiyo ni secret opportunity, usiulize mtu mwingine yoyote wala kusema sema kwa watu ovyovyo!).

-Sasa ukishajiunga tu na Qnet kwa kutoa zaidi ya 4.5milion ndio akili inafunguka na kujua kuwa umelizwa au kugundua kuwa umelionea siyo kitu kirahisi kabisa, sasa mtu ndio anahangaika kutafuta 'wajinga' wengine kadhaa ili wajiunge kwenye mnyororo wake ili kuanza kufidia kile ulicholizwa, na hapo inakuwa ni suala la kufa na kupona.


Kwa leo niishie hapa......
 
Akija mdada mzuri ananihubiria hiyo network marketing yake mie nam-baharia kistaarabu..
 
Mkuu ubarikiwe sana sana hakika umepita mule mule.
Ulivyo eleza ndivyo ilivyo, mtu alie kwisha jiunga NINGUMU kukwambia ukweli maana wewe kwake tayari ni fursa ili arudishe fedha alizo zitoa na ukienda kwenye ofisi zao umeisha kama huna akili ya ziada. Wapo vizuri kwenye ushawishi.
 
Ukweli mkubwa kuliko wote ni huu, hakuna fursa yoyote halali ya kibiashara duniani inayoweza kirahisi kirahisi kumtajirisha mtu yoyote. Epuka kabisa kukimbilia kitu kinachoitwa 'Fursa ya kuweza kutajirika haraka au kirahisi', maana wewe ndio utageuzwa kuwa fursa.
 
MKUU,NAKUOMBA KWA NGUVU ZUIA HILI JAMBO AISEE,

NAKUOMBA TENA MKUU,MUAMBIE HUYO BINTI ASIFANYE HILO JAMBO,SIO JAMBO JEMA KABISA
Asante sana mkuu nitafanya hivyo. Dakika chache zilizopita sister katoka kunipigia, kumbe kuna pesa 4.5m walishalipa kwa ajili ya degree course(undergraduate) ya online inayoendeshwa na na University moja inaitwa Quest University ipo Malaysia( ambayo ni Education Institution ya iliyo chini ya hao Qnet). Mtoto wa sister yupo UD mwaka wa kwanza sasa anataka kusoma online degree nyingine through hao Qnet

Kanitumia risiti ya hela waliyolipa bank naona kama ni malipo ya manunuzi ya commodities yaani hata haieleweki. Sasa mtoto ndio anawashinikiza wazazi wajiunge kununua products ili eti watengeneze pesa!
 
Mkuu ubarikiwe sana sana hakika umepita mule mule.

Ukienda kwenye ofisi zao umeisha kama huna akili ya ziada. Wapi vizuri kwenye ushawishi.
Hao jamaa ni hatari.
Ni kikosi kazi kamili.
Huwa wanamsoma kwanza mtu anayeletwa kuja kupigwa somo la kujiunga. Wakijua wewe ni mtu wa kidini, basi watajipanga hadi angle za kidini, wakijua wewe ni mtu kisayansi wataweka kikosi cha watu wanaojua sayansi, kama wewe ni mtu wa kiheshima basi utashaanga unakutana na kikosi kazi za waheshimiwa siku hiyo.

Hapo ni mwendo wa Good morning!!!!!
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Duh [emoji2811]
Soon na wewe utakuwa muhanga wakitaka na wewe ujiunge, na naamini utaleta mrejesho hapa.
 
Huyo binti hapo ndio tayari keshalizwa na Qnet. Ndivyo inavyokuwaga hivyo.
Sasa ajipange kuwa mtumwa wa Qnet mazima, muda sio mrefu ataanza kukushawishi na wewe ujiunge ili kufidia au kurudisha au kuelekea naye kuusaka umilionea alioteshwa ndani ya ofisi za Qnet.
Pole sana kwa dada yetu, maisha ni kujifunza, na wengine hujifunza kwa kulizwa!

Qnet wamejipanga sana kuvuna pesa za watu kirahisi huku wakificha kivuli cha Pyramid scheme kwenye mwamvuli wa bidhaa na huduma fulani fulani zinazoweza kulipwa katika hiyo 4.5milioni mtu anazolipa.
 
Jibu ni NDIYO.
Ila wanatumia saikolojia kubwa sana kukuaminisha kuwa wewe ndie mnufaika zaidi kuliko pesa ambayo umewapelekea.
Dah kuna watu ni wapigaji professional aisee, tena hasa wazungu kitu illegal wanakitengeneza kinakua kama legit kabisa
 
Hao wazazi ni wajinga,samahani lkn.
 
Mi fursa zote naona ni upigaji tu maana kama fursa mara nyingi mtu anaifanya peke ake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…