Bibi kizee anyofolewa masikio na mtoto wake wa kumzaa wakati akiwa amelala

Bibi kizee anyofolewa masikio na mtoto wake wa kumzaa wakati akiwa amelala

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mkazi wa Kitongoji cha Kalilangwa Kijiji cha Mchangani Kata ya Ikola, Tarafa ya Karema Wilaya ya Tanganyika, Mkoa wa Katavi Winfrida Athanas (63) amenyofolewa masikio yote na mtoto wake wa kumzaa mwenyewe baada ya kumvizia wakati akiwa amelala usingizi chumbani mwake.

Tukio hilo la kusikitisha na la kikatili limetokea hapo juzi majira ya saa tano usiku chumbani kwa mama huyo alipokuwa amelala kitandani.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Ikola Mwela Mrugwa amesema mama huyo amenyofolewa masiko yake mawili na mtoto wake wa kumzaa mwenyewe aitwaye Michael Msapi (40).

Siku hiyo ya tukio mtuhumiwa Michael Msapi alimvizia mama yake mzazi wakati akiwa amelala usingizi chumbani mwake na ndipo alipoingia ndani ya chumba hicho na kumnyofoa masikio yake yote mawili kwa kutumia meno yake na kumsababishia mama huyo maumivu makali sana.

Baada ya kuwa amefanya ukatili huu kwa mama yake mzazi mhumiwa huyo alitokomea baada ya kuwa mama yake amepiga mayowe ya kuomba msaada.

Mwela Mnugwa amesema baada ya majirani kusikia mayowe hayo walifika haraka kwenye eneo hilo na kumchukua Winfrida na kumkimbiza haraka kwenye kituo cha Afya cha Karema ambako hadi sasa anaendelea kupatiwa matibabu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Ally Hamad Makame amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo limeripotiwa katika jeshi la Polisi.

Chanzo: Walter Mguluchuma, Katavi
 
Mkazi wa Kitongoji cha Kalilangwa Kijiji cha Mchangani Kata ya Ikola, Tarafa ya Karema Wilaya ya Tanganyika, Mkoa wa Katavi Winfrida Athanas (63) amenyofolewa masikio yote na mtoto wake wa kumzaa mwenyewe baada ya kumvizia wakati akiwa amelala usingizi chumbani mwake.

Tukio hilo la kusikitisha na la kikatili limetokea hapo juzi majira ya saa tano usiku chumbani kwa mama huyo alipokuwa amelala kitandani.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Ikola Mwela Mrugwa amesema mama huyo amenyofolewa masiko yake mawili na mtoto wake wa kumzaa mwenyewe aitwaye Michael Msapi (40).

Siku hiyo ya tukio mtuhumiwa Michael Msapi alimvizia mama yake mzazi wakati akiwa amelala usingizi chumbani mwake na ndipo alipoingia ndani ya chumba hicho na kumnyofoa masikio yake yote mawili kwa kutumia meno yake na kumsababishia mama huyo maumivu makali sana.

Baada ya kuwa amefanya ukatili huu kwa mama yake mzazi mhumiwa huyo alitokomea baada ya kuwa mama yake amepiga mayowe ya kuomba msaada.

Mwela Mnugwa amesema baada ya majirani kusikia mayowe hayo walifika haraka kwenye eneo hilo na kumchukua Winfrida na kumkimbiza haraka kwenye kituo cha Afya cha Karema ambako hadi sasa anaendelea kupatiwa matibabu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Ally Hamad Makame amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo limeripotiwa katika jeshi la Polisi.

Chanzo: Walter Mguluchuma, Katavi
Hayo yanawezekana huko Tanganyika, mtu badala unyofoe mapesa kwa kufanya kazi halali unanyofoa maskio ya mama yako?#*!
 
Unajua waganga wajanja Sana,ameshakuahidi mafanikio ambayo hawezi kukusaidia kwahiyo cha kufanya,anakutengenezea zengwe na jamhuri,halafu Muda WA kwenda kwake huna uko busy kupambana na jamhuri yeye anaendelea Kula maisha
 
Unajua waganga wajanja Sana,ameshakuahidi mafanikio ambayo hawezi kukusaidia kwahiyo cha kufanya,anakutengenezea zengwe na jamhuri,halafu Muda WA kwenda kwake huna uko busy kupambana na jamhuri yeye anaendelea Kula maisha
Vina akili sana hivi vijishikaji
 
Tukiwa huko huko Sumbawanga Kuna mganga baada ya kula hela nyingi za mteja wake aliamua kumpa mteja tukio ili asimsumbue Tena. Alimuambia mteja kua Kuna dawa moja tu imebaki pesa zianze kutiririka lakini kabla ya hiyo dawa tembea na binti yako mkubwa Mara nne. Siku ya kwanza mteja alimla binti bila tabu, binti akajua labda mzee alilewa, Mara ya pili hivyo hivyo, Mara ya tatu binti akamuambia Bibi yake. Bibi akakuza lile Jambo Hadi jamaa akatokomea kusikojulikana.
Biashara zake zikafa hatujui Kama yu hai au la.
 
Tukiwa huko huko Sumbawanga Kuna mganga baada ya kula hela nyingi za mteja wake aliamua kumpa mteja tukio ili asimsumbue Tena. Alimuambia mteja kua Kuna dawa moja tu imebaki pesa zianze kutiririka lakini kabla ya hiyo dawa tembea na binti yako mkubwa Mara nne. Siku ya kwanza mteja alimla binti bila tabu, binti akajua labda mzee alilewa, Mara ya pili hivyo hivyo, Mara ya tatu binti akamuambia Bibi yake. Bibi akakuza lile Jambo Hadi jamaa akatokomea kusikojulikana.
Biashara zake zikafa hatujui Kama yu hai au la.
Waganga washenzi sana asee😂
 
Back
Top Bottom