Biblia inasema Fungu la kumi apewe mlawi, Je hapa Tanzania kuna walawi? Je wachungaji ndio walawi ?

Agano jipya linafuatwa sema kuna mabadiliko yalitokea kutokana na kuwa na mapungufu ndio mana likaja jipya kuhusu fungu ka kumi hata agano jipya walitoa fungu la kumi soma waebrania 7:1_10,ni lazima utoe sehem ya kumi ya mapato yako sadaka kama fungu la kumi sadaka nyingine ni sehem ya maamuzi yako.lkn hii ni amri.
 
Agano jipya fungu la kumi.limekusudiwa kulitegemeza kanisa kwa hyo hutumika katk shughuli za kikanisa kutokana namakubaliano mchungaji hukusqnya sadaka zote na kuzigawa kutokana na mipango ya kanisa husika
 
Agano jipya fungu la kumi.limekusudiwa kulitegemeza kanisa kwa hyo hutumika katk shughuli za kikanisa kutokana namakubaliano mchungaji hukusqnya sadaka zote na kuzigawa kutokana na mipango ya kanisa husika

Taja mstari wa biblia unaothibitisha uliyoyaandika
 
Fungi la kumi kwa uhalisia wa sasa Bora upeleke kwenye watu wenye mahitaji muhimu hospitali watoto yatima na wajane sasa unapeleka fungi la kumi kanisani unakutana mchungaji ananywea mvinyo Haina maana

hata kwenye agano la kale fungu la kumi walipewa wenye uhitaji kama hao kabila la walawi ambao walikosa ardhi

Neno "Fungu la Kumi" katika Biblia linarejelea sehemu ya kumi ya mapato au mavuno ambayo Waisraeli walipaswa kutoa kama sadaka kwa Mungu. Hii ilikuwa sehemu ya sheria ya Agano la Kale na ilitolewa kwa Walawi, maskini, wageni, mayatima, na wajane.
 
Umejibu vyema.
Makanisa ya kipenteconste, maarufua kama makanisa ya kiroho hufundisha kuwa torati siyo kwa ajili ya kanisa la sasa na tumeokoka hivyo hatuko chini ya sheria. Lakini ukiangalia fungu la kumi ni torati. Nisaidie hapoo
 
Shukrani mkuu, hata mm naamini utoaji Kwa Mungu haufungwi na sheria yoyote ktk agano jipya! mtu anaweza toa apendavyo, yaweza kuwa zaidi ya asilimia 10 au chini ya 10 kadri ya moyo wa mtu unavyomtuma kumtolea Bwana.
Naam, uko sahihi kabisa kibiblia!
 
Wakuu kwahiyo tutoe zaka au tuache? Tunangoja majibu.
Tutafanya chochote mtachosema.
Tuache kabisa kufuata hiyo sheria au shinikizo. Hatufungwi na sheria ya agano la kale la kulazimishwa. Tutoe kadri moyo upendavyo, iwe vyote, nusu, robo au tusitoe kabisa (2 Kro 9:7), hakuna dhambi. Kumbuka hata tukibaki navyo bado ni vya Mungu, tunakuwa tunasimamia tu na kula vya Mungu wetu.

Na kumbuka kuwa yeyote anayemfuata Yesu ni kuhani au Mtumishi wa Mungu. Anaruhusiwa kula au kutoa vya Mungu kwa ajili ya kazi yake. Na kwa kuhitimisha hakuna yeyote anayeweza kufuata sheria ya zaka kwa unyoofu, kwa kutoa asilimia 10 kwa kila apatacho - si pesa tu. Hayupo!
 
Mlawi maana yake siyo priest.
Yeye ni msaidizi.
Kama kwa mfano waimba kwaya ni Walawi.
Mlawi siyo main actor.Mlawi ni supporting cast.
 
Umejibu vyema.
Makanisa ya kipenteconste, maarufua kama makanisa ya kiroho hufundisha kuwa torati siyo kwa ajili ya kanisa la sasa na tumeokoka hivyo hatuko chini ya sheria. Lakini ukiangalia fungu la kumi ni torati. Nisaidie hapoo
Halituhusu kabisa, soma posts zangu zingine huko nyuma. Fungu la 10 au zaka lilikuwa kwa ajili ya kuhifadhi chakula ghalani kwa ajili ya Walawi (makuhani) ambao hawakupata urithi wowote. Makabila mengine yote 11 yalipata urithi (hususan ardhi).
 
Lawi ni mmoja kati ya watoto wa Yakobo
Walawi ni uzao wa Lawi
Sasa hawa wachungaji wa leo nao ni watoto wa Yakobo?
Hapana, si Walawi. Tukimwamini na kumpokea Yesu Kristo tunakuwa wana wa Mungu (Yohana 1:12), si wana wa Lawi!
 
Mlawi maana yake siyo priest.
Yeye ni msaidizi.
Kama kwa mfano waimba kwaya ni Walawi.
Mlawi siyo main actor.Mlawi ni supporting cast.

Mlawi sio mtumishi wa Mungu. Mlawi ni mlawi... mtu wa kabila la Lawi...

muimba kwaya mweusi mnyakyusa anakuwaje kabila la mlawi ?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ