Bila aibu wala woga, CCM yaitangazia dunia kuwa hakuna Mtanzania mwenye uadilifu!

Bila aibu wala woga, CCM yaitangazia dunia kuwa hakuna Mtanzania mwenye uadilifu!

Je mlezi wa Watanzania kwa ujumla wao ni nani? Kumbuka katoto kanazaliwa leo kanaikuta CCM madarakani, kanakua CCM iko madarakani, kanaaanza shule CCM iko madarakani, anamaliza shule CCM iko madarakani, anaajiriwa CCM iko madarakani, anaoa CCM iko madarakani, anaanza kuwapata watoto wake CCM iko madarakani, anastaafu CCM iko madarakani...
Wazazi
 
Ni kweli, tumeitangazia dunia kuwa sisi sio lolote katika utendaji. Wanasubiri nini kuleta mawaziri toka mataifa mengine watuongoze..
Mbona unawataja mawaziri tu!! Serikali nzima akiwemo Rais , mbona Kenyatta yupo tukimwomba awe Rais wetu wa mkataba atakataa?
 
Je unaamini kuwa sisi Watanzania ni viumbe tofauti na binadamu wengine? Mifumo hiyo itawekwa na nani? Je kuna mfumo wowote hivi sasa unaoruhusu wizi na ulaji rushwa? Kama ni viongozi ndio wahusika, kwa nini hatuwabani?
Sisi watanzania ni waoga sana, hivyo hatuna uwezo wa kuwabana watawala kwa namna yoyote ile...huu ndio ukweli
 
Baada ya CCM kuitangazia dunia...
  • Kwamba Watanzania hatuna mwenye uwezo wa kusimamia uendeshaji wa chombo kama Bandari kwa uadilifu!
  • Kwamba Watanzania kwa ujumla wetu ni watu wasio na uaminifu katika utendaji wa kazi popote pale tulipo...
Aliyezindika Nchi alitumia zindiko Kali sana.Nakumbuka Paul Kagame alisema kuwa alipewa bandari ya Dar atailisha Tanzania Bure.unajiuliza yeye angefanyeje?

Jibu ni kwamba anagesimamia uadilifu.Shida ya sisi watanzania ni kukosa uzalendo na uadilifu.mtanzania ukimwajiri anawaza kukuibia TU!! Wameniliza kwa kweli.

Wamechukua ngorongoro wanataka na bandari.daah
 
Shida ya sisi watanzania ni kukosa uzalendo na uadilifu.
Mbona huku ni kutudhalilisha Watanzania kwa ujumla wetu?
Badala ya kusema sisi Watanzania kwa nini usiite koleo kwa jina lake, SISI WANA CCM?
mtanzania ukimwajiri anawaza kukuibia TU!! Wameniliza kwa kweli.
Tafadhali sema mwana CCM ukimwajiri anawaza kukuibia TU! Kwa bahati mbaya huu ukoo wa panya ndio huo huo umeng’ang’ania madaraka nchini kwa kutumia dola.
 
Kama mlivyosikia nchi yetu Kwa mwezi Sasa tunasakata la kuuzwa Kwa BANDARI zetu huko nyuma rasilimali nyingi zimeuzwa lakini tumewaachia watu wachache watusemee hawa watu wachache nao wamechoka ,Sasa Ombi langu watanzania Kwa makundi yenu tuokoe nchi yetu ,maana kuanzia kuvuja Kwa mkataba huu Rais amekaa kimya,Bunge limekwenda kuwasaliti wananchi ,mahakama ndio hiyo ambayo jaji anaongezewa muda kanakwamba wasomi wamekwisha ,

Shime watanzania dawa iliyobaki ni kuandamana popote ulipo Kwa kufunga,kuzungumza Kwa vijiwe vyote na maeneo mengine niwashukuru chama cha wanasheria TLS Kwa kuonesha hasira zao ,niwaombe walimu,manesi,wauguzi,mabaharia,wachumi,machinga wote tupaze sauti zetu Kwa nguvu zote ,kila siku wafanyakazi wanalalama mishahara midogo ,manesi na wauguzi fanyeni kweli ,katiba yetu inatutaka tulinde rasilimali zetu muda wa kulinda ni sasa yaani kama ni nafasi ni sasa.Tujiulize swali mbona wenzetu Zanzibar wanakatiba Yao ya 2010 Sisi tunashangaa nini!!! Kwa nini watanzania ni wabinafsi sana yaani watoto wetu wataishi vipi?Kwa nini hatuwazi kesho?

Mimi wiki hii nimesambaza vipeperushi vingi maeneo ya Lindi na mtwara juu ya BANDARI zetu kuuzwa
 

Attachments

  • 20230629_233351.jpg
    20230629_233351.jpg
    248.1 KB · Views: 2
  • 20230628_223109.jpg
    20230628_223109.jpg
    22.5 KB · Views: 2
  • tweeload_33d67792.mp4
    2.4 MB
Mambo ambayo mnazungumza huko makanisani mmeshindwa kujizuia sasa mnayaleta hadharani,mtajuta safar hii.

Too bad Samia is here to lead till 2030 Inshallah...

PENGO kama anaumia mwambien ajitie kitanzi.
 
Mbona wako Watanzania wengi tu huko nje wanasifika kwa utendaji wao na uwajibikaji? Kwa nini hilo halipo hapa ndani ya nchi, je mchawi wetu ni nani?
Hata huku ndani wapo, ila sasa nafasi kama ni za teuzi anayeteua atajuaje watu wote 60M huku hakuna mifumo ya kuwajua professionals wote?

Dawa ni kuwe na kuomba kama wenzetu Kenya, ndiyo sababu uchumi wao unakaribia kuwa mara mbili ya huu wetu pamoja na kuwa nchi yetu ina both comperative and competitive advantages...
 
Hizi tabia tunazo kweli. Lakini tunapaswa kuweka mifumo ya kuwadhibiti watu ili walete ufanisi.
Umesema hizi tabia kweli tunazo ! Sasa unategemea tujiwekee hiyo mifumo na sheria kama zile za China 🇨🇳 ?!!
 
Back
Top Bottom