Bila kukusudia Haji Manara ameitia hasara kubwa Simba, Inaugua ugonjwa wa Manara Syndrome

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ili kukabiliana na athari za kuondoka kwa Haji manara Simba walilazimika kuingia mifukoni ili kufanikisha Simba day. Manara effect iliwaandama na inazidi kuwaandama Simba. Kila wanachofanya wanafanya ili kuzifuta nyao za Manara lakini wanafanya hivyo kwa kutumia nguvu kubwa zaidi ili kumkaribia au kumzidi Manara.

Wali pump watu actively kwenda uwanjani siku ya Simba day. Kumleta mpaka Mpoto, Prof J, Masau Bwire, wakongo, Salama Ngale, nk, nk, nk, nk, nk,nk, ni kuonyesha namna Simba ilivyoathirika kwa kuondokewa na Manara. Manara alikuwa akiujaza uwanja kwa mike tu bila kupewa kitu chochote. Kuna watoto wadogo wengi sana mitaani waliipenda simba na kuichukia Yanga kutokana na Manara. Sasa hivi kuna watoto wengi wataipenda Yanga na kuichukia Simba kutokana na Manara. Hakuna ubishi Manara Mwenyezi Mungu amembariki./

Ushauri wangu Simba watume wazee wenye akili waende kumuona Haji. Simba itazidi kupoteana kama mashabiki watazidi kumkejeli Manara na mporomoko huu utakuwa dhahiri siku Simba ikifungwa na Yanga.
 
Wanajua hilo ila watakubishia...Makolo vichwa [emoji3447]+[emoji90]
 
Mwana utopolo mbona unahangaika na Simba, sisi mashabiki tulisha move on nyie utopolo simumemusaji Manara ka mshambuliaji wenu mtumieni vizuri Ili mfanye vizuri kwenye ligi kuu maana Rivers ya Nigeria iliwapiga kitu kizito uwanjani.
 
Koffi olomide Manara alichukua Mike Tu halafu akaja, hamkutoa hela, na kwa hiyo wakati hao watu wanakuja kwa ajili ya Clouds, walikuwa wanakuja kuingia bure, bila kuja kwa mapenzi yao na kutoa hela zao mfukoni mwao? Acha uongo hakuna aliye mkubwa sehemu yyte, mbna mmesema Nugaz ndo alijaza watazamaji wakati yeye yuko Simba, alikuwa anatumia ushawishi gani sasa, matokeo ya timu ndo yanawafanya watu wanakuja, fungweni hpo mechi 5 halafu mkamwambie Manara akahamasishe waje tuone!
 
sio kweli, kila aliyekuja pale simba day alikuwa anaugua Manara Syndrome, hakuna ambae alimtaja Manara pale hata mmoja, yaani ilikuwa kama vile "kufa na kupona" dhidi ya Manara. Yaani watu walikopa viingilio ili waende wakamkomeshe Haji.

Mimi siku ile nilienda pia Simba day, nilichokiona siku ile ni kwamba mashabiki wengi walivaa jezi za zamani za simba au fulana yoyote nyekundu au nyeupe. Wako wengine walivaa jezi za man u, liverpool, arsernal, Bayern,nk. Kwenye tamasha la wananchi watu wengi kama sio wote walivaa jezz mpya za yanga.
 
Kwa akili yako kati ya simba na Yanga timu ipi imeuza jezi zaidi?

Yanga mnaona labda mmelamba dume kumwajiri Haji Manara, time will tell, mtamfukuza kama mbwa koko!
 
Uliona wamevaa jezi za zamani Kama hizi, eti? Usiwe unajipiga dongo mwenyewe maksudi!View attachment 1949670
 
Acha uongo nilikuwa uwanjani tena nilikaa VIP B mashabiki wote walikuwa na jezi mpya Hadi wadada walivaa jezi za kike hyo kusoma jezi za zamani si kweli tena ngoja nitafte picha nilizopiga uwanja wa taifa, kwanini unadaganya mchana kweupe for whose benefits why lying.
Hafu huyo mzungu pori hata hakutamkwa hata na mtu yoyote tulikuwa na vibe la simba day tena uzuri tulitumia wasanii wetu wadogo na shoo ilibamba kuliko nyie mulimuleta koffi Olomide ambaye performance yake ilikuwa ndogo.
Shida muliyo nayo Yanga ni ku invest kwenye propoganda ndio maana mumetolewa hatua za awali kabisa, Yani huyo manara ndio nembo yenu badala ya ushindi, nyie ni useless aisee, dundahead
 
Shabiki wa kweli huenda uwanjani kwa kuvutiwa na team inavofanya vizuri na sio mtu yoyote team ikiboronga hamna shabiki atakayejichosha kwenda uwanjjani.
 
Nimeshampa ya kichwa mkuu post namba 28, atuletee majibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…