Bila kwanza Hamas na Fatah kumaliza Tofauti zao, Hakuna Palestine moja na tulivu

Bila kwanza Hamas na Fatah kumaliza Tofauti zao, Hakuna Palestine moja na tulivu

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Fatah na Hamasi ni mahasimu wa kisiasa wa kihistoria. Yote yanayotokea huko hususani Ghaza kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya mgawanyiko uliopo baina yao wenyewe. Ni ngumu sana kupata suluhu ya mgogoro huu japo inawezekana. Hivi inawezekanaje, Ukingo wa Magharibi (west bank)kuna serikali yake inayoongozwa na Fatah chini ya Mahmud Abas na kule Ghaza kuna serikali yake inayoongozwa na Hamasi chini ya Ismail Hanniyeh. Na kila upande una mawaziri wake.

Ni nani baina ya mahasimu hawa waawili anawakilisha maslahi mapana ya wa Palestine wote?

Mgawanyiko miongoni mwa Jumuiya za kimataifa, na mataifa duniani yanakoleza moto wa mgawanyiko kwenye mgogoro huu, kwa wao kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa na kuwafadhili kwa hali na mali, hali ambayo inakoleza uhasama, vita, mauaji na kurefusha zaidi upatikanaji wa suluhu ya kudumu katika eneo hili muhimu la mashariki ya kati.
Uvamizi na uchokozi wa Hamasi dhidi ya Israel hivi karibuni ni matokeo ya ufadhili wa mataifa ya ulimwengu na kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa yaani Hamas na Fatah.

Bila kwanza kuwaweka chini na kuwapatanisha Hamasi na Fataha, ni ndoto kuwa na Taifa la Palestine, ispokua Taifa la Ghaza na Taifa la Ukingo wa Magharibi.

Wasalam...
 
Fatah na Hamasi ni mahasimu wa kisiasa wa kihistoria. Yote yanayotokea huko hususani Ghaza kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya mgawanyiko uliopo baina yao wenyewe. Ni ngumu sana kupata suluhu ya mgogoro huu japo inawezekana. Hivi inawezekanaje, Ukingo wa Magharibi (west bank)kuna serikali yake inayoongozwa na Fatah chini ya Mahmud Abas na kule Ghaza kuna serikali yake inayoongozwa na Hamasi chini ya Ismail Hanniyeh. Na kila upande una mawaziri wake.

Ni nani baina ya mahasimu hawa waawili anawakilisha maslahi mapana ya wa Palestine wote?

Mgawanyiko miongoni mwa Jumuiya za kimataifa, na mataifa duniani yanakoleza moto wa mgawanyiko kwenye mgogoro huu, kwa wao kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa na kuwafadhili kwa hali na mali, hali ambayo inakoleza uhasama, vita, mauaji na kurefusha zaidi upatikanaji wa suluhu ya kudumu katika eneo hili muhimu la mashariki ya kati.
Uvamizi na uchokozi wa Hamasi dhidi ya Israel hivi karibuni ni matokeo ya ufadhili wa mataifa ya ulimwengu na kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa yaani Hamas na Fatah.

Bila kwanza kuwaweka chini na kuwapatanisha Hamasi na Fataha, ni ndoto kuwa na Taifa la Palestine, ispokua Taifa la Ghaza na Taifa la Ukingo wa Magharibi.

Wasalam...

Ni watu wangapi watakaofufuliwa waishi mbinguni?​

Biblia inaonyesha kwamba watu 144,000 watafufuliwa waishi mbinguni. (Ufunuo 7:4)
Umo humu mtoa maada?
 
Fatah na Hamasi ni mahasimu wa kisiasa wa kihistoria. Yote yanayotokea huko hususani Ghaza kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya mgawanyiko uliopo baina yao wenyewe. Ni ngumu sana kupata suluhu ya mgogoro huu japo inawezekana. Hivi inawezekanaje, Ukingo wa Magharibi (west bank)kuna serikali yake inayoongozwa na Fatah chini ya Mahmud Abas na kule Ghaza kuna serikali yake inayoongozwa na Hamasi chini ya Ismail Hanniyeh. Na kila upande una mawaziri wake.

Ni nani baina ya mahasimu hawa waawili anawakilisha maslahi mapana ya wa Palestine wote?

Mgawanyiko miongoni mwa Jumuiya za kimataifa, na mataifa duniani yanakoleza moto wa mgawanyiko kwenye mgogoro huu, kwa wao kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa na kuwafadhili kwa hali na mali, hali ambayo inakoleza uhasama, vita, mauaji na kurefusha zaidi upatikanaji wa suluhu ya kudumu katika eneo hili muhimu la mashariki ya kati.
Uvamizi na uchokozi wa Hamasi dhidi ya Israel hivi karibuni ni matokeo ya ufadhili wa mataifa ya ulimwengu na kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa yaani Hamas na Fatah.

Bila kwanza kuwaweka chini na kuwapatanisha Hamasi na Fataha, ni ndoto kuwa na Taifa la Palestine, ispokua Taifa la Ghaza na Taifa la Ukingo wa Magharibi.

Wasalam...

Divide and rule,acha wa bomolewe vzr mpaka wawe wayahudi na waombe uraia wa israel tofauti na hapo hapana salama kwao.
 
Fatah na Hamasi ni mahasimu wa kisiasa wa kihistoria. Yote yanayotokea huko hususani Ghaza kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya mgawanyiko uliopo baina yao wenyewe. Ni ngumu sana kupata suluhu ya mgogoro huu japo inawezekana. Hivi inawezekanaje, Ukingo wa Magharibi (west bank)kuna serikali yake inayoongozwa na Fatah chini ya Mahmud Abas na kule Ghaza kuna serikali yake inayoongozwa na Hamasi chini ya Ismail Hanniyeh. Na kila upande una mawaziri wake.

Ni nani baina ya mahasimu hawa waawili anawakilisha maslahi mapana ya wa Palestine wote?

Mgawanyiko miongoni mwa Jumuiya za kimataifa, na mataifa duniani yanakoleza moto wa mgawanyiko kwenye mgogoro huu, kwa wao kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa na kuwafadhili kwa hali na mali, hali ambayo inakoleza uhasama, vita, mauaji na kurefusha zaidi upatikanaji wa suluhu ya kudumu katika eneo hili muhimu la mashariki ya kati.
Uvamizi na uchokozi wa Hamasi dhidi ya Israel hivi karibuni ni matokeo ya ufadhili wa mataifa ya ulimwengu na kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa yaani Hamas na Fatah.

Bila kwanza kuwaweka chini na kuwapatanisha Hamasi na Fataha, ni ndoto kuwa na Taifa la Palestine, ispokua Taifa la Ghaza na Taifa la Ukingo wa Magharibi.

Wasalam...

Kwanza, sentensi yako ya mwisho ina ukweli kwamba bila wao kupatana hakuna taifa la Palestina.

Kuna mambo mengi sana ima umeshindwa kuyaeleza au pengine kutoyaelewa au kutotaka kuyaelewa.

Ugomvi wa Hamas na Fataj si wa Kihistoria! Hamas imeanzishwa 1987, vipi unaweza kuita hilo ni jambo la Historia?

Ukweli wa sentensi yako ya mwisho ni kwamba Israel ndiyo inataka kuwepo Fatah na Hamas ili wasiweze kudai uwepo wa two states solution. Israel inasema wataongea na nani kuhusu state ya Palestina?

Ugomvi wa Fatah na Hamas una mambo mawili makubwa. Kwanza, Hamas walichoshwa na mazungumzo yasiyo na mwisho au uelekeo ya Fatah.

Pili, Hamas walichoshwa na rushwa iliyotamalaki ndani ya Fatah pesa zikipelekwa Paris , Swiss na kweingineko.

Mwaka 2006 Hamas ilishinda uchaguzi wa Palestina, Rais Jimmy Carter, mwakilishi wa Marekani pamoja na waangalizi wa kimataifa walithibitisha. Marekani na nchi za Ulaya walikataa kwasababu walitaka Fatah na si Hamas.

Israel ikachukua fursa hiyo kuwafungia ' Hamas pale Gaza' ili wasishirikiane na Fatah.

Hamas walishinda uchaguzi kwasababu pesa zote walizopata walizielekeza katika ujenzi wa shule na Hospitali na kutoa huduma za Maji, umeme na za kijaamii kusaidi wananchi.
Hivyo, chimbuko la Hamas ni pamoja na Rushwa ndani ya Fatah na kusua sua majadiliano

Kosa la Israel la kuita Hamas magaidi na kwamba wanawafungia Gaza kwa kila kitu ndilo limezua haya yote.

Na mwisho, inaonekana una meza habari bila kuchuja. Unaposema ''uchokozi' wa Hamas unaaminisha kabla ya Octoba 07 hali ilikuwa nzuri sana Palestina.

Hujui Gaza ni kambi za wakimbizi na kwamba masetla wanawapora Wapalestina ardhi na kuwaaua kila siku.

Mwaka 1948 Israel iliwapiga Wapalestina na kuwaondoa katika ardhi yao kwa staili hii hii ya Hamas (Nakba)
Huu mgogoro ni wa miaka 17 ya Hamas kutawala , 56 hadi 75 si wa wiki tatu

Mwaka jana peke Wapalestina 255 wameuawa na Israel, unajua hilo?

Hebu rejea mwaka huu kabla ya Octoba 07 Israel imeshambulia Gaza mara ngapi.
Unajua viongozi wangapi wa Hamas wameuawa na Israel achilia mbali Raia!

Kabla hujaandika mada fanya utafiti, halafu usitumie headlines za TV na Magazeti.
Usifunge akili yako kwa BBC au CNN au Al Jazeera. haya mambo ni mazito sana kuliko unavyo yaona.

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Kwanza, sentensi yako ya mwisho ina ukweli kwamba bila wao kupatana hakuna taifa la Palestina.

Kuna mambo mengi sana ima umeshindwa kuyaeleza au pengine kutoyaelewa au kutotaka kuyaelewa.

Ugomvi wa Hamas na Fataj si wa Kihistoria! Hamas imeanzishwa 1987, vipi unaweza kuita hilo ni jambo la Historia?

Ukweli wa sentensi yako ya mwisho ni kwamba Israel ndiyo inataka kuwepo Fatah na Hamas ili wasiweze kudai uwepo wa two states solution. Israel inasema wataongea na nani kuhusu state ya Palestina?

Ugomvi wa Fatah na Hamas una mambo mawili makubwa. Kwanza, Hamas walichoshwa na mazungumzo yasiyo na mwisho au uelekeo ya Fatah.

Pili, Hamas walichoshwa na rushwa iliyotamalaki ndani ya Fatah pesa zikipelekwa Paris , Swiss na kweingineko.

Mwaka 2006 Hamas ilishinda uchaguzi wa Palestina, Rais Jimmy Carter, mwakilishi wa Marekani pamoja na waangalizi wa kimataifa walithibitisha. Marekani na nchi za Ulaya walikataa kwasababu walitaka Fatah na si Hamas.

Israel ikachukua fursa hiyo kuwafungia ' Hamas pale Gaza' ili wasishirikiane na Fatah.

Hamas walishinda uchaguzi kwasababu pesa zote walizopata walizielekeza katika ujenzi wa shule na Hospitali na kutoa huduma za Maji, umeme na za kijaamii kusaidi wananchi.
Hivyo, chimbuko la Hamas ni pamoja na Rushwa ndani ya Fatah na kusua sua majadiliano

Kosa la Israel la kuita Hamas magaidi na kwamba wanawafungia Gaza kwa kila kitu ndilo limezua haya yote.

Na mwisho, inaonekana una meza habari bila kuchuja. Unaposema ''uchokozi' wa Hamas unaaminisha kabla ya Octoba 07 hali ilikuwa nzuri sana Palestina.

Hujui Gaza ni kambi za wakimbizi na kwamba masetla wanawapora Wapalestina ardhi na kuwaaua kila siku.

Mwaka 1948 Israel iliwapiga Wapalestina na kuwaondoa katika ardhi yao kwa staili hii hii ya Hamas (Nakba)
Huu mgogoro ni wa miaka 17 ya Hamas kutawala , 56 hadi 75 si wa wiki tatu

Mwaka jana peke Wapalestina 255 wameuawa na Israel, unajua hilo?

Hebu rejea mwaka huu kabla ya Octoba 07 Israel imeshambulia Gaza mara ngapi.
Unajua viongozi wangapi wa Hamas wameuawa na Israel achilia mbali Raia!

Kabla hujaandika mada fanya utafiti, halafu usitumie headlines za TV na Magazeti.
Usifunge akili yako kwa BBC au CNN au Al Jazeera. haya mambo ni mzaito sana kuliko unavyo yaona.

JokaKuu Pascal Mayalla
Asante sana Mkuu Nguruvi3
P
 
Kwanza, sentensi yako ya mwisho ina ukweli kwamba bila wao kupatana hakuna taifa la Palestina.

Kuna mambo mengi sana ima umeshindwa kuyaeleza au pengine kutoyaelewa au kutotaka kuyaelewa.

Ugomvi wa Hamas na Fataj si wa Kihistoria! Hamas imeanzishwa 1987, vipi unaweza kuita hilo ni jambo la Historia?

Ukweli wa sentensi yako ya mwisho ni kwamba Israel ndiyo inataka kuwepo Fatah na Hamas ili wasiweze kudai uwepo wa two states solution. Israel inasema wataongea na nani kuhusu state ya Palestina?

Ugomvi wa Fatah na Hamas una mambo mawili makubwa. Kwanza, Hamas walichoshwa na mazungumzo yasiyo na mwisho au uelekeo ya Fatah.

Pili, Hamas walichoshwa na rushwa iliyotamalaki ndani ya Fatah pesa zikipelekwa Paris , Swiss na kweingineko.

Mwaka 2006 Hamas ilishinda uchaguzi wa Palestina, Rais Jimmy Carter, mwakilishi wa Marekani pamoja na waangalizi wa kimataifa walithibitisha. Marekani na nchi za Ulaya walikataa kwasababu walitaka Fatah na si Hamas.

Israel ikachukua fursa hiyo kuwafungia ' Hamas pale Gaza' ili wasishirikiane na Fatah.

Hamas walishinda uchaguzi kwasababu pesa zote walizopata walizielekeza katika ujenzi wa shule na Hospitali na kutoa huduma za Maji, umeme na za kijaamii kusaidi wananchi.
Hivyo, chimbuko la Hamas ni pamoja na Rushwa ndani ya Fatah na kusua sua majadiliano

Kosa la Israel la kuita Hamas magaidi na kwamba wanawafungia Gaza kwa kila kitu ndilo limezua haya yote.

Na mwisho, inaonekana una meza habari bila kuchuja. Unaposema ''uchokozi' wa Hamas unaaminisha kabla ya Octoba 07 hali ilikuwa nzuri sana Palestina.

Hujui Gaza ni kambi za wakimbizi na kwamba masetla wanawapora Wapalestina ardhi na kuwaaua kila siku.

Mwaka 1948 Israel iliwapiga Wapalestina na kuwaondoa katika ardhi yao kwa staili hii hii ya Hamas (Nakba)
Huu mgogoro ni wa miaka 17 ya Hamas kutawala , 56 hadi 75 si wa wiki tatu

Mwaka jana peke Wapalestina 255 wameuawa na Israel, unajua hilo?

Hebu rejea mwaka huu kabla ya Octoba 07 Israel imeshambulia Gaza mara ngapi.
Unajua viongozi wangapi wa Hamas wameuawa na Israel achilia mbali Raia!

Kabla hujaandika mada fanya utafiti, halafu usitumie headlines za TV na Magazeti.
Usifunge akili yako kwa BBC au CNN au Al Jazeera. haya mambo ni mzaito sana kuliko unavyo yaona.

JokaKuu Pascal Mayalla
kwani historia ni nini hata kama Hamasi imeanzishwa 1987 na Fatah ikaanzishwa 2000 au hata 2005?
Huku kwetu pia CCM ni ya 1977 na Chadema ya 1990s na ni mahasimu wa kisiasa wa kihistoria nchini Tz.

sijaelewa unaiunga mkono Israel na nia yao ya kutaka pasiwepo na Palestine, bali Ghaza na west bank au unatoa wito Fatah na Hamasi wamalize tofauti zao waweza na nguvu na kauli moja ya kudai Taifa la Palestine au unaunga mkono Ghaza na Israel kuendelea kumwagwa damu au mambo yabaki vivyo hivyo?

Au unang'ang'ana na historia ya waliuawa wangapi juzi na Hamas, jana wa ngapi na Israel bila kuona namna gani mafarakano haya yanaweza kuhitimishwa kwa Amani?

Unapenda na kuyaelewa vema sana mabandiko ya Pascal Mayalla eehh,
hata mimi hakika nayakubali mno aise hapo tupo pamoja sana...

Hivi ni wap duniani hakuna Rushwa, hakuna upungufu au kasoro za kimaadili au kasoro katika huduma za kijamii, uchumi na siasa?

Kwani ukiitwa gaidi kwa mathalani kwa kulinganisha tabia, matendo na mtindo wa maisha yako na tabia za magaidi unakasirika na kuleta fujo?
Unasema kosa la Israel ni kuita Hamasi magaidi?
Mbona humu nchini Tz watu huitana manyumbu, mafisadi, majizi, ufipa, interahamwe, Kambale, Jiwe, buku saba, Lumumba na mambo yanakwenda vizur tu....
Au hao walioitwa magaidi na Israel ni magaidi kweli?

Sasa nadhani unaelewa madhara ya kukata tamaa, kutokua na ustahimilivu na subiira na hicho unachoita Hamasi kuchoshwa na hali ya rushwa na mazungumzo yasio isha.
Kinachotokea hivi sasa ndio gharama tena ni kidogo tu , ya hicho unachoita kuchoshwa na rushwa na mazungumzo yasio isha.

Watoto, wamama, wazee, wafa kila leo miundombinu kuharibiwa kwa uchovu wa watu wachache na kutokua na subra.....
Kuhesabu wapalestina wangapi wameuawa tangu lini au waisrael wameuawa wangapi au wamerusha makombora mangapi wap, hakutasadia chochote....
Yaliyopita si ndwele tugange ya sasa na yajayo......

Ni Imani yangu, Hamasi na Fataha wakiketi chini wakaelewana na kua sauti na kitu kimoja kama wapalestina, kunaweza kua mwanzo mujarabu sana wa kupatikana Suluhu ya kudumu mashariki ya kati..

Dunia kuchukua upande miongoni mwa Fatah au Hamasi ni kuchochea Moto wa vita Middle East...
 
sijaelewa unaiunga mkono Israel na nia yao ya kutaka pasiwepo na Palestine, bali Ghaza na west bank au unatoa wito Fatah na Hamasi wamalize tofauti zao waweza na nguvu na kauli moja ya kudai Taifa la Palestine au unaunga mkono Ghaza na Israel kuendelea kumwagwa damu au mambo yabaki vivyo hivyo?
Na hutaelewa kwasababu naliangalia tatizo la middle east katika historical context.
Naliangalia kwa facts na siyo fanaticism .
Hivi ni wap duniani hakuna Rushwa, hakuna upungufu au kasoro za kimaadili au kasoro katika huduma za kijamii, uchumi na siasa?
Hapa unapaswa kujua tunaongelea rushwa ya namna gani.
Unajua tofauti ya petty corruptions na Grand corruption? Unajua Fatah ilikuwa corruption ya namna gani?
Kwani ukiitwa gaidi kwa mathalani kwa kulinganisha tabia, matendo na mtindo wa maisha yako na tabia za magaidi unakasirika na kuleta fujo?
Hujaelewa! kitendo cha Israel, Marekani na nchi za Ulaya kuita Hamas gaidi kilimaanisha hawawezi kukaa pamoja nao kujadili chochote. Hilo likawalazimu Israel wawaweke katika ''kifungo' kwasababu hakuna maongezi.

Israel ikaona raha kwasababu imewatenga Gaza na West Bank. Kukawa na Palestina ya Ismail Hanniya na ya Mahmoud Abbas. Kwa miaka 17 hakuna mazungumzo kwasababu Israel inasema, itaongeaje na Fatah wakati kuna magaidi wa Hamas! Hilo likatoa nafasi ya Hamas kujijenga.

Tazama Afghanistan, Marekani walipotawala Talibani walikuwa magaidi. Mwisho wa siku Marekani iliona suluhu ni kuongea nao kwasababu kuwaacha msituni ni sawa na 'kuongea na kitu zero''. Trump aliwaita.

Baada ya US kuondoka Taliban kama serikali inawajibika katika sheria za Kimataifa.
Japo kuna nafuu kidogo kuliko hata wakati US wakiwepo, kwasababu kuna watu wa kuongea nao si wale wa msituni
Kinachotokea hivi sasa ndio gharama tena ni kidogo tu , ya hicho unachoita kuchoshwa na rushwa na mazungumzo yasio isha.
Ndiyo maana nakuambia kwamba hujui haya mambo.
Palestina wamelipa gharama na wanalipa gharama za damu kwa miaka 75. Wewe unalijua tatizo Oct 07 2023.
Ni Imani yangu, Hamasi na Fataha wakiketi chini wakaelewana na kua sauti na kitu kimoja kama wapalestina, kunaweza kua mwanzo mujarabu sana wa kupatikana Suluhu ya kudumu mashariki ya kati..
Tatizo si Fatah au Hamas! mbona huelewi?
Hebu jiulize yale makambi ya Jenin na Nablus yametoikeaje? Kwanini kuna Jerusalem Mashariki na Magharibi
Jiulize kwanini kuna Gaza strip na west bank?

Jiulize kwanini kuna wakimbizi wa Palestina Jordan wengi sawa na wananchi wa Jordan?
Jiulize kwanini kuliwa na Yom Kippur? Jiulize Nakba ni kitu gani?
Jiulize kwanini kuna Christian, Orthodox, Muslims, Jews katika kaeneo kadogo tu!
Kuna dots nyingi sana za kuunganisha, usikomalie ubishi kwa kitu usichokielewa.

Mwisho
Nakushauri uende kwenye KAVAZI la digital la Dr Salim Ahmed Salim ( ni bureee kabisa mtandaoni) ingia home page, chagua 'Digital archieves' halafu chagua academic paper halafu tatufa paper ya Dr SAS aliyowakilisha Columbia University. Tahadhari, imeandikwa kwa lugha kubwa kama kuna tatizo tuwasiliane.

Ukimaliza kusoma urudi hapa kwa majadiliano.

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Na hutaelewa kwasababu naliangalia tatizo la middle east katika historical context.
Naliangalia kwa facts na siyo fanaticism .

Hapa unapaswa kujua tunaongelea rushwa ya namna gani.
Unajua tofauti ya petty corruptions na Grand corruption? Unajua Fatah ilikuwa corruption ya namna gani?

Hujaelewa! kitendo cha Israel, Marekani na nchi za Ulaya kuita Hamas gaidi kilimaanisha hawawezi kukaa pamoja nao kujadili chochote. Hilo likawalazimu Israel wawaweke katika ''kifungo' kwasababu hakuna maongezi.

Israel ikaona raha kwasababu imewatenga Gaza na West Bank. Kukawa na Palestina ya Ismail Hanniya na ya Mahmoud Abbas. Kwa miaka 17 hakuna mazungumzo kwasababu Israel inasema, itaongeaje na Fatah wakati kuna magaidi wa Hamas! Hilo likatoa nafasi ya Hamas kujijenga.

Tazama Afghanistan, Marekani walipotawala Talibani walikuwa magaidi. Mwisho wa siku Marekani iliona suluhu ni kuongea nao kwasababu kuwaacha msituni ni sawa na 'kuongea na kitu zero''. Trump aliwaita.

Baada ya US kuondoka Taliban kama serikali inawajibika katika sheria za Kimataifa.
Japo kuna nafuu kidogo kuliko hata wakati US wakiwepo, kwasababu kuna watu wa kuongea nao si wale wa msituni

Ndiyo maana nakuambia kwamba hujui haya mambo.
Palestina wamelipa gharama na wanalipa gharama za damu kwa miaka 75. Wewe unalijua tatizo Oct 07 2023.

Tatizo si Fatah au Hamas! mbona huelewi?
Hebu jiulize yale makambi ya Jenin na Nablus yametoikeaje? Kwanini kuna Jerusalem Mashariki na Magharibi
Jiulize kwanini kuna Gaza strip na west bank?

Jiulize kwanini kuna wakimbizi wa Palestina Jordan wengi sawa na wananchi wa Jordan?
Jiulize kwanini kuliwa na Yom Kippur? Jiulize Nakba ni kitu gani?
Jiulize kwanini kuna Christian, Orthodox, Muslims, Jews katika kaeneo kadogo tu!
Kuna dots nyingi sana za kuunganisha, usikomalie ubishi kwa kitu usichokielewa.

Mwisho
Nakushauri uende kwenye KAVAZI la digital la Dr Salim Ahmed Salim ( ni bureee kabisa mtandaoni) ingia home page, chagua 'Digital archieves' halafu chagua academic paper halafu tatufa paper ya Dr SAS aliyowakilisha Columbia University. Tahadhari, imeandikwa kwa lugha kubwa kama kuna tatizo tuwasiliane.

Ukimaliza kusoma urudi hapa kwa majadiliano.

JokaKuu Pascal Mayalla

..umenikumbusha kuingia kwenye digital archive ya Salim Salim.🙏🏾🙏🏾
 
..umenikumbusha kuingia kwenye digital archive ya Salim Salim.🙏🏾🙏🏾
Mkuu kuna baadhi ya mambo sijayaona naona TISS wameyaondoa. Pitia kavazi ni muhimu na zuri kwakweli
Kuna mengi sana ya kujifunza hasa paper zake.
 
Fatah na Hamasi ni mahasimu wa kisiasa wa kihistoria. Yote yanayotokea huko hususani Ghaza kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya mgawanyiko uliopo baina yao wenyewe. Ni ngumu sana kupata suluhu ya mgogoro huu japo inawezekana. Hivi inawezekanaje, Ukingo wa Magharibi (west bank)kuna serikali yake inayoongozwa na Fatah chini ya Mahmud Abas na kule Ghaza kuna serikali yake inayoongozwa na Hamasi chini ya Ismail Hanniyeh. Na kila upande una mawaziri wake.

Ni nani baina ya mahasimu hawa waawili anawakilisha maslahi mapana ya wa Palestine wote?

Mgawanyiko miongoni mwa Jumuiya za kimataifa, na mataifa duniani yanakoleza moto wa mgawanyiko kwenye mgogoro huu, kwa wao kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa na kuwafadhili kwa hali na mali, hali ambayo inakoleza uhasama, vita, mauaji na kurefusha zaidi upatikanaji wa suluhu ya kudumu katika eneo hili muhimu la mashariki ya kati.
Uvamizi na uchokozi wa Hamasi dhidi ya Israel hivi karibuni ni matokeo ya ufadhili wa mataifa ya ulimwengu na kuchagua upande miongoni mwa mahasimu hawa yaani Hamas na Fatah.

Bila kwanza kuwaweka chini na kuwapatanisha Hamasi na Fataha, ni ndoto kuwa na Taifa la Palestine, ispokua Taifa la Ghaza na Taifa la Ukingo wa Magharibi.

Wasalam...
Uchambuzi mzuri sana wa kusomi
 
Back
Top Bottom