DOKEZO Bila Rushwa ya 50,000 au 100,000 kwa Viongozi wa viwanda vya Mo Dewji hupati kazi

DOKEZO Bila Rushwa ya 50,000 au 100,000 kwa Viongozi wa viwanda vya Mo Dewji hupati kazi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Ndugu zangu, Kuna mambo ya ajabu yanafanyika kwenye ajira za vibarua katika viwanda vya METL chini ya MO DEWJI. Kuna wanaojiita supervisors wa viwanda na wahusika wa kuajiri wafanyakazi na vibarua wamekuwa na utaratibu kuchukua rushwa ya Tsh. 50,000 hadi 100,000 kwa kila anayetaka kazi.

Kuna watu wengi wanajikuta wanaliwa pesa zao na kazi hawapati, wengine wanaingia kazini kwa ahadi ya malipo ya Tsh. 7000 kwa siku lakini zamu zao za kuingia kazi hazina mtiririko mzuri kwasababu wasimamizi hao wameshapokea pesa za watu wengi sana kwahiyo wanachokifanya ni kupanga zamu kutegemea na idadi ya pesa za watu walizochukua na sio idadi ya watu.

Sidhani kama MO ana taarifa kuhusu hili. Taasisi za Rushwa zifanyie kazi suala hili haraka kwasababu watu wengi wanaumizwa pale kila siku wanachukua hizo pesa kwa waombaji wapya.
 
Ungetaja jina la kiwanda tungekusaidia kwa njia moja au nyingine.
 
Bad news travels fast. Fake news travels faster! Propaganda, misinformation and disinformation controls the narrative nowadays because the truth doesn’t sell anymore. Verify before you amplify your stories!
Says, B.Gonzalez

Sent from my SM-G960F using JamiiForums mobile app
 
Bad news travels fast. Fake news travels faster! Propaganda, misinformation and disinformation controls the narrative nowadays because the truth doesn’t sell anymore. Verify before you amplify your stories!
Says, B.Gonzalez

Sent from my SM-G960F using JamiiForums mobile app
sasa wale vibarua wana elewaje ulicho andika?
usisahau kuna wanao jinufaisha kupitia matatizo ya wengi,
 
Back
Top Bottom