Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 593
- 1,376
Wakuu salam,
Bili za mwezi Februari zimetoka, jamani huku kwetu Mbezi Beach kila mtu anashangaa ubambikaji wa bili hizi. Yaani kwa kila mtu bili imeshoot kuliko kawaida wakati matumizi ni ya kawaida, sio kwamba ni shule au labda unafanya biashara ya kuuza maji.
Tena cha kushangaza zaidi ni kuwa maji yamekuwa ni ya kusuasua zana, mnakaa siku tatu nne hakuna maji, maji yakitoka presha ni ndogo sana yaani hata hayapandi kwenye matenki. DAWASA walitoa ushauri watu tuweke pump za maji lakini kutokana na presha ilivyo ndogo hata kuwa na pump ni kituko, maana zinakosa cha kubust, halafu eti bili inakuja umetumia unit 40, 50! Kivipi? Kwa maji yapi ya kufikia unit hizo?
Imagine kwenye nyumba mko watano, watatu hamshindi nyumbani, kuna safari za kufanya msiwepo nyumbani kwa wiki au hata zaidi, maji yanasua sua unaweza kusema kwa mwezi mmepata maji siku nzima bila kukata labda siku 3 halafu bili inakuja unit 40+, inaingia akilini kweli? Wizara ya Maji
Kama ndio mita zinahesabu upepo hii ya sasa imetia fora, itakuwa pump zinapigwa na kimbuka huko chini mpaka kupata units zote hizo.
Kwa upande wenu hali ikoje Wakuu? Bili zimekuja na uhalisia?
Wizara ya Maji
Bili za mwezi Februari zimetoka, jamani huku kwetu Mbezi Beach kila mtu anashangaa ubambikaji wa bili hizi. Yaani kwa kila mtu bili imeshoot kuliko kawaida wakati matumizi ni ya kawaida, sio kwamba ni shule au labda unafanya biashara ya kuuza maji.
Tena cha kushangaza zaidi ni kuwa maji yamekuwa ni ya kusuasua zana, mnakaa siku tatu nne hakuna maji, maji yakitoka presha ni ndogo sana yaani hata hayapandi kwenye matenki. DAWASA walitoa ushauri watu tuweke pump za maji lakini kutokana na presha ilivyo ndogo hata kuwa na pump ni kituko, maana zinakosa cha kubust, halafu eti bili inakuja umetumia unit 40, 50! Kivipi? Kwa maji yapi ya kufikia unit hizo?
Imagine kwenye nyumba mko watano, watatu hamshindi nyumbani, kuna safari za kufanya msiwepo nyumbani kwa wiki au hata zaidi, maji yanasua sua unaweza kusema kwa mwezi mmepata maji siku nzima bila kukata labda siku 3 halafu bili inakuja unit 40+, inaingia akilini kweli? Wizara ya Maji
Kama ndio mita zinahesabu upepo hii ya sasa imetia fora, itakuwa pump zinapigwa na kimbuka huko chini mpaka kupata units zote hizo.
Kwa upande wenu hali ikoje Wakuu? Bili zimekuja na uhalisia?
Wizara ya Maji