Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 9,140
- 15,963
Sawa King Kong III,Hahahaa ngoja niongee na rafiki yangu yero subai.
Ndio nazichanga hapa ,nikifikia pesa ya kununua RR nitakustua,vuta subira.
Lisichelewe sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sawa King Kong III,Hahahaa ngoja niongee na rafiki yangu yero subai.
Ndio nazichanga hapa ,nikifikia pesa ya kununua RR nitakustua,vuta subira.
Sawa hizo ton tano kwa yeye peke yake ametumia siku ngapi kuzitoa kuna juu jaman mnajua uzito wa ton tano na aziweke kusubir ton 5 hii nahisi kama tunapandishwa minazi ya rufiji sasaMkuu acha kukalili hayo madini sio ruby pure yako mixer au ndo walewale note ya mia mbili mmeambiwa inauzwa million mia moja ukiuliza wapi utaambiwa dar nioneshe mteja hamna
Hii tani 1 kupata hata 30m ni kazi,2017 enzi mundarara imechanganya tipa ulikua unauziwa 30m ....ukienda kusort inaweza rudisha mtaji na faida kiduchu au kukata mtaji wote.watu wengi mitaji ilikata wengine mpka leo wanayo majabali nyumbani hakuna watejaHizo Zina it was ruby zoisite zinapatikana longido,mundarara zinauzwaga kwa kg
Kila mawe upande wa grade inakuwaga n bei yake kwa kg kna kg 1 =25000 mpaka 500000 inategemea na quality
Kwa hyo kwa tani moja Kufika bln ni kawaida
Ova
...🙄🙄🙄...?Wewe ndio hujui. Ruby tani moja ni hela ambayo ni bajeti ya Tanzania kwa miaka mingi sana
NAAMINJ HATA WEWE HUJAELEWA ULICHOANDIKA,MKUU TANI 5 ZA RUBY HIVI UNAELEWA LAKINI AU NA WEWE NI MWANAKWAYA SAUTI YA TATUMkuu acha kukalili hayo madini sio ruby pure yako mixer au ndo walewale note ya mia mbili mmeambiwa inauzwa million mia moja ukiuliza wapi utaambiwa dar nioneshe mteja hamna
Katika jambo la kudhalilisha wanataaluma na wajuvi wa mambo ya madini ni hiki kitu kilicholetwa hapa kuhusu 'eti tani 5 za madini' haiingii akilini.Ndugu mtanzania mwezangu TANI TANO za RUBY walizitoa shimoni na Crane ama
Aisee Kitoabu njoo mara moja utupe muongozo
Hzo zinaitwa ruby zoisite,mwamba wa kijani una matone ya ruby
Caboshon zke zinatoka kma zilivyo Sema Mara nyingi soko lk guru
Ova
Nakumbuka kuna mhindi mmoja alikuwa anachimbaga huko wakati huo alikuwa anayazoaHii tani 1 kupata hata 30m ni kazi,2017 enzi mundarara imechanganya tipa ulikua unauziwa 30m ....ukienda kusort inaweza rudisha mtaji na faida kiduchu au kukata mtaji wote.watu wengi mitaji ilikata wengine mpka leo wanayo majabali nyumbani hakuna wateja
Gharama za kuchimba Tani 5 za madini huenda zikazidi gharama ya Bili 1.7 kama uchimbaji ni wa Open space,!! Kuna walakini hapo...Mchimbaji mdogo mdogo wa Madini ya Ruby yaliyopo katika kata ya Mundarara wilayani Longido Mkoani Arusha Sendeu Laizer ameibuka kuwa tajiri katika sekta hiyo baada kupata tani tano za madini hayo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.7.
Hiyo ni mara ya pili kwa wachimbaji wadogo wadogo kupata utajiri kwani mchimbani mwingine alikuwa Sanniu Laizer aliyefanikiwa kupata madini ya Tanzanite yenye thamani ya zaidi ya bilioni 8.
Akizungumza na wataalam na watendaji wa sekta ya madini waliotembelea mgodi huo mmliki wa mgodi huo Gabriel sendeu Laizer amesema mafanikio hayo ni matokeo ya hatua zinazochukuliwa na serikali kuwajengea wachimbaji wadogo mazingira mazuri ya uchimbaji.
Laizer ni kijana wa pili kutoka jamii ya wafugaji wa kimasai kuibuka Bilionea kupitia madini katika kipindi cha kifupi wa kwanza akiwa ni kijana mwingine Saniniu Laser ambaye alipata kilo zaidi ya 11 za madini ya Tanzanite yenye thamani ya zaidi ya Bilion 8.
Alisema na kuishukuru sekta ya madini hususani Rais Dr. John Magufuli kwa kuwathamini wachimbaji wadogo na kuwatetea hatua ambayo ndio iliyochangia mafanikio yake kwa sasa na sio vinginevyo.
Pia amewashauri wachimbaji wenzake wadogo wa madini kuendelea kuchimba bila kukata tamaa kwani kazi hiyo inahitaji uvumilivu na kujitoa kwa dhati.
Wakizungumzia hatua hiyo baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini hayo wamesema kupatikana kwa kiasi hicho kikubwa cha madini kimewaongezea ari ya kuendelea kuchimba japo wanasema wanakabiliwa na tatizo la mitaji na vitendea kazi ,
Mmoja wa wachimbaji wadogo katika eneo hilo Michael Lekule Laizer ambaye alikuwa mbunge mstaafu wa Jimbo la Longido na Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi{CCM} amesema upo uwezekano wa kunufaika na rasilimali hiyo kama taasisI za fedha zitaona umhimu wa kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ya muda mrefu.
Viongozi wa vyama vya wachimbaji wa madini mkoa wa Arusha akiwemo Alfred Antony ambaye ni mwenyekiti wa chama cha wachimbaji na Jeremia Simion ambaye ni mwenyekiti wa wachimbaji wa kati wamesema wachimbaji wote wadogo wana ari ya kuchimba na wanafurahia mazingira waliyowekewa.
Naye Mkuu wa wilaya ya Longido ,Frank Mwaisumbe amewataka wachimbaji wadogo kuona umuhimu wa kuuunganisha nguvu pamoja ili waweze kupata vitendeakazi vya kuwawezesha kuchimba kisasa zaidi na kunufaika na rasilimali za madini ambayo sasa yame wekewa utaratibu mzuri wa kuhakikisha yanawanufaisha wazawa.
Aidha mwaisumbe pia amewashauri wachimbaji wadogo kuendelea kutoa ushirikiano kwa serikali ukiwemo kudhibiti utoroshaji wa madini ili yaendeleee kuwanufaisha wananchi na taifa kwa ujumla.
Mtaalam wa kutoka wizara ya madini ambaye ni mjiolojia mwandamizi Mussa Shanyange amesema madini ya Ruby ni miongoni mwa madini yenye thamani kubwa ambayo yanapatikana kwa wingi katika eneo hilo
Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa Mkoa wa Arusha (RMO), Aidan Muhando amempongeza Sendeu Laizer kwa kuona umuhimu wa kufanya uchimbaji kwa uwazi na kufuata sheria na taratibu zilizowekwa hatua ambayo imemuwezesha kupata mafanikio yeye mwenyewe , serikali na jamii kwa ujumla.
Hata hivyo amewataka wachimbaji wengine wenye leseni za kuchimba katika maeneo hayo ambao hawajaanza kuhakikisha wanaanza kuchimba ili kuongeza uzalishaji .
Amesema baadhi ya wachimbaji wamepewa leseni lakini hawachimbi utaratibu ambao haukubali na kama hatua hiyo itaendelea watalazimika kuchukua hatua ya kuyachukua maeneo hayo na kuwapa watu wengine wenye uwezo wa kuchimba
Wananchi wa Kijiji cha Mundarara wamesema hatua ya kupatikana kwa bilionea katika Kijiji chao imewapa matumaini makubwa ya kuanza kupata ufumbuzi wa matatizo mengi yanayowakabili
Kwa mujibu wa kamishina Madini ya Ruby pamoja na kupatikana katika wilaya hiyo ya Longido Mkoa wa Arusha pia yanapatikana wilaya za mkoa wa Tanga , na wilaya za mkoa Dodoma
Mwisho
🤣Ni muda sasa wa kuwapa watoto wetu majina ya kina laizer , maana c kwa kismat hiki
🤣Ni muda sasa wa kuwapa watoto wetu majina ya kina laizer , maana c kwa kismat hiki
Mkuu, hii itasababisha wazazi wengi mwaka huu watawaita Laizer watoto wanao zaliwa