Bilionea mwingine kutoka jamii ya Kimasai aibuka nchini, ni mchimbaji wa Madini ya Rubi

Bilionea mwingine kutoka jamii ya Kimasai aibuka nchini, ni mchimbaji wa Madini ya Rubi

Nusu kilo ya rubi tu imeshazidi bilioni moja uje useme tani? [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Tanzania hii wendawazimu wanaongezeka kwa kasi sana!

Na hiyo Ruby ya tani moja ipatikane kwenye dunia hii hii au wanaifananisha na yale mawe ya kutengenezea cement

Kama hamjui vitu wakati mwengine ni kupita na kusoma comment za wenzio....
 
Hapo wamepasua mawe makubwa makubwa halafu unaanza kulichambua kwa kulivunja ndio ukutane na viruby vidogo gram 1 au 2....unaweza kutumia miezi kuchambua huo mzigo ni kazi ngumu
Sasa kwanini wasipime hizo gram au kg za ruby baada ya kuchambua hayo mawe makubwa?kulikuwa na haja ya kutuambia hizo tani za mawe?au ndio utaratibu?
 
Nikishaona mtu anaanza kutanguliza shukrani kwa awamu ya 5 na Rais basi kanipoteza.
Sitotilia maanani asilani!
Yaani uko kama mimi, kuchimba uchimbe wewe then uje na story za jiwe [emoji848], mimi huwa nahisi kuna utapeli hapo kama siyo propaganda. Tani tano walizitoaje ??
 
Mkuu acha kukalili hayo madini sio ruby pure yako mixer au ndo walewale note ya mia mbili mmeambiwa inauzwa million mia moja ukiuliza wapi utaambiwa dar nioneshe mteja hamna
Acha kurukaruka kama mahindi ya bisi, wapi kasema ni madini mchanganyiko? Yaani tani 5 =1.7 B?
 
Mchimbaji mdogo mdogo wa Madini ya Ruby yaliyopo katika kata ya Mundarara wilayani Longido Mkoani Arusha Sendeu Laizer ameibuka kuwa tajiri katika sekta hiyo baada kupata tani tano za madini hayo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.7.

Hiyo ni mara ya pili kwa wachimbaji wadogo wadogo kupata utajiri kwani mchimbani mwingine alikuwa Sanniu Laizer aliyefanikiwa kupata madini ya Tanzanite yenye thamani ya zaidi ya bilioni 8.

Akizungumza na wataalam na watendaji wa sekta ya madini waliotembelea mgodi huo mmliki wa mgodi huo Gabriel sendeu Laizer amesema mafanikio hayo ni matokeo ya hatua zinazochukuliwa na serikali kuwajengea wachimbaji wadogo mazingira mazuri ya uchimbaji.

Laizer ni kijana wa pili kutoka jamii ya wafugaji wa kimasai kuibuka Bilionea kupitia madini katika kipindi cha kifupi wa kwanza akiwa ni kijana mwingine Saniniu Laser ambaye alipata kilo zaidi ya 11 za madini ya Tanzanite yenye thamani ya zaidi ya Bilion 8.

Alisema na kuishukuru sekta ya madini hususani Rais Dr. John Magufuli kwa kuwathamini wachimbaji wadogo na kuwatetea hatua ambayo ndio iliyochangia mafanikio yake kwa sasa na sio vinginevyo.

Pia amewashauri wachimbaji wenzake wadogo wa madini kuendelea kuchimba bila kukata tamaa kwani kazi hiyo inahitaji uvumilivu na kujitoa kwa dhati.

Wakizungumzia hatua hiyo baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini hayo wamesema kupatikana kwa kiasi hicho kikubwa cha madini kimewaongezea ari ya kuendelea kuchimba japo wanasema wanakabiliwa na tatizo la mitaji na vitendea kazi ,

Mmoja wa wachimbaji wadogo katika eneo hilo Michael Lekule Laizer ambaye alikuwa mbunge mstaafu wa Jimbo la Longido na Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi{CCM} amesema upo uwezekano wa kunufaika na rasilimali hiyo kama taasisI za fedha zitaona umhimu wa kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ya muda mrefu.

Viongozi wa vyama vya wachimbaji wa madini mkoa wa Arusha akiwemo Alfred Antony ambaye ni mwenyekiti wa chama cha wachimbaji na Jeremia Simion ambaye ni mwenyekiti wa wachimbaji wa kati wamesema wachimbaji wote wadogo wana ari ya kuchimba na wanafurahia mazingira waliyowekewa.

Naye Mkuu wa wilaya ya Longido ,Frank Mwaisumbe amewataka wachimbaji wadogo kuona umuhimu wa kuuunganisha nguvu pamoja ili waweze kupata vitendeakazi vya kuwawezesha kuchimba kisasa zaidi na kunufaika na rasilimali za madini ambayo sasa yame wekewa utaratibu mzuri wa kuhakikisha yanawanufaisha wazawa.

Aidha mwaisumbe pia amewashauri wachimbaji wadogo kuendelea kutoa ushirikiano kwa serikali ukiwemo kudhibiti utoroshaji wa madini ili yaendeleee kuwanufaisha wananchi na taifa kwa ujumla.

Mtaalam wa kutoka wizara ya madini ambaye ni mjiolojia mwandamizi Mussa Shanyange amesema madini ya Ruby ni miongoni mwa madini yenye thamani kubwa ambayo yanapatikana kwa wingi katika eneo hilo

Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa Mkoa wa Arusha (RMO), Aidan Muhando amempongeza Sendeu Laizer kwa kuona umuhimu wa kufanya uchimbaji kwa uwazi na kufuata sheria na taratibu zilizowekwa hatua ambayo imemuwezesha kupata mafanikio yeye mwenyewe , serikali na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo amewataka wachimbaji wengine wenye leseni za kuchimba katika maeneo hayo ambao hawajaanza kuhakikisha wanaanza kuchimba ili kuongeza uzalishaji .

Amesema baadhi ya wachimbaji wamepewa leseni lakini hawachimbi utaratibu ambao haukubali na kama hatua hiyo itaendelea watalazimika kuchukua hatua ya kuyachukua maeneo hayo na kuwapa watu wengine wenye uwezo wa kuchimba

Wananchi wa Kijiji cha Mundarara wamesema hatua ya kupatikana kwa bilionea katika Kijiji chao imewapa matumaini makubwa ya kuanza kupata ufumbuzi wa matatizo mengi yanayowakabili

Kwa mujibu wa kamishina Madini ya Ruby pamoja na kupatikana katika wilaya hiyo ya Longido Mkoa wa Arusha pia yanapatikana wilaya za mkoa wa Tanga , na wilaya za mkoa Dodoma

Mwisho
Sina wasiwasi na fedha alizopata huyo bilionea. Wasiwasi wangu ni kuhusu huo uzito, tani tano za ruby ni uzito mkubwa sana. Ieleweke madini ya Vito hupata thamani yake kwa vile yanakuwa adimu na aghalabu uzito wake unakuwa katika gramu. Ili kupata tani tano za ruby, basi nafikiri mlima mmoja umesambazwa kabisa!
 
MCHIMBAJI mdogo wa madini ya rubi katika Kata ya Mundarara wilayani Longido mkoani Arusha, Sendeu Laizer ameibuka tajiri katika sekta hiyo baada kupata tani tano za madini hayo zenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.7.

Hiyo ni mara ya pili kwa wachimbaji wadogo kupata utajiri kwani mwingine alikuwa Sanniu Laizer aliyepata madini ya tanzanite yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 8.

Akizungumza na wataalamu na watendaji wa sekta ya madini waliotembelea mgodi huo, mmliki wa mgodi huo, Gabriel Sendeu Laizer alisema mafanikio hayo ni matokeo ya hatua zinazochukuliwa na serikali kuwajengea wachimbaji wadogo mazingira mazuri ya uchimbaji.

Aliishukuru sekta ya madini na serikali hususani Rais John Magufuli kwa kuwathamini wachimbaji wadogo na kuwatetea hatua ambayo ndio iliyochangia mafanikio yake kwa sasa na sio vinginevyo.

Pia aliwashauri wachimbaji wenzake wadogo wa madini kuendelea kuchimba bila kukata tamaa kwani kazi hiyo inahitaji uvumilivu na kujitoa kwa dhati.

Wakizungumzia hatua hiyo, baadhi ya wachimbaji wadogo wa rubi walisema kupatikana kwa kiasi hicho kikubwa cha madini kimewaongezea ari ya kuendelea kuchimba japo wanakabiliwa na tatizo la mitaji na vitendea kazi.

Mchimbaji mdogo katika eneo hilo, Michael Laizer ambaye alikuwa mbunge mstaafu wa Jimbo la Longido na Mwenyekiti mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, alisema upo uwezekano wa kunufaika na rasilimali hiyo kama taasisi za fedha zitaona umuhimu wa kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ya muda mrefu.

Viongozi wa vyama vya wachimbaji wa madini Mkoa wa Arusha akiwamo Alfred Antony ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji na Jeremia Simon ambaye ni Mwenyekiti wa Wachimbaji wa Kati wamesema wachimbaji wote wadogo wana ari ya kuchimba na wanafurahia mazingira waliyowekewa.

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe aliwataka wachimbaji wadogo kuona umuhimu wa kuuunganisha nguvu pamoja ili wapate vitendeakazi vya kuwawezesha kuchimba kisasa zaidi na kunufaika na rasilimali za madini ambayo sasa yamewekewa utaratibu mzuri wa kuhakikisha yanawanufaisha wazawa.

Aidha, Mwaisumbe aliwashauri wachimbaji wadogo kuendelea kutoa ushirikiano kwa serikali ukiwemo kudhibiti utoroshaji wa madini ili yaendeleee kuwanufaisha wananchi na taifa kwa ujumla.

Mtaalamu kutoka Wizara ya Madini ambaye ni Mjiolojia Mwandamizi Mussa Shanyange alisema madini ya rubi ni miongoni mwa madini yenye thamani kubwa ambayo yanapatikana kwa wingi katika eneo hilo.

Kamishna wa Madini wa Mkoa, Aidan Muhando alimpongeza Sendeu kwa kuona umuhimu wa kufanya uchimbaji kwa uwazi na kufuata sheria na taratibu zilizowekwa, hiyvyo kupata mafanikio binafsi, serikali na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo, amewataka wachimbaji wengine wenye leseni za kuchimba katika maeneo hayo ambao hawajaanza kuhakikisha wanaanza kuchimba ili kuongeza uzalishaji.

Alisema baadhi ya wachimbaji wamepewa leseni lakini hawachimbi jambo ambalo halikubaliki, na kama litaendelea watalazimika kuchukua hatua ya kuyachukua maeneo hayo na kuwapa watu wengine wenye uwezo wa kuchimba.

Wananchi wa Kijiji cha Mundarara wanasema hatua ya kupatikana kwa bilionea katika kijiji chao imewapa matumaini makubwa ya kuanza kupata ufumbuzi wa matatizo mengi yanayowakabili.

Kwa mujibu wa Kamishina Muhando, madini ya rubi pamoja na kupatikana katika wilaya hiyo ya Longido, pia yanapatikana wilaya za Mkoa wa Tanga na wilaya za Mkoa wa Dodoma.
 
Wewe ndio hujui. Ruby tani moja ni hela ambayo ni bajeti ya Tanzania kwa miaka mingi sana

Mjinga sana wewe hii ni biashara nafanya zaidi ya miaka15 sasa wewe sijui unaju nini [emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23]...
Hizo ni cabochon ruby hata sijui kama unaelewa maana ya hilo neno nenda ka Google usome uwelewe Ndio uje kubishana
 
Sina wasiwasi na fedha alizopata huyo bilionea. Wasiwasi wangu ni kuhusu huo uzito, tani tano za ruby ni uzito mkubwa sana. Ieleweke madini ya Vito hupata thamani yake kwa vile yanakuwa adimu na aghalabu uzito wake unakuwa katika gramu. Ili kupata tani tano za ruby, basi nafikiri mlima mmoja umesambazwa kabisa!

Huwo uzito si lolote hizo ni low quality ruby zinauzwa kwa matani hivyo hivyo ... ukisema ishu ya kutoa viti sijui yanaweza kugogwa na usipate viini chupa clean ukakutana na mikatiko kibao na bei ikawa chini zaidi
 
Sasa kwanini wasipime hizo gram au kg za ruby baada ya kuchambua hayo mawe makubwa?kulikuwa na haja ya kutuambia hizo tani za mawe?au ndio utaratibu?
Ndio serikali yetu ilivyo comedian,hayo wanatoa bei kabla hata hawajasort mawe hayo,thamani yake iko chini
 
Back
Top Bottom