Bilionea mwingine kutoka jamii ya Kimasai aibuka nchini, ni mchimbaji wa Madini ya Rubi

Bilionea mwingine kutoka jamii ya Kimasai aibuka nchini, ni mchimbaji wa Madini ya Rubi

Grm Sawa
Ila caboshon ya mundarara znakuwaga na shida syo kama ruby ya matombo au mahenge

Ova
Mimi 2017 nlinunua mawe fuso,kipindi hicho mundarara imechanganya matajiri wote wa tanzanite wananunua mawe,ujazo wa fuso ilikua 30m .
Wengi mitaji ilikata mana unaweza gonga mawe yote usipate hata gram 1000.ila mwenye mgodi ndio alikua anapata pesa kwenye kuuza
 
hata mi nimeshangaa manake ni story tofauti na aliyotuletea komredi kitoabu kuwa ruby kidogo tu utajili hoop sasa tani tano si useless kabisa michanga iyo

Hizo ni cabchon zinaitwa Yaani sio quality nzuri .. kama tanzanite quality mbaya pia zinauzwa kwa matani so ni sawa tu..
 
Huu ni uongo sasa!
TANI TANO za RUBY= Billion 1?
Hivi mtoa mada unaijua thamani ya Ruby kweli?
Kitoabu njoo utusaidie huu mjadala
 
Kwa sisi tuliopita kwenye machimbo ya Ruby kule Montpuez kwa mzee Filipe Jacinto Nyusi in the Republica de Mozambique hili swala kidogo tunaweza lidadavua.

Tuanzie kwanza bei ya Ruby
Bei ya ruby ina range kuanzia $10 mpaka $12,000 kwa carat au inaweza ikashuka mpaka kufikia $ 50/kg
,na hapa inategemea na hiyo ruby imechimbwa nchi gani maana kuna nchi ukichimba ruby ukapeleka kwenye world market hauwezi kuuza kabisa yaani ni priceless japo ni ruby hii kitu kwa sisi watu wa madini tunawezaita "blood mineral " pia tunaweza kuita "blood ruby" katika kesi yetu japo mara nyingi neno blood limekuwa ikitumika kwa kesi ya diamond kama tulivyoona "blood diamond" za kule Seara Leone ambako kulikuwa na machafuko but always this blood minerals are priceless sababu inatoka kwenye migodi iliyomwaga damu na nchi zenye umwagaji damu,au nchi zinazofadhiri vikundi vya wahasi.

Na wazungu walivyo wafitini hawa mabeberu wamezigawa ruby kwenye madaraja ya thamani kutokana na nchi zinazochimbwa kama ifuatavyo.
1.Burma au Myamar
2.Thailand ,Cambodia
3.Mozambique ,Madagascar
4.Kenya,Tanzania
5.Afganstan and Parkistan
Kwa vigezo vya ubora ,usambazaji na uchimbaji,na brand.
Na hii ndio iliyopelekea wabongo wengi kukimbilia machilbo ya ruby kule Montpuez Msumbiji japo Tz kuna ruby deposit nyingi,ila kuna kautofauti kidogo ka thamani ya ruby zinazochimbwa nchi hizi mbili tofauti katika same condition.


Ila vigezo vingine vinavyotumika kupima bei ya ruby kitaaramu tunaita 4C's +OT
1.Clarity-uangavu
2.Color-rangi hapa nyekundu inakuwa ghari (expensive)kuliko purpish red,orangish red,pinkish red
3.Carat weight-huu ni uzito na 1kg inakuwa sawa na 5000carat
4.Cut-hii ni shape baada ya ruby kukatwa zenye shape ya pembe kumi,duara,mraba,n.k hizi zenye shape ya pembe kumi ,duara,na mraba zinakuwa ghari sana
5.Origin - hapa tunazaungumza asili ya hiyo ruby imechimbwa wapi,mgodi gani,kampuni gani n.k.
6.Treatment level-hapa tuna refer njia zilizotulika katika uchenjuaji mpaka kupata refined ruby.

Pia kuna mambo kibao kama inclusions n.k ila ukibahatika kupata kitu inaitwa " pigeon blood ruby" wewe ni mtu mwengine kwenye hii dunia,ruby hizi zina bei kuliko hata diamonds unazozijua ww hizi ndio zile watoto wa uswazi wanaziita ruby birihani au ruby VPN yani hazina chenga pesa nje nje.

Twende kwenye point sasa
Bei ya ruby inaanzia $10 mpaka $12,000 kwa carat kwa kuzingatia vigezo tajwa hapo juu,pia inaweza ikawa $50 /kg .
Kumbuka 1kg ni sawa na 5000 carat .

Tukizingatia vigezo hivi hiyo 1.7Bilion inaweza ikawa ndio halali yake ,maana kuna makato ya kodi n.k.
 
Pia kuna jina la Janet

Mke wa Raisi Museveni anaitwa Janet, mke wa Raisi Kagame anaitwa Janet na mke wa Raisi Magufuli anaitwa Janet
Daaah kwel Aisee , na Mke Wangu pia anaitwa janeti, ngoja nijiandae 2025 nigombee uraisi, hopefully kwa visimart vya kua na wanawake wenye majina haya nitakua raisi tu . sema tatizo mm sio mbabe aisee
 
Tani tano
1606345735426.png
 
yani tani tano nilitegemea jamaa apewe hata tilion 50 hivi basi kitoabu anapoteza muda tu huko msumbiji
 
Nusu kilo ya rubi tu imeshazidi bilioni moja uje useme tani? 🤣🤣🤣🤣
Tanzania hii wendawazimu wanaongezeka kwa kasi sana!

Na hiyo Ruby ya tani moja ipatikane kwenye dunia hii hii au wanaifananisha na yale mawe ya kutengenezea cement
 
Hata kilo tano sio bei hio , ngoja tumsikilizo mnadhimu Kitoabu atupe muongozo elekezi
 
Back
Top Bottom