Bilioni 2 ni nyingi ila ndogo kwa Simba, Next time mfanye 5 kwenda mbele

Bilioni 2 ni nyingi ila ndogo kwa Simba, Next time mfanye 5 kwenda mbele

Randy orton

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2019
Posts
1,338
Reaction score
3,561
Hongera sana Simba na Vunja bei kwa makubaliano ya kihistoria mlioingia hii leo, kiukweli Simba imepiga hatua ukilinganisha na ilipokuwepo.

Twende kwenye facts sasa.

Uwekezaji uliofanyika ni wa shilingi za kitanzania Bilioni mbili (2) kwa miaka miwili.

Kimahesabu, Kama Investor ( Vunja bei) atauza pisi moja ya jezi kwa shilingi za kitanzia elfu kumi tu, atahitajika kuuza pisi laki mbili ili arudishe mtaji wake kwa muda wa mwaka mmoja.

Kwa ukubwa wa Simba hii ambayo ina uwezo wa kujaza uwanja wa Ben mkapa (zaidi ya watu elfu 50), ukijumlisha mashabiki wengi sana wa mikoani, na nje ya Tanzania, kimahesabu kama Simba itauza jezi chache kwa mwaka mmoja (1) zitakuwa si chink ya pisi laki tano ambazo kimsingi zitarudisha mtaji na faida ya Investor.

Hapo hujahesabia kuwa Simba imeshakuwa timu ya kimataifa hivyo yeyote anayesambaza jezi zake anapata access na soko la afrika yote ambapo simba inaenda kushiriki mashindano tofauti tofauti.

Nimesikia kwenye press kuwa sio jezi tuu, Investor atauza na vitu vingine, that means amepewa uwanja mpana wa kuingiza faida kwa shilingi bilioni mbili ile ile aliyowekeza kwa miaka miwili.

Nafahamu fika hakuna mtu anayetaka kuweka hela kwenye hasara hivyo nawapongeza Vunja bei kwa kuchagua brand itakayowaletea faida, pia nitakuwa mchoyo wa fadhila nikiacha kuwasifu Vunja bei kwa uwezo wao mkubwa wa kunegotiate.

Next time Simba isijidogeshe kwenye negotiations, bilioni mbili ni hela nyingi sana lakini ni hela ndogo kwa brand kubwa kama Simba bila kusahau kipindi cha uwekezaji ni cha muda mrefu wa miaka miwili

Ni mtizamo tuu.
 

Huyu walisema kapata deal ya bil.8.5 ila akaishia uDC
 
Kabla ya hapo walikuwa wanapata kiasi gani? Hebu tuanzie hapo kwanza
Sijui.

Ila nimeshasema kwenye uzi huu kuwa nimewapongeza kwa hatua waliyopiga maana kibongobongo ndio timu ya kwanza kutangaza mkataba wa bilioni 2 kwa usambazaji wa jezi.

Lakini hayo yote hayaondoi ukweli kuwa wamepigwa.
 
Sijui.

Ila nimeshasema kwenye uzi huu kuwa nimewapongeza kwa hatua waliyopiga maana kibongobongo ndio timu ya kwanza kutangaza mkataba wa bilioni 2 kwa usambazaji wa jezi.

Lakini hayo yote hayaondoi ukweli kuwa wamepigwa.
Yani unadhani manguli wa biashara kama kina Mo hawajaona hayo na kuyapigia mahesabu kuona kama biashara ni kichaa au inalipa?

Hivi sasa spotipesa wakitaka kupewa mkataba huu unadhani watatoa vijisenti walivyokuwa wanatoa au watazidisha?
 
... nitakuwa mchoyo wa fadhila nikiacha kuwasifu Vunja bei kwa uwezo wao mkubwa wa kunegotiate.
... Next time Simba isijidogeshe kwenye negotiations,
Mkuu, hakukuwa negotiations, iliitishwa zabuni kwa umma. Kama haufahamu mchakato wa zabuni, ni kwamba kila aliyebid hafahamu mwenzake amewekaje andiko lake. Kama kulikuwapo maadili yote ya zabuni, ni kwamba hata aliyeshinda hakuwa na nafasi ya kujieleza kama ulivyoandika 'negotiations'
 
Kabla ya hapo walikuwa wanapata kiasi gani? Hebu tuanzie hapo kwanza

mkataba unaoelekea ukingoni uliiingiwa miaka miwili au mitatu iliopita na jamaa wanajiita UHL. walikuwa wanaotoa vifaa vya michezo na 100M kwa mwaka, plus 20% au 25% ya mauzo ya jersy ( hapo kwenye % sina hakika ni asilimia ngapi)

in fact ndio aina ya mkataba wa "kit supplier" ambao wanao yanga na gsm pia ila wao wanapokea pesa nyingi kias kati ya 300m- 500mkwa mwaka ila wao hawapat % yoyote kutoka kwenye mauzo
 
Hongera sana Simba na Vunja bei kwa makubaliano ya kihistoria mlioingia hii leo, kiukweli Simba imepiga hatua ukilinganisha na ilipokuwepo...
Mtazamo wako ni finyu sana.

Haujaainisha kwa miaka ya nyuma Simba walikuwa wakiingiza kiasi gani kwa mauzo ya "MERCHANDISE" zake. Halafu miaka miwili ni muda mrefu sana. Vunja Bei ameingia mkataba wenye RISK nyingi sana. Vipi kama kwa mwaka mmoja mbele jezi za Simba zitakuwa haziuziki? Vipi kama upatikanaji wa malighafi utakuwa na changamoto?

Kumbuka biashara mpaka ifanyike kuna kodi na tozo kibao achilia mbali mali kuharibika au kupotea wakati wa kusafirisha.

Simba ina watu wenye uzoefu wa biashara kuliko wewe unayechukulia kuwa jezi zote zitauzwa siku moja na VB atapata faida hapo hapo.
 
Yani unadhani manguli wa biashara kama kina Mo hawajaona hayo na kuyapigia mahesabu kuona kama biashara ni kichaa au inalipa?

Hivi sasa spotipesa wakitaka kupewa mkataba huu unadhani watatoa vijisenti walivyokuwa wanatoa au watazidisha?
unaweza ukakuta hao manguli ni sehemu ya wawekezaji waliotoa B mbili
 
Sijui.

Ila nimeshasema kwenye uzi huu kuwa nimewapongeza kwa hatua waliyopiga maana kibongobongo ndio timu ya kwanza kutangaza mkataba wa bilioni 2 kwa usambazaji wa jezi.

Lakini hayo yote hayaondoi ukweli kuwa wamepigwa.

Kutoka kulipwa mil 100 kwa mwaka mpaka bilion 2 kwa miaka 2 unasema wamepigwa dah...huu mwanzo tu subiri tuone mwisho wa mkataba utajua nani kapigwa au kashinda.
 
Simba imepanda thamani, ni pesa ndogo sana.

Simba.imesambaa.nchi nzima wana uwezo wa chini kuuza jezi laki tano acha na vitu vingine kama kofia, bendera na bidhaz nyingine.
Kama kila jezi ni 20000 mauzo ni Bilioni 10 ukiondoa gharama nyingine wanapata si chini ya bilioni 5.

Halafu kwanini wanaingia mkataba wa miaka miwili wangeweka mwaka mmoja wakafanya tathimini
 
Sijui.

Ila nimeshasema kwenye uzi huu kuwa nimewapongeza kwa hatua waliyopiga maana kibongobongo ndio timu ya kwanza kutangaza mkataba wa bilioni 2 kwa usambazaji wa jezi.

Lakini hayo yote hayaondoi ukweli kuwa wamepigwa.
Kabla ya hapo walikuwa wanapata kiasi gani? Hebu tuanzie hapo kwanza
Wa mwanzo aliweka 100M.. Barbara kasema
 
Back
Top Bottom