Bilioni 650 za DP World Zamkuna Makala. Zaongeza Ufanisi wa Bandari ya Dar kutoka Makasha 7,000 Hadi Makasha 20,000

Bilioni 650 za DP World Zamkuna Makala. Zaongeza Ufanisi wa Bandari ya Dar kutoka Makasha 7,000 Hadi Makasha 20,000

..ndio nimekwambia SHERIA imekiukwa.

..kulipaswa kuwe na Zabuni, halafu makampuni yatie nia, na mshindi apatikane baada ya mchakato.

..sasa hivi tulivyofanya tuna uhakika gani kama Adani, au Dp, wametupa offer nzuri kuliko wote?
Abani alitangazwa mpaka kupatikana kwake, kwenye magazeti ya serikali lilikuwepo tangazo lake. DPW nimekwambia mara elfu moja sasa, kwamba nature ya biashara anayoifanya ilimpa yeye moja kwa moja nafasi ya uwekezaji.

DPW ana miliki bandari za UK na India nitafutie kampuni nyingine ya hadhi yake katika ulimwengu mzima wa biashara za shipping kwa sasa.
 
Mnajadili haya mambo kihisia na wote hamjui hata mnachojadili. Nani nawaambia tender ya kuendesha ghati namba 8-11 haikutangazwa?
Nguvu ya kujadili msichokijua mnaitoa wapi?

..kuna madai kwamba Adani alianza kazi kabla ya zabuni kutangazwa.

..yaani hiyo zabuni imetangazwa kihuni wakati anayetakiwa anajulikana.

..vilevile kama Adani alipata kazi kupitia zabuni kwanini Dpw yeye kupewa mkataba kibabe?

Cc Steven Joel Ntamusano
 
My Take
Wale wa Samia ameuza Mali zao za Urithi mnaitwa kuja kumwaga povu jingine.

Kwa taarifa yenu sio tuu shehena ya mzigo imeongezeka Bali muda wa kusubiria meli umetoka siku 14 Hadi siku 3.

Hongera sana Rais Samia Kwa Mageuzi haya yenye Tija Kwa Nchi na kuleta ushindani mzuri wa Bandari ya Dar.

Pia soma hapa DP World kuokoa Sh1.6 trilioni hadi Desemba



View: https://youtu.be/o3wT4BwqifA?si=TXvSwhowSbEj_FlY

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) imesema uwekezaji uliofanywa na Kampuni ya DP World katika bandari ya Dar es Salaam katika kipindi cha miezi mitatu umeonesha mafanikioa makubwa kwa shehena ya makasha kuongezeka kutoka 7,151 Aprili 2024 hadi kufikia 20,151 kufikia Julai 2024. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Uwekezaji huo wenye thamani ya takriban dola milioni 250 (Sh bilioni 675) kwa ajili ya uendeshaji wa magati 0-7 bandarini hapo umeleta manufaa makubwa kwa ni ongezeko la shehena ya makasha hayo ni sawa na ongezeko la asilimia 182.

Hayo yamebainishwa jana jijini Dar es Salaam na Meneja wa Shughuli na Uratibu wa TPA, Josephat Lukindo wakati akiwasilisha ripoti fupi ya utendaji wa bandari hiyo baada ya uwekezaji huo kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makala aliyefanya ziara yake badarini hapo.

Alisema pesa hizo imetumika kuboresha utendaji wa bandari hiyo katika maeneo matatu baada ya kukabidhiwa na mamlaka ya bandari Aprili 15, 2024.

“Kwa uzoefu tulionao katika uendeshaji wa bandari, tuliamua kuanza na uboreshaji wa maeneo matatu muhimu ili kuongeza ufanisi zaidi,” alisema Lukindo.

Amesema sehemu ya kwanza kabla ya kufanya kitu chochote kampuni ya DP World kupitia kampuni tanzu ya DP World Dar es Salaam iliyoanzishwa kusimamia bandari hiyo ilifanya manunuzi ya mitambo ya kisasa yenye thamani ya takriban bilioni 215.

Alisema pili ilifanya ukarabati wa mitambo mibovu iliyokuwa ikitumika bandarini hapo na kufanya manunuzi ya vifaa vipya yakiwemo matrekta ya kubebea mizigo 20 pamoja na matela 31, jenerela saba zenye ukubwa wa Kv 10,000 kila moja kwa ajili ya kuendeshea mitambo ikitokea umeme umekatika na vifaa vya kubebea mizigo mizito (cranes).

“Tatu, DP World ilifanya usimikaji wa mifumo ya kisasa ya TEHAMA kwa ajili ya uendeshaji wa bandari hiyo. Hapo awali, tulikuta mifumo ambayo imepitwa na wakati na kuamua kuweka mifumo ya kisasa kuendana na maendeleo ya teknolojia,” alisema.

Hivyo, alisema uwekezaji huo umeleta manufaa makubwa ndani ya kipindi cha miezi mitatu iliyochangia ongezeko la shehena ya makasha ikiwa sawa na ongezeko la asilimia 182.

Mwanahalisi

Mhh Kama ni mwanahalisi (gazeti) wameandika hivo then tuna waandishi bogus kabisa! Wameshindwa hata kuingia kwa website ya TPA na kuona meli zinasubiri kwa muda gani ili kushusha mzigo?😭😳😳😳
Hii hapa chini( attached) ni ratiba ya meli zinazosubiri kushusha mzigo, utaona kuna meli ina siku thelathini (30) na bado haijaingia/kupata nafasi ya kushusha mzigo
 

Attachments

  • IMG_0076.png
    IMG_0076.png
    442.4 KB · Views: 1
Asante kwa kunisahihisha. Nilichukulia ni sawa na ile ya magati namba 3-7 aliyopewa DPW.
Sawa mkuu, lakini mbona bado unakosea? Maghati 3-7???
Sijui kama unaelewa kweli hili jambo, lakini bado nauliza kwa nn unajadili Jambo ambalo linaonyesha pengine hulifahamu?
 
..kuna madai kwamba Adani alianza kazi kabla ya zabuni kutangazwa.

..yaani hiyo zabuni imetangazwa kihuni wakati anayetakiwa anajulikana.

..vilevile kama Adani alipata kazi kupitia zabuni kwanini Dpw yeye kupewa mkataba kibabe?

Cc Steven Joel Ntamusano
Mbona mnahangaika sana bila sababu za msingi?

Nimesema DP World ameingia Kwa mtindo wa Serikali Kwa Serikali kusaini MoU na hivyo Kuna preferential treatments Kwa sababu za kimahusiano baina ya Nchi kama tuu Arab Contractors wa Bwawa la Nyerere.

Huyo mwingine Tanzania na India Hazina kubaliana rasmi so alitumia open tendering.

Mwisho Cha muhimu ni matokeo au mchakato?
 
..kuna madai kwamba Adani alianza kazi kabla ya zabuni kutangazwa.

..yaani hiyo zabuni imetangazwa kihuni wakati anayetakiwa anajulikana.

..vilevile kama Adani alipata kazi kupitia zabuni kwanini Dpw yeye kupewa mkataba kibabe?

Cc Steven Joel Ntamusano
Kwanza mm nimewarekebisha mliposema haikutangazwa. Ukweli ilitangazwa

Kwa nini DP haikutangazwa, hiyo sijui ndio maana sikuigusa.
 
..DPW wangekuwa toka mwanzo na malengo ya kuendesha gati # 8 - 11 na mchakato ukawa wa wazi hakuna mtu angepiga kelele.

..tatizo lilikuwa ni IGA ambayo ilipitishwa na bunge na inakiuka sheria ya ulinzi wa rasilimali iliyopitishwa mwaka 2017.

..Na mimi nalazimika kuamini kwamba bila mayowe kupigwa DPW were coming for more than just gati # 8 - 11.

..Utakumbuka kwamba TICTS hakuhitaji IGA ili kuendesha gati za makontena bandarini. ADANI naye hakuhitaji IGA ili kukodishwa gati ktk bandari yetu.

..Sasa kama Ticts na Adani hawakuwa na IGA, kwanini mambo ni tofauti kwa DPW?

..Zaidi, waliopinga IGA wako wengi zaidi ya Adv.Mwabukusi. Wako wasomi wakubwa na wanaoaminika kama Prof.Issa Shivji. Maaskofu ktk umoja wao waliounga, na si kweli kwamba alikuwa Fr.Kitima peke yake. Shura ya Maimamu walisema IGA ina matatizo.

..Wakati mwingine nadhani Watanzania hatuna skills za kupambanisha hoja zinazohusu maslahi ya taifa letu. Tunajadili mambo mazito ya kisheria kana kwamba tunajadili Simba na Yanga. Vilevile hakuna uwazi hivyo kila unakuta watu wanabishania jambo la msingi bila kuwa na taarifa za kutosha.
DP world ghati namba 8-11??

Sema huu mjadala wenu mmechanganya mambo hadi basi aisee
 
wajinga ndio wataamini uekezaji ndio uongeze makasha?hao wateja wametokea wapi... walikuwa wateja wa bandari gani wa kaopt kushushia dar..unaweza kuta wateja wa holili ,tanga na mtwara wamelazimishwa kushushia dar kontena zao....maana mmiliki ni mjomba....niishie hapo
 
Akili huna wewe usiyefuatilia habari za maana. Kesi ya kupinga DPW asipewe uendeshaji kule Mbeya, Mwabukusi na wenzake waliangukia pua ndio SSH akaamuru mchakato wa kumkabidhi hayo magati namna 8-11 uanze mara moja.
Haya mnaandika kwa confidence huwa mnayatoa hewani? Dp world ghati 8-11????

Huu mjadala wenu kiboko aisee
 
DP world ghati namba 8-11??

Sema huu mjadala wenu mmechanganya mambo hadi basi aisee

..wanaotetea uchafu ndio wanachanganya mambo.

..sasa sio tunaowapinga tunaonekana tunashiriki kuwachanganya wasomaji.

..kuna kipindi tulikuwa tunadanganywa kwamba Dpw wameletwa kuwa-replace Ticts.
 
Abani alitangazwa mpaka kupatikana kwake, kwenye magazeti ya serikali lilikuwepo tangazo lake. DPW nimekwambia mara elfu moja sasa, kwamba nature ya biashara anayoifanya ilimpa yeye moja kwa moja nafasi ya uwekezaji.

DPW ana miliki bandari za UK na India nitafutie kampuni nyingine ya hadhi yake katika ulimwengu mzima wa biashara za shipping kwa sasa.
Kampuni zingine zenye hadhi kama DP? Mbona zipo nyingi.
PSA
Hutchison ports
Cosco
China merchants ports. (Hawa ndio walitaka kuja kujenga bagamoyo port kwa trillioni 20)

Mkuu Kuna sababu nzuri ya serikali yetu kuwapa DP world.
Bado nasisitiza tusiandike kitu hatukijui vizuri hasa kwenye vitu technical
 
..wanaotetea uchafu ndio wanachanganya mambo.

..sasa sio tunaowapinga tunaonekana tunashiriki kuwachanganya wasomaji.

..kuna kipindi tulikuwa tunadanganywa kwamba Dpw wameletwa kuwa-replace Ticts.
Sio kweli, DP world hajareplace ticts. Mara nyingi huwa nakuambia choice variables awe anaandika vitu ambavyo anavijua, sababu anachoandika haandikii watu wajinga

Pia ni jambo la ajabu kuandika na kuzungumza vitu technical ambavyo mtu huvijui kabisa
 
Sio kweli, DP world hajareplace ticts. Mara nyingi huwa nakuambia choice variables awe anaandika vitu ambavyo anavijua, sababu anachoandika haandikii watu wajinga

Pia ni jambo la ajabu kuandika na kuzungumza vitu technical ambavyo mtu huvijui kabisa

..wanaotetea huo uchafu huwa wanakuja na mambo mengi.

..kuna watu wako hapo kwa malengo maalum ya kupotosha, na kuharibu mijadala yetu.
 
..hoja zako zinaweza kuungwa mkono au kupingwa bila kujali kama umekosea namba za gati zinazozungumziwa huko bandarini.
Bila kujua dp world ana operate wapi sasa yote mtajadili si itakua ni hisia?
Hujui mchezaji anacheza namba gani, lakini unataka kumjaji? Si ndio itaanza kulalamika kwa nini bakari mwamnyeto hafungi magoli
 
Back
Top Bottom