Bima ya NHIF inasababisha Hospitali kushindwa kujiendesha kwa kutolipa madeni. Rais Samia angazia macho huko

Bima ya NHIF inasababisha Hospitali kushindwa kujiendesha kwa kutolipa madeni. Rais Samia angazia macho huko

Ukisema madhara ya mfuko huu unakosea kwa sababu NHIF huko nyuma ilijitahidi kuhudumia vizuri.

Matatizo yalianza baada ya ule utaratibu wa gawio.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hivi walikuwa wanatumia vigezo gani kugawa michango ya wafanyakazi wanayokatwa kila mwezi ili watibiwe?
 
Yako mengi mkuu hata NSSF, PSSSF, na taasisi zote za umma. Yaani kuna taasisi Moja inapokea pesa ya kujiendesha asililia [emoji817] kutoka serikalini lakini eti nazo zilichangia.

Wakati huo huo hawana hata pesa ya kujaza Mafuta magari yalipaki. Yaani uchaguzi ule wa 2020 na miradi ya Chattel hizi taasisi pamoja na wafanyabiashara wakubwa walichoka mno.

Na ili kurejesha mabillion waluliochanga ilibidi wapandishe bei za bidhaa na utashangaa ilipelekwa kiujanja ujanja Kisiasa. Mzee Yule alitutesa na ametuachia mateso.

Wafanyabiashara bado wanafidia pesa Yao Kwa kupandisha bei bidhaa na sasa wako huru mno kujifanyia Yao. Yaani kweli nchi aliyoniachia Baba wa Taifa ndiyo imefika hapa. Yaani kiongozi unadiriki kuchukua Bima za watu ambazo ni security Yao. Lilikuwa liuaji lile na Mungu akalinyoosha.

Sasa Tunamuomba Mh. Rais wetu Samia Suluhu Hassan aziache hizi taasisi hasa ambazo zimeshikilia uhai kama Bima ya Afya na hizo za Pensheni maana nako pension kupata kwa wakati ni mtihani. Tumechoka Sana Watanzania tulio wengi.
Leo nimeona hii....
Screenshot_20220330-182727.jpg
 
Mkuu kwenye mafao tatizo kubwa walichota pesa wakaacha kulipa wastaafu mafao ya mkupuo kwa wakati mpaka Yale ya mwezi. Matokeo take kuna malimbikizo ya kufa mtu. Hivyo hauwezi kabisa kuhimili makusanyo ya mwezi. Yaani lile Jamaa kichwani lilikuwa Empty Set kabisa. Yaani mtu unastaafu unafuatilia mafao hupati wakati inatakiwa siku unaondoka utumishi na siku hiyo hiyo yaingie. Mpaka wengine wamefariki kwa pressure ya kutopata mafao kwa wakati.
 
Mifuko binafsi itaibuka sasa na kupiga pesa
 
Mifuko binafsi itaibuka sasa na kupiga pesa
Kwenye Afya kuna gharama kubwa Sana angalia nchi zote zenye lifespan ndefu wamewekeza kwenye Afya na gharama za Matibabu ziko Juu
 
Back
Top Bottom