Binadamu tunaishi ili iweje? Au tupo duniani kufanya nini? Why Do We Live?

Binadamu tunaishi ili iweje? Au tupo duniani kufanya nini? Why Do We Live?

Dini za sasa zimekuwa zikipotosha watu na kushawishi watu kuwa wameumbwa wamtumikie Muumba wao lakini sio kwamba hapo sahihi, wapo sahihi lakini maana kamili imepungua uhalisia.

Sisi ni ulimwengu ulioendelea kwa mageuzi mpaka ukajitambua yaani kuwa na consciousness. Kinachofanya wewe uwepo ni ufahamu wa uwepo wako au consciousness yako. Kama ungekuwa hauna consciousness usingekwepo kwani ungekuwa hauna tofauti kati yako wewe na consciousness nyingine au wanadamu wengine. Nikimaanisha kuwa Consciousness yako au ufahamu wako ndicho kinachokutenganisha wewe na wanadamu wengine.

Mwanadamu ni zaidi ya dini zisemwavyo kuhusu yeye. Mwanadamu ni Image ya Muumbaji iliyojitambua au Sehemu ya Muumba (Sura na mfano wa Muumba wake). Lengo lake ni Kuwa na ufahamu sawa na aupendao Muumba au Ulimwengu kwa ujumla (Maana hata neno Mungu ni dogo sana kuelezea uwezo wake au kumuelezea, ila Muumba ni Ulimwengu kwani vyote vipo ndani yake).

Tumepewa miili na uhalisia wa kifizikia (kuonekana) kwa ajili ya kuwakilisha hisia na roho zetu kwa bila mwili vitu kama hisia usingeweza kuvionyesha kwani roho haina hisia. Pia mwili nao ni kipingamizi cha mwanadamu kujitambua kwa ujinga mwingi hutokea pale mwanadamu anapouhudumia mwili na sio roho. Mfano mwanadamu anaiba kupata pesa ambayo hutumia kuutumikia mwili badala ya roho, mfano kunywa pombe, wanawake, anasa, ufahari, utajiri, n.k. Vyote ni upotofu kwani tunapaswa kuitumikia roho, na kutumikia roho ni kusikiliza nafsi katika haki. Ndio maana kila ufanyapo kosa nafsi hukusuta kwani hujaitumikia bali umetumikia EGO. Na ndio maana wakuu wa imani kama Yesu, Buddha n.k walifundisha ili kujitambua acha kila ulicho nacho wakiwa na maana na uache EGO au SELF au ubinafsi na badala ya kutumikia mwili tumikia haki, amani, upendo, viumbe, dunia na sio mali, tamaa n.k

Thumuni la safari hii hapa duniani ni kujifunza, kujitambua, kusafisha roho zetu na kuishi katika upendo, haki, amani na kuachana na ujinga na tamaa.

Bless.
 
Umeelewa nilichokuuliza?

Nimekuelewa nami nakuuliza yaliyopo yapo ktk context IPI? Ni ktk context gani unaweza elezea biblia imezungumzia habari za teknolojia ya kompyuta?

Maana msigi Wa swali lako la awali ilikua ni kujua kipi hakimo kwenye biblia nimekwambia kompyuta unaniuliza kwa context IPI bila kwanza kujibu Kama ndiyo au hapana...
 
Utii huwezi kuutenganisha maana mauti ililetwa kwa wale walio kosa utii na Adam akaonekana kutotii kwa hiyo adhabu yake ni kufa milele na ndiyo ilikuwa hukumu.
Kwa nini awe Yesu well!
Sijajua wewe ni atheist au but I need to answer vividly.
Gharama ya ukombozi wa mwanadamu aliyeanguka ilifaa tu kwa damu kumwagika na Sio damu yeyote ile na Mungu kwasababu alitenganishwa Mawasiliano na mwanadamu kwa dhambi ilipaswa aje kwa mfumo wa mwanadamu ili amkomboe fillipi 2:5-9
Zaidi sana umbo la kibinadamu lilitumika kumkomboa mwanadamu kwa njia ya kristo Yesu

Imekaa kihadithi sana, jaribu kwende mbele zaidi
 

Bila-shaka hakuna swali lisilo na jibu japokuwa kila jibu litolewalo si lazima liwe sahihi. Waulize swali moja wanafunzi wa chekeachea, shule ya msingi, sekondari na vyuo kwa nini unasoma shule?

Majibu mengi yaliyotolewa yalikuwa majibu ya kunakili kutoka kwa wazazi au walezi wa hao watoto. Wangi wao walisema wanasoma hili maisha yao ya baadaye yawe mazuri. Nilipowauliza nini maana ya maisha mazuri?

Nilipokuwa nasoma chekechea ak.a kindergarten mwalimu alinifundisha kuwa moja toa mbili jibu lake ni haiwezekani. Nilipoingia darasa la kwanza mwalimu huyo huyo wa chekechea akanifundisha kuwa moja toa mbili jibu lake ni (-) hasi moja. Swali moja majibu mawili tofauti lakini yote ni sahihi.

Baada ya maelezo hayo machache nikukaribisheni mtoe maoni yenu katika kujibu swali hilo hapo juu.

jibu lake ni rahisi sana, kile kila mtu anakifanya hapa duniani basi ndo lengo lake la kuwa hapa, kama wewe kazi yako ni kutumikia wengine juwa ndo kilichokuleta hapa duniani. Ukiona Simba anakula swala basi juwa hiyo ndo kazi iliyomleta, ukiona unakufa halafu unageuka mbolea kwa ajili ya mimea juwa ndo moja ya lengo lako kuwepo hapa duniani.
 
Dini za sasa zimekuwa zikipotosha watu na kushawishi watu kuwa wameumbwa wamtumikie Muumba wao lakini sio kwamba hapo sahihi, wapo sahihi lakini maana kamili imepungua uhalisia.

Sisi ni ulimwengu ulioendelea kwa mageuzi mpaka ukajitambua yaani kuwa na consciousness. Kinachofanya wewe uwepo ni ufahamu wa uwepo wako au consciousness yako. Kama ungekuwa hauna consciousness usingekwepo kwani ungekuwa hauna tofauti kati yako wewe na consciousness nyingine au wanadamu wengine. Nikimaanisha kuwa Consciousness yako au ufahamu wako ndicho kinachokutenganisha wewe na wanadamu wengine.

Mwanadamu ni zaidi ya dini zisemwavyo kuhusu yeye. Mwanadamu ni Image ya Muumbaji iliyojitambua au Sehemu ya Muumba (Sura na mfano wa Muumba wake). Lengo lake ni Kuwa na ufahamu sawa na aupendao Muumba au Ulimwengu kwa ujumla (Maana hata neno Mungu ni dogo sana kuelezea uwezo wake au kumuelezea, ila Muumba ni Ulimwengu kwani vyote vipo ndani yake).

Tumepewa miili na uhalisia wa kifizikia (kuonekana) kwa ajili ya kuwakilisha hisia na roho zetu kwa bila mwili vitu kama hisia usingeweza kuvionyesha kwani roho haina hisia. Pia mwili nao ni kipingamizi cha mwanadamu kujitambua kwa ujinga mwingi hutokea pale mwanadamu anapouhudumia mwili na sio roho. Mfano mwanadamu anaiba kupata pesa ambayo hutumia kuutumikia mwili badala ya roho, mfano kunywa pombe, wanawake, anasa, ufahari, utajiri, n.k. Vyote ni upotofu kwani tunapaswa kuitumikia roho, na kutumikia roho ni kusikiliza nafsi katika haki. Ndio maana kila ufanyapo kosa nafsi hukusuta kwani hujaitumikia bali umetumikia EGO. Na ndio maana wakuu wa imani kama Yesu, Buddha n.k walifundisha ili kujitambua acha kila ulicho nacho wakiwa na maana na uache EGO au SELF au ubinafsi na badala ya kutumikia mwili tumikia haki, amani, upendo, viumbe, dunia na sio mali, tamaa n.k

Thumuni la safari hii hapa duniani ni kujifunza, kujitambua, kusafisha roho zetu na kuishi katika upendo, haki, amani na kuachana na ujinga na tamaa.

Bless.

Umeeleza vema sana mkuu,..wish watu wote tungejua huu ukweli kuhusu maisha yetu_dunian pangekua mahali pazuri sana pa kuishi.

BTW....Wellcome back mkuu Apollo_longtime no see you in here.
 
Sio hadith katika ulimwengu Wa theological analysis any thing based on theology you must apply the context. But what I saw in your mind it seems you have your own answer but the truth I have already gave you.
Kingine ni kwamba in human mind take it for me you can't conclude about the knowledge of God surely its above of our understanding.
Thus why God always will main God and the mystery of God to incarnate with human and to save the stupidity human who decided to fall with his motive will remains mystery forever.
My point is every human discuss what he only understand about God.
 
Nimekuelewa nami nakuuliza yaliyopo yapo ktk context IPI? Ni ktk context gani unaweza elezea biblia imezungumzia habari za teknolojia ya kompyuta?

Maana msigi Wa swali lako la awali ilikua ni kujua kipi hakimo kwenye biblia nimekwambia kompyuta unaniuliza kwa context IPI bila kwanza kujibu Kama ndiyo au hapana...

Hukuelewa kabisa nilichokuuliza na ndio maana unaendelea kufanya makosa

Nilikuuliza kile ambacho wewe unadhani hakijaandikwa kwenye Biblia,ukaja ukaniambia ndege na tarakilishi,nikakuuliza kwa context gani,ukaja kuiuliza tena mimi kwani kilichoandikwa kimeandikwa kwa context gani,hii inaonesha hujanielewa kwasababu mimi nilitaka kujua wewe unadai ndege na tarakilishi havijaandikwa kwa context ipi ili nikujibu

Aina ya swali lako linaonesha kama nakubali vimeandikwa wakati hata huko sijafika na hapo ndipo inapoonesha kwamba hukunielewa na bado hunielewi!
 
Hukuelewa kabisa nilichokuuliza na ndio maana unaendelea kufanya makosa

Nilikuuliza kile ambacho wewe unadhani hakijaandikwa kwenye Biblia,ukaja ukaniambia ndege na tarakilishi,nikakuuliza kwa context gani,ukaja kuiuliza tena mimi kwani kilichoandikwa kimeandikwa kwa context gani,hii inaonesha hujanielewa kwasababu mimi nilitaka kujua wewe unadai ndege na tarakilishi havijaandikwa kwa context ipi ili nikujibu

Aina ya swali lako linaonesha kama nakubali vimeandikwa wakati hata huko sijafika na hapo ndipo inapoonesha kwamba hukunielewa na bado hunielewi!


Mkuu acha siasa zama kwenye hoja awali uliuliza kitu gani hakimo kwenye biblia nikakwambia kompyuta na ndege wajibu wako ulikua kupinga kwa kuionesha ilipo au kukubali kuleta mpanuko Wa mada kwa maswali ni kukimbia wajibu...

In all contexts biblia haijajadili teknolojia ya kompyuta.
 
Mkuu acha siasa zama kwenye hoja awali uliuliza kitu gani hakimo kwenye biblia nikakwambia kompyuta na ndege wajibu wako ulikua kupinga kwa kuionesha ilipo au kukubali kuleta mpanuko Wa mada kwa maswali ni kukimbia wajibu...

In all contexts biblia haijajadili teknolojia ya kompyuta.

Mtu anapotaka kujibu kwa usahihi unadhani ni siasa,sijui hii chanzo chake nini ...

Mimi kutaka kujua hasa ulichokiuliza kunakuwa siasa kwa maana ipi?

Sijui hata kama unajua maana ya "all context",haya hii hapa na jisomee mwenyewe

Danieli 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danielii, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.
 
Mtu anapotaka kujibu kwa usahihi unadhani ni siasa,sijui hii chanzo chake nini ...

Mimi kutaka kujua hasa ulichokiuliza kunakuwa siasa kwa maana ipi?

Sijui hata kama unajua maana ya "all context",haya hii hapa na jisomee mwenyewe

Danieli 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danielii, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.
Nimekwambia onesha mahali bible imeongelea kompyuta...

Maarifa kuongezeka ndio context unazungumzia?
 
Nimekwambia onesha mahali bible imeongelea kompyuta...

Maarifa kuongezeka ndio context unazungumzia?

Ndio maana nilianza kukuuliza kwanza kabla ya kufika huku kwasababu nilijiua kutakuwa na haya maswali ambayo kama ungekuwa unatafakari hata kidogo tu ungeona kuwa yameshajibiwa na huo mstari niliouweka

Nilikuuliza ni kwa maana ipi unataka tarakilishi itamkwe kwenye biblia na hukuelewa sasa unauliza swali ambalo tungesaidiana kuliondoa ili tusipoteze muda lakini hukutaka ....

Sina namna ya kukusaidia hapa!
 
Kuna haja yeyote ya kitu kuwepo kama hakuna sababu ya uwepo wake?

Hujajibu swali.

Pia, unapoongelea "sababu" inabidi unyambulishe unamaanisha nini?

Sababu inaweza kutafsiriwa kama "cause" au "purpose".

Unamaanisha ipi?

Unajua tofauti yake?
 
Hujajibu swali.

Pia, unapoongelea "sababu" inabidi unyambulishe unamaanisha nini?

Sababu inaweza kutafsiriwa kama "cause" au "purpose".

Unamaanisha ipi?

Unajua tofauti yake?

Wakati mwingine maswali yako huwa yana maana sana ......!!
 
Back
Top Bottom