Binafsi nimeguswa na funga ya wakristo kipindi hiki cha kwaresma,Funga yenu haina kelele Wala majisifu

Binafsi nimeguswa na funga ya wakristo kipindi hiki cha kwaresma,Funga yenu haina kelele Wala majisifu

Kwenda kufuturu mbona maaskofu wako wanaenda😅😅... Ramadan ni heshima hata nyie mnakuja ofisini mmevaa vizuri ...Jamaa anaumia hata wao hawafungi .
 
Ukisikia muislamu anasema ukristo sio dini huyo mtu kakosa elimu sahihi ya dini!
Iwe kuabudu masanamu ni dini , kuabudu misalaba ndio isiwe dini!
Kwa taarifa yako hata upagani ni dini!
Dini ni aina yoyote ya mfumo wa maisha ambao mtu kauchagua kuwa ndio mwongozo wa maisha yake.
Kwa hiyo yule anayeabudu mizimu basi hiyo ndiyo dini yake na anayeabudu jua, mwezi, nyota, moto, mawe nk hcho anacho kuabudu na utaratibu wa kuabudu hiyo dini yake !
Kwahiyo uislamu ni dini, ukristo ni dini, uyahudi ni dini, ubudha ni dini, uhindu ni dini, ubaniani ni dini nk.
Dini ziko nyingi sana ila DINI YA HAKI NA SAHIHI MBELE YA ALLAAH NI UISLAMU kama alivyosema mwenyewe Allaah katika Suurat Aali Imrani Aya ya 19 ya kwamba :,
"{ إِنَّ ٱلدِّينَ عِندَ ٱللَّهِ ٱلۡإِسۡلَٰمُۗ
Bila ya shaka Dini (ya haki na sahihi)mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. "

Na akasema pia katika sura hiyohiyo Aalu Imrani Aya ya 85 ya kwamba :.
"{ وَمَن يَبۡتَغِ غَيۡرَ ٱلۡإِسۡلَٰمِ دِينٗا فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡهُ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ }

Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kupata hasara"
Uko sahihi ,kila mtu ana dini.
 
Ongezea na hii.... Hakuna kufatiliana kama umefunga kwani kufunga ni kati ya mtu na Mungu na siyo kuwindana nani anakula ili kuchapana viboko na kupeana majina ya ajabu ajabu.
Mbaya zaidi ni pale ambapo hadi vitoto vya darasa la kwanza na la pili vinalazimishwa kufunga! Sijui kwa dhambi gani vilizonazo masikini na sijui kama vinaelewa maana ya kufunga au wanavitia kwenye mkumbo tu na kuvitesa bure kwa sababu ya ujinga wa kutoelewa maandiko
 
Mbaya zaidi ni pale ambapo hadi vitoto vya darasa la kwanza na la pili vinalazimishwa kufunga! Sijui kwa dhambi gani vilizonazo masikini na sijui kama vinaelewa maana ya kufunga au wanavitia kwenye mkumbo tu na kuvitesa bure kwa sababu ya ujinga wa kutoelewa maandiko
Utaumia sana kama hautokuwa busy na mambo yako ,unaumia hayo tu ila omba omba unawapita pale acha unafiki ni mpumbavu.

Waislamu tutaendelea mpaka siku ya mwisho ,wewe mwenyewe mbinafsi unafuatulia ya wengine ...Fanya yako uislamu unakua kwa kasi sana utaendelea kukonda.

Sisi hatujui ya kwenu ila nyie mnajua yetu 😅
 
Funga ya kristo ni kufunga usiku na mchana siku 40.
Siyo unafunga mchana usiku unakula halafu ujiita mkristo!
Mkristo gani mroho mwenye Imani ndogo anayeshindwa kujifunza kwa kristo?!

Yesu alifunga siku 40 kwa kusudi la kipekee, lakini hakuagiza Wakristo kufunga kwa namna ileile. Badala yake, aliwahimiza kufunga kwa dhati, kwa moyo safi, na kwa uongozi wa Mungu. Ndiyo maana Wakristo hufunga kwa njia tofauti, kulingana na uelewa wao wa kiroho na mazingira yao.

Yesu alifunga kwa muda wa siku 40 mfululizo jangwani (Mathayo 4:1-2, Luka 4:1-2). Alifanya hivi kama maandalizi ya huduma yake ya kuhubiri na kuokoa wanadamu. Pia, ilikuwa njia ya kushinda majaribu ya Shetani na kujionyesha kuwa Mwokozi wa kweli aliyekuwa tayari kufuata mapenzi ya Mungu kikamilifu.

Hakuna sehemu maalum katika Biblia inayotoa agizo moja la kufunga kwa Wakristo wote kwa namna fulani au kwa muda fulani. Hata hivyo, Yesu alizungumzia kufunga kama tendo muhimu la kiroho:

• Mathayo 6:16-18 – Yesu alisema, “Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki…” Akimaanisha kuwa kufunga ni tendo la binafsi kati ya mtu na Mungu.


• Mathayo 9:14-15 – Yesu alisema wanafunzi wake hawatafunga wakati akiwa nao, lakini watakapofiwa naye, watafunga.


• Matendo 13:2-3, 14:23 – Kanisa la mwanzo lilifunga kabla ya kufanya maamuzi makubwa kama kuchagua viongozi.


Tofauti katika kufunga kwa Wakristo zinatokana na mambo kadhaa:


1. Uhuru wa Kiroho – Hakuna amri ya lazima ya kufunga kwa siku 40 kama Yesu, hivyo Wakristo wana uhuru wa kufunga kulingana na hali zao za kiroho na kimwili.


2. Mazingira na Uwezo – Yesu alikuwa jangwani peke yake, bila shughuli za kila siku, lakini Wakristo wengi wana majukumu ya kila siku yanayohitaji nishati.


3. Desturi za Madhehebu – Madhehebu tofauti yana mitazamo tofauti kuhusu kufunga. Mfano:


• Wakatoliki hufunga kipindi cha Kwaresima (Lent).


• Waprotestanti wengi hufunga kwa namna zao binafsi.


• Waorthodoksi wana vipindi vya kufunga mara kadhaa kwa mwaka.


4. Uongozi wa Roho Mtakatifu – Wakristo wanahimizwa kufunga kwa uongozi wa Roho Mtakatifu, si kwa sheria ngumu.
 
Yesu alifunga siku 40 kwa kusudi la kipekee, lakini hakuagiza Wakristo kufunga kwa namna ileile. Badala yake, aliwahimiza kufunga kwa dhati, kwa moyo safi, na kwa uongozi wa Mungu. Ndiyo maana Wakristo hufunga kwa njia tofauti, kulingana na uelewa wao wa kiroho na mazingira yao.

Yesu alifunga kwa muda wa siku 40 mfululizo jangwani (Mathayo 4:1-2, Luka 4:1-2). Alifanya hivi kama maandalizi ya huduma yake ya kuhubiri na kuokoa wanadamu. Pia, ilikuwa njia ya kushinda majaribu ya Shetani na kujionyesha kuwa Mwokozi wa kweli aliyekuwa tayari kufuata mapenzi ya Mungu kikamilifu.

Hakuna sehemu maalum katika Biblia inayotoa agizo moja la kufunga kwa Wakristo wote kwa namna fulani au kwa muda fulani. Hata hivyo, Yesu alizungumzia kufunga kama tendo muhimu la kiroho:

• Mathayo 6:16-18 – Yesu alisema, “Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki…” Akimaanisha kuwa kufunga ni tendo la binafsi kati ya mtu na Mungu.


• Mathayo 9:14-15 – Yesu alisema wanafunzi wake hawatafunga wakati akiwa nao, lakini watakapofiwa naye, watafunga.


• Matendo 13:2-3, 14:23 – Kanisa la mwanzo lilifunga kabla ya kufanya maamuzi makubwa kama kuchagua viongozi.


Tofauti katika kufunga kwa Wakristo zinatokana na mambo kadhaa:


1. Uhuru wa Kiroho – Hakuna amri ya lazima ya kufunga kwa siku 40 kama Yesu, hivyo Wakristo wana uhuru wa kufunga kulingana na hali zao za kiroho na kimwili.


2. Mazingira na Uwezo – Yesu alikuwa jangwani peke yake, bila shughuli za kila siku, lakini Wakristo wengi wana majukumu ya kila siku yanayohitaji nishati.


3. Desturi za Madhehebu – Madhehebu tofauti yana mitazamo tofauti kuhusu kufunga. Mfano:


• Wakatoliki hufunga kipindi cha Kwaresima (Lent).


• Waprotestanti wengi hufunga kwa namna zao binafsi.


• Waorthodoksi wana vipindi vya kufunga mara kadhaa kwa mwaka.


4. Uongozi wa Roho Mtakatifu – Wakristo wanahimizwa kufunga kwa uongozi wa Roho Mtakatifu, si kwa sheria ngumu.
Sioni kama ni mjadala kwa sababu mwenzio ndiye kaleta mada.


Kumbuka sisi waislamu kama mimi sijui hiyo funga yenu yaani sipatilizi ila nyie hata wenye biashara wanaweka tangazi '' Punguzo mwezi wa Ramadhan '' imekuwa kama identify na kwetu iko kwenye nguzo za Uislamu ni ibada kabisa.


Kwa vile unaona waigizaji sio wanaofunga real ,katika uislamu funga ni siri baina ya mja na mola wake ...Mtu anaweza kudanganya au kufanya uzinzi ,wizi huko machoni anajifanya kafunga.

Kufuturu pamoja ni jambi jema naona ndugu yako analia lia hapo hata viongozi wa kikristo wanakuja kujumuika ni utaratibu mzuri ..Pia, ni sehemu muhimu ya kuwakumbuka wenye uhitaji.
 
1. Yesu ni Mungu na Mwanadamu kwa Wakati Mmoja

Katika Ukristo, Yesu anafahamika kama Mungu aliyefanyika mwili (Yohana 1:1, 14). Hii inamaanisha kwamba Yesu alikuwa na asili mbili:

• Asili ya Uungu – Kama Mungu, Yesu ana uwezo wote, anajua yote, na yuko kila mahali.

• Asili ya Ubinadamu – Kama mwanadamu, Yesu alihisi njaa, uchovu, na majaribu kama binadamu wengine.

Katika Wafilipi 2:5-8, Biblia inaeleza kuwa Yesu alijinyenyekeza na akajifanya mdogo kwa kuvaa ubinadamu, ingawa alikuwa sawa na Mungu. Hii inamaanisha kwamba alipokuwa duniani, aliamua kwa hiari yake kutokuwa na baadhi ya haki zake za uungu ili aweze kuishi kama mwanadamu kamili.

2. Kwa Nini Yesu Aliruhusu Kujaribiwa?

Yesu hakujaribiwa kwa sababu alikuwa na udhaifu wa kiroho, bali kwa sababu alikuja kuwa mfano kwa wanadamu wote. Biblia inasema:

• Waebrania 4:15 – “Kwa maana hatuna Kuhani Mkuu asiyeweza kushiriki nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.”

Kwa hivyo, Yesu alijaribiwa ili aonyeshe jinsi wanadamu wanavyoweza kushinda majaribu kwa kutegemea Mungu na Neno Lake.

3. Kwa Nini Shetani Alimjaribu Yesu?

Shetani hakujaribu Yesu kwa sababu hakujua kuwa ni Mungu, bali alijaribu kumshawishi Yesu atumie nguvu zake za uungu kwa ajili yake mwenyewe badala ya kutii mapenzi ya Mungu Baba.

Majaribu aliyopitia Yesu yanafanana na yale wanadamu wanakutana nayo kila siku:

1. Kubadilisha mawe kuwa mkate (Mathayo 4:3) – Jaribu la tamaa ya mwili (njaa).

2. Kurukwa kutoka juu ya hekalu (Mathayo 4:5-6) – Jaribu la majivuno na kutaka kujionyesha.

3. Kupewa falme za dunia kwa kumsujudia Shetani (Mathayo 4:8-9) – Jaribu la tamaa ya mali na mamlaka.

Yesu alishinda kila jaribu kwa kutumia Neno la Mungu, akisema “Imeandikwa…” kila mara, akionyesha kuwa nguvu ya kweli ni katika kuitii Biblia.

4. Je, Shetani Aliwezaje Kumpandisha Yesu Juu ya Hekalu na Milima?

Katika Mathayo 4:5 na Mathayo 4:8, Biblia inasema kwamba Shetani “alimchukua” Yesu juu ya kinara cha hekalu na juu ya mlima mrefu. Hii inaweza kufasiriwa kwa njia mbili:

• Kwa kweli – Shetani alimsogeza Yesu kimwili kwa uwezo wa kipepo.

• Kwa maono – Yesu alionyeshwa haya katika maono, kama ndoto ya kiroho.

Haijalishi ilivyotokea, kilicho muhimu ni kwamba Yesu alikataa kumtii Shetani na kushikilia ukweli wa Mungu.

Yesu alijaribiwa sio kwa sababu hakuwa Mungu, bali kwa sababu alikuwa pia mwanadamu. Aliruhusu hilo ili aweze kuwa mfano mzuri kwa wanadamu na kutufundisha namna ya kushinda majaribu. Shetani alijaribu kutumia udhaifu wa kibinadamu wa Yesu (njaa, mamlaka, na utukufu), lakini Yesu alisimama kwa Neno la Mungu na hakushindwa.
 
Hivi sasa ni saa 11:25 alfajiri,naruhusiwa kudakua au nimechelewa?
Uko mkoa gani?
Kama upo Kagera, Kigoma, Rukwa na Mbeya unazo kama dakika kama 20 hivi za kula daku. Ama Kama upo mikoa ya mashariki na pwani ya bahari ya Hindi kuanzia Arusha , Kilimanjaro, Tanga, Pwani hadi Lindi na Mtwara muda wa daku imeisha.
 
Binafsi nimeguswa na funga ya wakristo wa madhehebu yote yanayofunga kipindi hiki Cha kwaresma,Funga yenu haina kelele Wala majisifu.

Sijasikia mkristo yeyote akijisifu utakatifu Kwa kufunga kwake.

Sijaona wakristo wakizuia wengine kula hadharani Wala kuonesha kuchukizwa na Hilo

Sijaona wakristo wakihangaika na vikombe vya uji Wala sahani za magimbi muda wa kufuturu.

Sijasikia wakristo wakipiga kelele alfajiri kwamba wanakula chakula Ili waweze kuvumilia njaa ya mchana kutwa Hadi muda wa kufuturu.

Sijaona vijana wa kikristo wakihangaika kwenda kula chakula kanisani kipindi hiki Cha mfungo wao.

Nimechunguza mengi Kwa wakristo na nimegundua wanafanya mambo Yao kiungwana bila kubugudhi wengine.

Nimeambiwa wakristo wanafunga siku arobaini na mwisho wa kula au kunywa ni saa 5 dakika 59 usiku baada ya hapo mkristo hatakiwi kula Wala kunywa ila wanaruhusiwa kusafisha kinywa Kwa mswaki na maji,na kuoga pia.

Hongera sana wakristo,BWANA wenu awabariki nyote katika mfungo wenu na iweni na kwaresma njema
Ukweli usemwe sisi wanaofunga ni chini ya 5%. Sio kwamba hatuna mbwembwe ukweli ni kuwa wengi wetu hatufungi.
 
Allaah ametuagiza tuwaambieni hivi :
"{ قُلۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡكَٰفِرُونَ }

Sema: Enyi makafiri!

{ لَآ أَعۡبُدُ مَا تَعۡبُدُونَ }
Siabudu mnacho kiabudu;

{ وَلَآ أَنتُمۡ عَٰبِدُونَ مَآ أَعۡبُدُ }
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

{ وَلَآ أَنَا۠ عَابِدٞ مَّا عَبَدتُّمۡ }

Wala sitaabudu mnacho abudu.

{ وَلَآ أَنتُمۡ عَٰبِدُونَ مَآ أَعۡبُدُ }
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

{ لَكُمۡ دِينُكُمۡ وَلِيَ دِينِ }

NYINYI MNA DINI YENU NA MIMI NINA DINI YANGU. .

--mwisho wa kunukuu--

Kwanini mnataka tufanane?!
Nyinyi mna dini yenu na sisi tuna dini yetu!
Nyinyi mna ibada zenu na sisi tuna ibada zetu!
Nyinyi mna sala zenu na sisi tuna swala zetu!
Nyinyi mna zaka na sadaka zenu na sisi tuna zaka na swadaqa zetu!
Nyinyi mna funga zenu na sisi tuna swaumu zetu!
Nyinyi mna hija zenu na sisi tuna hija na Umra zetu!
Msilazimishe tufanane wakati dini zetu ni tafauti na hivyo swala zetu haziwezi kufanana na sala zenu!
Zaka na swadaqa zetu haziwezi fanana na zaka na sadaka zenu!
Swaumu zetu haziwezi fanana na funga zenu?
Hija zetu haziwezi fanana na hija zenu!.
Sisi tunafanya ibada kulingana na tulivyofundishwa na mtume صلى الله عليه وآله وسلم wala hatuigi dini ya mtu yeyote kwa sababu
NYINYI MNA DINI YENU NA SISI TUNA DINI YETU katu! Ibada za kiislamu haziwezi fanana na ibada za dini yoyote nyingine.
Sasa kama mnaona nyinyi ndio mnafunga sawasawa endeleeni hivyohivyo na sisi tunafunga kulingana na tulivyofundishwa na mtume wetu
صلى الله عليه وآله وسلم.
Lakini mwisho nawauliza tena swali ambalo hamtaki kulijibu.
Yesu alifunga siku arobaini usiku na mchana!
Nyinyi ni shetani gani aliwafindisha kufunga mchana na kula usiku?!
Andiko la kuruhusiwa kula usiku mumefundishwa na nani?!
Kwanini mnashindwa kumuiga bwana yesu au imani zenu ni ndogo ?!
Kulinganisha haina maana ya kulazimisha kufanana,

Lakini pia yote uliyosema hayana uhalisia kwa sababu ukristu na biblia vilikuwepo kabila ya uislamu uliokuja miaka 500 baadae. Kwa hiyo kama kwenye uislamu kuna Zaburi na Torati pamoja na mitume kama Mussa bhasi hapo utajua vilitokea wapi

Na kingine hakuna mkristu aliyewahi kuforce mitume wala desturi zenu kufanana na ukristu ila ni waislamu ambao huwa wanamtanabaisha Yesu kama nabii Issa na Bikira Mariamu kama Maryam mama wa nabii Issa mwenye sura nzima kwenye Quran..

Hakuna mkesha wa wakristu unaoongelea uislamu HATA SIKU MOJA ila ni ninyi waislamu ambao huwa mnaweka mihadhara ya kuchambua Biblia na ni juzi tu mliweka muhadhara wenye jina YESU...

Kwa hiyo HAKUNA MKRISTO katika SESSION zal ukristu zenye kutaja UISLAMU ila ni ninyi waislamu ambao huwa mnautaja ukristu na Yesu katika session zenu..

Kwa kawaida yangu huwa sijihusishi na mijadala ya dini kwa mlengo huu ila kwa upotoshaji walo imebidi nikuweke sawa kutokana na uhalisia.. WAKRISTU hawana obsession na uislamu ila vice versa is true
 
Maaskofu wenu, wachungaji na maparoko wakialikwa iftaaaaaari ikulu au kwa kiongozi yoyote wa mkoa au wilaya au kwa tajiri fulani wanakuwa wakwanza kuwahi nafasi kuwashinda hata hao waislamu waliofunga na mkitaka ushahidi wa picha naweka!.
Hiyo inaitwa socialization
 
kila mtu ashinde mechi zake BOSS
We mwenyewe hapo unakubari huu mwenzi wa ramadhani unauona kabisa huu ni mwenzi wa ramadhani 7bu unaona kila MUISLAM anafunga katika kutaka kupata AFYA na MSAMAHA kwa mola wake
ipo hivyo

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app

Na ile kupiga kelele na vopaza sauti kila siku kuanzia saa 2 usiku hadi saa 4 usiku inahusianaje na kufunga? Yaani ukipita kwenye mitaa ya misikiti ni mwendo wa kelele. Sijui wanao kaa karibu na misikiti wanaishije.
 
Back
Top Bottom