Binti kamaliza form 6 na ndoto za kusomea udaktari kwa matokeo ya Division 1 ya 9; Physics C, Chemistry C, Biology C, Maths C, amekosa mkopo

Binti kamaliza form 6 na ndoto za kusomea udaktari kwa matokeo ya Division 1 ya 9; Physics C, Chemistry C, Biology C, Maths C, amekosa mkopo

Sio fake Kwa sasa BAM unaweza kufaulu kwa grade yoyote ile had A unapata ukifaulu na sio kuandikiwa S
Hizo credit kwenye Mathematics ni fake kwa sababu combination ilikuwa ni PCB na Maths alisoma kama subsidiary ambayo akifaulu huwa ni S na si zaidi ya hapo ila pungufu ya hapo huwa ni F! Usitudanganye hapa!
 
1 point 6 anapata,tena PCB
Labda kama course imejaa,kwa maana ufaulu Mwingi Wa 1.3 mpaka 1.5
Aopt Course Nyingine,Mkopo Chap
Hivi huwa mnasoma vizuri kweli mada,ni wapi kasema binti ana 1.6?
 
Acha uongo,mbona allocations za mikopo bado hata deadline haijafika?na pia udaktari ni unapewa mkopo tena 100%

Sijasema uongo, nimepewa maelezo nakaona sielewi heri nije kwenu kwa ushauri
 
Uko sahihi BAM siku hizi unawekewe credit
 
Nadhani kuna kitu hajui kuhusu mikopo, kwanza majina ya mikopo kwa mwaka huu bado hayatolewa, na kwa ufaulu wake mkopo atapata 100% lakini kwa vyuo vya private itabidi aongezee ada ambayo pamoja na kupata mkopo ataongezea kama mil 2.5+, ambayo nadhani hawezi kuimudu.

Mshauri aombe UDOM, awamu ya pili, kama akikosa hapo basi aombe kozi nyingine ambayo anaweza soma, au aende kwenye taasisi nyingine za ufhadhili kama MO foundation.
 
Kwahio BAM ina A ?
Na Je PCB Ukipata AAF na BAM A hapo una point ngapi ? Je wanaweza wakaacha hayo masomo yako principal na wakachukua hili subsidiary na ukawa na point 3 ?

Total Confusion.... Anyway kila zama na vitabu vyake....
 
Na Je PCB Ukipata AAF na BAM A hapo una point ngapi ? Je wanaweza wakaacha hayo masomo yako principal na wakachukua hili subsidiary na ukawa na point 3 ?

Total Confusion.... Anyway kila zama na vitabu vyake....
Hiyo ipo tu lakini kwenye ufaulu wa kombinesheni haihesabiwi. Zinahesabiwa zile za PCB tu. Haiongezi wala kupunguza point zako.
 
Aliye pata division 1 ya PCB anakosaje mkopo? na wakati bado kuna second na third selections zinakuja mwezi September?
 
Habari za jioni wakuu mabibi na mabwana

Huyu binti namfahamu tangu akiwa mtoto. Anatoka kwenye mazingira magumu kuliko ngumu wenyewe.

Hamjui baba yake mzazi, hajawahi kumsikia wala kumuona.

Mazingira ambayo mama yake hawezi kumiliki hata simu ya elfu20, hawezi lipa kodi vyumba2 vya elfu 60 uswahilini kwetu huku, hana uhakika wa kulisha watoto wake milo miwili kwa siku lakini amepambana hadi binti kafika kidato cha sita kwa msaada wa serikali na amepata hayo matokeo hapo.

Alipofaulu kidato cha nne kwenda kidato cha tano mkoani hata nauli wachana na Ile ada ya elfu70 ya Magufuli ilikua shughuli kubwa. Wakati wa kufunga shule ndio ilikua hadi walimu wapige simu kwa namba atakazowapa za ndugu na jamaa ndio arudi njiani. Yaani kwa kifupi amekua kwenye mazingira magumu nyakati zote shuleni na nyumbani

Pamoja na kuwa amesoma shule zetu za serikali tangu chekechea hadi kidato cha sita na matokeo yake ni hayo hapo, amejitahidi kadri ya uwezo wake kwa lengo la kuja kusomea masomo ya utabibu kama udaktari au maana ya lakini leo nimeumia kidogo baada ya kumkuta kajikunyata kwa huzuni baada ya kukosa ufadhili au mkopo wa serikali kwa kozi hizo ambazo ada zake zipo juu

Nimewaza nikaona nije hapa jukwaani kwa wajuzi wa mambo maana najua hapa kuna wazoefu, walimu, wasomi, washauri, wazazi wenye mapenzi mema labda Huyu binti anaweza saidika

Mtoto wa mwenzio no mtoto wako, natanguliza shukrani

Nawasilisha🤝

Cc Dada Ummy Wizara ya Afya Tanzania
Amekosa udahili au ufadhili? ninachojua yametoka matokeo ya udahili,round ya pili imeshafunguliwa.aombe tena.ajaribu na vyuo vya private
 
Amekosa udahili au ufadhili? ninachojua yametoka matokeo ya udahili,round ya pili imeshafunguliwa.aombe tena.ajaribu na vyuo vya private
Ada ya private kwa maelezo haya sidhani kama ataweza, mkopo anawezapata lakini ada ya private ni mil 5+, pamoja na kupata mkopo itabidi aongeze ada ambayo hatamudu.
 
Mambo yako tight sana siku hizi..... Div. 1.9 PCB siku hizi sahau kupata kozi za afya,siyo udaktari tuu hata ufamasia,nursing,maabara...

Cha msingi hapo ajaribu kuomba nursing na maabara anaweza kupata..
 
Back
Top Bottom