Binti wa Dkt. Wilbert Kleruu atoa ya moyoni

Binti wa Dkt. Wilbert Kleruu atoa ya moyoni

Mkuu wa Mkoa wa iringa Dr. Kleruu alidhani kila mtu ni mkristo kwa kumlazimisha Mzee Saidi mwamwindi aache kulima ili asherehekee Krismas matokeo yake ndiyo hayo! mauaji dhidi ya binaadamu wenzetu hayakubaliki! lakini kutumia mamlaka uliyopewa na wananchi kuwadhalilisha raia zako pia haikubaliki!
Uamuzi wa binti wa dr. Kleruu kutaka kujenga mahusiano na familia ya Marehemu Saidi Mwamwindi ni uamuzi wa busara ambao kila mpenda amani atayakaribisha! ila kifo cha Kleruu ni fundisho kwa kila dikteta na kiongozi anaeongoza kimabavu!

Kisa kizima cha mauaji ya Dr. Kleruu gonga hapa: Raia Mwema - Kwa nini mkulima Mwamwindi alimpiga risasi RC Dk. Kleruu? VII

Ninadhani unakosea kusema haya uliyoyasema. Dr. W.Kleruu alikuwa Mkristo, siku aliyopigwa risasi ilikuwa siku ya X-mas siku kuu ya Wakristo, ambapo yeye hakuenda Kanisani na badala yake alikwenda kuangalia kazi za kilimo. Kuna sababu zingine tofauti na muono wako ambazo zimejificha nyuma ya pazia kufuatia mauaji hayo. Mwaka 1971 mimi nilikuwa ninaishi Iringa vijijini nikiwa kijana mkubwa wa takribani miaka 18.
 
Duu sawa na ile ya DC kagera kuwachapa waalimu viboko.Hawa watawala wa ccm hawa!!!
Umenikumbusha Mnali,hivi yuko wapi huyu DC baada ya kuachishwa,lakini kwa mazingira fulani hapa Taqnzania tunahitaji watu kama Mnali ili warudishe discpline na uetndaji kazi unaotakiwa.I personally like Mnali
 
Kama unaijua familia ya kina Mwamwindi, usijipendekeza! Tafuta mbinu mbadala wakutambue.... Washenzi kweli hawa, unatoa uhai wa mwenzako wewe mungu? BORA ULINYONGWA KWA KAMBA, maana ilistahili kunya mavi wakati wa kunyongwa!
 
Dr. Kleruu alipofika shambani kwa Mwamwindi asubuhi ile kitu cha kwanza akamuuliza "mbona unafanya kazi siku ya Krismasi"?

That right there tells you that Mzee Kleruu alikuwa na psychological problems and was calling for his fate.
We umeamka Jumapili ya Xmass kwenda ku enforce ma policy ya nchi kama Mkuu wa Mkoa, halafu unamwambia mwenzako kwa nini unafanya kazi siku ya Krimasi!

Kwa hiyo tunategemea labda yeye kaja shambani kwa mwenzie kula Krismasi, tatizo kaja na fimbo, akawa anamchoma choma mkulima wakati wa maongezi. So obviously hata yeye hakuja na nia njema ya kula Xmass.

Hii ni kwa mjibu wa shuhuda au nani? Hila huyu RC alijichanganya inakuwake unamfuata mtu shambani tena siku ya Christmass tena ukiwa peke yako? Inawezekana walikuwa na visasi binafsi.
 
Mnara.jpg
<br />
<br />
&quot;Ni vigumu, kuvumilia hali hii, bali naamini haya ni matokeo na ni mipango ya Mungu kuifanya hali hii, baba yetu alikuwa ni muumini wa Ujamaa na Kujitegemea aliyesimamia sera za Ujamaa na kujitegemea kama ilivyokuwa kwa wakati ule enzi za Mwalimu Nyerere.&quot; <br />
<br />
&quot;Serikali ilikuwa inahimiza vijiji vya Ujamaa, ili wanananchi washiriki kwa pamoja kwenye Kilimo cha Kufa na Kupona, baba alifuatilia kwa kina maagizo ya Mwalimu, inawezekana hili ndilo lililosababisha kuuawa akiamini alichosimamia kilikuwa sahihi,’’anasema Eva Wilbert Kleruu huku akibubujikwa na machozi.<br />
<br />
Picture+029.jpg
<br />
<i><br />
Eva Kleruu akifuta machozi baada ya kukumbuka jambo juu ya mauaji ya baba yake miaka 43 iliyopita</i><b>.<br />
<br />
</b>&quot;Samahani umenikumbusha mbali sana miaka 43 sasa baada ya kifo cha baba yangu, nilikuwa bado binti mdogo miaka ile ya mwanzo ya miaka ya 70, baba alikuwa ni mfuasi wa Ujamaa na Kujitegemea na alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliyeagizwa kusimamia siasa ya Ujamaa na Kujitegemea,’’anasema.<br />
<br />
Anasema ni hali ambayo imekuwa ngumu kuisahau kutokana na aina ya tukio lenyewe lilivyojiri na kwamba ingekuwa kifo kile kilitokana na ugonjwa jambo hilo lingezoeleka kwa haraka, bali hata hivyo anaamini kilichotendeka kilitokana na uelewa mdogo juu ya mpango wa serikali kuimarisha vijiji vya Ujamaa na kujitegemea.<br />
<br />
Anafafanua kuwa anaamini kifo cha baba yake kilikuwa ni sawa na kujitolea mhanga katika harakati za Ujamaa na Kujitegemea kwani baba yake alikuwa ni miongoni mwa waumini wa Ujamaa ambao walisimamia na kuamini kuwa siku moja nchi inaweza kujitegemea kwa sera ya ujamaa na Kujitegemea.<br />
<br />
Anasema serikali wakati ule ilisimamia mpango kwa nia ya kuboresha huduma za wananchi wka pamoja na kuondoa ukiritimba wa ubepari kwa mtu mmoja kuhodhi eneo kubwa la ardhi jambo ambalo baadhi ya watu wasioenda maendeleo walikuwa wakilipinga.<br />
<br />
Aidha anasema hata hivyo anayofursa ya kuishukuru serikali kwa kuwajali na kuwasomesha kwa ngazi ya juu ya elimu ambapo yeye alisoma hadi nchini Burgaria na mdogo wake alipelekwa nchini Urusi katika nchi zilezile zilizokuwa zinaamini siasa ya Ujamaa na Kujitegemea.<br />
<br />
Anasema pamoja na tukio hilo kukatisha mapenzi baina ya baba na familia yake kwa kukatishwa maisha kikatili serikali ilikuwa bega kwa bega na familia ya marehemu Dkt Kleruu kwa hali na mali ambapo Mwalimu Julius Nyerere, Mzee Abeid Karume ambapo kwa bahati mbaya mzee Karume aliuawa akiwa katika harakati za kuendelea kuienzi familia hiyo.<br />
<br />
&quot;Mzee Karume alikuwa upande wetu sana alijitahidi kwa hali na mali kuhakikisha tunaishi kwa upendo, amani na utulivu, lakini bahati mbaya naye aliuawa mwaka uliofuatwa kwa risasi,’’ anazungumza Eva huku akibubujikwa na machozi.<br />
<br />
Anasema hata mrithi wa Marehemu Karume Mzee Aboud Jumbe naye aliendeleza mahusiano ya kuijali familia yetu ambapo pia Mzee Rashid Kawawa na Mama Getrude Mongela nao walikuwa mstari wa mbele katika kutufariji.<br />
&quot;Mama yetu bado yupo hai amestaafu alikuwa akifanya kazi katika ofisi ya Mkuu wa mkoa, baada ya kutoka Iringa kufuatia mauaji yale tulirudi Moshi, tukaendelea kusomeshwa na serikali Mzee Karume alikuwa mstari wa mbele kutusaidia.<br />
<br />
Picture+036.jpg
<br />
<br />
<br />
‘’Mama yetu kwa sasa anaishi Moshi, niko na wadogo zangu, watatu, mmoja anaitwa Andrew, mwingine Carmen ambaye ni Bibi Afya na Edwin ambaye ni mjasiriamali wote tulisomeshwa kwa ngazi za juu, tunaishukuru serikali kwa kutujali,’’ anabainisha.<br />
<br />
Kadhalika anasema kuwa katika kuendelea kujisahaulisha tukio lile la kikatili lililofanywa dhidi ya baba yake amepanga kukutana na familia ya marehemu Mwamwindi ambaye ndiye aliyemuua baba yake, ili wazungumze na kuanzisha ukurasa mpya wa maisha.<br />
<br />
&quot;Unajua visasi vinarithishwa kimaumbile, bila kukutana na familia ile vizazi vyetu vinaweza kujikuta vikiingia katika dhambi isiyotarajiwa, napenda nikutane na mtoto mkubwa wa Mzee Mwamwindi, ili tufungue ukurasa mpya wa maisha, hatujawahi kukutana hata mara moja wala hatujuani,’’ anasema Eva.<br />
<br />
Anasema nia ya kukutana naye ni kuanzisha uhusiano mpya ambao ulitoweka kwa zaidi ya miaka 40 huku viongozi wa wakati huo Mwalimu Nyerere, na Mzee Karume nao wakiwa wametangulia mbele ya haki hivyo anaamini kwa kukutana na wanafamilia hao utaanzishwa uhusiano chanya wenye lengo la kudumisha amani na utulivu.<br />
<br />
&quot;Sifikirii wala sijawahi kufikiria kulipiza kisasi, tulikaa kama familia tukamuomba Mungu atulinde na vitendo vya kishetani, tunaamini Mungu anaendelea kutulinda na kilichotokea kilikuwa ni dhamira iliyosukumwa na vitendo vya kishetani,’’ anasema Eva.<br />
<br />
Chanzo: BINTI WA DKT WILBERT KLERUU ATOA YA MOYONI, WALIOMUUA BABA YAKE MKOANI IRINGA MIAKA 43 ILIYOPITA ~ FASIHI MEDIA INC. 'Mwanafasihi Mahiri'
Binafsi namfahamu mmoja tu kati ya watoto wa mamwindi, na anafanya kazi serika
lini, sijui kama yeye ndio mkubwa ama la, kama kweli una nia nzuri ya kufanya hivyo ni heri uk
akutana nae
 
Hila huyu RC alijichanganya inakuwake unamfuata mtu shambani tena siku ya Christmass tena ukiwa peke yako?
Hii ilikuwa the low point of siasa ya Ujamaa lakini Mwalimu bado aka manage ku sink even lower, akaendeleza ukatili. Wakulima masikini wa Iringa wakachangishana hela kuleta mawakili wa kumtetea mkulima mwenzao kesi ya murder. Nyerere akatuma political police waje kuwa arrest wananchi wote, vijiji vizima, waliochanga hela ya mawakili wa Mwamwindi. How ruthless and imperial is that?

Tunamtukuza Mwalimu Nyerere, lakini kuna utu fulani alikuwa hana.

Julius Nyerere kwangu mimi ni national ID popote duniani, nenda pembe yeyote ya dunia, ukiulizwa unatoka wapi, ukisema Tanzania wanasema ooh, Nairere! Unajisikia duu, angalau na sisi historically tulitoa larger-than-life figure fulani anaefanya ka nchi ketu kanapata heshima mpaka leo. Lakini upande wa pili wa Nyerere ndio huo, kweli jamani unawafunga ndugu na marafiki wanaochangishana hela za kumtetea mwenzao mwenye kesi ya murder akipinga ma policy ya Vijiji vya Ujamaa ambavyo ulivitunga mwenyewe chumbani bila maoni ya mtu? I mean, there was no Tume ya Warioba in those days. Na waliolipa kwa damu unilateral decisions za Mwalimu ndio kama hawa wakuu wa mikoa.
 
Mkuu EMT, asante kwa hii kitu!, mimi ni interested party nilisoma na Edwin darasa moja pale Ilboru!.
Jamaa wa humble and down to earth!. Mwamwindi ndie mtu pekee Nyerere alining Capital punishment yake itekelezwe, nasikia katika utekelezaji ilisumbua, baada ya kunyogwa mara ya kwanza, hakunyongeka na kufa, then mtu akishahukumiwa kunyongwa, ukinyongwa bila kufa unapaswa kuachiliwa, maana utekelezaji wa adhabu ilikuwa ni "kunyongwa"
Nasikia ikatolewa order, sio tuu anyongwe, bali ni "anyongwe mpaka afe!", from then hukumu ya kunyongwa inapaswa kuandika "Anyongwe Mpaka Afe!"

Kiukweli hukumu hii ni "barbaric!" thanks God, we'll do away kwenye katiba mpya!, japo kwenye rasimu bado ipo!.
Pasco.



Mkuu Pascal Mayalla,

Umesema;- Saidi "Mwamwindi ndiye alikuwa mtu pekee Nyerere kusaini the capital punishment yake itekelezwe"

👆🏻sio, kweli kwamba ni huyo pekee alipata kunyongwa bali wapo wengine wachache walionyongwa na mmoja wao alikuwa ni mtanzania mwenye asili ya kihindi aliyeua mkewe kwa kutumbukiza gari yake mlima Kitonga huku mkewe akiwa ndani ili kwa tukio hilo apate manufaa fulani (malipo ya bima ?).

Unasema:- " kiukweli hukumu hii ni "Barbaric" thanks God we'll do away kwenye katiba mpya"

👆🏻Nadhani hayo ni maoni yako na kila mtu anayo fikra yake na uhuru wake kusema chochote anachoona ni kizuri, kwa maoni yangu hukumu hii siyo "barbaric" (ya kikatili) hata kidogo kwa mtu yule "mwenye hatia" kwani ukiangalia licha ya kuwepo kwa hii hukumu na adhabu lakini bado matendo ya mauaji yapo kila uchao sasa vipi hukumu ya kifo ikiondolewa?? don't you see It will be like opening a door for free perpetuation of the crime?!, maandiko yote ya Mungu yana support adhabu hiyo vipi wewe uione haifai je, unataka tuuane kama kuku??,

Na hadi pale itakapokusibu tukio la mauaji ndipo utakapoona adhabu ya kifo ni mjarabu, angalia anaingia jambazi nyumbani kwako anaua na kutoweka na fedha nk, akikamatwa afungwe tu au ??.

Nadhani tuingalie hiyo adhabu kwa mapana yake kabla hatujatoa comment yoyote.
 
Mkuu Pascal Mayalla,

Umesema;- Saidi "Mwamwindi ndiye alikuwa mtu pekee Nyerere kusaini the capital punishment yakyakee itekelezwe"

👆🏻sio, kweli kwamba ni huyo pekee alipata kunyongwa bali wapo wengine wachache walionyongwa na mmoja wao alikuwa ni mtanzania mwenye asili ya kihindi aliyeua mkewe kwa kutumbukiza gari yake mlima Kitonga huku mkewe akiwa ndani ili kwa tukio hilo apate manufaa fulani (malipo ya bima ?).

Unasema:- " kiukweli hukumu hii ni "Barbaric" thanks God we'll do away kwenye katiba mpya"

👆🏻Nadhani hayo ni maoni yako na kila mtu anayo fikra yake na uhuru wake kusema chochote anachoona ni kizuri, kwa maoni yangu hukumu hii siyo "barbaric" (ya kikatili) hata kidogo kwa mtu yule "mwenye hatia" kwani ukiangalia licha ya kuwepo kwa hii hukumu na adhabu lakini bado matendo ya mauaji yapo kila uchao sasa vipi hukumu ya kifo ikiondolewa?? don't you see It will be like opening a door for free perpetuation of the crime?!, maandiko yote ya Mungu yana support adhabu hiyo vipi wewe uione haifai je, unataka tuuane kama kuku??,

Na hadi pale itakapokusibu tukio la mauaji ndipo utakapoona adhabu ya kifo ni mjarabu, angalia anaingia jambazi nyumbani kwako anaua na kutoweka na fedha nk, akikamatwa afungwe tu au ??.

Nadhani tuingalie hiyo adhabu kwa mapana yake kabla hatujatoa comment yoyote.
Mkuu Mokaze, kwanza asante kunikumbusha yule mhindi, ni kweli Nyerere alinyonga wawili.

Lengo la adhabu zaidi ya punishment, ni correctional. Adhabu ya kifo hairekebishi lolote. Kwa nchi yetu adhabu hii inatekelezwa kwa kunyongwa kwa kamba mpaka kufa, it's very barbaric for a human being, wenzetu marekani wanatumia electric chair or lethal injection ambazo death inatokea instantly within a split of second hivyo ni less painful.

Hakuna uthibitisho wa uwepo wa adhabu ya kifo hupunguza vitendo vya mauaji. Uingereza wameifuta na matukio ya mauaji yamepungua, Marekani bado wanayo na mauji bado yako juu!.

Karibu na mitaa hii
Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo - JamiiForums
Wana JF tuungane kusema NO hukumu ya kifo - JamiiForums

Magufuli shujaa, ataka 68 wa madawa wanyongwe! Kikwete alikuwa dhaifu mno, aliomba wasinyongwe! - JamiiForums
Mhe. Rais Magufuli, Anza na Kusaini Hati za Wote Waliohukumiwa Kifo, Wanyongwe Haraka Haraka Mpaka.. - JamiiForums

Idadi ya walionyongwa tokea uhuru Tanzania ni 232 - JamiiForums

Account Suspended

P
 
Kwa maelezo nliyosimuliwa na Marehemu Bibi Yangu Miaka mingi kidogo, Bwana Kreruu alikua mkatili sana, bibi anasema siku ambayo mwamwindi alimpiga risasi taharifa zilivuma kwa haraka maeneo ya Iringa mjini na viunga vyake. Bibi anasema baada ya tu taharifa kuzagaa wakinamama wa kihehe walisogea kwenye vibongonyera (Pembe za Nyumba) wananena (Wanasema au kuomboleza) maneno ya kihehe baada s kunena hayo maneno wanapiga vigeregere.

Bibi anasema kwa wakati huo, ilikua ni kama sherehe kreruu kuuwawa, Mwamwindi kwa jamii ya wahehe alionekana kama Shujaa na Mkombozi dhidi ya udhalimu wa kreruu.

Ubaya ni kwamba Bibi Alifariki, ila nitarejea siku moja kwa wazee Kalenga kuweza kupata historia zaidi ya nini kilichotokea.
 
Mkuu Mokaze, kwanza asante kunikumbusha yule mhindi, ni kweli Nyerere alinyonga wawili.

Lengo la adhabu zaidi ya punishment, ni correctional. Adhabu ya kifo hairekebishi lolote. Kwa nchi yetu inatekelezwa kwa kunyongwa mpaka kufa, it's very barbaric for a human being, wenzetu marekani wanatumia electric chair or lethal injection ambazo death inatokea instantly within a split of second hivyo ni less painful.

Hakuna uthibitisho wa uwepo wa adhabu hiyo kupunguza vitendo vya mauaji. Uingereza wameifuta na matukio ya mauaji yamepungua, Marekani wanayo na mauji bado yako juu!.

Karibu na mitaa hii
Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo - JamiiForums
Wana JF tuungane kusema NO hukumu ya kifo - JamiiForums

Magufuli shujaa, ataka 68 wa madawa wanyongwe! Kikwete alikuwa dhaifu mno, aliomba wasinyongwe! - JamiiForums
Mhe. Rais Magufuli, Anza na Kusaini Hati za Wote Waliohukumiwa Kifo, Wanyongwe Haraka Haraka Mpaka.. - JamiiForums

Idadi ya walionyongwa tokea uhuru Tanzania ni 232 - JamiiForums

Account Suspended

P



Mkuu pascal Mayalla, labda mimi sijakupata vyema, suala ni aina ya adhabu ya kifo au adhabu ya kifo iondolewe??
 
Kwa maelezo nliyosimuliwa na Marehemu Bibi Yangu Miaka mingi kidogo, Bwana Kreruu alikua mkatili sana, bibi anasema siku ambayo mwamwindi alimpiga risasi taharifa zilivuma kwa haraka maeneo ya Iringa mjini na viunga vyake. Bibi anasema baada ya tu taharifa kuzagaa wakinamama wa kihehe walisogea kwenye vibongonyera (Pembe za Nyumba) wananena (Wanasema au kuomboleza) maneno ya kihehe baada s kunena hayo maneno wanapiga vigeregere.

Bibi anasema kwa wakati huo, ilikua ni kama sherehe kreruu kuuwawa, Mwamwindi kwa jamii ya wahehe alionekana kama Shujaa na Mkombozi dhidi ya udhalimu wa kreruu.

Ubaya ni kwamba Bibi Alifariki, ila nitarejea siku moja kwa wazee Kalenga kuweza kupata historia zaidi ya nini kilichotokea.



Mkuu Von tosy, nadhani sio jambo zuri hata kidogo kuzungumzia juu ya "unayoona mabaya" ya mtu aliyeishafariki kwa sababu yeye tena hana nafasi ya kuja kujitetea kama angaliweza kufanya hivyo angalikuwa hai na hapo ni kukosa "absolute justice", juu ya yote marehemu anao watu wa karibu naye ambao kwa namna moja waliguswa na pengine wataendelea kuguswa na msiba wa mpendwa wao pale watakaposikia marehemu akitajwa katika njia ya "ubaya", busara inataka tuyaeleze mema yake ili nasi tujifunze na kuhusu mabaya tumuachie Mungu pekee na pia zingatia hakuna mtu mkamilifu.
 



Nimeelewa, "ni kupinga adhabu ya kifo".🤔🤔

Mimi ninayo maoni tofauti kwamba adhabu ya kifo isiondolewe kwa sababu vitabu vyote vya Mungu vinaunga mkono hiyo adhabu na itolewe kwa mtu aliyekuwa na hatia ya mauaji na si vinginevyo.

Nini falsafa ya adhabu yoyote??, adhabu ina falsafa kuu mbili, kwanza ni kumfahamisha muhusika juu ya kosa lake ili arekebike na asirudie tena kosa lake na pili ni watu wengine wajifunze ili wasifanye makosa kama ya mwenzao, sasa kuhusu adhabu ya kifo falsafa ya pili ndiyo inayochukua nafasi, yaani kutokana na adhabu ya kifo watu wengine wajifunze na waogope mauaji ili amani itamalaki.

Sheria zimewekwa ili watu tuishi kwa amani na kwa ustaarabu na bila sheria zote za Mungu na zile za nchi watu tungeishi kama wanyama na mbaya zaidi watu ni wepesi sana kusahau na kupuuza licha ya sheria kuwepo "and that's human nature" sasa vipi uondoe sheria ya adhabu ya kifo??, na ukiiondoa mbadala wake unaweka kitu gani??, the sentence after death is life sentence,on implementing, the prisons will be full of life sentence culprits.

Jambo lolote ambalo Mungu ameliruhusu au kulikataza akienda kinyume nalo unajitafutia matatizo na mbaya zsidi jamii zetu hazitii sheria bila shuruti.

Lifting the murder case law is the same as opening a pandora box🤔🤔.
 
Hivi watu wameanzia wapi hadi kuanza kutukumbusha mambo ya 43 years ago? Can someone tell me how do we go from mourning the victims of MV Nyerere to discussing nineteenth centuary communism?
 
Mie nilivyosikia, kileruu, alimchukua mke wa huyo Mwamundi, tena akawa anamkejeli mwenye mke wake
 
R.I.P Shujaa wetu Mwamwindi, tutakukumbuka na ulikufa kishujaa.
 
Back
Top Bottom