Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Hahahah umelenga mule mule!
 
[QUOTE="]Huyu binti ni mpuuzi wa kutupwa ukute ndo hawa wanaonunua degree huko vyuo mbuzi marekani au degree za pichu[/QUOTE]

Wewe Uliyeandika hii Quote ndie mpuuzi halisi. Total idiot
 
Hhahahahahaaa sio kweli, saa ingine Ddadii huwa ananiandikiaga vitu vya kujibu huku JF.

Mie nnayotoa kichwani kwangu ni Mahaba tuu, mengine chaliii heheheheee

Thanks by the way.


Nakuelewa dyadya!
 
Yule jamaa wa kihindi alitushika pale ..mashatri ya scholarship yalim'bana tu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo hawatutangazi hata mie nna digrii na nauza maandazi, mi kwake sioni ajabu hapo
 
Kiukweli umeongea point ya maana lakin walio wengi humu Kwa unafki wao hatokosa sababu ya kupinga hoja yako ila kiukweli mitaji ndio inawakwamisha sana vijana katika kufikia malengo
Mitaji ya kuuza makande na ice cream na biashara kama hizo??

Hebu scan simu na nguo wanazomiliki..
Inashindikana kupunguza unbasic needs (vitu ambavyo hata ukivikosa hufi) ili kuhifadhi mtaji?

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
 
Wengine hawana mtaji,wengine ni masistaduu yaani akiwa na degree au masters ahangaike na umama ntilie wakati ana PHD ya sura na Makalio na mjini yanatoa ajira.
Hayo makande na biashara kama hizo zinahitaji mtaji shing ngapi??

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
 
Mkuu kwanza hongera

Naona umeongea kwa ghadhabu sana, nadhani lengo ni kuonesha kwamba hata watu wenye vipato vikubwa, wanafanya kazi zinazoonekana ni za watu wa hali ya chini

Hapa naona lengo kubwa ni kupeana motisha na inspiration

Ndio maana hata wewe mwenye degree na unachoma mahindi umeona kama unahitaji promotion wakati pia kuna tabaka la watu wengine wasio na degree ambao wewe/jamii inaona kama ni haki yao kuchoma mahindi

Lengo lilikuwa ni kuwaonesha watu inawezekana na wafanye kazi bila kujali kazi zao, bila kujali status zao
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa akili yako yeye hyo kazi ya kuuza makande hajachagua? Kila mtu anafanya anachopenda acha ku underate wengine.

kidonyole
 
Mitaji ya kuuza makande na ice cream na biashara kama hizo??

Hebu scan simu na nguo wanazomiliki..
Inashindikana kupunguza unbasic needs (vitu ambavyo hata ukivikosa hufi) ili kuhifadhi mtaji?

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
Umenena vyema kabisa kwani wengi tunakimbilia changamoto ya mtaji kutafuta huruma lakini ukweli mitaji ipo tatizo wengi ukiwauliza wanataka mtaji wa shilingi ngapi watakujibu milioni kadhaa wakati katika maisha ya kawaida unakuta hatuna hata laki 2 tunayomilki. Hivyo badala ya kuwaza mtaji wa kuanzia milion moja na kuendelea, tunatakiwa tuanze na kile ambacho kipo ndani ya uwezo kukipata yaani kama laki 2 tu kuishika ni tabu basi level zetu za kuanzia ziwe humo humo kwenye fifty mpaka laki 2 nina imani tukifikiria katika mtazamo huo tutatoka na ndio msemo wa wahenga unapokuja "mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe" yaani anza pale ulipo kwa wakati huo mengine yatakuja ikiwa pamoja na connections
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…