Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

nazani ulivyo fundishwa biashara ni kuuza Magari. vipi angefungua Yard ya kuuza Magari pia ungeongea hivi?

Yeye kaona furusa na bishara bi Biashara hata kama ni ya kuuza paka. kikubwa kuna profiti.

nyie ndo mmemezeswa kwamba biashara ni kuuza Magari na kufungua maduka ya nguo hizo ndo biashara mnazo zijua

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahah umelenga mule mule!
 
Kuna jamaa alikataa mshahara wa USA akarudi bongo akafungua ofisi mwaka jana ofisi yake ikashirikia shindano ikashinda zaidi ya 200M.

Huyu dada, Degree na Master ya Nje. Anauza makande.

Mimi sidhani kama mtu kufanya biz ya chini inatakiwa ihesabiwe kama inspiration kwa job seeker. Alitakiwa atuonyeshe tofauti yake kama huyo jamaa aliyekataa ule mshahara.

Hapa Tz tayari tuna degree holder anauza uji mwingine anauza mihogo. Yaani ni kwamba degree na master ya nje imewaza sawasawa na degree ya bongo jua kali.
Yule jamaa wa kihindi alitushika pale ..mashatri ya scholarship yalim'bana tu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nna degree ya SAUT nachoma mahindi hapa darajani hapa Mbeya.Huyo hafanyi biashara anajitangaza,tupo wengi huku tunatokea kwenye familia maskini mnoooo nadhani ndiyo maana hamtutangazi.....HAKUNA MTU HAPENDI KUFANYA KAZI,HAKUNA MTU ANAPENDA KULA BURE,SHIDA NI MTAJI NA KUPATA KAZI YENYEWE.
Ndiyo hawatutangazi hata mie nna digrii na nauza maandazi, mi kwake sioni ajabu hapo
 
Kiukweli umeongea point ya maana lakin walio wengi humu Kwa unafki wao hatokosa sababu ya kupinga hoja yako ila kiukweli mitaji ndio inawakwamisha sana vijana katika kufikia malengo
Mitaji ya kuuza makande na ice cream na biashara kama hizo??

Hebu scan simu na nguo wanazomiliki..
Inashindikana kupunguza unbasic needs (vitu ambavyo hata ukivikosa hufi) ili kuhifadhi mtaji?

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
 
Wengine hawana mtaji,wengine ni masistaduu yaani akiwa na degree au masters ahangaike na umama ntilie wakati ana PHD ya sura na Makalio na mjini yanatoa ajira.
Hayo makande na biashara kama hizo zinahitaji mtaji shing ngapi??

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
 
Mkuu kwanza hongera

Naona umeongea kwa ghadhabu sana, nadhani lengo ni kuonesha kwamba hata watu wenye vipato vikubwa, wanafanya kazi zinazoonekana ni za watu wa hali ya chini

Hapa naona lengo kubwa ni kupeana motisha na inspiration

Ndio maana hata wewe mwenye degree na unachoma mahindi umeona kama unahitaji promotion wakati pia kuna tabaka la watu wengine wasio na degree ambao wewe/jamii inaona kama ni haki yao kuchoma mahindi

Lengo lilikuwa ni kuwaonesha watu inawezekana na wafanye kazi bila kujali kazi zao, bila kujali status zao
Mimi nna degree ya SAUT nachoma mahindi hapa darajani hapa Mbeya.Huyo hafanyi biashara anajitangaza,tupo wengi huku tunatokea kwenye familia maskini mnoooo nadhani ndiyo maana hamtutangazi.....HAKUNA MTU HAPENDI KUFANYA KAZI,HAKUNA MTU ANAPENDA KULA BURE,SHIDA NI MTAJI NA KUPATA KAZI YENYEWE.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa akili yako yeye hyo kazi ya kuuza makande hajachagua? Kila mtu anafanya anachopenda acha ku underate wengine.

kidonyole
 
Mitaji ya kuuza makande na ice cream na biashara kama hizo??

Hebu scan simu na nguo wanazomiliki..
Inashindikana kupunguza unbasic needs (vitu ambavyo hata ukivikosa hufi) ili kuhifadhi mtaji?

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
Umenena vyema kabisa kwani wengi tunakimbilia changamoto ya mtaji kutafuta huruma lakini ukweli mitaji ipo tatizo wengi ukiwauliza wanataka mtaji wa shilingi ngapi watakujibu milioni kadhaa wakati katika maisha ya kawaida unakuta hatuna hata laki 2 tunayomilki. Hivyo badala ya kuwaza mtaji wa kuanzia milion moja na kuendelea, tunatakiwa tuanze na kile ambacho kipo ndani ya uwezo kukipata yaani kama laki 2 tu kuishika ni tabu basi level zetu za kuanzia ziwe humo humo kwenye fifty mpaka laki 2 nina imani tukifikiria katika mtazamo huo tutatoka na ndio msemo wa wahenga unapokuja "mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe" yaani anza pale ulipo kwa wakati huo mengine yatakuja ikiwa pamoja na connections
 
Back
Top Bottom