Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Kuna jamaa alikataa mshahara wa USA akarudi bongo akafungua ofisi mwaka jana ofisi yake ikashirikia shindano ikashinda zaidi ya 200M.

Huyu dada, Degree na Master ya Nje. Anauza makande.

Mimi sidhani kama mtu kufanya biz ya chini inatakiwa ihesabiwe kama inspiration kwa job seeker. Alitakiwa atuonyeshe tofauti yake kama huyo jamaa aliyekataa ule mshahara.

Hapa Tz tayari tuna degree holder anauza uji mwingine anauza mihogo. Yaani ni kwamba degree na master ya nje imewaza sawasawa na degree ya bongo jua kali.
Acha kuwaza kitoto,Kila mtu ana njia yake ya kupita,uyo aliepata mapesa mengi ndio njiaaliyoandikiwa na mungu,fanya hesabu kidogoo wunafahamu watu wenye degree walioajiriwa mishahara yao ni sh ngapi na hao wenye masters?Dada anasema anaweza kuuza mpaka sahani 40 kwa siku ambapo kila sahani anauza kwa elfu tano piga hesabu kwa mwezi anakusanya kiasi gani? na piga iyo mara mwaka ana pesa ngapi? alafu tafuta jibu kwa wenye degree na masters walioajiriwa hasa serikalini utapata jibu achana nambo ya Benja
 
Hivi kwanini watu mliofanikiwa kupata kitu fulani kwenye maisha huwa mnakosa akili na busara? Wengine tulienda shule ili tusiwe wauza karanga au wachoma mahindi,tungetaka kuchoma mahindi au kuuza karanga tungeishia kidato cha nne na kuanza kuuza karanga.....hizi kejeri mnamezeshwa na serikali yenu ya CCM kuwa vijana wajiajiri,mmeshindwa kuzalisha ajira na mmeshindwa kuwawezesha vijana kujiajiri kwa mali au hali,MSITAKE VIJANA TUONEKANE WAVIVU WAKATI TUMEWAKABIDHI HII NCHI ILI MTENGENEZE MWANGA WA MAISHA YA WATANZANIA....narudia tena HAKUNA ASIYEPENDA KUFANYA KAZI WA KULA BURE.
Inategemea unauza karanga kwa namna gani. Biashara ni ubunifu. Shule inaweza kukupa maarifa ukauza karanga kisomi zaidi. Ukawa unanua kwa jumla kutoka kwa wakulima ukawa unafanya nice packaging na kutengeneza an efficient distribution channel au business process. Hapa bado tutakuita muuza karanga lakini hauko sawa na yule muuza karanga za mia mia pale stendi. Huyo dada muuza makande si sawa na muuza makande yoyote unayemfahamu. Ana uelewa juu ya concept ya branding na market segmentation. Angalia video ona sehemu kande zinapoandaliwa na packaging inayotumika. Kande zake si za kula kila mtu, zina wateja wa class fulani. MBA yake ipo kazini hapo. Huitaji kufanya rocket science kufanikiwa. Kuongeza tu thamani kwenye kile kidogo kunaweza kukupa mafanikio ya juu. Haya tuje kwa mtu anaitwa Mak Juice/ Mak Chicken. Kipi kinamfanya awe maarufu kuzidi wenye juice bar na wauza chicken hapa Dar? Branding and Packaging plus marketing strategy yake inatumia socialites na celebrities. Huyu ni muuza juice na kuku lakini anauza kuku na juisi kwa namna ya tofatuti. Hii ndo maana halisi ya kuwa mjasiriamali. Lazima ujifunze kuwa wa tofauti .The fact kwamba huyo dada tayari anaongelewa ina maana bi9ashara yake in ina prospects nzuri. Sasa kama huna cha kujifunza ina maana una uelewa mdogo sana wa dunia inaendaje. Tujitahidi kupanua uelewa wetu wa mambo ili tuondokane na hizi aibu ndogo ndogo za kuropoka ropoka kama hatukwenda shule.
 
Habari wadau...

Nimekutana na habari ya Nancy Lema wa Mwanza nikaona ku-share nanyi wadau mtoe maoni.. je binti yupo sahihi au wrong?

Kafanya Shahada yake St Marys University of Minnesota na masters university of Minnesota huko USA.

Baada ya kumaliza masomo yake akaamua kurudi nyumbani kujiajiri kwa kuuza makande kisasa na kwao ni mambo safi hasa hasa...

Nawaza tu why dada zetu maskini hawapendi kujishughulisha huku washua hawachagui kazi.

Nimemkumbuka na Mercy Kitomari Nelwa Gelato naye ana degree ya U.K ila amerudi Tanzania anauza ice cream tu kisasa


msomi huyo kunamchongo anauandaa uki ticki,ili atoke na baadaye mbakie kusema alikuwa anauza makande tu hapa
 
Kuna point ya msingi sana kaongea ambayo Wengi wenu hamuitilii maanani. Kasema hivi fanyeni kitu mnachokipenda. Ofcoz yeye anapenda kuuza makande it doesn’t matter imemchukua miaka mingapi kutambua kwamba anapenda kuuza makande. Mbona kuna watu ni na professor kitambo but wamekuja jitambua juzi kuwa kumbe ni wanasiasa. We jiulize mpaka sa hivi hapo ulipo are happy with your job? Au ndo hivo tonge kinywani. If you do what you makes you happy money will come naturally. Na Ndo maana unaona kuna mtu ni mpiga picha na Ana passion nayo anatoboa ila we unaepiga picha sababu huna option hutakaa utoboe. Hii story itumie kujiaccess wewe zaidi kuliko huyo dada, after all nani kasema kapoteza muda? Kwani anawahi wapi?


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu hawapendi kujifunza hawa watu na kazi kujifanya wajuaji. Huu ujuaji ungekuwa na faida Tanzania ingekuwa mbali kimaendeleo. Ila wengi ni zero brain halafu hawataki kukubali kwamba hawana exposure. Ukiona tu mtu anaropoka ropoka kujifanya anajua kuna mawili, kwamba exposure yake ni ndogo, na mbili hana muda wa kujisomea kujifunza zaidi
 
Inategemea unauza karanga kwa namna gani. Biashara ni ubunifu. Shule inaweza kukupa maarifa ukauza karanga kisomi zaidi. Ukawa unanua kwa jumla kutoka kwa wakulima ukawa unafanya nice packaging na kutengeneza an efficient distribution channel au business process. Hapa bado tutakuita muuza karanga lakini hauko sawa na yule muuza karanga za mia mia pale stendi. Huyo dada muuza makande si sawa na muuza makande yoyote unayemfahamu. Ana uelewa juu ya concept ya branding na market segmentation. Angalia video ona sehemu kande zinapoandaliwa na packaging inayotumika. Kande zake si za kula kila mtu, zina wateja wa class fulani. MBA yake ipo kazini hapo. Huitaji kufanya rocket science kufanikiwa. Kuongeza tu thamani kwenye kile kidogo kunaweza kukupa mafanikio ya juu. Haya tuje kwa mtu anaitwa Mak Juice/ Mak Chicken. Kipi kinamfanya awe maarufu kuzidi wenye juice bar na wauza chicken hapa Dar? Branding and Packaging plus marketing strategy yake inatumia socialites na celebrities. Huyu ni muuza juice na kuku lakini anauza kuku na juisi kwa namna ya tofatuti. Hii ndo maana halisi ya kuwa mjasiriamali. Lazima ujifunze kuwa wa tofauti .The fact kwamba huyo dada tayari anaongelewa ina maana bi9ashara yake in ina prospects nzuri. Sasa kama huna cha kujifunza ina maana una uelewa mdogo sana wa dunia inaendaje. Tujitahidi kupanua uelewa wetu wa mambo ili tuondokane na hizi aibu ndogo ndogo za kuropoka ropoka kama hatukwenda shule.
Naona we ndo umeropoka kama hujaenda shule,kwa mtaji wa shilingi ngapi unaweza kufanya package na branding ya biashara yako kama ulivyosema hapo juu? Mshasema huyo binti ni wa kishua......WATU MKISHAFANIKIWA MNAJUA SANA KURAHISISHA MAMBO.
 
Hongera zake. Aendelee hvi hvi mdogo mdogo mpaka afungue kiwanda kama vile kwenye Food Factory!
 
Tatizo mtaji pia, sio kwamba watu hawapendi kujiajiri

Sent using Jamii Forums mobile app
Unapozungumzia mtaji ni kama shilingi ngapi mkuu? anza na kile ulichonacho "mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe". Tatizo watu wanazunguuka sana na bahasha at the time anakumbuka kufanya biashara unakuta umri umeongezeka na majukumu pia yameongezeka na rafiki zake aliosoma nao wengine wameoa ama wamepiga hatua flani ya maisha na ndipo tunapokuja na kauli ya "TATIZO MTAJI" kwa kuwa kadri umri unavyosogea ndivyo matamanio ya kuwa na mtaji mkubwa yanavyoongezeka yaani mtu anafikiria milioni 5 ama 3 kumbe mtaji hata 300,000 (laki tatu zinatosha kama ukiamua)

Nachotaka kusema hapa maamuzi ya kujiajiri yafanyike ukiwa ungali mdogo kiasi kwamba ukipata laki 200,000 inaweza ikakubadilishia maisha tofauti na mtu anaanza kuja na wazo la kujiajiri tayari amegonga 30 and above years
 
Makande hayo usije ukakuta bei yake sawa na pizza, mtoto wakishua hawezi kuuza bei local sawa na uswahilini

Sent using unknown device
 
Wewee, hivi unadhani alichukua tu mahindi na maharage akapika makande wateja wakaja? Yaani napata picha hapa uswahilini kwetu nipike tu makande watu waje kula? Kwanza jina lake tu ni mtaji tosha, umeenda kuangalia hayo makande anayauzia sehemu gani? Anayapikaje? Anayapack vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
ndo Visingizio hivyo? ninacho wapendea Wabongo wenzangu ni hapo tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani kwangu mtu yoyote aliefika kusoma au kuishi marekani au nchi za ulaya,halafu akarudi huku analialia habari za hela huo ni upopoma mkubwa,hata huyo anaeuza kande wakati amesoma marekani/kuishi marekani ni mpumbavu wa hali ya juu,siwatanii

Sent using Jamii Forums mobile app
nazani ulivyo fundishwa biashara ni kuuza Magari. vipi angefungua Yard ya kuuza Magari pia ungeongea hivi?

Yeye kaona furusa na bishara bi Biashara hata kama ni ya kuuza paka. kikubwa kuna profiti.

nyie ndo mmemezeswa kwamba biashara ni kuuza Magari na kufungua maduka ya nguo hizo ndo biashara mnazo zijua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jamaa alikataa mshahara wa USA akarudi bongo akafungua ofisi mwaka jana ofisi yake ikashirikia shindano ikashinda zaidi ya 200M.

Huyu dada, Degree na Master ya Nje. Anauza makande.

Mimi sidhani kama mtu kufanya biz ya chini inatakiwa ihesabiwe kama inspiration kwa job seeker. Alitakiwa atuonyeshe tofauti yake kama huyo jamaa aliyekataa ule mshahara.

Hapa Tz tayari tuna degree holder anauza uji mwingine anauza mihogo. Yaani ni kwamba degree na master ya nje imewaza sawasawa na degree ya bongo jua kali.
Hizi ndo mentality za umasikini. kwa mawazo haya wacha tuendelee kuajiriwa na wachina na Wahindi na wazungu.

Unataka afanye kile unacho penda wewe?

sasa kama yeye hiyo ndo Hoby yake unataka aiache kwa sababu hampendi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Piga hesabu kwasiku anapata wateja wangapi halafu zidisha mala 5000, ela anayoingiza kwa siku sidhani kama mwenye hiyo degree akiajiriwa anaweza akalipwa kiasi icho
Ana wateja wake huyo wale wazee wa CRDB ambao 70% ya mishahara yao huishia kwenye mambo ya kuupendelea mwili kuanzia kula, mavazi, usafiri na kupanga nyumba kali

Sent using unknown device
 
Lengo lake kubwa ni kujulikana tu kama kwao mboga nane matunda kibao juice na vyoda, lakini anauza makande na ame somea marekani hilo ndo lengo lake. Hakuna cha makande ya kisasa wala nini kande ni kande tu hakuna kisasa wala nini!

Sent using Jamii Forums mobile app
Idea yake haiwezi kukufurahisha wewe. vipi angefungua saloon? au vipi angefungua duka La Viatu? ungeongea? make hizo ndo biashara mnazo zijua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom