Binti wangu hawezi kuolewa na mtu maskini - Elon Musk

Binti wangu hawezi kuolewa na mtu maskini - Elon Musk

Yeah,maana anaweza akapata heart attack bintiye akimletea chokoraa
... tycoon la kimarekani kama lile linapata ripoti toka FBI bintiye yuko kwenye makambi ya wale jamaa Afghanistan au Somalia na ni mjamzito hakosi ibada! Ha ha ha!
 
Nimeamua nitafsiri mawazo ya Elon yamenivuti sana. Soma mpaka mwisho uelewe anachomaanisha kuhusu mtu maskini.
-------------------------------------------------------
Kabla ya yote, elewa kwanza utajiri haimanishi kuwa na pesa nyingi kwenye akaunti ya benki. Hatua ya awali, utajiri ni uwezo wa kutengeneza utajiri.

Kwa mfano, mtu anayeshinda bahati nasibu au kamali. Hata kama anashinda milioni 100 yeye siyo tajiri. Yeye ni maskini mwenye pesa nyingi. Hii ndio sababu asilimia 90 ya watu milionea wa bahati nasibu huwa maskini tena baada ya miaka mitano.

Pia kuna watu matajiri ambao hawana pesa.

Kwa mfano, wajasiriamali wengi wapo tayari kwenye njia ya utajiri hata kama hawana pesa, kwa sababu wanaimarisha mianya ya pesa, na huo ndio utajiri.

Ni vipi tajiri na maskini hutofautiana?

Kwa urahisi tu. Tajiri anaweza kufa na kupona ili awe tajiri, wakati maskini ataua ili awe tajiri.

Kama unamuona kijana ambaye anaamua kufunza, kujifunza vitu vipya, ambaye hujaribu kujiimarisha yeye mwenyenyewe, jua huyo ni mtu tajiri.

Kama unamuona kijana ambaye hufikiri kwamba tatizo ni nchi, ambaye hufikiri kwamba matajiri wote ni wezi, na yeye ni kukosoa tu, jua huyo ni mtu maskini.

Matajiri wanashawishika kwamba wanahitaji taarifa na mafunzo ili kuanza, lakini maskini hufikiri kwamba wengine lazima wawape pesa ili kuanza.

Katika kuhitimisha, ninaposema kwamba binti wangu hataolewa na maskini, siongelei kuhusu pesa. Ninaongelea kuhusu uwezo wa kutengeneza utajiri ndani ya mtu huyo.

Samahani kwa kusema hivi, lakini wahalifu wengi ni maskini. Wanapokuwa mbele ya pesa, wanapoteza ufikiri ndio maana wanafanya ujambazi, wanaiba, wanaua, wanatakatisha pesa nk. Kwao ni neema kwa sababu hawajui ni vipi wangeweza kupata pesa zao wenyewe.

Siku moja, mlinzi wa benki aliokota begi lenye pesa nyingi, alilichukua begi na kulipeleka kwa meneja wa benki.

Watu walimuita mtu huyu mjinga, lakini katika uhalisia mtu huyu alikuwa ni tajiri ambaye hakuwa na pesa.

Mwaka mmoja baadae, benki ilimpa ofa kama mtu wa mapokezi. Miaka mitatu baadae akawa meneja wa wateja. Miaka kumi baadae aliongoza utawala wa kanda wa benki hii. Aliongoza mamia ya waajiriwa na kila mwaka bonasi yake ilizidi kile kiwango ambacho angeweza kuiba.

Utajirini hali ya kufikiri kwanza.

Kwa hiyo, wewe ni tajiri au maskini?
 
Yuko sahihi. Masikini wa nanjilijili atakutana wapi na mtoto wa Elon?
 
NIMEGUNDUA HUMU JF KUNA MAJITU MAJINGA SN SN MAKURUPUKAJI NA UWENDA WENGI WAMESOMA THREAD TITLE TU HAWAJASOMA CONTENTS KBS nafatilia majbu mnayojbu ni kama hamjaelewa jamaa amemaanisha nn. shaaabashiiii
 
Yeye mwenyewe alikuwa njaa tupu, watu wanasahau walipotoka, kwanza mtoto wake wa kike kamkimbia na hataki uhusiano naye na mpaka jina kabadilisha hataki kuitwa Musk na hataki pesa za baba yake kasema atatengneza za kwake, lakini siku hizi Musk amezidi kuwa fala sana na racism yake iko wazi wazi sasa
 
Yeye mwenyewe alikuwa njaa tupu, watu wanasahau walipotoka, kwanza mtoto wake wa kike kamkimbia na hataki uhusiano naye na mpaka jina kabadilisha hataki kuitwa Musk na hataki pesa za baba yake kasema atatengneza za kwake, lakini siku hizi Musk amezidi kuwa fala sana na racism yake iko wazi wazi sasa
Una uhakika unaijua vyema historia ya Elon kuanzia baba yake mzazi ambaye alikuwa mfanya biashara huko Zambia?

So far umeelewa content ya thread au umekimbilia kujibu kitu ambacho ulikihifadhi kwa muda moyoni?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Elon sio masikini hivyo kuhangaika na maisha ya watoto wake, acha kumsingizia. Kwanza mtoto wake wa kiume ana mpango wa kubadilisha jinsia
 
NIMEGUNDUA HUMU JF KUNA MAJITU MAJINGA SN SN MAKURUPUKAJI NA UWENDA WENGI WAMESOMA THREAD TITLE TU HAWAJASOMA CONTENTS KBS nafatilia majbu mnayojbu ni kama hamjaelewa jamaa amemaanisha nn. shaaabashibi

NIMEGUNDUA HUMU JF KUNA MAJITU MAJINGA SN SN MAKURUPUKAJI NA UWENDA WENGI WAMESOMA THREAD TITLE TU HAWAJASOMA CONTENTS KBS nafatilia majbu mnayojbu ni kama hamjaelewa jamaa amemaanisha nn. shaaabashiiii
Sijui kwa nini Watanzania wengine ni wavivu wa kusoma mpaka mwisho. Nimejaribu kutafsiri kwa Kiswahili lakini naona watu bado wanamponda Elon wakidhani anazungumzia maskini wa pesa.
 
Sijui kwa nini Watanzania wengine ni wavivu wa kusoma mpaka mwisho. Nimejaribu kutafsiri kwa Kiswahili lakini naona watu bado wanamponda Elon wakidhani anazungumzia maskini wa pesa.
Kwa kuwa watanzania elimu yetu ni ya kwenda kuombea ajira ya utendaji wa kijiji/kata, polisi nk uwezo wetu wa kuelewa mambo ni mdogo sana na ndio maana asilimia kubwa ya wasomaji wameshindwa kabisa kuelewa Gist ya Elon Musk.

It's a pity.
 
Amuoe yeye si ndiyo tajiri namba moja na walio chini yake ni masikini wote kulinganishwa na yeye
Umesoma maelezo yake lakini?? Kuna somo zuri sana hapo oh Nyerere na hichi kiswahili wakati yeye bingwa wa Ngelee
 
Ishu ya kuoa au kuolewa haipo juu ya Baba, au mama au yeyote. Ipo juu ya mhusika Mwenyewe.
Hata Mungu hawezi kuchagulia utakayemuoa au atakayekuoa
Lengo lake lilikuwa kutoa hilo darasa ambalo ndio muhimu kuliko hiyo ndowa..hebu kijadiliwe alichozungumza..kama tungekuwa na watanzania milion moja tu wapo hivi alivosema tungekuwa tunatowa misaada badala ya kuomba.
 
Back
Top Bottom