Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
BINTI YANGU, KAMWE USIKUBALI KUISHI NA MWANAUME ANAYEKUPIGA AU KUKUTUKANA MATUSI YA NGUONI. KAMWE!
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Sisi watibeli hatupigi Wake zetu, Wala binti zetu hawapigwi Wala kutukanwa MATUSI ya nguoni.
Wala hatutishii kuwapiga, Wala wao hawatishiwi kupigwa. Na katika hayo hakuna kuteleza, hakuna bahati mbaya, hakuna kuzidiwa na hasira.
Tangu mwanzo mwambie mchumbaako kuwa moja ya mambo ambayo hutoruhusu na Wala kuvumilia ni kupigwa hata Kofi moja, Wala kutukanwa matusi yoyote ya nguoni.
Na endapo itatokea mwanaume akafanya hivyo usisite kumchukulia hatua zinazomstahili. Mtendee HAKI. Jicho lako lisiwe na huruma. Kama yeye alivyokosa huruma vivyohivyo nawe mchukulie hatua stahiki.
BINTI yangu, Mimi Baba yako nimeshuhudia mengi, zaidi ninaijua saikolojia ya watu wenye uwezo wa kupiga Wake Zao. Wenye uwezo wa kutukana MATUSI ya nguoni Wake Zao.
Hawana adabu.
Hawawezi kudhibiti hisia zao.
Hawajui nini chakufanya, hawana maamuzi sahihi.
Wanadharau na kukuona wewe ni Kama mnyama au mtoto au mtumwa au sio lolote sio chochote.
Binti yangu, mwanaume akikupiga jiulize huo ujasiri WA kukupiga umetoka wapi? Je ni ukichaa?
Je ni dharau juu yako?
Je ni ukosefu wa adabu?
Je ni ukosefu wa maarifa?
Wewe ni mtu.
Wewe ni mwanamke kama alivyo yeye ni mwanaume.
Hakuna sababu hata moja ya maana, na ya HAKI inayomfanya astahili kukupiga au kukutukana matusi ya nguoni. Hakuna hiyo sababu.
Nilikuambia, binti yangu ili uwe mtu lazima uweze kujitegemea. Lazima ufanye Kazi. Lazima uweze kuyaongoza maisha yako wewe mwenyewe. Sio umtegemee mumeo kwa kila kitu kama mtoto mdogo. Ndio maana utapigwa na kutukanwa matusi ya nguoni kama Mtu aliyedharauliwa, aliyelaanika.
Mwambie, watibeli hawanaga huruma kwa watu wenye dharau za makusudi kabisa. Watibeli hawanaga huruma na waovu wanaofanya uovu kimakusudi wakitegemea kuomba msamaha.
Asije akakudanganya mtu kuwa hutaolewa binti yangu.
Kama kuolewa kwenyewe ni kuolewa na wanaume wasiotenda HAKI ni Bora usiolewe kabisa.
Nilikuambia siku zote utende HAKI.
HAKI ni pamoja na kujiheshimu na kuheshimu wengine.
Usimuinulie sauti mwanaume , mheshimu mwanaume lakini kwa mambo ya HAKI. Kamwe! Kamwe! Kamwe! Usije ukakubali kumheshimu mtu yeyote aliyeamua kuivua heshima yake kwenyewe. Hiyo Sio HAKI.
Wasije wanaume wapumbavu wakakuambia maneno ya kipuuzi kuwa Mungu alituumba Sisi waume tuwatawale hata katika mabaya.
Asije akakuambia mtu yeyote kuwa unatakiwa umtii mumeo hata kwa Mabaya. Nope! Sio kwa Sisi Watibeli.
Mwanaume utamtii kwa mambo mema. Na sio Mabaya.
Mvumilie Mumeo kwa changamoto za maisha kama Hali za kiuchumi, labda kipato kidogo kutokana na riziki kuwa Haba.
Mvumilie Mumeo kwa Maradhi.
Lakini kamwe usimvumilie kwa mambo ya uovu.
Ndoa sio sehemu ya kuvumiliana maovu. Kuvumilia uovu ni kuusapoti uovu.
Makosa yanavumilika lakini sio uhalifu. Makosa yanavumilika lakini sio uovu/dhambi.
Makosa ni Kama wewe upige ugali uunguze, au unyooshe nguo iungue. Uvunje kitu kwa bahati mbaya.
Upoteze pesa kwa bahati mbaya (uzembe).
Sio mtu anakutukana matusi kwa dhamiri kabisa ili akuumize, anamtukana Mama yako, alafu mbaya zaidi sio mara moja yaani ni kila mara.
Mwambie Wala usimuogope, kama pombe akinywa zitamfanya akose akili ya kujizuia akafanya uovu akakupiga au kukutukana mwambie wewe hutohesabu kama ni pombe.
Ni aidha achague Pombe au Wewe.
Usiogope Wala kusita kuvunja ndoa na mwanaume anayepigapiga au kukutukana matusi ya nguoni. Mwanaume asiye HAKI.
Watibeli hatupo hivyo binti yangu.
Hayo yote ayajue mapema kabisa Kipindi cha mwanzoni ili yatakapoenda kinyume asije kusema hukumwambia. Mhakikishie kuwa hutokuwa na huruma.
Nimekufundisha kutenda HAKI. Basi iishi hiyo HAKI.
Acha Baba yako nipumzike sasa.
Nawatakia maandalizi Mema ya Sabato.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Sisi watibeli hatupigi Wake zetu, Wala binti zetu hawapigwi Wala kutukanwa MATUSI ya nguoni.
Wala hatutishii kuwapiga, Wala wao hawatishiwi kupigwa. Na katika hayo hakuna kuteleza, hakuna bahati mbaya, hakuna kuzidiwa na hasira.
Tangu mwanzo mwambie mchumbaako kuwa moja ya mambo ambayo hutoruhusu na Wala kuvumilia ni kupigwa hata Kofi moja, Wala kutukanwa matusi yoyote ya nguoni.
Na endapo itatokea mwanaume akafanya hivyo usisite kumchukulia hatua zinazomstahili. Mtendee HAKI. Jicho lako lisiwe na huruma. Kama yeye alivyokosa huruma vivyohivyo nawe mchukulie hatua stahiki.
BINTI yangu, Mimi Baba yako nimeshuhudia mengi, zaidi ninaijua saikolojia ya watu wenye uwezo wa kupiga Wake Zao. Wenye uwezo wa kutukana MATUSI ya nguoni Wake Zao.
Hawana adabu.
Hawawezi kudhibiti hisia zao.
Hawajui nini chakufanya, hawana maamuzi sahihi.
Wanadharau na kukuona wewe ni Kama mnyama au mtoto au mtumwa au sio lolote sio chochote.
Binti yangu, mwanaume akikupiga jiulize huo ujasiri WA kukupiga umetoka wapi? Je ni ukichaa?
Je ni dharau juu yako?
Je ni ukosefu wa adabu?
Je ni ukosefu wa maarifa?
Wewe ni mtu.
Wewe ni mwanamke kama alivyo yeye ni mwanaume.
Hakuna sababu hata moja ya maana, na ya HAKI inayomfanya astahili kukupiga au kukutukana matusi ya nguoni. Hakuna hiyo sababu.
Nilikuambia, binti yangu ili uwe mtu lazima uweze kujitegemea. Lazima ufanye Kazi. Lazima uweze kuyaongoza maisha yako wewe mwenyewe. Sio umtegemee mumeo kwa kila kitu kama mtoto mdogo. Ndio maana utapigwa na kutukanwa matusi ya nguoni kama Mtu aliyedharauliwa, aliyelaanika.
Mwambie, watibeli hawanaga huruma kwa watu wenye dharau za makusudi kabisa. Watibeli hawanaga huruma na waovu wanaofanya uovu kimakusudi wakitegemea kuomba msamaha.
Asije akakudanganya mtu kuwa hutaolewa binti yangu.
Kama kuolewa kwenyewe ni kuolewa na wanaume wasiotenda HAKI ni Bora usiolewe kabisa.
Nilikuambia siku zote utende HAKI.
HAKI ni pamoja na kujiheshimu na kuheshimu wengine.
Usimuinulie sauti mwanaume , mheshimu mwanaume lakini kwa mambo ya HAKI. Kamwe! Kamwe! Kamwe! Usije ukakubali kumheshimu mtu yeyote aliyeamua kuivua heshima yake kwenyewe. Hiyo Sio HAKI.
Wasije wanaume wapumbavu wakakuambia maneno ya kipuuzi kuwa Mungu alituumba Sisi waume tuwatawale hata katika mabaya.
Asije akakuambia mtu yeyote kuwa unatakiwa umtii mumeo hata kwa Mabaya. Nope! Sio kwa Sisi Watibeli.
Mwanaume utamtii kwa mambo mema. Na sio Mabaya.
Mvumilie Mumeo kwa changamoto za maisha kama Hali za kiuchumi, labda kipato kidogo kutokana na riziki kuwa Haba.
Mvumilie Mumeo kwa Maradhi.
Lakini kamwe usimvumilie kwa mambo ya uovu.
Ndoa sio sehemu ya kuvumiliana maovu. Kuvumilia uovu ni kuusapoti uovu.
Makosa yanavumilika lakini sio uhalifu. Makosa yanavumilika lakini sio uovu/dhambi.
Makosa ni Kama wewe upige ugali uunguze, au unyooshe nguo iungue. Uvunje kitu kwa bahati mbaya.
Upoteze pesa kwa bahati mbaya (uzembe).
Sio mtu anakutukana matusi kwa dhamiri kabisa ili akuumize, anamtukana Mama yako, alafu mbaya zaidi sio mara moja yaani ni kila mara.
Mwambie Wala usimuogope, kama pombe akinywa zitamfanya akose akili ya kujizuia akafanya uovu akakupiga au kukutukana mwambie wewe hutohesabu kama ni pombe.
Ni aidha achague Pombe au Wewe.
Usiogope Wala kusita kuvunja ndoa na mwanaume anayepigapiga au kukutukana matusi ya nguoni. Mwanaume asiye HAKI.
Watibeli hatupo hivyo binti yangu.
Hayo yote ayajue mapema kabisa Kipindi cha mwanzoni ili yatakapoenda kinyume asije kusema hukumwambia. Mhakikishie kuwa hutokuwa na huruma.
Nimekufundisha kutenda HAKI. Basi iishi hiyo HAKI.
Acha Baba yako nipumzike sasa.
Nawatakia maandalizi Mema ya Sabato.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam