Biteko: Shida ya umeme sasa basi, megawati 235 zimeingia Grid ya Taifa
Kwani kilichokwamisha ujenzi toka enzi za Nyerere miaka ya 70 , Mwinyi, Mkapa, Kikwete kilikuwa ni nini? Na JPM aliwezaje?

..hakuna Raisi wa Tz ambaye hakujenga mradi wa umeme.

..JK alikuja na mkakati wa miradi ya kufua umeme wa gesi.

..Magufuli aliachana na mkakati wa JK akaamua kujenga mradi kufua umeme wa maji.

..Mgao wa umeme ungemalizika mapema zaidi kama Magufuli angetekeleza mradi mdogo au wa kati usiochukua muda mrefu kama mradi wa Stieglers gorge.

NB:

..Tuliambiwa umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji ni wa bei nafuu zaidi. Je, tutegemee serikali kupunguza bei ya umeme?

..Watanzania tupinge jitihada za kutaka kuiuza Tanesco baada ya kuhangaika nayo wenyewe mpaka mgao umekwisha.
 
..serikali ishushe bei ya umeme.
Kwani Mheshimiwa mkubwa kabisa Mandondo c alisema umeme hautoshuka bei !!?
Aliyeshiba hamjui mwenye njaa !
Mungu wa mbinguni anawaona 🙏🙏🙏
 
Mashine namba 1 hadi 8 wanawasha lini, maana tunataka bei ya umeme ishuke, maji mengi sana hayo, hakuna sababu ya kuyabania
 
Naibu Waziri Mkuu na waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko ameshuhudia uwashwaji wa mtambo namba tisa katika bwawa la kuzalisha umeme la Julis Nyerere JNHPP ambao umeanza kusambaza umeme megawat 235 katika gridi ya Taifa.

Akishuhudia uwashwaji wa Mtambo huo wa kuzalisha umeme Dkt biteko amesema uzalishaji huo wa megawat 235 utapunguza mgao wa Umeme kwa asilimia 85 na hivyo wananchi wataondokana na kero ya umeme.

"Hata hivyo uzinduzi rasmi wa mitambo miwili, mtambo namba nane na mtambo namba tisa utafanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mwezi ujao wa tatu ambapo mitambo yote hiyo miwili itakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme megawati 470" amesema Dkt Biteko

Pia soma:
- Dkt. Biteko: Nataka niwahakikishie tutawapa umeme Watanzania
Kwa Sasa ni sawa ila tuwe na mbadala (standby) maana haya mabadiliko ya Hali ya hewa hayaeleweki.Ukitokea ukame WA muda mrefu mgao utarudi tena.
 
Kwa Sasa ni sawa ila tuwe na mbadala (standby) maana haya mabadiliko ya Hali ya hewa hayaeleweki.Ukitokea ukame WA muda mrefu mgao utarudi tena.
Hakuna huo ukame in the near future !
Labda ifanyike hujuma tu !
Kataa Wahuni #Polepole !
 
Naibu Waziri Mkuu na waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko ameshuhudia uwashwaji wa mtambo namba tisa katika bwawa la kuzalisha umeme la Julis Nyerere JNHPP ambao umeanza kusambaza umeme megawat 235 katika gridi ya Taifa.

Akishuhudia uwashwaji wa Mtambo huo wa kuzalisha umeme Dkt biteko amesema uzalishaji huo wa megawat 235 utapunguza mgao wa Umeme kwa asilimia 85 na hivyo wananchi wataondokana na kero ya umeme.

"Hata hivyo uzinduzi rasmi wa mitambo miwili, mtambo namba nane na mtambo namba tisa utafanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mwezi ujao wa tatu ambapo mitambo yote hiyo miwili itakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme megawati 470" amesema Dkt Biteko

Pia soma:
- Dkt. Biteko: Nataka niwahakikishie tutawapa umeme Watanzania
Shida ya umeme bado ipo. Hapa nilipo umeme umekata. Na nilidhani tatizo limeisha ndo maana nikatoa “like” kwenye hili bandiko. Nimerudi hapa baada ya umeme kukatika.
 
Shida ya umeme bado ipo. Hapa nilipo umeme umekata. Na nilidhani tatizo limeisha ndo maana nikatoa “like” kwenye hili bandiko. Nimerudi hapa baada ya umeme kukatika.
Hapa nilipo... Ni mji upi, kata ipi.......Mtaa upi....
Mimi niko kijijini Ifakara... Nguzo za umeme bado hazijafika, hivyo bado tunatumia mafuta ya taa.

Wenzetu mliopo mijini mnasemaje juu ya umeme, toka tutangaziwe mwisho wa mgao. Ni siku ya 5 leo, hivyo inatosha kutoa maelezo kama kwa siku hizi Mgao umetokomea.
 
Kwani Mheshimiwa mkubwa kabisa Mandondo c alisema umeme hautoshuka bei !!?
Aliyeshiba hamjui mwenye njaa !
Mungu wa mbinguni anawaona 🙏🙏🙏

..kwanini usishuke bei wakati gharama za kuzalisha umeme zimepungua?
 
Naibu Waziri Mkuu na waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko ameshuhudia uwashwaji wa mtambo namba tisa katika bwawa la kuzalisha umeme la Julis Nyerere JNHPP ambao umeanza kusambaza umeme megawat 235 katika gridi ya Taifa.

Akishuhudia uwashwaji wa Mtambo huo wa kuzalisha umeme Dkt biteko amesema uzalishaji huo wa megawat 235 utapunguza mgao wa Umeme kwa asilimia 85 na hivyo wananchi wataondokana na kero ya umeme.

"Hata hivyo uzinduzi rasmi wa mitambo miwili, mtambo namba nane na mtambo namba tisa utafanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mwezi ujao wa tatu ambapo mitambo yote hiyo miwili itakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme megawati 470" amesema Dkt Biteko

===========For English Audience Only===========

Deputy Prime Minister and Minister of Energy, Dr. Dotto Biteko, has witnessed the commissioning of unit number nine of Julius Nyerere Hydropower Plant (JNHPP) that has started supplying 235 megawatts of electricity to the national grid.

While witnessing the commissioning of the power plant, Dr. Biteko stated that the production of 235 megawatts would reduce power rationing by 85%, relieving citizens off the burden of electricity shortages.

"However, the official inauguration of the two units, unit number eight and unit number nine, will be done by President Samia Suluhu Hassan next March, where both units will have a combined capacity to generate 470 megawatts of electricity," said Dr. Biteko.

Despite the commencement of power supply from the Julius Nyerere Hydropower Plant (JNHPP) across the country, the public opinion indicates that power shortages persist. While the JNHPP is a significant step towards addressing the energy deficit, the public has expressed concerns about overreliance on hydropower. The prevailing sentiment among the public suggests that the government should explore alternative and diversified sources of energy to ensure a more reliable and sustainable power supply. This calls for a broader energy strategy reflects the desire for a resilient power infrastructure that can mitigate the impact of fluctuations in water levels and environmental conditions on electricity generation.




Pia soma:
- Dkt. Biteko: Nataka niwahakikishie tutawapa umeme Watanzania
Matatizo ya kukatika ovyo kwa umeme yako pale pale! Actually kwa mwezi wa February ndiyo hali inazidi kuwa mbaya zaidi. Umeme tunajua ulimuwepo siku zote bali miundombinu na infrastructure nzima ya usambazaji has collapsed. Ndiyo maana walianza kusema tatizo ni ukame, mvua zikinyesha tutapata umeme. Mvua zimenyesha na umeme hatukupata. Wameongeza 235MW ambazo ni kubwa kuliko power generation ya bwawa zima la Kidatu, lakini matatizo yako pale pale. Watajaribu to appease watu wa Dar msipige kelele lakini ukweli ni kwamba umeme haupo hadi sijui lini. Kiwanda changu kimekosa umeme for 26 hours now. Uzalishaji umesimama. HALI NI MBAYA SANA SANA!
 
Hapa nilipo... Ni mji upi, kata ipi.......Mtaa upi....
Mimi niko kijijini Ifakara... Nguzo za umeme bado hazijafika, hivyo bado tunatumia mafuta ya taa.

Wenzetu mliopo mijini mnasemaje juu ya umeme, toka tutangaziwe mwisho wa mgao. Ni siku ya 5 leo, hivyo inatosha kutoa maelezo kama kwa siku hizi Mgao umetokomea.
Mkuu ni kweli mgao ni kama umepungua. Ispokuwa kuna wakati wanakata na unarudi baada ya dakika hivi. Kama wanachosema ni kweli na mgao utaisha, ni mategemeo yetu bei itapungua.
 
Serikali yenyewe ina viongozi ambao hawaongei kwa sauti moja.

Wakati Waziri Biteko anasema tatizo linaisha kwa bwawa jipya kuanza kazi, RC wa Dar Chalamila alisema tatizo halitaisha kwa sababu kuna matatizo mengi katika distribution network, hivyo hata baada ya bwawa kuanza kazi kuna changamoto.

So far inaonekana Chalamila alikuwa muwazi zaidi na Biteko analeta siasa zaidi kuliko uhalisia.
 
Umepungua kwa siku ngapi sasa?

Bado nina mashaka….muda utatueleza!

Tutaona hali itakavyokuwa miezi mitatu ijayo, miezi sita ijayo, miezi tisa inayo, na miaka ijayo.

Siku mbili tatu za afueni haziwezi kunisahaulisha kauli zao za huko nyuma.
Mkuu kwa jinsi mgao ulivyokuwa mkali, sidhani hata kama wiki imepita tokea huo mgao umeanza kupungua.

Ni sawa na kuishi kwa njaa muda mrefu halafu ukipata chakula kwa siku tatu mfululizo unaweza ukahisi kwamba baa la njaa limekwisha. Ni saikolojia tu.

Hivyo nakubaliana na wewe kuhusu muda. Maana ni kweli ni siku mbili tatu umeme haujakatika. Na ukikata unarudi hapo hapo. Na hilo siyo jambo zuri bado.
 
Kwa hali nnayoiona kuanzia jumapili kwa hapa Mbeya ni mgao haupo. Umeme upo na umekuwa wa uhakika katika siku mbili tatu hizi

Kazi imefanyika✌
 
Back
Top Bottom