Biteko: TANESCO inanunua umeme wa Megawati 31 kutoka Uganda na Zambia

Kama kawaida ya siku zote, naona maneno mengi tu... Haya yote hayataleta umeme.

Na isingekuwa kichaa Magufuli, hata hizo 2115 MW za Bwawa la Nyerere tusingekuwa tunaziwazia, pamoja na kuwa mradi huo ulikuwepo toka enzi za Mwalimu.
Tuna vyanzo vingi vya kupata umeme zaidi ya bwawa,tungeweka mitambo ya gas,jua,upepo,joto Ardhi na mabwawa kwenye Mikoa mingine bila Rufiji.

Kwani baada ya bwawa la JNHPP ndio muarobaini wa umeme Tzn? Haifiki hata 2030 megawatt zote 3,000 zitakuwa exhausted so lazima kuendelea vyanzo vipya na kazi hiyo inaendelea.
 
Shida sio wao shida ni akili Yako Ginyu yenye uelewa mdogo.

Kwani kununua umeme Nje ya Nchi imeanza Leo? Iko hivyo Toka uhuru wa Tzn na pia hata sisi tutaanza kuuza huko tukiunganisha grid
Elewa statement kwamba Nchi ina Umeme wa kutosha hadi kuuza jirani.

Then Fanya comparison na hiyo statement ya kwamba Nchi inatumia kiasi kadhaa cha fedha kununua Umeme Uganda na Zambia.

Kwa maelezo rahisi ni kwamba unapokuwa na kitu cha ziada urahusiwa kuuza kinyume chake ni kwamba unapokuwa na pungufu (deficit) ndiyo unapoanza kununua nje
 
Kuwa na umeme wa kutosha ndio nini? Unaweza kuwa na umeme wa kutosha lakini ukingalia source ya kutufikisha unapotaka upande wako ni expensive kuliko upande wa jirani so unatumia wa jirani.
 
Leo wanakwambia Umeme wetu hautoshi hivyo kama Nchi tunapaswa kununua Nchi za Jirani za Uganda na Zambia

Hii Nchi aliyeturoga amekufa haki ya nani 🙌

Hapa huenda Waziri kajichanganya, huenda umeme ukawa unatosha, ila hiyo mikoa kama ya Rukwa na Kagera na kuiweka katika Grid ni jambo la kimkakati na lenye kuchukua muda kutokana na mahitaji ya mikoa hiyo.

Mfano kuna mradi wa TAZA project, huu mradi ni wa 400kV unatokea Iringa kwenye substation ya Tagamenda unaenda Zambia, kupitia mradi huu lazima Rukwa itaingia katika grid ya Taifa. Kwa mkoa wa Rukwa kwa Sasa hauihitaji tena 66kV inayotoka Zambia, sababu inaonekana mahitaji yamekuwa makubwa.

Shida kwa Sasa ni miundo mbinu ya usafirishaji haijawa tayari, ila umeme upo wa kutosha na ziada.
 
Kwa maelezo rahisi ni kwamba unapokuwa na kitu cha ziada urahusiwa kuuza kinyume chake ni kwamba unapokuwa na pungufu (deficit) ndiyo unapoanza kununua nje

Hii sio maana yake mzee. Shida Kuna vitu hamna elimu navyo ila mnavijadili.

Unatakiwa ujue Kuna uwepo wa umeme kwa maana ya uzalishaji, lakini Kuna miundo mbinu ya kusafirisha huo umeme kutoka point Moja kwenda nyingine.

Kwa kipindi cha nyuma na mpaka sasa ilikuwa ni lazima ncho inunue umeme kutoka nchi jirani sababu ya urahisi wa upatikani wa umeme huo, kuliko kujenga miundo mbinu ya masafa marefu kwa gharama kubwa kuliko mahitaji yake.

Ila kwa sasa sababu miradi ipo, nchi inaelekea katika kujenga hiyo miundo mbinu ya kusafirisha umeme huo.
 
Nimekuelewa Mkuu

Nashukuru Kwa darasa 🙏
 
Kuna mdau hapo juu ameelezea kuhusu hili, kama una nafasi pitia maelezo aliyonikoti then uone kama anajibu hoja au ameamua kujibu kisiasa kama Waziri mwenye dhamana 🤗
 
Vijiji vipi hivyo ikiwa 97% ya Vijiji vyote Tzn vina umeme?
Utaniwia radhi kwa kutumia lugha hii, lakini imenilazimu baada ya kusoma ulicho andika hapa. Ni kichaa pekee anayeweza kusema "97% ya vijiji vyote Tanzania vina umeme."
Wakati mwingine nadhani akili huwa zinawaruka kichwani, kwa sababu mnazozijuwa nyinyi wenyewe.
Kuwa na nguzo na nyaya za umeme haina maana kuna umeme kwenye waya hizo.

Siku tutakayofikia hatua hiyo ya kuwa na umeme wenye uhakika kwenye vijiji asili mia 97, tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana kimaendeleo.
 
Hahahaa
 
🤣🤣🤣 Hawa majamaa si walienda juzi kati kutaka kuuza umeme Uganda?. Meza imezunguka sasa? Au tunadanganyw kununua kumbe tunajiuzia??
Yule mtoto wa fulabi aliyeenda Ikulu kw Mseveni sasa mtaelewa alienda kufanya nini.
 
Ni wapi uliposoma nimeandika Bwawa pekee ndio muarobaini? Kuna mahali nimeandika hivyo vyanzo vingine visitumike?
 
Kuwa na umeme wa kutosha ndio nini? Unaweza kuwa na umeme wa kutosha lakini ukingalia source ya kutufikisha unapotaka upande wako ni expensive kuliko upande wa jirani so unatumia wa jirani.
Acha ujinga ndugu yangu.
Hapa Tanzania kwa sasa hakuna mkoa ambao bado haujaunganishwa na gridi ya taifa.
Mikoa ikishaunganishwa na gridi ya taifa maana yake, switch ya kugawa umeme kitaifa ikiwashwa (kwa mfano pale Ubungo) kila mkoa unaweza kupata umeme.

Jiulize hili swali ili kupima akili yako.
Kwanini walati wa mgao wa umeme, mikoa yote iliathiriwa hata hiyo inayoelezwa kupokea umeme wa kununuliwa nje ya nchi?
Na kwanini baada ya mgao wa Umeme kwisha, pia hiyo mikoa haina tena mgao?
 
Bwege wewe,Rukwa na Katavi imeungwa na Grid ya Taifa? Kigoma yenyewe umeme wa grid ya Taifa umewashwa pale Mjini? Lindi na Mtwara Je?
 
Huko wanakonunua ni maeneo ambayo gridi ya Taifa bado haijafika.
Nani kasema?
Hivi unajua Kagera inao umeme wa gridi ya taifa kabla ya Kigoma, Lindi na Mtwara?

Sasa kama haiko kwenye gridi ya taifa kwanini wakati wa mgao wa kitaifa (kwa sababu ya upungufu wa umeme wa gridi ya taifa) nchi nzima iliathiriwa (yakiwemo hiyo mikoa ya umeme wa kununua nje ya nchi)?
 
Bwege wewe,Rukwa na Katavi imeungwa na Grid ya Taifa? Kigoma yenyewe umeme wa grid ya Taifa umewashwa pale Mjini? Lindi na Mtwara Je?
Sawa mimi ni Bwege.
Wewe mwenye akili timamu sasa niambie ilikuwaje wakati wa mgao wa umeme wa nchi nzima, hiyo mikoa ya Rukwa, Katavi na Kagera mgao ndio ulikuwa mkali kupita maelezo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…