Blue ticks za whatsapp: Ni kwamba huyo mtu yupo busy sana au ameamua tu kukuonesha dharau za waziwazi?

Blue ticks za whatsapp: Ni kwamba huyo mtu yupo busy sana au ameamua tu kukuonesha dharau za waziwazi?

Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania eti;

Wewe binafsi unalichukuliaje hili suala la blue ticks za whatsapp kukaa muda mrefu (wiki moja)? Ni kwamba, huyo mtu yupo busy sana au ameamua tu kukuonesha dharau?

View attachment 1623490

MFANO MDOGO APRIL 2018
=========
Unakuta una-chat na mtu ambaye ni classmate wako vizuri tu siku ya weekend jumamosi usiku, yeye anakaa Mwanza na wewe upo Dar, labda kuhusiana na masuala ya mpira wa simba na yanga.

Ukimtumia message ndani ya sekunde chache tu zinatokea zile ticks mbili za blue na ndani ya sekunde hizo hizo classmate anajibu na mnaendelea hivyo hivyo hata kwa muda wa dakika 5 huku mkichekeana na emoji mpaka zile za kurusha miguu juu.

Sasa gusia tu suala la kutaka kukopa pesa kisha umrudishie mwakani 2019 ghafla utaona zile blue ticks mbili zimetokea alafu mtu hajibu tena. Hajibu tena na chat chat ndio imeisha hapo hapo. Utangojea weeeeee mpaka basi.

Baada ya week kama tatu hivi classmate huyo huyo ndiye amepata shida ya ghafla na amekutumia message Whatsapp saa 12 asubuhi na wewe umekuja kuiona na kumjibu saa 10 jioni utamsikia "Daaah mwanangu vp, ina maana message ya tangia muda ule ndio unanijibu sasa hivi mkuu?"
=====

Mifano ni mingi kweli kweli na nikisema yote niiweke humu hakika hapatatosha.

USHAURI WANGU: Hao Whatsapp kama wanaweza pale katika emoji zao waweke "quick text" ambayo mtu akibonyeza mara moja itaandika "Nimepokea ujumbe wako na nitakujibu nikipata nafasi, kwa sasa nipo busy"

Wewe binafsi unalichukuliaje hili suala la blueticks za whatsapp kukaa muda mrefu (wiki moja)?

NDUGU YANGU USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya mdau
=====
Nafanyaje isitokee blue tick? Najaribu ashindwa, napenda mtu asijue kama nimepokea mag yake
 
Wakati mwingine watu huwa wanalazimika 1. kufungua hizo message tu ile whatsapp isiendelee kuipop up hiyo message kwenye notification kila wakati.
2.Wengine wanashindwa kukujibu kwa wakati huko kwa sababu wanajua wakijibu utaendeleza mazungumzo na wana shughuli nyingine. Watu hawa hujibu hiyo message pale tu wanapoona wana muda wa kutosha kuchat hata ukiendeleza mazungumzo.
3. Dharau eidha kwa hoja au mtu anayeitoa. Kama umetuma message yakawaida tu, wakat mwingine mtu anaona hana haja ya kujibu. Au kama wewe huna umuhimu sana ,kwa nini akujibu.
4. Wapiga mizinga. Wale wa babe nikwambie kitu? Au wale wa habari za huko? Huku maisha magumu..... Message za hivi lazima ziishie blue tick.
5. Kwa wenye mahusiano kama mtu anataka muachane kidiplomasia bila vita baridi, anaamua kubluetick tu.
6. Kufungua data na kukuta message nyingi kwenye simu. Wengi hufanya hii. Unawasha data ,unakuta message 3000. Unajikuta unascan zote haraka haraka , halafu unaendelea na kazi. Utajibu moja moja hasa za muhimu zaidi ukiwa free.
SIO MARA ZOTE BLUE TICK INAMAANISHA UMEPUUNZWA!
 
Kuondokana na bluetick tumia whatsapp pori kama GB WhatsApp , au badili mpangilio kwenye simu yako. Kama ambavyo hutaki waone umewablue tick message zao, seti pia usione bluetick kwa message zako. Inakula kotekote!
Alisemaga Jakaya
 
Back
Top Bottom