Bluray and the Role of Preciseness/Precision in Development

Bluray and the Role of Preciseness/Precision in Development

Sorry folks...ila waafrika wengi wetu.. sisi tuna matatizo..tunaridhika haraka mno.no wonder akina Mangungo walituuza kwa wajeremani..kwa vipande vya kanzu na mvinyo...

You are damn right! Mwafrika screwing Mwafrika started long time ago and it still goes on to this day.
 
Huwezi kusema huu mkate hovyo kwasababu umekosa amira,kama umekosa amira huo tayari siyo mkate,umeshakosa ingredient muhimu unayoufanya uitwe "mkate" sambamba na hali ya Afrika kwa ujumla,Afrika kama Afrika si Afrika minus History,sijui umenipata?History ni ingredient muhimu sana pale unaposema "Afrika" hivi ama "Afrika" vile....Na ndio maana narudia tena na tena pls revisit history....Waafrika si wajinga.

Nachokubali ni kwamba waafrika si wajinga na waafrika shall overcome provided that there will always be unwavering patriots,the spirit shall live generations to generations,na kama ilivyo kwa jamii nyingi duniani historically,mapinduzi might one day be a solutions provided the spirit is there and the only other ingredient is the right enviroments or situation to ignite a revolution,history can back that up,please revisit.

Hata niki revisit history nitaona kitu hicho hicho tu: ujinga wa Mwafrika. Hivi Mangi unadhani ku sign mkataba bogus wakati hujui kusoma na kuandika ni stroke of genius? Unadhani kuwauza binadamu wenzio in exchange for material goods ni werevu? Unadhani kujilimbikizia kinyume na sheria wakati umezungukwa na watu wenye dhiki isiyo na kifani ni ishara ya akili? Hivi unadhani kucha kutwa kuchagua mijitu ambayo unajua wazi kuwa ni mijizi ni ishara ya kuwa na akili?

Hiyo historia unayotaka nii revisit itakuumbua mwenyewe. Taking a page right out of Companero's playbook ain't gonna help anything.
 
Hata niki revisit history nitaona kitu hicho hicho tu: ujinga wa Mwafrika. Hivi Mangi unadhani ku sign mkataba bogus wakati hujui kusoma na kuandika ni stroke of genius? Unadhani kuwauza binadamu wenzio in exchange for material goods ni werevu? Unadhani kujilimbikizia kinyume na sheria wakati umezungukwa na watu wenye dhiki isiyo na kifani ni ishara ya akili? Hivi unadhani kucha kutwa kuchagua mijitu ambayo unajua wazi kuwa ni mijizi ni ishara ya kuwa na akili?

Hiyo historia unayotaka nii revisit itakuumbua mwenyewe. Taking a page right out of Companero's playbook ain't gonna help anything.

Sijui una maana gani hapo?
 
Mangi..you bring an interesting point kuhusu history na patriotism. Hivi niambie wanaoscrew Africa leo si ndo hao hao wasomi? au unataka mpaka waafrika wote twende vyuo vikuu? ndo tujikomboe? Leo wanaokula rushwa na kuchota pesa BOT za kufanyia kampeni si hao hao wasomi unaowaongelea? AND WHY DO THEY DO IT? PRECISELY BECAUSE WANAJUA HAWANA WA KUWAULIZA. Wakigundua kwamba unakelele sana..you will be co-opted kwenye meza ya ufisadi. And the game continues...

Tuache kujipa hopes na kuisingizia historia. Africa....ndo bara pekee hatujifunzi kutokana na historia yetu. Jiulize..tulinyanyaswa na mzungu kama makoloni..na mateso mengineyo..lakini leo hii..ni sisi hawa hawa..tunasaini mikataba ya miaka 20 ambayo haitusaidii kabisa.Implication yake ni nini? ...huwezi kutegemea kwamba umasikini utaisha in our life time! Maana sasa tunasaini mikataba ya miaka 20-30..ambayo inapora raslimali zetu! Ambazo zingetusaidia kusonga mbele..upo?

Nimefuatilia mkutano wa Copenhagen...ukiangalia China...kila siku anasema ni mwenzetu kwa vile "eti" na yeye ni developing country..lakini ukweli umeona kabisa..jamaa alivyokataa kata kata...kujicommit na emissions na anajua zinatuumiza sisi masikini ambao anasema eti ni wenzake....sasa kama anaona ni big brother wetu...si angesema jamani.....nitawasidia hivi..political deal aliyo clinch ni yake na Obama....na wengine..Simply say...hali yetu ni ngumu sana and we dont learn. Sijui tupate matatizo yapi..zaidi ya tuliyonayo..kusudi tuweze kujifunza. Labda unisaidie kwa hilo...

Anayoyasema Julius hapa....mimi sioni tatizo lake..maana the chap is confronting you with hard facts...prove him otherwise.
 
Nadhani wakuu hapa tuangalie bigger picture. Ukitoa mfano wa Founding fathers wa US miaka 300 iliyopita nadhani hujitendei haki. Yes, US walipitia huko, je ina maana na sisi lazima tupitie huko? why should we reinvent the wheel? Kuna mambo mengi sana tunaweza kujifunza bila kuanza kuhangaika kuanza upya.

Bottom line is: The major task remains with WE THE PEOPLE. Hivi jiulize..leo hii watanzania baba zetu na mama zetu wanakufa njaa kwa magonjwa nk....lakini ni hao hao kesho utakuta wanaimba idumu CCM! baada ya kupewa tshirts mbili..... Effectively tumeshindwa kulink matatizo yetu na prevailing governance failure! Any democracy inahitaji accountability. Yote mtayasema, lakini ukweli ni kwamba Waafrika hatuhitaji mkombozi zaidi yetu sisi wenyewe. Nenda ulaya au America au kwingineko. Bila wananchi kushika hatamu..we are no where near the promised land.

Africa/Tanzania itakombolewa na watu wenyewe. Mpaka watu watakapoamka na kujua wajibu wao kama raia. Hakuna wasomi kutoka Harvard, Oxford au LSE wa uchumi watakaotukomboa. Hao watakomboa familia zao. We simply need ourselves. So we can blame anybody..ccm, Kikwete, Sofia Simba nk....bottomline is those folks will NEVER change kama WANANCHI hawatawalazimisha.

Its high time tuache hizi mediocre excuses za ujinga, umasikini, njaa...kwa maamuzi mabovu ya wananchi ambao ndo sisi. Huu ujinga na njaa havitaisha kwa kauli mufilisi za akina Makamba et al. Zitaisha tuu pale ambapo..tutaweka SOCIAL CONTRACT kati yetu na watawala. Na wala msitegemee kwamba wananchi wote wataenda shule ndipo wafanye uamuzi sahihi. Mi ndo maana nasema tena....waafrika, sad to say..we are simply stupid. Though haina maana kwamba huu ujinga ni permanent. Tukiamua tunaweza kutoka. But so far....we are the ones to blame. Hakuna maendeleo pasipo uwajibikaji. NEVER.

Infact mtu akishasoma na yeye anataka part of the cake..anakaa kimya..the common mwananchi anaendelea kupiga mark time...Ndo maana mimi wasomi wa Afrika siwafagilii kabisa..na wao ni mijinga tuu..maana ikishasoma inakuwa mibinafsi..haina mpango wa common good...ila hapa watakuja kama mbogo..eti wameitwa wajinga..yet hiyo elimu yao inaishia kwenye vitabu vyao huko huko waliko......

Sorry folks...ila waafrika wengi wetu.. sisi tuna matatizo..tunaridhika haraka mno.no wonder akina Mangungo walituuza kwa wajeremani..kwa vipande vya kanzu na mvinyo...

Masanja:

We don't need to reinvent the wheel. Nilitoa mfano wa founding fathers wa USA kwa sababu vitu viwili vya mwanzo walivyofanya vya kutangaza uhuru na kutunga katiba yenye check and balance, human rights, na transparent kuwa vitu vya kuigwa.

Huwezi kusema mataifa makubwa yalipitia matatizo yetu bila kuangalia frameworks na tools zilizowasaidia kutatua matatizo yao. Bila na kuwa na frameworks na tools za kukabiliana na matatizo yako, utaendelea kuwa masikini tu. Kwa mfano, ikiwa matatizo yako yanatokana na ujinga, kuyaondoa itabidi ufute ujinga tu. Hakuna short cut. Ukifuta ujinga na baadaye ukawa una matatizo yanayotokana na ulimbukeni au ushamba, itabidi utafute njia za kuondoa ulimbukeni na ushamba.

Tunakaribia miaka 50 toka tupate uhuru. Hivyo visingizio vingine tuvidondoshe na kuangalia mapungufu yetu ya sasa.
 
Hata niki revisit history nitaona kitu hicho hicho tu: ujinga wa Mwafrika. Hivi Mangi unadhani ku sign mkataba bogus wakati hujui kusoma na kuandika ni stroke of genius? Unadhani kuwauza binadamu wenzio in exchange for material goods ni werevu? Unadhani kujilimbikizia kinyume na sheria wakati umezungukwa na watu wenye dhiki isiyo na kifani ni ishara ya akili? Hivi unadhani kucha kutwa kuchagua mijitu ambayo unajua wazi kuwa ni mijizi ni ishara ya kuwa na akili?

Hiyo historia unayotaka nii revisit itakuumbua mwenyewe. Taking a page right out of Companero's playbook ain't gonna help anything.

Juli:

Je hiyo historia ya kutawaliwa ni ya mtu mweusi peke yake? Waingereza walitawaliwa. Wachina walitawaliwa. Wakorea walitawaliwa.

Kuna professa mmoja hapa kutoka South Korea. Anasema miaka ya 50, 60 wanawake walikuwa watafuta kuni kama Afrika. Amepoteza ndugu zake kwa TB.

Ukisiliza anayosema unaweza kupata hisia kuwa katika miaka hiyo mtu aliyeishi Kilimanjaro au Zambia alikuwa somehow better.
 
Juli:

Je hiyo historia ya kutawaliwa ni ya mtu mweusi peke yake? Waingereza walitawaliwa. Wachina walitawaliwa. Wakorea walitawaliwa.

Kuna professa mmoja hapa kutoka South Korea. Anasema miaka ya 50, 60 wanawake walikuwa watafuta kuni kama Afrika. Amepoteza ndugu zake kwa TB.

Ukisiliza anayosema unaweza kupata hisia kuwa katika miaka hiyo mtu aliyeishi Kilimanjaro au Zambia alikuwa somehow better.

Hapana, siyo ya mtu mweusi peke yake. Hakika ni ya wengine pia. Lakini hao wengine haikuwazuia kupiga hatua za kimaendeleo. Wengi wetu kila siku wanalialia eti historia this, historia that, so what? Yaliyopita yashapita, sasa hivi tunaweza kufanya nini?

Hivi Zakumi ngoja nikuulize swali ambalo kwa maoni yangu ni rahisi tu. Ni kanuni gani ya kisayansi, kimahesabu, kifizikia, kikemia (hivi hayo yote si sayansi, au?) inayohitajika kujenga majengo imara (madarasa) ya shule na kuhakikisha yanakuwa na mahitaji yote yote ya msingi kama ubao, madawati/viti, madirisha, milango n.k.

Mimi nasema hivi, tushindwe kuunda miroketi ya kwenda angani sawa, tushindwe kujenga mibomu ya nyuklia na mi submarine poa, lakini siyo tushindwe hata kutengeneza madawati na vitanda vya hospitali. Khaaaaa!!!!

maendeleo.jpg
 
Hii ni aibu....huyo mtoto akiporonyoka hapo itakuwaje? But man, African women are tough. I just don't know how they make it. Shout out to all the hardworking African women in the motherland

maji.jpg
 
Hivi kwa wazungu kuna mafisadi? Je nchi zote za wazungu zina mazingira mazuri na watu wake wote wananufaika na utajiri wa nchi hizo? Je nchi hizo zina maskini? Je watu wote kwenye nchi hizo wanafurahia sawa utajiri wa nchi zao?
 
Hii ni aibu....huyo mtoto akiporonyoka hapo itakuwaje? But man, African women are tough. I just don't know how they make it. Shout out to all the hardworking African women in the motherland

maji.jpg

Julius.. we ushawahi kusikia mtoto kachoropoka mgongoni mwa mama?
 
Hapana, siyo ya mtu mweusi peke yake. Hakika ni ya wengine pia. Lakini hao wengine haikuwazuia kupiga hatua za kimaendeleo. Wengi wetu kila siku wanalialia eti historia this, historia that, so what? Yaliyopita yashapita, sasa hivi tunaweza kufanya nini?

Hivi Zakumi ngoja nikuulize swali ambalo kwa maoni yangu ni rahisi tu. Ni kanuni gani ya kisayansi, kimahesabu, kifizikia, kikemia (hivi hayo yote si sayansi, au?) inayohitajika kujenga majengo imara (madarasa) ya shule na kuhakikisha yanakuwa na mahitaji yote yote ya msingi kama ubao, madawati/viti, madirisha, milango n.k.

Mimi nasema hivi, tushindwe kuunda miroketi ya kwenda angani sawa, tushindwe kujenga mibomu ya nyuklia na mi submarine poa, lakini siyo tushindwe hata kutengeneza madawati na vitanda vya hospitali. Khaaaaa!!!!

maendeleo.jpg


Kuhusu swali lako la kanuni, hivyo ni vitu vinavyoeleweka na vilivyofanyiwa kazi kwa miaka mingi tu. Tunachotakiwa ni kutumia tu bila kuumiza kichwa.

Kuna thread moja inasema Pengo anasema kilimo kwanza hazafai kwa sababu hazitoi elimu kwa mkulima.

Ukweli wa mambo serikali ina sera mbovu. Lakini je elimu ya kulima mahindi inatakiwa kweli? au hiki ni kitu tulichotakiwa ku-master? Mazao yote yanayolimwa Tanzania yana zaidi ya miaka 100.

Marekani ni wakulima wazuri sana duniani. Na walianza kulima vizuri kabla ya kwenda shule. Na kwanini sisi tunashindwa ku-channel skills za kukopi tu?

Sometimes we are pathetic.
 
Hivi kwa wazungu kuna mafisadi? Je nchi zote za wazungu zina mazingira mazuri na watu wake wote wananufaika na utajiri wa nchi hizo? Je nchi hizo zina maskini? Je watu wote kwenye nchi hizo wanafurahia sawa utajiri wa nchi zao?

Mwanakijiji:

Mafisadi wako kila sehemu. Hivyo matatizo yetu ya kimsingi kama maradhi, malazi, ujinga na mengineyo yataendelea kuwepo hata kama nchi itakuwa free kutokana na ufisadi.

Na kuna uwezekano mkubwa kuwa ufisadi unakuwepo kwa sababu tumeshindwa kutatua matatizo ya kimsingi ambayo yanakabili jumuia zetu.

Kwa mfano watu wamesha-observe kuwa sehemu zenye upungufu wa vitu watu wanakuwa walafi sana. Mtanzania ambaye kwa kipato chake hawezi kunye bia kila siku, siku akifika Marekani na kupata kipato ambacho kinamwezesha kunywa Heineken 5 kila siku, basi anaweza kuwa mlevi kupindukia kuliko Mmarekani ambaye ana access ya kunywa bia toka akiwa mtoto.

Jamii inapobadilika kunakuwa behavioral changes ambazo zina positive and negative impacts kwa jamii na kiuchumi. Hivyo mafisadi wa Ulaya na Wa Tanzania wanaweza kufanya kitendo kimoja kwa nchi zao lakini wakawa na impacts tofauti kabisa kwa jamii zao.
 
Mwanakijiji:

Mafisadi wako kila sehemu. Hivyo matatizo yetu ya kimsingi kama maradhi, malazi, ujinga na mengineyo yataendelea kuwepo hata kama nchi itakuwa free kutokana na ufisadi.

Na kuna uwezekano mkubwa kuwa ufisadi unakuwepo kwa sababu tumeshindwa kutatua matatizo ya kimsingi ambayo yanakabili jumuia zetu.

Kwa mfano watu wamesha-observe kuwa sehemu zenye upungufu wa vitu watu wanakuwa walafi sana. Mtanzania ambaye kwa kipato chake hawezi kunye bia kila siku, siku akifika Marekani na kupata kipato ambacho kinamwezesha kunywa Heineken 5 kila siku, basi anaweza kuwa mlevi kupindukia kuliko Mmarekani ambaye ana access ya kunywa bia toka akiwa mtoto.

Jamii inapobadilika kunakuwa behavioral changes ambazo zina positive and negative impacts kwa jamii na kiuchumi. Hivyo mafisadi wa Ulaya na Wa Tanzania wanaweza kufanya kitendo kimoja kwa nchi zao lakini wakawa na impacts tofauti kabisa kwa jamii zao.

Zakumi.. that is exactly my point; wenzetu wanayo matatizo kama tuliyonayo na wakati mwingine ni vigumu kuwapata wao watupe sababu ya kwanini wana matatizo hayo. Jiji la Detroit hapa watoto wao wa shule wanatia aibu kwa taifa zima la Wamarekani; yaliyotokea New Orleans wakati wa Katrina tumeyaona; tumeona ulipotokea mgomo wa kukusanya takataka kule California (kama tulivyoona kule Italia);

Wenzetu wamegundua jinsi ya kutotukuza umaskini wao na matatizo yao na kuyaona kuwa ni kero ya kushughulikia. Leo hii Wamarekani wamewafunga watu kama kina Maddoff na huko aliko amefungwa na wezi wengine wa kalamu na hata mabosi wa makampuni makubwa. Wenzetu kama hapa hawana kuremburiana macho na ufisadi.

Leo hii Ufaransa wamemfungulia mashtaka aliyekuwa Rais wao Chirac kama vile Waisraeli walivyomfungulia mashtaka aliyekuwa Rais wao (kwa kubaka). Siyo hivyo tu Waitalia wamemfungulia mashtaka Rais wao aliyeko madarakani kama vile Afrika Kusini walivyomfungulia mashtaka mwanasiasa wao ambaye baadaye amekuwa Rais.

Kwa hivyo, tusijikute tunajiona duni kwa mambo yanayofanywa na wanasiasa wetu na kuamini kuwa "miafrika ndivyo tulivyo". Ukweli wa mambo ni kuwa "binadamu ndivyo tulivyo". Mwanadamu yeyote akipewa nafasi ya kufanya ufisadi na kujinufaisha kwa mgongo wa mwanadamu mwingine atafanya hivyo bila kujali rangi, dini, au eneo la jiografia alipo.

Tofauti yetu kubwa ni jinsi gani tunawashughulia watu wa namna hiyo.
 
Hivi kwa wazungu kuna mafisadi? Je nchi zote za wazungu zina mazingira mazuri na watu wake wote wananufaika na utajiri wa nchi hizo? Je nchi hizo zina maskini? Je watu wote kwenye nchi hizo wanafurahia sawa utajiri wa nchi zao?

Oh mafisadi wapo. Italia kuna mafisadi kibao lakini Italia huwezi ukailinganisha na nchi yeyote Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.

Nchi zote za wazungu watu wake wote hawanufaiki na utajiri wa nchi hizo. Well, I guess inategemea na unamaanisha nini kunufaika? Welfare, SSI, n.k. zina count?

Kutokuwa kabisa na maskini ni vigumu kwa sababu binadamu kibinafsi tumetofautiana mengi. Kuna wavivu, kuna walafi, kuna wachapa kazi, kuna wenye kupenda kukata kona, kuna wenye mitazamo tofauti, n.k. Mtu mvivu kama hatajishughulisha na kujibidiisha ataishia kuwa maskini.

Na watu wote kwenye nchi hizo hawafurahii sawa utajiri wa nchi zao. Duniani hapa huwezi ukamfurahisha na kumridhisha kila mtu.
 
Kwa hivyo, tusijikute tunajiona duni kwa mambo yanayofanywa na wanasiasa wetu na kuamini kuwa "miafrika ndivyo tulivyo". Ukweli wa mambo ni kuwa "binadamu ndivyo tulivyo". Mwanadamu yeyote akipewa nafasi ya kufanya ufisadi na kujinufaisha kwa mgongo wa mwanadamu mwingine atafanya hivyo bila kujali rangi, dini, au eneo la jiografia alipo.

Tofauti yetu kubwa ni jinsi gani tunawashughulia watu wa namna hiyo.

Sawa, unachosema pengine kina ukweli lakini ninachoshindwa kuelewa ni kwa nini katika bara zima kusini mwa jangwa la sahara hali za kimaendeleo zinafanana (zote ni nchi za ulimwengu wa tatu). Ina maana wote tuna tabia sawa (ya kutowashughulikia mafisadi)?

NB: Umetolea mfano Detroit na New Orleans...mara ya mwisho kuangalia miji yote hiyo iko chini ya Miafrika...Lol
 
Oh mafisadi wapo. Italia kuna mafisadi kibao lakini Italia huwezi ukailinganisha na nchi yeyote Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.

Kama ufisadi upo kwa watu weupe na labda una gharama kubwa zaidi (kifedha) then ina maana ufisadi siyo wa watu weusi tu au ni laana ya watu wa Kusini mwa Jangwa la sahara.

Nchi zote za wazungu watu wake wote hawanufaiki na utajiri wa nchi hizo. Well, I guess inategemea na unamaanisha nini kunufaika? Welfare, SSI, n.k. zina count?

Hata hizo tukizikubali bado hazioneshi ukweli wowote kuwa watu wake wote wananufaika na utajiri huo... hapa kwa Obama nako si ndio wanaongeza wiki za unemployment n.k na bado watu wengine wako in the fringes of the economy..


Kutokuwa kabisa na maskini ni vigumu kwa sababu binadamu kibinafsi tumetofautiana mengi. Kuna wavivu, kuna walafi, kuna wachapa kazi, kuna wenye kupenda kukata kona, kuna wenye mitazamo tofauti, n.k. Mtu mvivu kama hatajishughulisha na kujibidiisha ataishia kuwa maskini.

Hili ni kweli na halihusiani na rangi ya mtu au jiografia yake.

Na watu wote kwenye nchi hizo hawafurahii sawa utajiri wa nchi zao. Duniani hapa huwezi ukamfurahisha na kumridhisha kila mtu.

Ni kweli na hili halihusiani na mtu yuko Juu ya Jangwa la Sahara au chini yake. Na Waafrika hawana tofauti yoyote ya kuwafanya wawe duni mbele ya watu weupe kwani majanga yale yale yanayowakuta weusi leo hii yamewakuta na yanaendelea kuwakuta watu weupe.
 
Sawa, unachosema pengine kina ukweli lakini ninachoshindwa kuelewa ni kwa nini katika bara zima kusini mwa jangwa la sahara hali za kimaendeleo zinafanana (zote ni nchi za ulimwengu wa tatu). Ina maana wote tuna tabia sawa (ya kutowashughulikia mafisadi)?

Mbona Atlanta iko chini ya Mwafrika and so is Philly, and so are so many other well performing cities in these USs.

Hata hivyo swali la "kwa nini katika bara zima kusini mwa jangwa la sahara hali za maendeleo zinafanana".. well yapo majibu mengi.. ya kihistoria hasa.

Karibu nchi zote jangwa la sahara zina historia moja vile vile; zote zilijikuta zinatoka katika jamii ya kale na kusalimishwa chini ya utawala wa kikoloni ambao lengo lake lilikuwa ni kujenga nchi za watawala. Hivyo, kwa muda mrefu sehemu hii ya Afrika Kusini ilitumika kujenga chumi za huko ng'ambo huku makoloni yakitumika kwa ajili ya lengo hilo na maendeleo yoyote ya wakati wa mkoloni yalikuwa si katika kuendeleza makoloni ili yajitegemee bali yalikuwa yajitegemee kuendeleza nchi mama tawala.

Na hili kufanikisha hili wakoloni walitumia mbinu zilie za kuua hisia yoyote ya uhuru na kujitegemea na kumtukuza mtu mweupe. Wakati Wafaransa walitimua ile ya assimilation wao Waingereza na wengine walitumia kama ile ya indirect rule na combination mbalimbali. Matokeo yake athari kubwa zaidi ya ukoloni haikuwa katika kutoendeleza maeneo yetu bali ilikuwa katika fikra zetu.

Wakoloni walifanikiwa kutufanya tusijiamini na tushindwe kufikiri nje ya kile walichokijenga ndani yetu. Walifanikiwa kutufanya tuwe tegemezi kwao na hadi leo hii tumeendelea kuwa tegemezi kwa kiasi cha utumwa. Ndio maana Nyerere alipokuja mwanzoni kabisa alijenga hili wazo la "kujitegemea". Lengo lake lilikuwa ni kutuondoa katika utegemezi wa kiakili. Bahati mbaya sana leo hii tumekuwa wategemezi kwa kiasi cha kutisha zaidi kwani wakati wazazi wetu walikuwa na utegemezi kwa kulazimishwa na wakoloni kizazi chetu cha leo kinatengeneza utegemezi wa kupenda wenyewe!

Na hili kwa kudokeza tu unaliona pia kati ya Wamarekani weusi hapa Marekani kwani na wao wameathirika zaidi kiakili baada ya miaka 400 ya Utumwa na unakiona hata Afrika ya Kusini ambako chini ya utawala wa weupe kwa miaka kama 400!

Ndio maana ndugu yangu haya tunayaita mapambano ya kifikra kwani huko kwingine kote tutafika endapo tutaweza kutoka hapa tu!
 
Aisee inawezekana imeshawahi kutokea lakini mimi binafsi sijawahi kusikia!


LOL.. hiyo ikitokea itakuwa ni sawa na paka kumuua mtoto wake kwa kumbeba shingoni au kuku kuua kifaranga kwa kukikanyaga! Kuna vitu havitokei.
 
Back
Top Bottom