Bluray and the Role of Preciseness/Precision in Development

Bluray and the Role of Preciseness/Precision in Development

Mbona Atlanta iko chini ya Mwafrika and so is Philly, and so are so many other well performing cities in these USs.

Hata hivyo swali la "kwa nini katika bara zima kusini mwa jangwa la sahara hali za maendeleo zinafanana".. well yapo majibu mengi.. ya kihistoria hasa.

Karibu nchi zote jangwa la sahara zina historia moja vile vile; zote zilijikuta zinatoka katika jamii ya kale na kusalimishwa chini ya utawala wa kikoloni ambao lengo lake lilikuwa ni kujenga nchi za watawala. Hivyo, kwa muda mrefu sehemu hii ya Afrika Kusini ilitumika kujenga chumi za huko ng'ambo huku makoloni yakitumika kwa ajili ya lengo hilo na maendeleo yoyote ya wakati wa mkoloni yalikuwa si katika kuendeleza makoloni ili yajitegemee bali yalikuwa yajitegemee kuendeleza nchi mama tawala.

Na hili kufanikisha hili wakoloni walitumia mbinu zilie za kuua hisia yoyote ya uhuru na kujitegemea na kumtukuza mtu mweupe. Wakati Wafaransa walitimua ile ya assimilation wao Waingereza na wengine walitumia kama ile ya indirect rule na combination mbalimbali. Matokeo yake athari kubwa zaidi ya ukoloni haikuwa katika kutoendeleza maeneo yetu bali ilikuwa katika fikra zetu.

Wakoloni walifanikiwa kutufanya tusijiamini na tushindwe kufikiri nje ya kile walichokijenga ndani yetu. Walifanikiwa kutufanya tuwe tegemezi kwao na hadi leo hii tumeendelea kuwa tegemezi kwa kiasi cha utumwa. Ndio maana Nyerere alipokuja mwanzoni kabisa alijenga hili wazo la "kujitegemea". Lengo lake lilikuwa ni kutuondoa katika utegemezi wa kiakili. Bahati mbaya sana leo hii tumekuwa wategemezi kwa kiasi cha kutisha zaidi kwani wakati wazazi wetu walikuwa na utegemezi kwa kulazimishwa na wakoloni kizazi chetu cha leo kinatengeneza utegemezi wa kupenda wenyewe!

Na hili kwa kudokeza tu unaliona pia kati ya Wamarekani weusi hapa Marekani kwani na wao wameathirika zaidi kiakili baada ya miaka 400 ya Utumwa na unakiona hata Afrika ya Kusini ambako chini ya utawala wa weupe kwa miaka kama 400!

Ndio maana ndugu yangu haya tunayaita mapambano ya kifikra kwani huko kwingine kote tutafika endapo tutaweza kutoka hapa tu!

Hapa ndio kwenye mtiani wenyewe particularly kwenye uongozi tabia zikiweza badiliki juu ujue chini zitafuta with or without compliance.
 
Mbona Atlanta iko chini ya Mwafrika and so is Philly, and so are so many other well performing cities in these USs.

Atlanta proper iko chini ya mweusi. Njoo kwenye surburbs!!! Kuna amani (relatively speaking). Kuna facilities na services bomba. Makampuni na mashirika makubwa yanahama Atlanta na kuhamia kwenye surburbs ambako Republicans (I just had to rub it in) wameshika hatamu. Juzi juzi tu hapa Atlanta Journal-Constitution wamehamishia makao yao makuu toka Atlanta kwenda Dunwoody. Kama unahitaji tiba halafu uende Grady Memorial Hospital utajuta kwa nini ulienda hapo. Lakini ukienda Northside Hospital, Emory Crawford Long, St. Joseph's utaapa kutorudi tena Grady.

Uhalifu umeongezeka sana downtown hasa kwenye Campus za Georgia Tech, Georgia State, Clark Atlanta, Morehouse, na Spellman. Bondia mashuhuri Vernon Forest alipoteza maisha yake within Atlanta city limits.

Macelebrity wote wanaishi kwenye surburbs kwa ma Republicans na baadhi yetu sisi Waafrika tunapenda sana kuishi kwenye surburbs (ushawahi kujiuliza ni kwa nini?)...Lol
 
Mangi..you bring an interesting point kuhusu history na patriotism. Hivi niambie wanaoscrew Africa leo si ndo hao hao wasomi? au unataka mpaka waafrika wote twende vyuo vikuu? ndo tujikomboe? Leo wanaokula rushwa na kuchota pesa BOT za kufanyia kampeni si hao hao wasomi unaowaongelea? AND WHY DO THEY DO IT? PRECISELY BECAUSE WANAJUA HAWANA WA KUWAULIZA. Wakigundua kwamba unakelele sana..you will be co-opted kwenye meza ya ufisadi. And the game continues...

Tuache kujipa hopes na kuisingizia historia. Africa....ndo bara pekee hatujifunzi kutokana na historia yetu. Jiulize..tulinyanyaswa na mzungu kama makoloni..na mateso mengineyo..lakini leo hii..ni sisi hawa hawa..tunasaini mikataba ya miaka 20 ambayo haitusaidii kabisa.Implication yake ni nini? ...huwezi kutegemea kwamba umasikini utaisha in our life time! Maana sasa tunasaini mikataba ya miaka 20-30..ambayo inapora raslimali zetu! Ambazo zingetusaidia kusonga mbele..upo?

Nimefuatilia mkutano wa Copenhagen...ukiangalia China...kila siku anasema ni mwenzetu kwa vile "eti" na yeye ni developing country..lakini ukweli umeona kabisa..jamaa alivyokataa kata kata...kujicommit na emissions na anajua zinatuumiza sisi masikini ambao anasema eti ni wenzake....sasa kama anaona ni big brother wetu...si angesema jamani.....nitawasidia hivi..political deal aliyo clinch ni yake na Obama....na wengine..Simply say...hali yetu ni ngumu sana and we dont learn. Sijui tupate matatizo yapi..zaidi ya tuliyonayo..kusudi tuweze kujifunza. Labda unisaidie kwa hilo...

Anayoyasema Julius hapa....mimi sioni tatizo lake..maana the chap is confronting you with hard facts...prove him otherwise.

Na Wachina walivyo smart, msemaji wa kundi (G77+China) ni Bw. Lumumba kutoka Sudan. Mwisho wa siku, Bw. Lumumba ndio anashtuka kuwa Wachina si wa kundi lake. Anaishia kulaumu wakati Premier Wen na wenzake washaondoka. Sasa Sudan au Tanzania ni sawa na China kweli linapokuja suala la GHGs emissions? Ni kweli hatujifunzi! Tatizo la Africa ni kubwa mno na ninadhani bado halijafahamika. Maybe Dr.Watson was right.
 
Mbona Atlanta iko chini ya Mwafrika and so is Philly, and so are so many other well performing cities in these USs.

Hata hivyo swali la "kwa nini katika bara zima kusini mwa jangwa la sahara hali za maendeleo zinafanana".. well yapo majibu mengi.. ya kihistoria hasa.

Karibu nchi zote jangwa la sahara zina historia moja vile vile; zote zilijikuta zinatoka katika jamii ya kale na kusalimishwa chini ya utawala wa kikoloni ambao lengo lake lilikuwa ni kujenga nchi za watawala. Hivyo, kwa muda mrefu sehemu hii ya Afrika Kusini ilitumika kujenga chumi za huko ng'ambo huku makoloni yakitumika kwa ajili ya lengo hilo na maendeleo yoyote ya wakati wa mkoloni yalikuwa si katika kuendeleza makoloni ili yajitegemee bali yalikuwa yajitegemee kuendeleza nchi mama tawala.

Na hili kufanikisha hili wakoloni walitumia mbinu zilie za kuua hisia yoyote ya uhuru na kujitegemea na kumtukuza mtu mweupe. Wakati Wafaransa walitimua ile ya assimilation wao Waingereza na wengine walitumia kama ile ya indirect rule na combination mbalimbali. Matokeo yake athari kubwa zaidi ya ukoloni haikuwa katika kutoendeleza maeneo yetu bali ilikuwa katika fikra zetu.

Wakoloni walifanikiwa kutufanya tusijiamini na tushindwe kufikiri nje ya kile walichokijenga ndani yetu. Walifanikiwa kutufanya tuwe tegemezi kwao na hadi leo hii tumeendelea kuwa tegemezi kwa kiasi cha utumwa. Ndio maana Nyerere alipokuja mwanzoni kabisa alijenga hili wazo la "kujitegemea". Lengo lake lilikuwa ni kutuondoa katika utegemezi wa kiakili. Bahati mbaya sana leo hii tumekuwa wategemezi kwa kiasi cha kutisha zaidi kwani wakati wazazi wetu walikuwa na utegemezi kwa kulazimishwa na wakoloni kizazi chetu cha leo kinatengeneza utegemezi wa kupenda wenyewe!

Na hili kwa kudokeza tu unaliona pia kati ya Wamarekani weusi hapa Marekani kwani na wao wameathirika zaidi kiakili baada ya miaka 400 ya Utumwa na unakiona hata Afrika ya Kusini ambako chini ya utawala wa weupe kwa miaka kama 400!

Ndio maana ndugu yangu haya tunayaita mapambano ya kifikra kwani huko kwingine kote tutafika endapo tutaweza kutoka hapa tu!

Eniwei, nyinyi endeleeni tu kutoa hivyo visingizio (mimi siviiti sababu) vya kihistoria. I'm not buying it! Na nadhani wengi wenu mnasukumwa na majivuno (pride) tu.

Yaani mpaka wakoloni wanakuja, wanatutawala na kuua hisia za uhuru na kujitegemea na kutufanya kuanza kuwatukuza wao, tayari kuna kitu walikuwa wametuzidi.

Pia umesema walifanikiwa kutufanya tusijiamini na "tushindwe kufikiri nje ya kile walichokijenga ndani yetu. Well, umewahi kujiuliza kwa nini haikutokea sisi ndio tukawafanya wao kama unavyosema walitufanya sisi? Hasa ukizingatia kuwa tulikuwa kwetu...wao ndio walikuja!

Yaani mtu anakuja nyumbani kwako na kuanza kukutawala. Anakutawala katika almost kila nyanja. How is that possible kama huyo mtu hajakuzidi maarifa?
 
Tatizo la Africa ni kubwa mno na ninadhani bado halijafahamika. Maybe Dr.Watson was right.

Tatizo linafahamika bana sema tu watu ni wabishi kwa sababu ya majivuno lakini deep down nadhani wanakubali ninachokisema. Tatizo ni sisi Miafrika.
 
Lol....ona hawa mabondia. Hawa wanahitaji kunywa protein shakes hawa. Ngoja nicheki na watu wa GNC nione kama wanaweza kunipa discount nikizinunua kwa wingi protein shakes na weight gainers. Nataka ninunue niwapelekee

5.jpg
 
Atlanta proper iko chini ya mweusi. Njoo kwenye surburbs!!! Kuna amani (relatively speaking). Kuna facilities na services bomba. Makampuni na mashirika makubwa yanahama Atlanta na kuhamia kwenye surburbs ambako Republicans (I just had to rub it in) wameshika hatamu.

Lakini nchi hii ni ya weupe..

Juzi juzi tu hapa Atlanta Journal-Constitution wamehamishia makao yao makuu toka Atlanta kwenda Dunwoody. Kama unahitaji tiba halafu uende Grady Memorial Hospital utajuta kwa nini ulienda hapo. Lakini ukienda Northside Hospital, Emory Crawford Long, St. Joseph's utaapa kutorudi tena Grady.

Bado wapo watu weupe Atlanta au wote ndio wanakimbilia to the 'burbs? Unafikiri ni kwa sababu wanaogopa watu weusi au kuna sababu nyingine zaidi kama za kiuchumi n.k


Uhalifu umeongezeka sana downtown hasa kwenye Campus za Georgia Tech, Georgia State, Clark Atlanta, Morehouse, na Spellman. Bondia mashuhuri Vernon Forest alipoteza maisha yake within Atlanta city limits.

Na huko kwenye suburbs watu hawauawi, na hakuna drugs, na watoto wakizungu wote wako safi (hawavuti bangi, no drugs, n.k)?


Macelebrity wote wanaishi kwenye surburbs kwa ma Republicans na baadhi yetu sisi Waafrika tunapenda sana kuishi kwenye surburbs (ushawahi kujiuliza ni kwa nini?)...Lol

I moved out the D miaka karibu sita iliyopita... so I really have no idea why we do what we do.. I thought I got a good deal ya nyumba, nice school district (nilipowapeleka kina Jr nilidhani nimewapeleka chuoni!)!
 
Hiyo historia unayotaka nii revisit itakuumbua mwenyewe. Taking a page right out of Companero's playbook ain't gonna help anything.

Sasa mimi nahusikaje? Kwani ni uongo kuwa Misri ya kale ilikuwa 'precise' katika kutengeneza Mapiramidi na Ma-Sphinx marefu kama Skycrappers? Yaani sio kweli kuwa Zimbabwe Kuu ilikuwa 'precise' katika kujenga ng'ome imara za mawe na kuchimba dhahabu nyingi kuliko Barrick? Au unataka kupingana na historia ya Afrika ya Kale?
 
Sasa mimi nahusikaje? Kwani ni uongo kuwa Misri ya kale ilikuwa 'precise' katika kutengeneza Mapiramidi na Ma-Sphinx marefu kama Skycrappers? Yaani sio kweli kuwa Zimbabwe Kuu ilikuwa 'precise' katika kujenga ng'ome imara za mawe na kuchimba dhahabu nyingi kuliko Barrick? Au unataka kupingana na historia ya Afrika ya Kale?

Hao wa Misri ni weusi kama mimi na wewe au ni Waarabu? Na huko Zimbabwe nini sasa kilitokea? Mbona hizo ngome zao hazikuwazuia wazungu kuwavamia na kuwatawala...Lol...I guess zilikuwa ngome za matofali ya udongo
 
Hiyo ndio ngome ya Mwenemutapa?

Hapo ni Meroe kwa Wanubi na ni weusi kuliko wewe na mimi kama walivyokuwa weusi wa Misri ambao unataka kudai ni Waarabu - kuna Uarabu au Uzungu gani hapa katika huu uso na pua ya Sphinx hapo chini?


 
Lakini nchi hii ni ya weupe..

Nchi hii siyo ya weupe peke yao.

Bado wapo watu weupe Atlanta au wote ndio wanakimbilia to the 'burbs? Unafikiri ni kwa sababu wanaogopa watu weusi au kuna sababu nyingine zaidi kama za kiuchumi n.k

Kweli watu weupe wapo Atlanta na idadi yao inaongezeka huku idadi ya weupe ikipungua. Weird! Juzi hapa kulikuwa na uchaguzi wa meya na kwa vile hakuna aliyepata 50 plus 1 kwenye general election kukalazimika kuwepo na runoff iliyo wa pit mama wa kizungu (Mary Norwood) na Kasim Reed (mweusi). Norwood alishindwa kwa kura 714 tu! The closest any white candidate has ever lost since the city elected Maynard Jackson as it's first African American mayor. Safari ijayo usije shangaa ukisikia ATL ina meya mzungu.

Kwa hiyo kwa kweli kuna sababu nyingi zinazowafanya wazungu waanze kurudi Atlanta na weusi kuanza kuhama. Hizi siasa za race ukizifuatilia sana utachanganyikiwa tu. Wazungu wanaongezeka huku weusi wakipungua. Makes no sense but it is what it is.

Na huko kwenye suburbs watu hawauawi, na hakuna drugs, na watoto wakizungu wote wako safi (hawavuti bangi, no drugs, n.k)?

Hapana, uhalifu upo kila mahali. Kinachotofautiana ni kiwango au viwango vya uhalifu. You are more likely get jacked in Atlanta than you are in Sandy Springs.

Ninachotaka kusema mimi ni kwamba, sisi kama taifa we can do better than let our kids sit on the floor at school or let the sick sleep on the floor in hospitals. It is doable but we don't do it and that's where the stupidity is.
 
Hapo ni Meroe kwa Wanubi na ni weusi kuliko wewe na mimi kama walivyokuwa weusi wa Misri ambao unataka kudai ni Waarabu - kuna Uarabu au Uzungu gani hapa katika huu uso na pua ya Sphinx hapo chini?



Hiyo pua na huo uso ni kuchongwa! Weka picha ya mnubi tuione
 
Wakuu 'Weusi' wa Misri ya Kale Walipokuwa Wakihudumiwa na 'Weupe'

Nubian-kemsit.jpg
 
Hebu nitajie "precise societies" tatu na "imprecise societies" tatu.
 
Back
Top Bottom