Bodaboda wanapataje leseni maana ajali kwao fasta

Shining Light

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2024
Posts
406
Reaction score
523
Hivi bodaboda wanapataje leseni, maana uendeshaji wao upo rough sana mpaka unajiuliza huyu mtu amesoma sheria za barabara, Kwa namna moja au nyingine hii ndio sababu kubwa sana ya bodaboda nyingi jijini Dar es Salaam kupata Ajali.

Mtu yupo kwenye foleni ila anakimbiza pikipiki balaa, mara wagongane na watu barabarani wakiwa wanavuka, mara baiskeli, mara ajali hiyo.. Tafrani tu loh!
 
Kama watoa leseni wenyewe wanakuambia leseni haiendeshi chombo cha moto unategemea nini
 
Hivi unadhani wanaopata ajali ni wasi ona leseni pekee?
 
Ila wengi wao.. wanajua walipofuzu kupata leseni.. utafikiri hawapo na chomboncha Moto na pia hawajali maisha yao na haswa ya wengine kabisa. Hatari sana.. inaonyesha nchi yetu ipoje kwenye usalama wa raia wake. Mabadiliko yanawezekana na kunyoosha waheshimu mengi...
 
Hii nchi nini kinashindikana? Maana hata nembo ya bibi na bwana inapatikana tu ukiamua!
 
Bodaboda na leseni wapi na wapi.

Hao kwenye pikipiki wanachojua ni kuweka na kutoa gia tu.

Nothing less nothing more.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…