Bodi ya Simba upande wa mashabiki wanataka kumtapeli Mo Simba yake

Bodi ya Simba upande wa mashabiki wanataka kumtapeli Mo Simba yake

Acha kutetea ujinga huyo unayemuita CPA zipo rekodi zake akikiri wazi kabisa kuwa bilion 20 zipo.

Wewe huwezi kuwa na mawazo mazuri dhidi ya Simba na sikulaumu kwa hilo kwasababu hata mimi ningefanya the same kwenye ishu ya Yanga
Ungesikiliza mahojiano ya Julio na wasafi anasema wakati Simba inatakiwa kuingia kwenye uwekezaji Abubakari Bakhresa alikubaliana na viongozi wa Simba ajenge uwanja Bunju, awape bilioni 3 za usajili Kila mwaka na pia Kuna maji yangetengenezwa na kupewa jina la Simba mapato yangepatikana wangegawa. Baada ya mo kupata habari ndio akawaundia kesi kina Aveva ili awaondoe aweze kuingia.
Ukimsikiliza Kigwangala anasema Kama mo angetoa bilioni 20 zingewekwa treasure bond na Kila mwaka Simba ingepata bilioni 3 na ushee lakini mo alikataa udhamini wa Azam ambao kwa miaka 10 ungewapa bilioni 40 na akasema Simba ikiishiwa atatoa pesa zake mfukoni Sasa iweje Leo afai alikuwa anakopeshwa na ziingizwe kwenye hesabu ya bilioni 20.
Mo alisema Leo naondoka Simba haipitii nusu saa tayari mwekezaji atakuwa kapatikana
 
Mgogoro mkubwa sana unanukia Simba.

Naona ni kama mgogoro wa Glazer Family na Man Utd. Mtu kashikilia timu hela hatoi, timu mafanikio yanadorora kila siku, na kuiachia hataki sababu kupitia timu biashara zake zinaenda.
Glazerbhai hiyo.
 
Mbona hili swala linatuweka dilemma sisi mashabiki wenye uelewa hafifu
Ni hivi.. Mo alikuja na propasal ya mabadiliko ya uendeshaji wa simba kama taasisi ambapo alitaka apewe 49% na wanachama wapewe 51% na katika izo hisa 49% anazozitaka Mo atazilipia bilioni 20.. katika mchakato wa kuidhinisha kisheria hayo mabadiliko mamlaka husika zilitaka marekebisho katika prospectus ya mabadiliko ambapo ilitakiwa upande wa mmiliki yaani kwenye zile 49% kuwe na wawekezaji angalao watatu takwa ambalo halikutimizwa kwaiyo kisheria mpaka sasa hivi tuseme mchakato wa mabadiliko umekwama.

Sasa basi ndani ya hiki kipindi cha miaka 7 ambacho mchakato wa mabadiliko unasuasua Mo alikua anatoa pesa zake mfukoni kuendesha klabu.

Kutokana na fukuto linaloondelea uko simba Mo katoa machaguo mawili ni either arudishiwe hela alizotoa au zihesabiwe kama ile bilioni 20 ambayo alipaswa kuitoa ili anunue 49% ya hisa.

Bodi upande wa wanachama yaani wamiliki wa zile 51% ya hisa wamekataa. Hoja zao ni kwamba izo pesa zilitolewa kama msaada sio deni vile vile Mo hana umiliki wowote simba kwa sababu mchakato wa mabadiliko uliishia njiani.

My take; Mo amefanya makosa ya kisheria na wanachama wamefanya makosa ya kinadamu. Mahakamani wanachama watashinda ila kwenye mioyo ya watu Mo atashinda.
 
Ungesikiliza mahojiano ya Julio na wasafi anasema wakati Simba inatakiwa kuingia kwenye uwekezaji Abubakari Bakhresa alikubaliana na viongozi wa Simba ajenge uwanja Bunju, awape bilioni 3 za usajili Kila mwaka na pia Kuna maji yangetengenezwa na kupewa jina la Simba mapato yangepatikana wangegawa. Baada ya mo kupata habari ndio akawaundia kesi kina Aveva ili awaondoe aweze kuingia.
Ukimsikiliza Kigwangala anasema Kama mo angetoa bilioni 20 zingewekwa treasure bond na Kila mwaka Simba ingepata bilioni 3 na ushee lakini mo alikataa udhamini wa Azam ambao kwa miaka 10 ungewapa bilioni 40 na akasema Simba ikiishiwa atatoa pesa zake mfukoni Sasa iweje Leo afai alikuwa anakopeshwa na ziingizwe kwenye hesabu ya bilioni 20.
Mo alisema Leo naondoka Simba haipitii nusu saa tayari mwekezaji atakuwa kapatikana
Kuna angle ambayo hujaifikiria bado.

Bakhressa alitaka kuichukua Simba lakini hiyo ni baada ya kuiona ipo katika nafasi nzuri ambayo imetengenezwa na MO.


Sasa kuna vitu ambavyo vilikuwa vikisemwa ambavyo siwezi kuvithibitisha kuwa ni kweli ila unapofufuliwa huu mjadala hatuwezi kuacha hizo hoja kuziweka ili ku connect dots.

Inasemekana kilichotokea ni kwamba Bakhressa alitoa fungu kwa baadhi ya viongozi wafanye kampeni za kumpindua MO ili yeye aingie madarakani.

Na ndio maana baada ya MO kuwasanukia akaamua kuwatimua.

Na hii kasumba ya Bakhressa kutoa rushwa ili kufanikisha adhma yake imekuwa kawaida.

Kama utakumbuka kwenye ishu ya broadcasting Bakhressa inasemekana pia alitoa hongo kubwa kwa TFF ili wasimpe nafasi Supersport ambaye alikuwa mshindani wake mkuu.


We unashawishika na hoja ya Kingwangala kuwa kuna 3B ambayo Simba ingeweza kuipata kila mwaka na kuona hiyo kama ndio pesa nyingi kuliko zile zinazotumika kutoka mfukoni mwa MO.

Una amini kuwa 3B ambayo ungekuwa unaipata kila mwaka ilikuwa ni pesa nyingi kuliko summation ya pesa zote kwa mwaka ambazo zinatumika kupitia mkono wa MO?

Kamsikikize huyo CPA alivyokuwa anaeleza Agost 23 mwaka jana. Alisema zile 20B ambazo zipo escrow zinajizalisha kila mwaka na pesa inaingia kwenye Club ila hakutaja kiwango.

Lakini pia kuna pesa nyingine nyingi za uendeshaji ambazo MO anatoa ukiachana na hiyo 20B.

Bado pesa hizo thamani yake huioni?

Halafu kitu kingine unabidi ujue changamoto ya Simba kwa sasa sio pesa ni uongozi.

Kama umewasikikiza Che Malone na Cadena utaona hawalalamiki kuhusu mishahara yao kutolipwa kwa wakati.

Wanalalamika kuhusu mfumo wa uongozi ambao ndio hao wajumbe ambao wanataka Mo aondoke.
 
Ni hivi.. Mo alikuja na propasal ya mabadiliko ya uendeshaji wa simba kama taasisi ambapo alitaka apewe 49% na wanachama wapewe 51% na katika izo hisa 49% anazozitaka Mo atazilipia bilioni 20.. katika mchakato wa kuidhinisha kisheria hayo mabadiliko mamlaka husika zilitaka marekebisho katika prospectus ya mabadiliko ambapo ilitakiwa upande wa mmiliki yaani kwenye zile 49% kuwe na wawekezaji angalao watatu takwa ambalo halikutimizwa kwaiyo kisheria mpaka sasa hivi tuseme mchakato wa mabadiliko umekwama.

Sasa basi ndani ya hiki kipindi cha miaka 7 ambacho mchakato wa mabadiliko unasuasua Mo alikua anatoa pesa zake mfukoni kuendesha klabu.

Kutokana na fukuto linaloondelea uko simba Mo katoa machaguo mawili ni either arudishiwe hela alizotoa au zihesabiwe kama ile bilioni 20 ambayo alipaswa kuitoa ili anunue 49% ya hisa.

Bodi upande wa wanachama yaani wamiliki wa zile 51% ya hisa wamekataa. Hoja zao ni kwamba izo pesa zilitolewa kama msaada sio deni vile vile Mo hana umiliki wowote simba kwa sababu mchakato wa mabadiliko uliishia njiani.

My take; Mo amefanya makosa ya kisheria na wanachama wamefanya makosa ya kinadamu. Mahakamani wanachama watashinda ila kwenye mioyo ya watu Mo atashinda.
Nimekuelewa braza
 
Umeongea point kabisa awa jamaa ni wajanja kumbe wako kimasirahi binafsi ndomana hawatak kujiudhuru

Lengo lao ni kutaka kuivuluga timu ,mimi naamin hawa watu nyuma yao kuna kikundi kinawasapoti sio bure,

Haiwezekan wawe na ujasiri mbele ya mtu alie kuteua afu uje ugomee maamuzi yake
 
Kuna angle ambayo hujaifikiria bado.

Bakhressa alitaka kuichukua Simba lakini hiyo ni baada ya kuiona ipo katika nafasi nzuri ambayo imetengenezwa na MO.


Sasa kuna vitu ambavyo vilikuwa vikisemwa ambavyo siwezi kuvithibitisha kuwa ni kweli ila unapofufuliwa huu mjadala hatuwezi kuacha hizo hoja kuziweka ili ku connect dots.

Inasemekana kilichotokea ni kwamba Bakhressa alitoa fungu kwa baadhi ya viongozi wafanye kampeni za kumpindua MO ili yeye aingie madarakani.

Na ndio maana baada ya MO kuwasanukia akaamua kuwatimua.

Na hii kasumba ya Bakhressa kutoa rushwa ili kufanikisha adhma yake imekuwa kawaida.

Kama utakumbuka kwenye ishu ya broadcasting Bakhressa inasemekana pia alitoa hongo kubwa kwa TFF ili wasimpe nafasi Supersport ambaye alikuwa mshindani wake mkuu.


We unashawishika na hoja ya Kingwangala kuwa kuna 3B ambayo Simba ingeweza kuipata kila mwaka na kuona hiyo kama ndio pesa nyingi kuliko zile zinazotumika kutoka mfukoni mwa MO.

Una amini kuwa 3B ambayo ungekuwa unaipata kila mwaka ilikuwa ni pesa nyingi kuliko summation ya pesa zote kwa mwaka ambazo zinatumika kupitia mkono wa MO?

Kamsikikize huyo CPA alivyokuwa anaeleza Agost 23 mwaka jana. Alisema zile 20B ambazo zipo escrow zinajizalisha kila mwaka na pesa inaingia kwenye Club ila hakutaja kiwango.

Lakini pia kuna pesa nyingine nyingi za uendeshaji ambazo MO anatoa ukiachana na hiyo 20B.

Bado pesa hizo thamani yake huioni?

Halafu kitu kingine unabidi ujue changamoto ya Simba kwa sasa sio pesa ni uongozi.

Kama umewasikikiza Che Malone na Cadena utaona hawalalamiki kuhusu mishahara yao kutolipwa kwa wakati.

Wanalalamika kuhusu mfumo wa uongozi ambao ndio hao wajumbe ambao wanataka Mo aondoke.
Bakhresa alitaka kuchukua Simba kabla mchakato hatujaanza, kumbuka kauli ya Mulamu Ng'ambi wakati wa mchakato aliposema mtu mmoja haruhusiwi kumiliki timu moja lakini mtu huyohuyo alipoulizwa wakati mnasimamia mchakato mlijua thamani ya Simba akasema hafahamu..
Thamani ya timu ni pamoja na idadi ya washabiki alionao.
Kila mtu Simba hata kina Kilomoni wanataka mabadiliko tatizo ni jinsi mchakato ulivyoendeshwa.
 
Lilikua swala la muda Tu...
Wakati Yanga wamemaliza migogoro na kujenga timu yenye ushindani, vipaji na nidhamu nyie nilikua klbize kusema inabebwa mara bahasha....
Sasa kimeumana [emoji81]binafsi nasimama na Mo... Kama alikua anawapiga hela mbona hamkulaumu Mpaka Leo maji yalipozidi unga
Unadhani Yanga wao wapo salama?
 
Wajumbe wa bodi wanaitisha mkutano na waandishi barabarani mbele ya maduka ya watu..
Kwa Hilo tu hata Kama walikua na hoja nawaona wajinga.

Kumbuka mchakato wa mabadiliko ndani ya Simba ulikuwa haujakamilika hivyo zile fedha ziliwekwa 'escrow account'..
Sasa watu haohao upande wa wanachama kwa makusudi kabisa wamechelewesha na kukwamisha mchakato na Mo ameendelea kutoa fedha nje ya zile billioni 20 mpaka zimezidi tena billion 20 nyingine..

Kama uliwasikia vizuri hoja zao hao wajumbe wa bodi, wanataka Mo aendelee kutoa hela ila asizisimamie wala kuzitolea maamuzi. Wanataka wapewe wao ndio wafanye maamuzi..
Wapumbavu kweli na njaa ndio zinazowaongoza.

Yani wewe hutoi hata mia, ila unataka Mimi nitoe hela uzisimamie wewe, Tena unaongea kwa uchungu kwelikweli..shenzi type!
Ok! Wanachama wanna 51%, bebeni basi budget ya msimu huu..
Partnership maana yake uwajibike kutokana na asilimia zako zilivyo.

Sasa wewe unatoka nyumbani kwako na nauli ya boda unasema, Mo akisajili kocha hatafundisha Simba, mpaka wewe upewe pesa ndio usajili...kitunguu, nyanya, ndizi, embe, parachichi..kwanza tikiti maji wahed
Mkuu ni ajabu sana. Simtetei MO lakini Kuna namna hawamtetendei Sawa.
 
Ndo makubaliano ya kimkataba ayo? Walikubaliana kwamba ukifinance miaka 7 ndio zinabadilishwa kuwa mtaji wa b.20? Ebu acha ujinga basi, aonyeshe bilioni 20 alikoziweka mengine yaendelee!
Kwa hiyo alikuwa akiwapa hizo fedha wanatumia walidhani kunafedha za Bure.Hawa wajumbe wa bidard wanatakiwa kupigwa mawe kwanza kwa kuwadanganya wanachama wenzao siku za nyuma
 
Ungesikiliza mahojiano ya Julio na wasafi anasema wakati Simba inatakiwa kuingia kwenye uwekezaji Abubakari Bakhresa alikubaliana na viongozi wa Simba ajenge uwanja Bunju, awape bilioni 3 za usajili Kila mwaka na pia Kuna maji yangetengenezwa na kupewa jina la Simba mapato yangepatikana wangegawa. Baada ya mo kupata habari ndio akawaundia kesi kina Aveva ili awaondoe aweze kuingia.
Ukimsikiliza Kigwangala anasema Kama mo angetoa bilioni 20 zingewekwa treasure bond na Kila mwaka Simba ingepata bilioni 3 na ushee lakini mo alikataa udhamini wa Azam ambao kwa miaka 10 ungewapa bilioni 40 na akasema Simba ikiishiwa atatoa pesa zake mfukoni Sasa iweje Leo afai alikuwa anakopeshwa na ziingizwe kwenye hesabu ya bilioni 20.
Mo alisema Leo naondoka Simba haipitii nusu saa tayari mwekezaji atakuwa kapatikana
Hayo wanayo yasema ya Mo kukataa issue ya Backresa Yako kwenyw maandishi
 
Back
Top Bottom