Bomba la mafuta EACOP toka Uganda lazima lijengwe

Bomba la mafuta EACOP toka Uganda lazima lijengwe

Sijui una maana gani hapa, lakini kama hunijui mimi ni mtu wa mwisho kabisa kujidharau, na hali ni hivyo hivyo inapohusu taifa langu, na wengine wote tunaodharauliwa kwa kuwa na hali duni.

Lakini inaelekea hukuelewa nilichoandika hapo, nawe ukadhani ni "kujidharau".

Ninaelewa, wengi wetu hapa haya maswala ya mazingira bado hatuyaelewi vya kutosha. Na yanapochagizwa na hawa wakoloni, ndipo tunapoamsha mori na kudhani (pengine kiuhakika), kwamba ni watu wasiotutakia sisi mema.

Ndiyo, humo humo, kuna wanaotumia mwanya huu katika kutafuta mwendelezo wa hali zetu duni. Wamo wengi sana. Lakini hawa wasitupotezee lengo nasi tukakosa weledi wa kujua hatari halisi inalalia wapi. Tukijua hivyo, ni wajibu wetu kujiandaa, na kujipa ufahamu mzuri juu ya haya mambo ili tusiwe tunaburuzwa tu inapokuja katika maamuzi yanayotuhusu na yanayohusu raslimali zetu tunazotaka kuzitumia ili nasi zitukwamue, kama wao za kwao zilivyowakwamua na matiokeo ya kutumia raslimali hizo wakapata maendeleo kwa mgongo wa kuharibu mazingira kwa wote, siyo kwa wao peke yao.

Ninahimiza tufanye nini?

Kwanza, tuelewe ukweli wa hali hatarishi iliyopo duniani kutokana na uharibifu wa mazingira. Hii siyo propaganda tena, ni ukweli unaothibitishwa kisayansi. Tusibeze, kwa vile wengi wa wanaopiga kelele ni hao tunaodhani hawatutakii mema.

Pili, pamoja na kujua uharibifu wa mazingira uliopo sasa, sehemu kubwa ikiwa imesababishwa na mataifa makubwa yaliyoendelea, na ambayo sasa yanatuminya nasi tusitumie raslimali zetu kama walivyozitumia wao kujiletea maendeleo, ni wajibu wetu kufanya kila juhudi kutafuta njia za kuzitumia raslimali hizo kila inapowezekana, hasa panapokuwepo na njia za kupunguza huo uharibifu kwa kutumia teknologia mpya zilizopo.
Huu ni wajibu wetu, lakini hatuwezi kuutimiza kama kazi tunayoweza ni kupiga tu kelele kujibishana na hao wasiotutakia mema. Ni lazima tujijengee uwezo wa kuzitumia sisi wenyewe. Tuachane na hizi tabia za kulialia kila mara, kila tunabobanwa juu ya haya maswala ya mazingira.

Tatu, kama inatuwia vigumu kuchimba mkaa wetu sisi wenyewe na kuutumia kwa maendeleo yetu, na hatuwezi kupata ufadhiri kutoka nje kwa vile mkaa ni bidhaa inayochafua mazingira, inabidi sasa nasi tuwe mbele, pengine kuzidi wengine wote katika maswala ya teknologia inayohusu njia zisizokuwa za uchafuzi wa mazingira. Tusikae tu na kubweteka tukisubiri hao wengine ndio wawe watu wa kuja hapa kututengenezea vitu kwa kutumia nyenzo tulizo nazo sisi wenyewe.
Jua tunalo hapa kila siku ndani ya mwaka mzima, kwa nini ushiriki wetu katika kutumia raslimali hii aliyotupendelea Mwenyezi Mungu kuwa nayo hapa sisi wenyewe na tulazimike kuombeleza kwa hao hao tunaosema wanatunyanyasa?
Sasa kama ni "Kujidharau" katika kuhimiza haya, huku tukirudi kule kule kwa kujidhani hatuwezi chochote, hapo nitakubaliana nawe kwamba tunajidharau.

Ningependa kumwona kiongozi anayejiamini na kuamini uwezo wetu tulio nao sasa, na kama haupo, ambaye yupo tayari kuwahimiza wananchi kuwa na ujasiri huo wa kujiamini kufanya mambo yetu wenyewe. Hili halina maana kwamba tutaacha kushirikiana na wengine duniani, ili tupanue uwezo wetu haraka na zaidi.

Mkuu 'Masopa', ninakupmba sana, usiniweke tena katika kundi hilo la "kujidharau". Sina chembe hata kidogo ya sifa hiyo.

Mwisho: Nina mashaka makubwa, kama gesi yetu kule baharini kuna siku itachimbwa. Labda mambo ya Putin yazidi kuwa mazito.

Ninashukuru pia kusikia maneno juu ya Bandari yetu ya Bagamoyo. Kama yasemwayo ni kweli kuhusu kuanza kazi sisi wenyewe juu ya bandari hiyo, nitatafuta niliyowahi kuandika humu JF kuhusu kazi ya namna hiyo kuianza sisi wenyewe kukupa ushahidi kwamba mimi siyo mtu wa kujidharau, au kudharau uwezo wa wananchi wetu kufanya mambo.
Kitu pekee kinachokosekana ni uongozi wa kutuaminisha kwamba uwezo tunao mwingi sana wa kubadili hali zetu sisi wenyewe, hapahapa Tanzania.

Hukousiyo "KUJIDHARAU."
Ningependa kkubaliana na wewe mkuu lakini naona hulioni tatizo kubwa la wenzetu, tatizo la " me first".
Wenzetu wana tabia isiyoisha ya kujifikiria kwanza kuliko kitu kingine chochote.

Kwa tatizo la mazingira, uchumi za nchi zao zimechangia kwa zaidi ya asilimia 75 wakati sisi hatuchangii matatizo ya mazingira kwa hata asilimia 2 dunia nzima.

Wazo la kusitisha miradi yetu ya maendeleo lingekuwa na mantki kama wao wangekuwa wa kwanza kusitisha matumizi ya nishati zilizopo.
Hatujasahau kuwa hata mradi wa Umeme wa Rufiji, JNHHP waliukosoa na kukataa kuukopesha kwa vigezo hivyo hivyo.
KIFUPI, hawa wenzetu hawatutakii mema na tukiendelea kuwasikiliza tutaendelea kuwa tegemezi daima dumu.
Na ndio maana tamko la Waziri Mkuu lazima liungwe mkono.
 
Bora ninyi mnapingwa kwenye makaratasi huo mradi,pale Msumbiji wanakotaka kuanza ujenzi, engineer na timu yake wanakoswakoswa na risasi si usiku si mchana.Kinachohuzunisha ni mwanachama mwenzao wa EU,mbaya zaidi ni wanachama wenzie wawili wa EU walompelekea kundi la ISIS.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu toa codes japo kiduchu ya hao EU you wawili wadhamini wa ISS
 
Mkuu hao wakubwa wana ajenda zao za siri za kukandamizi nchi za uchumi mchanga ili ziendelee kuwa masoko ya bidhaa zao.
Leo wanatuambia gesi, mafuta ni nishati chafuzi lakini wanalia na Urusi kuwanyima gesi kwa ajili ya viwanda vyao.
Kwa kifupi hawa wenzetu si wa kuwaamini sana kama unataka kuendelea.
Sijui nisemeje hapa ili nieleweke vizuri.

Haya unayosema hapa ni kweli kabisa na hayana pingamizi kwangu hata kidogo.

Hawa siyo watu wanaotutakia mema. Siyo watu wanaotaka tuwe huru, bila ya kuwategemea wao.Siku zote wanatafuta njia za wao kutuweka chini ya 'influence' yao, tuwasikilize wao wanasema nini, na kila maamuzi tunayofanya kwanza yawafikie wao na kuyaridhia. Huu ndio msukumo unaotawala maamuzi yao juu yetu.

Sasa, baada ya kusema hayo, naomba unielewe ninaposimamia.

Ni kwamba sisi wenyewe katika matendo yetu tunajiweka kuwa daima chini ya himaya yao. Hatuamini kwamba nasi tunaweza kufanya juhudi za kujinasua ili kila mara tusiwe watu wa kuwakimbilia hawa wakubwa na kuwategemea kwa mambo hata yaliyo chini ya uwezo wetu.
Wao walipokuwa wanachafua mazingira wakati wa ujenzi wa chumi zao hawakukimbilia kwetu kuja kuuliza wafanye nini; kwa sababu walihangaika wenyewe kutafuta njia za kujinasua na umaskini wa nchi zao.

Tofauti na sisi,kila jambo dogo ni kutegemea wao na wala hatuonyeshi makasiriko tunaposimangwa kama wanavyofanya sasa hivi, kwa nini?
Ni sisi wenyewe tunajiweka katika hali duni ya kiutegemezi kwao, ndiyo maana hawaoni aibu kabisa ya kutudharau kama watoto.

Miaka zaidi ya 60, baada ya kupata fursa ya kujiamlia mambo yetu wenyewe, bado tunaonekana kama watoto wadogo? Tutakuwa wakubwa lini?

Kabla sijaondoka hapa, ngoja nikupe mfano dhahiri kabisa unaoendana na mradi huu wa EACOP, unaotufanya tuwe kama watoto na hawa washenzi kutudharau kama wanvyofanya sasa.
Haya maswala ya "Uchafuzi wa Mazingira", na mambo ya "Haki za Binaadam", kwa nini yawe mambo magumu sana kwetu kuyatimiza bila hata kutumiwa kama fimbo ya kutupigia na hao wakubwa?

Kuna ugumu gani wa kueleza/kudadavua yote yanavyohitajiwa kwenye mradi husika na kuyaweka wazi kwa kila anayetaka kujua ajue? Kwa nini tufanye mambo yetu kizembezembe na kuficha au kutotoa taarifa kamilifu?

Hawa wapumbavu wanatumia mianya ya uzembe wetu na kutufanya tuonekane kama hatuna akili.

Kama kuna watu wanaotakiwa kuhamishwa kupisha mradi, kuna ugumu gani wa kuonyesha hatua zote zilizotumika na makubaliano na hao raia wetu hadi wakakubali kujengewa nyumba kwa mfano? Badala yake, sisi tunazuga tu, nyumba zilizojengwa hazionekani, inakuwa kama stori tu!

Ni mambo ya uzembe kama haya, kutotaka kufanya mambo yetu katika tratibu ndiyo yanayoleta maudhi, na kuwaruhusu hawa washenzi kutunyanyasa. Na yapo mengi sana ya aina hii yanayotufanya tuonekane kama majuha.
 
Big Up Mheshimiwa Cassim Majaliwa Kassim, Waziri Mkuu wa JMT.

Suala la bomba la mafuta toka Uganda kuelekea Tanga, inapitia kwa umbali mrefu zaidi nchini Tanzania.

Uchumi wa Tanzania utafaidika sana na ujenzi wa bomba hili, kwani kuna wananchi watafaidika moja kwa moja kwa kupata kazi na mafao mengine.
Zaidi ya hapo uchumi wa Tanzania utafaidika kwa vile hii ni biashara ambayo itawashirikisha wengi toka nje ya nchi na mataifa mengine zaidi ya Uganda na Tanzania.

Kelele tulizoona zinapigwa vikundi vya mazingira, hao ni wabaya wetu kimaendeleo.
Tumeona watu hao hao wakipinga kuondolewa wamasai mapori tengefu Loliondo na Ngorongoro.

Kumbe kuwa watu toka Kenya wanaingiza ng'ombe na kulisha/kunenepesha ng'ombe hao Tanzania.

Na hili la bomba la East African Crude Oil Pipeline(EACOP), wanaopinga ni wale wale waliokosa tender na sasa wanataka kuuvuruga mradi wenye faida kwa nchi zetu.

Mbaya zaidi ni mataifa ya Ulaya kulibebea bango suala hili, hili halijakaa vizuri.

Inabidi EU nao wajieleze kwa Watanzania na Waganda kwa nini hawataki nchi hizi ziendelee na kujitegemea.

Hivyo basi nampongeza sana Waziri Mkuu Kassim kwa kupigilia nyundo kuonyesha azama ya nchi zetu hizi kujitegemea kiuchumi kwa mradi huu.

Big up Bro Kassim Majaliwa!
Cassim ndio nani bwashee?
 
Ningependa kkubaliana na wewe mkuu lakini naona hulioni tatizo kubwa la wenzetu, tatizo la " me first".
Wenzetu wana tabia isiyoisha ya kujifikiria kwanza kuliko kitu kingine chochote.
Katika hili sina tofauti yoyote na wewe.

Lakini wakati huo huo nasi inalazimu tukubali kwamba tunachangia katika kufanya hao watuone katika mwonekano huo.
Hili ndilo tatizo kwetu. 'Mentality' hii nayo, utaanza kuona tunapewa heshima tunayostahiri kupewa.

Wazo la kusitisha miradi yetu ya maendeleo lingekuwa na mantki kama wao wangekuwa wa kwanza kusitisha matumizi ya nishati zilizopo.
Hatujasahau kuwa hata mradi wa Umeme wa Rufiji, JNHHP waliukosoa na kukataa kuukopesha kwa vigezo hivyo hivyo.
KIFUPI, hawa wenzetu hawatutakii mema na tukiendelea kuwasikiliza tutaendelea kuwa tegemezi daima dumu.
Tena hawana hata aibu wanapoonyesha waziwazi kutopenda sisi tujikwamue toka kwenye utegemezi kwao.

Sasa kuhusu hilo unaloita "...wazo la waziri mkuu", shida yangu ndipo hapo inapoanzia.
Tumuunge mkono kwa kitu gani, kwa kupiga kelele bila ya kufanya lolote kutuwezesha sisi wenyewe kukataa kunyanyaswa?
Tuunge mkono kitu gani, "kulalamika"?

Kesho Waziri Mkuu akitoka na kutoa hotuba inayotoa mwongozo/dira ya kulifanya taifa la Tanzania kujitambua na kuanza juhudi za kujiondoa kwenye manyanyaso haya, nami utanisikia nikiunga mkono Waziri Mkuu wangu.
Hapa sioni chochote cha kuunga mkono.

Hao Total Energies, ambao ni kampuni raia wa huko wanakotuadabisha, wakitishiwa, unadhani mradi utaendelea? Si tutabaki na kelele zetu tu?
Ninachotaka, hata tusipige kelele, tuwe tayari kufanya mambo yetu, tuwe na aina fulani ya uwezo wa kutotikiswa mara kwa mara na hawa watu kila wanapotaka kututisha.
 
Nitawakopesha. EU wakae na pesa zao.
Big Up Mheshimiwa Cassim Majaliwa Kassim, Waziri Mkuu wa JMT.

Suala la bomba la mafuta toka Uganda kuelekea Tanga, inapitia kwa umbali mrefu zaidi nchini Tanzania.

Uchumi wa Tanzania utafaidika sana na ujenzi wa bomba hili, kwani kuna wananchi watafaidika moja kwa moja kwa kupata kazi na mafao mengine.
Zaidi ya hapo uchumi wa Tanzania utafaidika kwa vile hii ni biashara ambayo itawashirikisha wengi toka nje ya nchi na mataifa mengine zaidi ya Uganda na Tanzania.

Kelele tulizoona zinapigwa vikundi vya mazingira, hao ni wabaya wetu kimaendeleo.
Tumeona watu hao hao wakipinga kuondolewa wamasai mapori tengefu Loliondo na Ngorongoro.

Kumbe kuwa watu toka Kenya wanaingiza ng'ombe na kulisha/kunenepesha ng'ombe hao Tanzania.

Na hili la bomba la East African Crude Oil Pipeline(EACOP), wanaopinga ni wale wale waliokosa tender na sasa wanataka kuuvuruga mradi wenye faida kwa nchi zetu.

Mbaya zaidi ni mataifa ya Ulaya kulibebea bango suala hili, hili halijakaa vizuri.

Inabidi EU nao wajieleze kwa Watanzania na Waganda kwa nini hawataki nchi hizi ziendelee na kujitegemea.

Hivyo basi nampongeza sana Waziri Mkuu Kassim kwa kupigilia nyundo kuonyesha azama ya nchi zetu hizi kujitegemea kiuchumi kwa mradi huu.

Big up Bro Kassim Majaliwa!
 
Katika hili sina tofauti yoyote na wewe.

Lakini wakati huo huo nasi inalazimu tukubali kwamba tunachangia katika kufanya hao watuone katika mwonekano huo.
Hili ndilo tatizo kwetu. 'Mentality' hii nayo, utaanza kuona tunapewa heshima tunayostahiri kupewa.


Tena hawana hata aibu wanapoonyesha waziwazi kutopenda sisi tujikwamue toka kwenye utegemezi kwao.

Sasa kuhusu hilo unaloita "...wazo la waziri mkuu", shida yangu ndipo hapo inapoanzia.
Tumuunge mkono kwa kitu gani, kwa kupiga kelele bila ya kufanya lolote kutuwezesha sisi wenyewe kukataa kunyanyaswa?
Tuunge mkono kitu gani, "kulalamika"?

Kesho Waziri Mkuu akitoka na kutoa hotuba inayotoa mwongozo/dira ya kulifanya taifa la Tanzania kujitambua na kuanza juhudi za kujiondoa kwenye manyanyaso haya, nami utanisikia nikiunga mkono Waziri Mkuu wangu.
Hapa sioni chochote cha kuunga mkono.

Hao Total Energies, ambao ni kampuni raia wa huko wanakotuadabisha, wakitishiwa, unadhani mradi utaendelea? Si tutabaki na kelele zetu tu?
Ninachotaka, hata tusipige kelele, tuwe tayari kufanya mambo yetu, tuwe na aina fulani ya uwezo wa kutotikiswa mara kwa mara na hawa watu kila wanapotaka kututisha.
Asante sana mkuu
 
Ukweli ni kwamba halitajengwa! Sio kwasababu wazungu hawalitaki, ila kwasababu wakati wa kujenga miradi mikubwa ya mafuta ya petrol na dizel umekwisha kutokana na mwenendo wa hali ya uchafuzi wa mazingira duniani. Tunaofuatilia maswala na renewable energy transition tunajua kuwa si zaidi ya miaka 15 ijayo magari yanayotumia petrol au dizel yatakuwa machache sana na kwa nchi nyingi tu duniani yatakuwa yamepigwa marufuku. Hivyo ya nini kuwekeza kwenye mradi matrilioni yote haya na mradi hautafanya kazi miaka michache tu ijayo?
Mafuta aina yote ya mitambo,lazima ya tumike,mitambo ni vyuma,lazima kuwepo na Oil ya kulainisha hivyo vyuma.Huko viwandani,Oil inatumika kulainishia vyuma visisuguane.
 
20220927_105336.jpg

Wadau wamaendeleo ya nchi yetu wameanza kukubaliana na msimamo wa nchi uliotolewa na Mh. waziri Mkuu Majaliwa.
Argument kubwa na nzuri ni pamija na matumizi ya petroleum products.
Benki ya Standard imesema hadharani kuwa mradi huu una manufaa makubwa kwa Tanzania na zuganda.
 
Awamu hii wanapenda sana pesa za kudownload.

Wataendelea kupambana na tozo na kuachana na miradi kama hii.
 
Bora ninyi mnapingwa kwenye makaratasi huo mradi,pale Msumbiji wanakotaka kuanza ujenzi, engineer na timu yake wanakoswakoswa na risasi si usiku si mchana.Kinachohuzunisha ni mwanachama mwenzao wa EU,mbaya zaidi ni wanachama wenzie wawili wa EU walompelekea kundi la ISIS.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona kimafumbo zaidi waogopa nini? Aheri usingandika kabisa!
 
Sababu kubwa ya Ulaya kuupinga huu mradi ni vile Uganda ina uhusiano wa karibu sana na Urusi. Hawa watu wana chuki na kiburi huwezi kuamini. Afrika kukitokea mgogoro siku ya pili wanatuma wajumbe kadhaa eti kusuluhisha kwa amani na kwamba vita haina tija. Walikuwa wanatufanya kama watoto wajinga tusiokuwa na issues za kuhalalisha vita. Wao wakijiona wamekomaa na hawawezi kamwe kupigana tangu vita vya 1945. Sasa kumbe wanaona wao ni binadamu tu kama binadamu wengine na wana mihemuko na chuki zile zile. Inawauma sana hii vita ya Ukrania. Imewaumbua!
 
Wenye uchungu na nchi hii wako wengi tu toka enzi za Mwalimu.
Miaka hii hakuna mkuu. Akina miguru?. Anajifanya mzerondo kutwa na skafu yenye bendera ya taifa. Kapewa nafasi nyeti anavuruga vuruga tu na kujipigia sana. Yupo na mwenzie makatani kapewa nafasi wizara nyeti,umeme unakatika siku nzima. Kipindi cha mwanzo ametupiga fix eti marekebisho. Marekebisho gani kila siku? kipindi cha Magu umeme ilishaanza kuwa historia kukatika
 
Miaka hii hakuna mkuu. Akina miguru?. Anajifanya mzerondo kutwa na skafu yenye bendera ya taifa. Kapewa nafasi nyeti anavuruga vuruga tu na kujipigia sana. Yupo na mwenzie makatani kapewa nafasi wizara nyeti,umeme unakatika siku nzima. Kipindi cha mwanzo ametupiga fix eti marekebisho. Marekebisho gani kila siku? kipindi cha Magu umeme ilishaanza kuwa historia kukatika
Kuwa mzalendo siyo lazima uwe Waziri.
Kuna wazalendo(unsung heroes) wengi tu wanaowapiga lock hao wanaojiitia uzalendo kumbe wana agenda zao.
 
Back
Top Bottom