Huyo DED aache uongo kuwa hajui. Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ni DC, na siku ya uvunjaji DC Gondwe alikuwepo. Hivyo huyo DED anayesema ataitisha kikao cha kamati ya ulinzi na usalama nikupotezea hilo swala kisiasa.
Ukweli ni kwamba wenye mijengo ya maana iliyokamilika haikuvunjwa, waliovunjiwa ni wale wenye chumba kimoja, viwili na nyumba ambazo hazijakamilika au ambazo siyo kali.
Bomoa bomoa ililenga eneo la NSSF. Ila wazito wanaoishi kwenye eneo hilo na eneo jirani linalopakana na nssf wakaamua kuwaondoa maskini katikati yao ili mji ujengeke (noble neighbour hood)kwa madai kuwa nako ni eneo la serikali(nssf). Kote kulikobomolewa ni maeneo ya uvamizi hivyo hata hao vigogo nao walivamia au kuuziwa na wavamizi ila hawakuguswa