Bomoabomoa yaacha simanzi Mabwepande, nyumba za matajiri zaachwa

Bomoabomoa yaacha simanzi Mabwepande, nyumba za matajiri zaachwa

Hayo maeneo yalikua ni mapori makubwa(non-habitable) tokea uhuru. Wavamizi wamesafisha, wameokota mafuvu ya watu, wamefukuza chatu hadi pameonekana panafaa kuishi binadamu. Wamepelekewa umeme na kufungiwa na TANESCO, TARURA wakatengeneza barabara na DAWASA wamewapeleka maji na kuwafungia kabisa. Leo wanakuja na kudai ni eneo la serikali na kuwavunjia waondoke ili wapime viwanja wauziane wenyewe kwa wenyewe viwanja vya low-density. Hao maskini wataweza kununua viwanja 20m? Kwanini wasiwafikirie japo wawapunguzie bei? Na walioachwa kubomolewa ni wale walioweza kulipa hiyo pesa. Kiufupi matajiri wametamani lile eneo maana limekamilika (habitable) na sasa njia ni kuwafutilia mbali waanzilishi
Watu wajiandae kisaikolojia tu. Kumbe maviwanja ni ya low density hayo. Hapo mpango ni kuwafukuza tu ili wabakie wao matajiri.

Haki ya mungu huu ushenzi Magufuli asingeubariki kabisa kwa sababu una roots za ouvu wa matajiri dhidi ya watu maskini. Hakika mtamkumbuka sana yule jamaa.
 
Waache ujinga hao wananchi.
Suala ni hivi tumebomoa na hizo zilizobaki zitabomolewa.
Mwenye malalamiko aende mahakamani . Kama serikali ikipatikana na hatia italipa kwa fidia.
Unavamia maeneo halafu unalialia.
Serikali ipo haijalala, unaweza ukavunja sheria ukadhani serikali imekupuuzia au haijakuona kumbe tunakulia timing tu.
Napenda sana utawala wa kisheria sio ule ukienda court unatekwa hukohuko.
Magufuli alibomoa sana Pugu, Kimara n.k bila fidia na virungu juu.
 
Hebu tufafanulie,huko Tanga,ni mwarabu gani katoa pesa,na kujengewa maskini,na ni Tanga,sehemu gani?
Ni swala la kutumia akili tu. Ngorongoro haiwezi kuuzwa kama Goba 😂😂😂!

Mfano mtu akupe trillion 2O utashindwa kutoamo billion 1O ya kuwajengea wanakijiji nyumba za fasta.
 
Watu wajiandae kisaikolojia tu. Kumbe maviwanja ni ya low density hayo. Hapo mpango ni kuwafukuza tu ili wabakie wao matajiri.

Haki ya mungu huu ushenzi Magufuli asingeubariki kabisa kwa sababu una roots za ouvu wa matajiri dhidi ya watu maskini. Hakika mtamkumbuka sana yule jamaa.
Magu huyuhuyu aliyesemaga msiwabomolee nyumba watu wa mwanza kwa sababu walinipigia kura?

Alikuwa na ushetani kwenye baadhi ya mambo.,
 
Magu huyuhuyu aliyesemaga msiwabomolee nyumba watu wa mwanza kwa sababu walinipigia kura?

Alikuwa na ushetani kwenye baadhi ya mambo.,
Watu wamevunjiwa nyumba Mwanza. Hizo siasa tu ila watu walivunjiwa kama kawaida
 
Hii
Hayo maeneo yalikua ni mapori makubwa(non-habitable) tokea uhuru. Wavamizi wamesafisha, wameokota mafuvu ya watu, wamefukuza chatu hadi pameonekana panafaa kuishi binadamu. Wamepelekewa umeme na kufungiwa na TANESCO, TARURA wakatengeneza barabara na DAWASA wamewapeleka maji na kuwafungia kabisa. Leo wanakuja na kudai ni eneo la serikali na kuwavunjia waondoke ili wapime viwanja wauziane wenyewe kwa wenyewe viwanja vya low-density. Hao maskini wataweza kununua viwanja 20m? Kwanini wasiwafikirie japo wawapunguzie bei? Na walioachwa kubomolewa ni wale walioweza kulipa hiyo pesa. Kiufupi matajiri wametamani lile eneo maana limekamilika (habitable) na sasa njia ni kuwafutilia mbali waanzilishi
hii ndio shida ya wavamizi kudhani kinondoni ni porini

Basi wakafyeke kapori ka lugalo pale pia
 
Waache ujinga hai wananchi.
Suala ni hivi tumebomoa na hizo zilizobaki zitabomolewa.
Mwenye malalamiko aende mahakamani . Kama serikali ikipatikana na hatia italipa kwa fidia.
Unavamia maeneo halafu unalialia.
Serikali ipo haijalala, unaweza ukavunja sheria ukadhani serikali imekupuuzia au haijakuona kumbe tunakulia timing tu.
Napenda sana utawala wa kisheria sio ule ukienda court unatekwa hukohuko.
Magufuli alibomoa sana Pugu, Kimara n k bila fidia na virungu juu.
Umevimbewa wali maharage ya shemeji
 
Hii

hii ndio shida ya wavamizi kudhani kinondoni ni porini
Enzi za Abdala Zombi na mauaji Mabwepande kuna mtu alikuwa anasogelea pande hizo hata umpe kiwanja bure? Msitu wa mabwepande na maeneo yanayozunguka huo msitu hakuna aliyekuwa anathubutu kuishi maeneo hayo kwani yalikua mapori haswa, wewe umekua juzi kwenye lami na kukuta maghorofa ndio maana unasema hivyo. Huko walikovunjiwa ni maeneo jirani na pori la mabwe
 
Hayo maeneo huko ni tatizo kubwa. Ukitaka kununua kiwanja kuanzia Kisauke, Kulangwa, Mbopo, Kinondo, Nyakasangwe, Msakuzi, Mabwepande, Msumi na jirani ya hizo sehemu jiridhishe mara tatu tatu. Kuna jamaa wajanja sana wanavamia maeneo makubwa ya watu wanagawa viwanja vya 20 X 20 wanauza tena utakuta bei rahisi kabisa na balozi/mjumbe wa kuchonga yupo viwanja vikishauzwa vikaisha wao wanasepa wanahama kabisa wanaenda kuvamia sehemu nyingine.

Ukifika kununua kiwanja ukisika eneo lina jina la ajabu ajabu sijui mwanaukome, kahama (mwenye eneo kahama) na yanayofanana na hayo kuwa mwangalifu sana na ikiwezekana kimbia na pesa zako. Mwenyewe eneo akija unakuta eneo limepimwa kisheria kabisa na lina hati na mhusika analipia kodi wizarani kila mwaka. Hapo ndio balaa linaanzia kwa sababu unakuta baadhi ya waliouziwa tayari wameshajenga tena kwa pesa waliyodudunduliza au kukopa..
 
Enzi za Abdala Zombi na mauaji Mabwepande kuna mtu alikuwa anasogelea pande hizo hata umpe kiwanja bure? Msitu wa mabwepande na maeneo yanayozunguka huo msitu hakuna aliyekuwa anathubutu kuishi maeneo hayo kwani yalikua mapori haswa, wewe umekua juzi kwenye lami na kukuta maghorofa ndio maana unasema hivyo. Huko walikovunjiwa ni maeneo jirani na pori la mabwe
Itakua yalikua na hati wenye nayo wametulia nazo tu wanasubiri mji ukue

Kama pori ni issue mtu unaweza enda kujikatia kiwanja serengeti saivi?ama kapori ka'lugalo pale?

Ni yaleyale ya WazoHill eneo la kiwanda watu wamevamia

Nashauri tufuate taratibu za umiliki hata kama ni porini
Nje ya mji bei za serikali ni ndogo mnooo
 
Hayo maeneo huko ni tatizo kubwa. Ukitaka kununua kiwanja kuanzia Kisauke, Kulangwa, Mbopo, Kinondo, Nyakasangwe, Msakuzi, Mabwepande, Msumi na jirani ya hizo sehemu jiridhishe mara tatu tatu. Kuna jamaa wajanja sana wanavamia maeneo makubwa ya watu wanagawa viwanja vya 20 X 20 wanauza tena utakuta bei rahisi kabisa na balozi/mjumbe wa kuchonga yupo viwanja vikishauzwa vikaisha wao wanasepa wanahama kabisa wanaenda kuvamia sehemu nyingine.

Ukifika kununua kiwanja ukisika eneo lina jina la ajabu ajabu sijui mwanaukome, kahama (mwenye eneo kahama) na yanayofanana na hayo kuwa mwangalifu sana na ikiwezekana kimbia na pesa zako. Mwenyewe eneo akija unakuta eneo limepimwa kisheria kabisa na lina hati na mhusika analipia kodi wizarani kila mwaka. Hapo ndio balaa linaanzia kwa sababu unakuta baadhi ya waliouziwa tayari wameshajenga tena kwa pesa waliyodudunduliza au kukopa..
Kweli kabisa mkuu. Mimi mwenyewe niliwahi kutapeliwa kwa kuuziwa kiwanja cha uvamizi ila kwenye kiwanja kimoja tumeuziwa watu watatu. Ingawa kesi ya uvamizi eneo hilo wananchi walishinda kwakuwa ilikuwa ni shamba pori(lisiloendelezwa tokea uhuru na hati zilifutwa na serikali), ila hadi kesho hakuna anayejenga kwani ukijenga mwenzako anakuja kubomoa anadai ni kiwanja chake. Wauzaji walishasepa na wengine wapo gerezani
 
Wavamizi unaweza kuwazuia?

Si waonyeshe nyaraka za umiliki

Nnavyojua Serikali haibomoi bila kuhakiki umiliki

Ukosa sahihi,
Nilicho maanisha ni kutokana na hii:

“Tulifika Mabwepande kama Serikali ya Wilaya tukazungumza na wananchi, nao walieleza malalamiko yao na tuliwataka wote waliovamia maeneo wahame kwa sababu yanatakiwa kuendelezwa,” alisema.


Kama eneo tayari tumebaini kuna wavamizi, na vikao tumekaa nao.
kwa nini hatukuzuia ujenzi waliokuwa wakifanya? je ni mpaka nyumba/vyumba vikamilike ndio tuje kubomoa?
je gharama za kubomoa boma nyumba zaidi ya 400 na kuzuia ujenzi zipi kubwa?
 
Ukosa sahihi,
Nilicho maanisha ni kutokana na hii:

“Tulifika Mabwepande kama Serikali ya Wilaya tukazungumza na wananchi, nao walieleza malalamiko yao na tuliwataka wote waliovamia maeneo wahame kwa sababu yanatakiwa kuendelezwa,” alisema.

Kama eneo tayari tumebaini kuna wavamizi, na vikao tumekaa nao.
kwa nini hatukuzuia ujenzi waliokuwa wakifanya? je ni mpaka nyumba/vyumba vikamilike ndio tuje kubomoa?
je gharama za kubomoa boma nyumba zaidi ya 400 na kuzuia ujenzi zipi kubwa?
Hivi ni kazi ya Serikali kulinda msijenge ama kazi yao ni kutoa Hati miliki?

Wakuzuie kujenga we mbona hujizuii kujenga na huna miliki ya hilo eneo?
Waliojenga wana hata vibali vya ujenzi?ama ni kiholela?

Acheni vurugu jmn fatenj taratibu stahiki za umiliki
Mtu ukitamani kapori unafyeka unaishi basi hii nchi ingekua na vita kubwa sana
Ni taratibu zinafuatwa
Watu wamebomolewa Morogoro Rd sembuse huko ndani?
 
Kweli kabisa mkuu. Mimi mwenyewe niliwahi kutapeliwa kwa kuuziwa kiwanja cha uvamizi ila kwenye kiwanja kimoja tumeuziwa watu watatu. Ingawa kesi ya uvamizi eneo hilo wananchi walishinda kwakuwa ilikuwa ni shamba pori(lisiloendelezwa tokea uhuru na hati zilifutwa na serikali), ila hadi kesho hakuna anayejenga kwani ukijenga mwenzako anakuja kubomoa anadai ni kiwanja chake. Wauzaji walishasepa na wengine wapo gerezani
Tafuteni hati

Ama mliuziwa mkarelax

Kwenye hati ni mwisho wa reli
Migogoro yote inakua bayana
 
Back
Top Bottom