Bomu la Nyuklia: Jielimishe hapa

Bomu la Nyuklia: Jielimishe hapa

Mmmh! umenikumbusha mbali sana "terminologies" hizo. Mara nuclear fusion, isotopes e.t.c. Mimi hapa cna msaada kwakweli (zaid ya "likes" na kuwafagilia kina Gay-Lussac!, bhaaas!).

Natamani Dr.Ghalib Bilal (V.President) angekuwa humu ndani. Ni moja ya watanzania nadra sana wenye Elimu & Kisomo cha mambo haya.

Respect!

Shangaa tu kwa sasa kawa mtaalamu wa kuzindua miradi na kwa professional wa kukata utepe, angekuwa chuo anazalisha wataalam wa hii kitu balaa.
 
Shangaa tu kwa sasa kawa mtaalamu wa kuzindua miradi na kwa professional wa kukata utepe, angekuwa chuo anazalisha wataalam wa hii kitu balaa.

mkuu nijuze ana level gan ya elimu ktk mambo haya na aliipatia wapi kama hutajali anika historia yake ktk taaluma hii TuntemekeSanga & Easymutant
 
Last edited by a moderator:
hawezi kuwa noma mpk tutakapojua amefanya successful project ipi inayojihusisha na mambo ya nuclear

huyu uwezo wake ni zaid ya taaluma ya nyuklia aliyonayo taaluma yake hasa ktk physics angeweza kuzalisha watu muhimu sana ktk taifa letu zaidi ya alivyo mwanasiasa sasa kaz kutembea na mkas mfukon
 
Wakubwa russia sio mchezo mi watu hatari sana, wanakabomu kadogo sana wala sio cha nuklia ni cha maangamizi tu cha masafa ya kati lakini ulaya nzima wanambwela kinaitwa ISkander ni balaaa ukiliona linakatiza unasema drone. Mmarekani anasubili sana kwa mrusi
 
Tukumbushane kidogo kuwa nchi ya kwanza kutengeneza silaha za nyukilia ilikuwa ni marekani chini ya mradi wao wa Manhattan Project ambapo walitumia mabomu mawili ya atomic dhidi ya Japan kwa kupiga miji ya Nagasaki na Hiroshima na kulazimisha vita ya pili ya dunia iishe. Miaka ya sitini pale Tanga kulikuwa na bendi inaitwa Atomic Jazz kwa kukumbukia makali ya bomu hilo la Atomiki lilioangushwa Japan. Kuanzia mwaka 1948 hadi leo hakuna bomu la namna hiyo lililowahi kutumika katika vita; nchi nyingi zimekuwa zinayatengeza kama retardant tu, yaani ukijulikana unalo basi hakuna atayekusogelea. Ubaya wa mabomu hayo ni kuwa yanaua waliomo na wasiokuwamo, kwa mfano bomu moja la nyuklia likilipuliwa nchi moja basi hata majirani watapata madhara yake. Katika teknologia ya Nyuklia, ni Ukraine tu wakati ikiwa chini ya USSR iliyowahi kuwa na ajali kubwa ya kiufundi iliyotokea Chernobyl mwaka 1986 ambayo yaliathiri hata nchi za Ulaya. Ajali ya tetemeko la ardhi ya Japan iliyosababisha ajali ya Fukushima Daaichi haikujaweza kufikia ile ya Chernobyl.

Kwa hiyo hata kama Urusi wana mabomu mengi ya aina hiyo, hayasaidii chcchote kwani hayatumiki vitani na hata yanapotumika hyaawezi kuwa zaidi ya mawili katika vita moja, hafalu mwishoni ni kuwa Urusi imeshaprove kutokuwa na uwezo mzuri wa kulinda silaha hizi hasa kwa vile ilishindwa kulinda Chernobyl.
 
huyu uwezo wake ni zaid ya taaluma ya nyuklia aliyonayo taaluma yake hasa ktk physics angeweza kuzalisha watu muhimu sana ktk taifa letu zaidi ya alivyo mwanasiasa sasa kaz kutembea na mkas mfukon

Hahaha mangi umenichekesha kweli, jamaa kazi yake kutembea na mkasi na kuvaa miwani mieusi
 
Mkuu hapo umeniacha mbuzi kidogo, kuna tofauti gani kati ya tactical weapons na strategy weapons?
mkuu kwa ushallo wangu wa masuala ya kivita na elimu yangu ninayoipata kupitia Discovery Channel kila nipatapo muda ni kuwa tactical weapons ni zile silaha ambazo huwa deployed kwenye uwanja wa mapambano (hapo tayari vita imeshaanza hivyo inakuw ni sehemu ya mbinu ya kivita) wakati strategic weapons ni zile ambazo hutumik na upande mmoja kuudhoofisha mwingine kwa kupiga maeneo nyeti kama viwanda, milliary base na maeneo mengine kabla ya vita kuanza au kabla vita haijachanganya.likewise kwa hayo makombora.I stand to be corrected though.
 
hizo makitu wakijua kutengeneza hawa ndugu zetu wa damu si watatumaliza??

hao makundi ya kiisilamu ya kigaidi
Acha ushenzi, ina maana wanaoua watu kwa hizo mass weapons huwaoni au kuwatafuta tu waislamu, hivi kwa nini ninyi watu mkawa na roho mbaya kuliko hata ya shetani, hebu niambie: yule aliyeangusha nuclear bomb kule Hiroshima alikuwa muislamu...? vipi kuhusu wale waliochoma watu kwa kutumia white phosphorus kule IRAQ nao walikuwa waislamu, ama yule aliyetumia chemical weapons kule Vietnam nae alikuwa muislamu, nadhani kama hauna cha kuchangia bora ukajisomea tu bila ya kupost,nikikuuliza walau nchi moja mnayoiita ya kiislamu ambayo imetumia mass destructive weapons utabaki mdomo wazi.
 
Asante sana Kichuguu nimeipenda sana hii mada though sina uelewa wa haya mambo pamoja ya kuwa nilikuwa nasikia tu juu juu,ila hii yako imenipa mwanga wa nini kinaendelea kuhusiana na nuclear weapons.
 
Last edited by a moderator:
hizi habari mimi ninavyojua ni siri ya nchi... .. .na kama wameamua ku expose inamaana ishakuwa outdated, kwa hiyo kujua nani anaongoza kwa sasa katika hii technology itabaki kuwa siri tuuu...na hizi zote ni tetesi tu!
 
Ninaanzisha thread hii ili kuwakaribisha wataalamu wa Nuclear phyiscis watupe elimu kuhusu Nuclear energy.

Bomu la nyuklia hutengenezwa kutokana na madini yenye asili ya Radioactive kama vile Uraninum au Plutonium. Madini haya yana tabia kuwa yakistuliwa kidogo tu basi yanaanza process inayoitwa nuclear fission ambapo hupasuka vipande vidogo vidogo huku yakiwa yaanaachia joto jingi sana.

Madini ya uranium yana mifumo (isotopes) mbili, Uranium U-235 na Uranium U-238. Mfumo wenye nguvu za nuklia nie ule wa U-235, hata hivyo madini ya uranium ya asili kama yanayochimbwa hapa kwetu yana kama nusu asilimia tu ya U235, wakati asilimia karibu 99.5 ni U-238.

Bomu moja la Nyukilia huhitaji U-235 kama kilo hamsini hivi hivi, kwa hiyo ili kuzipata hizo kilo hamsini inabidi uwe na uranium asili zaidi ya tani mia moja halafu uichuje kwa kutumia chekecheo ziitwazo centrifuge ili kuondoa U-238 ambayo ni nzito kidogo na kuacha U235 ambayo ni nyepesi. Kuchuja tani moja ya Uraniuma inaweza kuchukua miaka miwili au hata mitano kutegemea na ubora wa centrifuge ulizo nazo.

Ukishaweka U235 iliyochujwa mahali palipotulia, unachohitaji ni kuidisurtb kidogo tu hata kwa kuiangushia mchanga, halafu yenyewe inaaza nuclear fission inayosababisha kitu kinaitwa chain reaction ambayo hutoa joto kali sana na kuunguza kila kiliocho hapo katika maeneo yake. Nguvu za nuklia hutumia joto hilo badala ya makaa ya mawe kuchemsha maji kutoa mvuke wa kuendesha mashine za kufua umeme.

Yale mabomu ya atomiki yalioangusha Nagasaki na Hiroshima yaliuwa watu kwa sababu ya joto ikafikia hata mifupa ya watu ikiwa inayeyuka kwa sababu ya joto. Mabomu conventional yanayotumia baruti huua watu na kubomoa majengo kwa ajili ye pressure lakini Nyuklia huwasha moto tu.

Wana fizikia wa nuklear physiscs ingieni hapa mtupe elimu kuhus nishati hii inayoogopwa duniani kote.

uranium au atomik bomb inakuwa na effect kubwa ikitengezwa na hidrogen gas...yaani hidrogen nuclear bomb..HATAARII
 
Hayo mabom unayosema ya Pakistan na India ni ya masafa mafupi km kilometres 250, hivyo hayamdhuru mmarekani kwani lengo la mabomu hayo ni wao kwa wao Pakistan na India kisha mbili ana.
 
Back
Top Bottom