Bongo Flava ya sasa ni uozo mtupu

Nope sijamaanisha wote,wapo wachache wanafanya vizuri.Kama unabisha washa radio au television ukiwa na mtu unaye mheshimu 3/4 ya nyimbo zitakazo chezwa ni ngono tupu.
sasa hivi mziki ni matusi ila zamani sio matusi yani umeweka double standard kwanini??

Dully Sykes anakuambia "nipe japo kiduchu nishachoka kupiga puchu"

KR Mulla anakuambia "we ukitaka tende chukua lakini .... unapanua"

unataka za Temba??

Hata zamani matusi yalikuwepo bwana tena ya wazi tu ila walichobarikiwa ni kwamba mashairi yao mpaka bado yanaishi tofauti na sasa.
 
Kiukweli hata Mimi sisikilizi nyimbo hzo aisee , japo wapo wanaozipenda Ila hamna kitu ....mara moja moja wanajaribu, rayvanny nyimbo zake za slow waweza sikiliza Ila hzo nyegezi mhhhh

NImenza kuwa shabiki wa Qchief kwa hizi nyimbo mpya alizotoa, zinasikilizika bila shida.
 
Ndiyo mziki wa sasa ni ngono tupu corus na verse zote ni matusi jirekebisheni wasanii.
 
2pac alishawahi kusema kuwa., sisi ni ma'rapa, tunaimba vitu tunavyoviona na kuvifanya, tukiimba kuwa tunavuta bangi, ni kweli tunavuta bangi, kwa hiyo wazazi inabidi wafanye kazi yao.

Kwa hiyo acha kulalamika mzee.
 

Nay wa mitego - Kwa Mpalange. Mkuu ushausikiliza huu wimbo, itabidi kwenye somo la kiswahili ile topic ya Uhakiki wa fasihi wanafunzi waanze kuhakiki na nyimbo za bongofleva aseee[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
2pac alishawahi kusema kuwa., sisi ni ma'rapa, tunaimba vitu tunavyoviona na kuvifanya, tukiimba kuwa tunavuta bangi, ni kweli tunavuta bangi, kwa hiyo wazazi inabidi wafanye kazi yao.

Kwa hiyo acha kulalamika mzee.
Siyo kila kitu cha kuiga mkuu, Rashidi benzino awe Omar shakur kweli,waige na kupigana risasi basi.
 
Mkuu nakubaliana....ila wa sasa wanaenda na soko linavyotaka....na ndo wamepaisha fani kimataifa...
 
Siyo kila kitu cha kuiga mkuu, Rashidi benzino awe Omar shakur kweli,waige na kupigana risasi basi.
Kuna vitu vikifika level fulani ni ngumu kuvizuia bali kuvitengenezea mazingira na utaratibu mzuri.
Kuna kipindi niliwahi andika uzi humu wa kufanya censorship ya nyimbo kwa utaratibu huu.

1. Mamlaka zinazohusika na kusimamia sanaa ziandae mgawanyo wa kimaudhui. Mfano nyimbo zote zinazotaja mambo ya ngono, vilevi, madawa ya kulevya, matumizi ya silaha ziwekwe kwenye kundi tuliite labda E'rated. Halafu nyingine zenye maudhui ya kawaida ziwe rated kama tuseme labda A'rated. Na mwongozo huu unatakiwa ufuatwe na kila msanii.

2. Msanii anapotaka kutoa wimbo lazima aufanyie tathmini ili ajue unadondokea wapi kati ya E'rated au A'rated na atatakiwa au'lebel kulingana na kundi unapodondokea.

3. Nyimbo zote ambazo ni E'rated hazitatakiwa kuchezwa redioni, kwenye tv, kwenye saluni au eneo lolote la umma. Na yeyote ambaye atabainika itabidi aadhibiwe kulingana na sheria ambayo itakuwa imetungwa (inatakiwa iwe kali sana). Nyimbo ambazo ni E'rated zitapatikana mitandaoni tu sehemu ambapo mtu anainngia kwa ridhaa yake.

4. Kama msanii ana wimbo ambao ni E'rated na anataka uchezwe redioni au kwenye tv, basi anapaswa kutengeneza clean version ambayo itakuwa rated kama A'rated.

Huu ni utaratibu mzuri unaohitajika kwa sasa ila unahitaji usimamizi wa karibu sana ili ufanye kazi. Bora huku kuliko kupiga kelele nyimbo zifungiwe kitu ambacho hakiwezekani.
Kwa upande wa filamu wanafanya hii kitu, tofauti ni kuwa kwa wao ni lazima upeleke filamu yako wanaikagua then wanaipa daraja.
 
Basata na Tcra wafanye hili kuokoa kizazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…