Boniface Jacob: Rais Samia tunaomba Afande Mafwele anayetuhumiwa kumteka Sativa achunguzwe

Boniface Jacob: Rais Samia tunaomba Afande Mafwele anayetuhumiwa kumteka Sativa achunguzwe

1. Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
2. Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Hamad Masauni.
3. Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Camillus Mongoso Wambura
4. Jaji Mkuu wa Tanzania, Ibrahim Juma
5. Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Jacob Nkunda
6. Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, DIGS, Suleiman Mombo
7. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Hamza Johari

1. Mheshimiwa Rais, Wakati huu nchi ikiwa katika taharuki kubwa na sintofahamu ya watu kutekwa na kupotea kwa watu kisha mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Makao Makuu, Ali Muhammad Kibao.

Niruhusu nimlete kwenu mtumishi wa serikali na afisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ACP Faustine Mafwele katika tuhuma za Mtanzania Mwenzetu Edger Edson Mwakabela (SATIVA).

2. Mheshikiwa Rais, napenda kukukumbusha kwamba, Edger Edson Mwakabela (Sativa) kijana ambaye alitekwa 23 June 2024 na kupatikana 27 June 2024 akiwa amejeruhiwa na risasi ya kichwa katika mapori ya hifadhi ya Taifa ya katavi, Mkoa wa Katavi na baadae RAIS ukamchangia matibabu ya jeraha la risasi kiasi cha Tsh Millioni 30.

3. Mheshimiwa, Rais Edger Edson Mwakabela kwa sasa amepona na hana itilifafu yoyote ya kumbukumbu wala akili pamoja na kupitishwa na katika madhira makubwa ya ukatili mbaya sana dhidi ya binadamu.

4. Mheshimiwa Rais, 27 June 2024 Edger Edson Mwakabela akiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Mkoa katavi alihojiwa na gazeti la Nipashe kwa njia ya video



Katika mahojiano hayo SATIVA anasema kwa kumbukumbu kuwa alitekwa Jumapili usiku na kupelekwa katika Karakana ya Kituo cha Polisi Oysterbay na siyo kituoni ndani kabla ya kusafirishwa kupelekwa Mkoani Arusha na baadae Katavi.

5. Mheshimiwa Rais, kwa muda wote huu Edger Edson Mwakabela alishahojiwa na Jeshi la Polisi na baadae walipotaka maelezo ya nyongeza Edger Edson Mwakabela alikuwa katika upasuaji katika hospitali ya Aga Khan.

Mwezi August Edger Edson Mwakabela aliwataarifu Jeshi la Polisi kuwa tayari ameondolewa vyuma vya taya na sasa yupo tayari kwa mahojiano na Jeshi la Polisi, akawauliza, Je, afike kituo gani na muda gani kwa mahojiano?

Soma Pia:

Kwa masikitiko makubwa Jeshi la Polisi kupitia Afande James wa kutoka Ofisi ya DCI - Dodona, alimjibu kuwa watamtafuta kwa mahojiano siku wakipata nafasi na mpaka leo Jeshi la Polisi halijawahi kupata nafasi ya kumuhoji Sativa.

6. Mheshimiwa Rais, 21 August 2024 baada ya kupotea Vijana watatu wanachama na Viongozi wa chadema Godwin Mlay, Deusdedith Soka na Frank Mbise Watanzania walianza kusambaza watu wanaowatuhumu kwa matukio ya kuteka watu kutoka katika vyombo vya dola, mmoja ya watu ambao picha zao zilisambazwa alikuwa ni ACP Faustine Mafwele

7. Mheshimiwa Rais, Kijana wako Edger Edson Mwakabela alipo iona picha ya ACP Faustine Mafwele, 22 August 20224 alitutaarifu watu wake wa karibu ikiwamo mimi, kuwa mtu yule ambaye picha yake ilikuwa ikisambaa mitandaoni ndiye alifika nje ya Kituo cha Polisi Oysterbay usiku wa Jumapili ya 23 June majira ya Saa 2:00 kuelekea majira ya Saa 3:00 usiku.

Na kwamba ACP Faustine Mafwele alimuhoji Edger Edson Mwakabela maswali matatu 1.Unaitwa nani 2. Unafanya shughuli gani 3.Unajua kwanini upo hapa?

Baada ya mahojiano hayo mafupi ACP Faustine Mafwele aliwafuata watu waliomteka Edger Edson Mwakabela na kwenda kuongea nao mazungumzo ambayo Edger Edson Mwakabela hakuyasikia, kilichofuata hapo ni watu wengine kufika muda kidogo wa baadae na kuanza naye safari ya kwenda Arusha na baadae Katavi walipoenda kutekeleza mauaji waliyopanga

8. Mheshimiwa Rais, upo uthibitisho wa Kieletroniki wa Edger Edson Mwakabela kuwepo eneo hilo siku ya Jumapili ya tarehe 23 June 2024 majira ya 2 na Dakika 45 usiku. Kwa bahati mbaya watekaji wa Edger Edson Mwakabela walisahau kuzima simu yake namba 0757637880 wakati wote waliokuwa nayo tangu wamteke eneo la Kimara Korogwe.

CDR (Call detail Records) ya simu ya Sativa namba 0757637880 inaonyesha kuwa simu yake iliendelea kupigigwa na kupokea meseji ikiwa eneo la Kituo cha Polisi Oysterbay kwa uthibitisho wa mnara aliokuwa anapokelea mawasiliano pamoja na simu yake kusomeka kwa Latitude na longitude za CDR

Bila shaka kwa kupitia CDR ya simu namba 0757637880 ya Edger Edson Mwakabela hakuna wasiwasi kuhusu tuhuma kuwa Edger Edson Mwakabela kufikishwa eneo la Oysterbay.

9. Mheshimiwa Rais, Kijana wako Edger Edson Mwakabela ndiye mtu pekee ambaye amewahi kwenda Kuzimu na kurudi (survivor). Ni mtu pekee aliye hai mwenye ushahidi juu ya nani anatoa amri za watu kutekwa, anashirikiana na kina nani kuteka na wanaoteka wanafananaje na mwisho wanaoteka na kwenda kuua wanavyofanya kazi yao kwa uaminifu.

Liwekwe graride la Utambuzi, Kijana Edger Edson Mwakabela amtambue ACP Faustine Mafwele. Huyu ni ZCO kanda Maalum ya Polisi, Dar es Salaam.

10. Mheshimiwa Rais, ndiyo maana unaona kila Mtanzania anakupinga unaposema unasubiri kuletewa report juu ya matukio ya utekaji na mauaji kutoka kwa Jeshi la Polisi au vyombo vya dola wakati viongozi wakubwa wa Jeshi la Polisi ni sehemu ya watuhumiwa wa kazi hii chafu ya utekaji na mauaji. Je watakuletea report gani kama na wao ni watuhumiwa..?

10. Mheshimiwa Rais, kwakuwa tunaye tayari mtuhumiwa mmoja wa kuanza naye ambaye ni ACP Faustine Mafwele ambaye bado yupo ofisi za umma anatoa amri na anaendelea na usimamizi wa vikosi vya serikali;

1.Tunaomba ahojiwe Edger Edson Mwakabela haraka sana
2.Tunaomba ahojiwe ACP Faustine Mafwele haraka sana
3.Tunaomba ubatilishe uamuzi wako wa sisi wasamaria wema wenye taarifa kupeleka raarifa za utekaji na mauaji kwa Jeshi la Polis.

Badala yake tunaomba uunde tume huru ya Kijaji itakayo kusaidia kubaini ukweli na kukuletea taarifa Juu ya tatizo la utekeji na mauaji ya watu.

Ahsante kwa ushirikiano wako.

Boniface Jacob
Ex-Mayor, Kinondoni & Ubungo.
0712 239 595
The voice of the silenced Majority

Inasikitisha sana. Haya yamefanywa na binadamu kweli? Mungu anawaona na anawajua na atawapa haki yao.
 
1. Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
2. Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Hamad Masauni.
3. Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Camillus Mongoso Wambura
4. Jaji Mkuu wa Tanzania, Ibrahim Juma
5. Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Jacob Nkunda
6. Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, DIGS, Suleiman Mombo
7. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Hamza Johari

1. Mheshimiwa Rais, Wakati huu nchi ikiwa katika taharuki kubwa na sintofahamu ya watu kutekwa na kupotea kwa watu kisha mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Makao Makuu, Ali Muhammad Kibao.

Niruhusu nimlete kwenu mtumishi wa serikali na afisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ACP Faustine Mafwele katika tuhuma za Mtanzania Mwenzetu Edger Edson Mwakabela (SATIVA).

2. Mheshikiwa Rais, napenda kukukumbusha kwamba, Edger Edson Mwakabela (Sativa) kijana ambaye alitekwa 23 June 2024 na kupatikana 27 June 2024 akiwa amejeruhiwa na risasi ya kichwa katika mapori ya hifadhi ya Taifa ya katavi, Mkoa wa Katavi na baadae RAIS ukamchangia matibabu ya jeraha la risasi kiasi cha Tsh Millioni 30.

3. Mheshimiwa, Rais Edger Edson Mwakabela kwa sasa amepona na hana itilifafu yoyote ya kumbukumbu wala akili pamoja na kupitishwa na katika madhira makubwa ya ukatili mbaya sana dhidi ya binadamu.

4. Mheshimiwa Rais, 27 June 2024 Edger Edson Mwakabela akiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Mkoa katavi alihojiwa na gazeti la Nipashe kwa njia ya video



Katika mahojiano hayo SATIVA anasema kwa kumbukumbu kuwa alitekwa Jumapili usiku na kupelekwa katika Karakana ya Kituo cha Polisi Oysterbay na siyo kituoni ndani kabla ya kusafirishwa kupelekwa Mkoani Arusha na baadae Katavi.

5. Mheshimiwa Rais, kwa muda wote huu Edger Edson Mwakabela alishahojiwa na Jeshi la Polisi na baadae walipotaka maelezo ya nyongeza Edger Edson Mwakabela alikuwa katika upasuaji katika hospitali ya Aga Khan.

Mwezi August Edger Edson Mwakabela aliwataarifu Jeshi la Polisi kuwa tayari ameondolewa vyuma vya taya na sasa yupo tayari kwa mahojiano na Jeshi la Polisi, akawauliza, Je, afike kituo gani na muda gani kwa mahojiano?

Soma Pia:

Kwa masikitiko makubwa Jeshi la Polisi kupitia Afande James wa kutoka Ofisi ya DCI - Dodona, alimjibu kuwa watamtafuta kwa mahojiano siku wakipata nafasi na mpaka leo Jeshi la Polisi halijawahi kupata nafasi ya kumuhoji Sativa.

6. Mheshimiwa Rais, 21 August 2024 baada ya kupotea Vijana watatu wanachama na Viongozi wa chadema Godwin Mlay, Deusdedith Soka na Frank Mbise Watanzania walianza kusambaza watu wanaowatuhumu kwa matukio ya kuteka watu kutoka katika vyombo vya dola, mmoja ya watu ambao picha zao zilisambazwa alikuwa ni ACP Faustine Mafwele

7. Mheshimiwa Rais, Kijana wako Edger Edson Mwakabela alipo iona picha ya ACP Faustine Mafwele, 22 August 20224 alitutaarifu watu wake wa karibu ikiwamo mimi, kuwa mtu yule ambaye picha yake ilikuwa ikisambaa mitandaoni ndiye alifika nje ya Kituo cha Polisi Oysterbay usiku wa Jumapili ya 23 June majira ya Saa 2:00 kuelekea majira ya Saa 3:00 usiku.

Na kwamba ACP Faustine Mafwele alimuhoji Edger Edson Mwakabela maswali matatu 1.Unaitwa nani 2. Unafanya shughuli gani 3.Unajua kwanini upo hapa?

Baada ya mahojiano hayo mafupi ACP Faustine Mafwele aliwafuata watu waliomteka Edger Edson Mwakabela na kwenda kuongea nao mazungumzo ambayo Edger Edson Mwakabela hakuyasikia, kilichofuata hapo ni watu wengine kufika muda kidogo wa baadae na kuanza naye safari ya kwenda Arusha na baadae Katavi walipoenda kutekeleza mauaji waliyopanga

8. Mheshimiwa Rais, upo uthibitisho wa Kieletroniki wa Edger Edson Mwakabela kuwepo eneo hilo siku ya Jumapili ya tarehe 23 June 2024 majira ya 2 na Dakika 45 usiku. Kwa bahati mbaya watekaji wa Edger Edson Mwakabela walisahau kuzima simu yake namba 0757637880 wakati wote waliokuwa nayo tangu wamteke eneo la Kimara Korogwe.

CDR (Call detail Records) ya simu ya Sativa namba 0757637880 inaonyesha kuwa simu yake iliendelea kupigigwa na kupokea meseji ikiwa eneo la Kituo cha Polisi Oysterbay kwa uthibitisho wa mnara aliokuwa anapokelea mawasiliano pamoja na simu yake kusomeka kwa Latitude na longitude za CDR

Bila shaka kwa kupitia CDR ya simu namba 0757637880 ya Edger Edson Mwakabela hakuna wasiwasi kuhusu tuhuma kuwa Edger Edson Mwakabela kufikishwa eneo la Oysterbay.

9. Mheshimiwa Rais, Kijana wako Edger Edson Mwakabela ndiye mtu pekee ambaye amewahi kwenda Kuzimu na kurudi (survivor). Ni mtu pekee aliye hai mwenye ushahidi juu ya nani anatoa amri za watu kutekwa, anashirikiana na kina nani kuteka na wanaoteka wanafananaje na mwisho wanaoteka na kwenda kuua wanavyofanya kazi yao kwa uaminifu.

Liwekwe graride la Utambuzi, Kijana Edger Edson Mwakabela amtambue ACP Faustine Mafwele. Huyu ni ZCO kanda Maalum ya Polisi, Dar es Salaam.

10. Mheshimiwa Rais, ndiyo maana unaona kila Mtanzania anakupinga unaposema unasubiri kuletewa report juu ya matukio ya utekaji na mauaji kutoka kwa Jeshi la Polisi au vyombo vya dola wakati viongozi wakubwa wa Jeshi la Polisi ni sehemu ya watuhumiwa wa kazi hii chafu ya utekaji na mauaji. Je watakuletea report gani kama na wao ni watuhumiwa..?

10. Mheshimiwa Rais, kwakuwa tunaye tayari mtuhumiwa mmoja wa kuanza naye ambaye ni ACP Faustine Mafwele ambaye bado yupo ofisi za umma anatoa amri na anaendelea na usimamizi wa vikosi vya serikali;

1.Tunaomba ahojiwe Edger Edson Mwakabela haraka sana
2.Tunaomba ahojiwe ACP Faustine Mafwele haraka sana
3.Tunaomba ubatilishe uamuzi wako wa sisi wasamaria wema wenye taarifa kupeleka raarifa za utekaji na mauaji kwa Jeshi la Polis.

Badala yake tunaomba uunde tume huru ya Kijaji itakayo kusaidia kubaini ukweli na kukuletea taarifa Juu ya tatizo la utekeji na mauaji ya watu.

Ahsante kwa ushirikiano wako.

Boniface Jacob
Ex-Mayor, Kinondoni & Ubungo.
0712 239 595
The voice of the silenced Majority

umeongea facts Jacob,,most of ZCO wa Dar uhutafuta U RPC kwa nguvu na jasho even kwa kuua watu wasio na hatia
 
Sasa jamaa awe ndiyo jirani yako, afu mna mgogoro wa mpaka ...
akipiga hodi unajua zamu yako ya kwenda kuzimu ishawadia.
 
1. ACP Faustine Mafwele kwa mara ya kwanza amethibitishwa hadharani na kutambuliwa na Edger Edson Mwakabela (Sativa) kama afisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania ambaye alitoa amri ya kubebwa kwake kisha kusafirishwa kwenda Arusha na katavi kupigwa risasi ya kichwa kabla ya kunusurika kuuawa.

2. ACP Faustine Mafwele amewahi kuwa OC-CID mwaka 2011-2015 wa kituo cha Polisi Arusha na baadae akawa RCO wa Mkoa wa Arusha

Wakati wa mauaji ya wanachama wa CHADEMA maandamano ya Arusha ya 04 January 2011 alikuwa OC-CID.

Wakati huo Faustine Mafwele akiwa na cheo cha ni Mrakibu Msaidizi wa Polisi

Tarehe 05 January 2012 akiwa Mrakibu Msaidizi wa Polisi Faustine Mafwele alipigwa risasi na Jambazi Jijini Arusha kati ya majibizano ya risasi baina yake na Jeshi la Polisi,hata hivyo askari mmoja wa Jeshi la Polisi aliuawa kwa risasi na Mafwele aliendelea kutibiwa hospitali ya Seriani.

3.Amewahi kuwa Zonal Crime Officer (ZCO) wa Kanda maalum ya MKIRU yani Mkuranga, Kibiti, Rufiji.

4.katika kesi za watu wanaolalamika kwangu ndugu zao kutekwa, kupotea au kukutwa wameuwawa asilimia 90 wanamtuhumu ACP Faustine Mafwele kama mtu ambaye ndiyo mtekelezaji wa shughuli hizi mbaya.

5.ACP Faustine Mafwele amekuwa ni Afisa wa Jeshi la Polisi ambaye hana madaraka makubwa sana ila anaogopwa hadi na viongozi wake wa Jeshi la Polisi kuanzia Kanda Maalum ya Dar es saalam hadi Makao Makuu ya Polisi,Dodoma

6.Kuna hisia ambazo hazijathibitishwa kuwa ni Penetrating Officer (PE) wa Idara ya Usalama wa Taifa ambaye anafanya kazi mbili kwa pamoja kiasi cha Viongozi wa Jeshi la Polisi kumuogopa wakiamini ni Mtu ambaye kazi zake zina baraka ya Idara ya Usalama wa Taifa.

7.Baada ya Kazi Maalum ya MKIRU (Mkuranga, Kibiti Rufiji) kumalizika akiwa kama Crime zonal Officer (ZCO) alihamishiwa kwenda Kuwa RCO wa Mkoa wa Mwanza

Huko Dunia ilianza kufahamu ukatili wa ACP Faustine Mafwele baada ya 2021 Mzee William Sije kulalamika kuwa RCO Mafwele wa Mkoa wa Mwanza amemuua Mtoto wake James William Sije.

8.IGP Simmon Sirro alimuhamishia Mkoa wa Dar es Salaam kuja kuwa Zonal Crime Officer (ZCO) wa Kanda maalum ya Dar es saalam 06 April 2022 kwa kazi maalum dhidi ya Panya road na ujambazi wa kutumia Silaha.

9.Misheni na siri nyingi anazozijua ndiyo chanzo cha Viongozi wa Serikali ya CCM kumuogopa na kumlinda wakiamini anaweza kwenda kusema mambo mabaya zaidi anayoyajua.

Kupitia hoja hiyo, ACP Faustine Mafwele amelalamikiwa mara nyingi sana lakini Viongozi wizarani na serikalini wanamuogopa sana kuchukua hatua.

10. Mafwele pia anatuhumiwa na familia nyingi kama mtu ambaye ameshiriki mauaji kwa moja katika kuwapoteza ndugu wa baadhi ya familia zao
kupotea kwa

1.Mfanyabiashara Musa Mziba
2.Kupotea kwa Deo Mugasa
3.Kupotea kwa Adinani Hussein Mbezi
4.Kupotea kwa Vijana watano wa Aggrey
5.kutekwa na Kupigwa risasi kwa Edger Edson Mwakabela.
6.Faustine Mafwele na genge lake tarehe 22 August 2024 alituhumiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kuhusika kwake ktk Kupotea kwa Kina Godwin Mlay,Deusdedith Soka na Frank Mbise

11.Katika kuonyesha jeuri na kuogopewa na wenzake ACP Faustine Mafwele amejipa ukiranja wa kuwa mwenyekiti wa Ma-RCO wa Jeshi la Polisi Tanzania tofauti na utamaduni wa Jeshi la Polisi ulio zoeleka wa Ma-RCO kuwa chini ya usimamizi wa DCI

12.Nimeona niweke kumbukumbu hizi vizuri na wasifu mfupi wa ACP Faustine Mafwele mjue kazi kubwa iliyopo mbele yetu kuhakikisha Faustine Mafwele anafikishwa mbele ya vyombo vya sheria na kujibu tuhuma zake

Bila kelele za kutosha hakuna Jambo litakalotokea kwa sababu nilizozitaja hapo juu

Boniface Jacob
Ex-Mayor Kinondoni & Ubungo
0712 239 595
The voice of the silenced Majority
IMG_7547.jpeg
 
Unaweza kutuhumiwa hivi na ukakaa kimya kama hauhusiki?

Kuna wengine Maria Sarungi nae kawaanika kwa tuhuma hizi hizi za watu kupotea ambapo kawaanika kupitia mtandao wa X.

Inaonekana kuna watu wamevujisha siri maana wametajwa.kwa majina na vyeo.

Wacha tuone.
 
Hata hivyo wasifu wake unatosha kusema sio mtu wa kawaida katika maswala ya ulinzi, kwa hio wakati taarifa na tuhuma zake zikisambazwa tahadhari kubwa ichukukiwe.
 
Back
Top Bottom